ad

ad

HARUSI YA 2FACE KUFANYIKIA DUBAI

LAGOS, NIGERIA
ACHANA na wenye fedha! 2Face Idibia na mwenza wake Annie Macaulay wametangaza kwenda kufanya harusi yao Dubai badala ya Abuja kama ilivyotangazwa awali.
Annie ameanika hayo kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku akitaja siku ya harusi yao kuwa Machi 23, mwaka huu.
2Face ambaye ni msanii wa muziki na Annie wa filamu, tayari wamefunga ndoa ya kimila Mei 2, mwaka huu, ambayo ilikuwa ya siri.
Annie alikwenda Dubai hivi karibuni kununua vifaa kwaajili ya ndoa na kufanya ‘booking’ ya ukumbi kwaajili ya sherehe ya harusi yao.
Pia alikwenda New York, Marekani kununua gauni lake la harusi.
Habari zimepasha kuwa, wawili hao wamepanga kwenda Dubai pamoja na marafiki wachache na ndugu wafamilia, ambao watakodiwa ndege maalumu.
Kwamba tayari wawili hao wamefanya ‘booking’ ya vyumba kadhaa kwenye hoteli chache huko Dubai, ikiwemo Burj Al Arab – hoteli ya kifahari zaidi duniani, ambayo wenza hao pia watakwenda ‘kujiachia’ baada ya ndoa yao.
Powered by Blogger.