ad

ad

Sadifa Aachiwa kwa Dhamana, Apewa Masharti Magumu

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Dodoma iemwachia kwa dhamana aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis (Mbunge) anayekabiliwa na mashtaka ya kutoa rushwa wakati wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa UVCCM Taifa.

Sadifa ameachiwa leo Desemba 19, 2017 baada ya mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa mashtaka ambao waliliwasilisha mahakamani hapo kuweka zuio la kupewa dhamana.

Mtuhumiwa huyo ametakiwa kudhaminiwa na watu watatu pamoja na kusaini bondi ya Tsh. Milioni 1, huku akipewa masharti ya kutosafiri nje ya nchi.

No comments

Powered by Blogger.