THEO WALCOTT AKUBALI KUBAKI ARSENAL
HATIMAYE
Theo Walcott amekubali mkataba mpya Arsenal na nyota huyo wa timu ya
taifa England mwenye umri wa miaka 23, leo anatarajiwa kusaini mkataba
wa pauni 100, 000 kwa wiki, linaandika la gazeti la The Sun.
Kocha
wa Arsenal, Arsene Wenger amethibitha: “Natumai mkataba utakuwa
umesainiwa kabla ya wikiendi. Kuna uwekezakano. Kwa mtazamo wangu ni
asilimia 99 sasa.
Wenger
alikuwa anahofia kumpoteza mshambuliaji huyo baada ya mvutano juu ya
mkataba wake na alihofia kuwa amepoteza mchezaji mwingine mkubwa.
Kocha
huyo ameshuhudia majina makubwa kama Cesc Fabregas, Samir Nasri, Robin
van Persie na Alex Song wakiondoka klabuni ndani ya misimu miwili.
Wenger alikiri: “Kutokana na uzoefu nilioupata, niliingia woga katika hatua fulani kwamba angeweza kuondoka .
“Wakati mambo yanapochukua muda mrefu, si dalili nzuri.
“Imetuchukua muda mrefu kufika tulipotaka. Bado halijakamilika, lakini tunatumai hadi wikiendi litakuwa limekwisha”

Post a Comment