ad

ad

Simba yapigwa tena Oman

MABIGWA wa Ligi Kuu ya Vodacom, Simba SC, wameendelea kufanya vibaya katika michezo yao ya kirafiki nchini Oman, baada ya jana kutandikwa mabao 3-1 na timu ya Qaboos kwenye Uwanja wa Qaboos nchini humo.

Kwa mujibu wa kocha wa zamani wa Simba, mwenye makazi yake nchini Oman, Talib Hilal, licha ya kipigo hicho, Simba ilionyesha kandanda safi na ya kuvutia, huku bao la kufutia machozi likipachikwa na mshambuliaji, Haruna Moshi ‘Boban’.

Simba ambayo iko huko tangu wiki iliyopita, kwa kambi maalumu ya kujiandaa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika, juzi ililala bao 1-0 kwa timu ya taifa ya Vijana ya Oman chini ya miaka 23.
Aidha Simba inayonolewa na Patrick Liewig, inatarajiwa kucheza mechi nyingine ya kirafiki na Fanja Fc, kabla ya kurejea nchini Januari 23, tayari kwa kuanza mzunguko wa pili wa ligi unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 26.
Powered by Blogger.