CASSIM MGANGA KUPELEKA UTAJIRI WA MAHABA LINDI NA MTWARA
MWIMBAJI mkali wa nyimbo za mahaba Cassim Mganga wiki anatarajiwa kufanya maonyesho matatu katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
Maonyesho
hayo yamechukuliwa kama mwendelezo wa shangwe za msimu wa wapendanao
ambapo Ijumaa hii Cassim atakuwa ndani ya ukumbi wa BR uliopo Masasi
mkoani Mtwara.
Jumamosi
Cassim atakuwa Lindi mjini katika ukumbi wa Paris Club kabla ya
Jumapili kuelekea Mtwara mjini na kufanya onyesho lake la mwisho kwenye
ukumbi wa Maisha Club.
Miongoni mwa nyimbo zinazomfanya Cassim asubiriwe kwa hamu kubwa na wakazi wa mikoa hiyo ni “Tajiri wa Mahaba”.
Post a Comment