ad

ad

Pacome Atembelewa Hospitalini na Uongozi wa JKT Tanzania

 

Uongozi wa Klabu ya JKT Tanzania pamoja na mchezaji Hassan Wahabi wamemtembelea kiungo wa Yanga SC, Pacome Zouzoua leo kwenye hospitali ya Aga Khan, ambaye anaendelea na matibabu hoospitalini hapo baada ya kupata jeraha katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kati ya JKT Tanzania na Yanga SC, uliochezwa Juni 30, 2025, kwenye Uwanja wa Major General Isamuhyo.

Pacome alipata jeraha hilo baada ya kugongana na Hassan Wahabi walipokuwa wakiwania mpira, hali iliyomlazimu kuondolewa uwanjani na kukimbizwa hospitalini kwa ajili ya kupatiwa matibabu.



 

No comments

Powered by Blogger.