ad

ad

BAYERN MUNICH YAIBUKA MBAMBE VITA VYA KUMSAKA GUARDIOLA

MUNICH, UJERUMANI
BAYERN MUNICH imeshinda vita ya kuwania kumsainisha Pep Guardiola, aliyeibebesha Barcelona mataji 14 ndani ya misimu minne aliyokuwapo Nou Camp.

Pep Guardiola - Bayern Munich
Taarifa hiyo imekuwa mwisho wa klabu kadhaa za Premier League, zikiwamo Manchester City na Chelsea zilizokuwa zikimfukuzia.
Kocha huyo Mhispania mwenye miaka 41 pia alikuwa akihusishwa na klabu za Arsenal na Manchester United — endapo Arsene Wenger na Alex Ferguson wangeachia ngazi.
Lakini baada ya miezi kadhaa ya tetesi za hapa na pale, kocha huyo amechagua kujiunga na miamba hiyo ya Ujerumani kuanzia mwezi Julai.
Guardiola, ambaye anautumia msimu huu kwa mapumziko jijini New York, Marekani amesaini dili la mkataba wa miaka mitatu Allianz Arena.
Mtendaji Mkuu wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge alisema: “Tuna furaha kubwa kwamba tumefanikiwa kumshawishi mtaalamu wa soka, Pep Guardiola, ambaye alikuwa akihitajika na kuwasiliana na klabu nyingi kubwa, kuja Bayern Munich.
“Guardiola ni mmoja wa makocha wenye mafanikio makubwa duniani na tuna hakika kwamba anaweza kuleta mafanikio makubwa si kwa Bayern Munich pekee, lakini pia kwa soka ya Ujerumani kwa ujumla.”

Guardiola atachukua mikoba kutoka kwa Jupp Heynckes ambaye aliamua kutoongeza mkataba wake, na atastaafu.
Kabla ya kumwaga wino Bayern, Guardiola alisema ana nia ya kwenda England kufundisha soka katika moja ya klabu za Premier League siku za usoni.

Alisema hayo katika ujumbe wa video alioutuma kwa Chama cha Soka England (FA) kukipongeza kutimiza miaka 150 tangu kuanzishwa.
"Kama mchezaji, sikuweza kutambua ndoto yangu kucheza huko," alisema.
"Lakini natumaini, katika siku zijazo, nina changamoto kuwa kocha huko na kuhisi uzoefu wa makocha wote na wachezaji ambao wamekuwa huko.
"Ni ya kipekee, kucheza katika ligi ile (Premier League). Nataka kuhisi mashabiki, mazingira, vyombo vya habari na staili ya wachezaji. Mara zote nimebaini soka ya Kiingereza inavutia. Sapoti kwa timu ya nyumbani ni ya kushangaza.
"Ndani ya Italia, Latini watu watakusapoti wakati mnapocheza, na endapo utapoteza, watakuua. Ndani ya England, mara zote nimeshangazwa kwamba watu wanasapoti kila kitu.
"Hiyo ni nzuri na kwanini, labda, mimi bado ni kijana, kama miaka 41 tu, natumaini kuwa na changamoto au fursa ya kutoa mafunzo huko."
Powered by Blogger.