Rasmi Sportpesa Yaikabhi Serikali Uwanja Wa Taifa, Nyasi Saafi
Kampuni ya kubashiri matokeo ya SportPesa Tanzania, jana imeikabidhi serikali Uwanja wa Taifa wa jijini Dar es Salaam.
Tukio
hilo la kihistoria lilifanyika jana kwenye uwanja huo lililoenda
sambamba na ufunguzi wa mashindano ya bunge la Afrika Mashariki wa Kati.
Akikabidhi
uwanja huo, Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa, Abbas
Tarimba alisema wamekabidhi uwanja huo baada ya ukarabati kumalizika na
tayari kwa matumizi.
Tarimba
alisema, ukarabati huo umetumia zaidi ya shilingi bilioni 1.4 kwenye
sehemu ya uwanja ikiwemo upandaji wa nyasi na udongo.
“Nina
furaha ya dhati kusimama mbele yenu kama mwakilishi wa kampuni ya
SportPesa na leo (jana) hii katika tukio la kihistoria katika tasnia ya
soka nchini la kukabidhi uwanja wa Taifa kwa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania, hakika ni siku ya kukumbukwa.
“Ukarabati
huo uliochukua miezi mitatu katika utengenezaji wa ‘pitch’ kwa maana ya
kuotesha uwanja na kuzikuza hadi kufikia hapa.
“Uwanja
huu baada ya ukarabati utakaa miaka kumi bila ya kuzikarabati, hivyo
utaona ni jinsi gani uwanja huo tumeukarabati kwa kiwanmgo cha juu,”
alisema Tarimba.
Kwa
upande wa serikali, Waziri wa Habari Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni
na Michezo Dk Harrison Mwakyembe yeye alisema kuwa “Niseme kuwa
serikali imeridhika kwa kiwango cha juu cha ukarabati wa uwanja huu wa
taifa.
“Niwapongeze
na kuwashukuru SportPesa kwa kuomba kujitolea kukarabati uwanja huu, ni
jambo jema kwetu, uukarabati huu utatufanya kuutumia kwa muda wa miaka
kumi bila ya ukarabati na nimeukagua uwanja huu kiukweli una viwango
vizuri,”alisema Mwakyembe.
Post a Comment