ad

ad

Ujumbe wa Dogo Janja kwa Irene Uwoya, ‘Unanifanya nacheka usingizini’

Msanii wa muziki Bongo, Dogo Janja ameandika ujumbe wa kumtakia kheri ya siku ya kuzaliwa mke wake, Irene Uwoya.


Ikiwa siku ya jana ndio ilikuwa birthday ya Irene, Dogo Janja ametumia ukurasa wake wa Instagram kuandika haya machache;

    Umebadilisha maisha yangu kutoka nanii kua nanii!! Unanifanya nacheka mda wote hata nikiwa usingizini!! Ww ni mke wangu wakwanza na nimke wangu wamwisho!!tuipeleke dunia kwenye mwangaza waajabu tuwamulike wasioamini wakaamini kua sisi ni wazazi mwakani, wengi wameoana ila sisi tumefunga ndoa!! Happy birthday mke wangu  #MrsAbdul
Taarifa za Dogo Janja na Irene Uwoya kufunga ndoa zilianza kuchipuka November 25 mwaka huu, hata hivyo ni vigumu kutaja tarehe kamili kutokana na namna walivyoliweka suala hilo.

No comments

Powered by Blogger.