ad

ad

Michirizi Ya Damu - 04

“Lakini mbona unanikataa?” aliuliza Fareed.
“Naomba uniache!”
“Nikuache upumzike?”
“Yaani uniache moja kwa moja. Usinijuejue,” alisema Dk. Fabby na kukata simu.
Fareed alihuzunika lakini hakuwa na jinsi, hakutaka kuwasiliana na Dk. Fabby kwani hakumpenda kama alivyompenda Keith ambaye alikuwa tayari kumpa kiasi chochote cha fedha japokuwa hakutaka kumwambia ukweli.
“Haina shida.”

Akakaa na kumsubiria mzee huyo. Alimwambia kwamba angefika nyumbani hapo muda si mrefu. Akajiachia kochini huku moyo wake ukiwa na amani kwamba alifanikiwa kulala na Dk. Fabby, hata kama hakumtaka tena kwake wala hakulijali sana.
Baada ya saa moja, Keith akafika nyumbani hapo. Alipomuona Fareed, akamfuata na kumkumbatia. Alimkumbuka na muda wote alikuwa akimuwaza yeye tu. Walikaa na kuzungumza, Keith hakutaka kumwambia ukweli Fareed jinsi alivyokuwa akijisikia ila alijua kwamba mwanaume tata huyo alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
“Umefanikiwa?” aliuliza Keith.
“Ndiyo!”
“Safi sana, hebu nione,” alisema mwanaume huyo na kutaka kuonyeshewa.
Hilo halikuwa tatizo kwa Fareed, akavua nguo zake na kisha kumwangalia. Mapigo ya moyo wa Keith yalikuwa yakienda kasi, hakuamini kama alikuwa akimwangalia mwanaume huyo.
Mwili wake ukamsisimka, hakutaka kukubali, akamchukua Fareed na kwenda naye kitandani, hapo, akaanza kumwambia maneno mengi ya mahaba, jinsi alivyokuwa akimpenda, hakuacha kumsifia kwa kila kitu kiasi kwamba Faredd akajiona kuwa mzuri kuliko watu wote duniani.
“Kweli?”
“Ndiyo! Wewe ni malaika wangu, ni mrembo kuliko warembo wote waliowahi kutokea katika hii dunia!” alisema Keith maneno ambayo alikuwa na uhakika kwamba hayakuwa kweli bali alitaka kukamilisha kile alichokitaka.
Fareed akaachia tabasamu pana, akajiangalia, akahisi kwamba kweli alikuwa mrembo kuliko warembo wote waliowahi kutokea katika dunia hii. Akashikwa mkono, akaacha, akashikwa bega, akaacha, kila alipokuwa akishikwa huku na kule, aliacha na mwisho wa siku, baada ya saa moja wote kujikuta wakiwa hoi kitandani.
“Ahsante,” alisema Fareed huku akimwangalia Keith kwa uso uliokuwa na tabasamu pana.
“Umeridhika?”
“Sana mpenzi! Kumbe nilikuwa najichelewesha tu!” alisema Fareed huku akimwangalia mwanaume huyo.
Penzi jipya likaanzishwa, kila mmoja alikuwa bize na mwenzake, japokuwa Keith alikuwa na familia yake jijini New York lakini hakutaka kurudi huko, alitekwa na biashara zake zote alizihamishia huko, mahesabu akawa anapelekewa hukohuko alipokuwa.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, mapenzi ya jinsi moja yalimpeleka puta na hakukumbuka kitu chochote kile. Siku wiki moja baadaye akaamua kumfanyia sapraizi Fareed, alitaka kumnunulia gari jipya kwani hakutaka kuona akipata tabu yoyote ile.
Siku hiyo akakaa na kuzungumza naye mengi, ilipofika saa sita mchana, akamchukua na kisha kuondoka nyumbani hapo. Wakati wametoka ndani ya jumba hilo kubwa na kushika barabara, ghafla akaliona gari moja likiwafuata kwa nyuma.
Wakawa na hofu kwa kuhisi kwamba inawezekana watu waliokuwa humo walikuwa majambazi waliotaka kuwaua au kuwaibia hivyo. Kila Keith alipokuwa iongeza mwendo, gari la nyuma likawa linaongeza kasi kiasi kwamba wakaona huo ndiyo ungekuwa mwisho wao.
Walichokifanya ni kuingia kwenye barabara kubwa ambapo walikwenda mpaka sehemu iliyokuwa na watu wengi, akalisimamisha gari hilo kwa kuamini kwamba hata kama watu hao wangeteremka kwenye gari na kuwafuata, wasingeweza kuwaua kutokana na wingi wa watu mahali hapo.
Gari lile la nyuma likasimama na mwanaume mmoja kuteremka. Hawakuzungumza kitu, walibaki wakimwangalia mwanaume huyo ambaye alionekana kuwa na hasira kubwa.
Fareed hakumtambua mpaka alipofika karibu, Keith akateremsha kioo, macho ya Fareed yakatua kwa mwanaume aliyekuwa akimfahamu, alikuwa Godfrey aliyeonekana kuwa mwenye hasira kupita kawaida.
Akaanza kuwaangalia wote wawili kwa macho yaliyokuwa na shari, kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa tayari kufanya jambo lolote lile kwani hata mwili wake ulianza kutetemeka kwa hasira kali.
 ****
“What can I help you, sir?” (nikusaidie nini bwana mkubwa?) aliuliza Keith huku akimwangalia Godfrey aliyekuwa na hasira kali.
“I want my bae,” (namtaka mpenzi wangu)
“Your bae? Who the hell is she?” (mpenzi wako? Ndiye nani huyo?) aliuliza Keith huku akimwangalia mwanaume huyo machoni.
Godfrey akayahamisha macho yake na kumwangalia Fareed ambaye alikuwa akitetemeka tu. Kwa kitendo kile cha kumwangalia Fareed, Keith akajua mtu aliyekuwa akizungumziwa na hivyo kumuuliza Fareed kama alikuwa akimfahamu mwanaume huyo.
“I don’t know him,” (wala simfahamu) alisema Fareed huku akimwangalia Godfrey kwa macho yaliyojaa mshangao, alionekana kama kweli hamfahamu mwanaume huyo.
“Fareed, look at my eyes! Don’t you know me? Look at my eyes bastard,” Fareed, yaangalie macho yangu! Hunifahamu? Yaangalia macho yangu mwanaharamu weee) alisema Godfrey huku akionekana kuwa na hasira kali zaidi.
Bado Fareed aling’ang’ania kwamba hakuwa akimfahamu mwanaume huyo na hiyo ndiyo siku ya kwanza kumuona machoni mwake. Keith hakutaka maswali zaidi, alichokifanya ni kumwambia dereva wake aliondoe gari mahali hapo na kufanya hivyo.
Godfrey alibaki akiwa amelowa, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea, kukataliwa na Fareed mchana kweupe namna ile kulimuumiza mno moyoni mwake. Watu wote walikuwa wakimwangalia, wengine walimpigia honi kumaanisha kwamba walimtaka aondoke mahali pale ili waendelee na safari yao.
Akarudi ndani ya gari, akaingia na kutulia kwenye usukuni, alikuwa na wazo tele na muda mwingine alikuwa akitokwa na machozi, kwa kile kilichokuwa kimetokea kwake kilionekana kuwa kama ndoto ya mchana. Hakukaa sana mahali hapo, akaondoka zake huku akiwa na hasira kifuani.
Moyo wake ukajaa ghadhabu, hakufikiria kitu kingine kama kumuua Fareed. Aliutesa moyo wake, hakuwa radhi kumuona mwanaume tata huyo akiendelea kuishi na wakati aliuumiza moyo wake kupita kawaida.
“Ni lazima nimuue, nitatumia gharama zangu zote kumuua huyu mpumbavu,” alisema Godfrey huku akionekana kuwa na hasira sana. Moyo wake ukapanga kumuua Fareed kama kumlipizia kisasi kwa kile alichokifanya.
***
Wanaume wote waliokuwa wakitembea na Fareed walichanganyikiwa, hawakuamini kama alikuwa akijua sana kitandani. Mioyo yao iliuchanganyikiwa, walipokutana naye, hawakutaka kumuacha, waliendelea kumtafuta zaidi na zaidi.
Kitendo cha kuwa na Keith kwake yalikuwa mateso makubwa, alibanwa sana kwani mwanaume huyo hakutaka kumuona akiondoka kuelekea sehemu yoyote ile.
Alipokea simu kutoka kwa matajiri wengi ambao walimuahidi kumpa kiasi kikubwa cha fedha lakini kuonana nao suala hilo lilikuwa gumu sana. Aliwasiliana nao kwenye simu, aliwatumia picha zilizokuwa zikionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa mzuri.
Hakuzoea kuwa na mwanaume mmoja, tangu alipompata wakala wake, Asteria, alikuwa akitoka na wanaume mbalimbali, hayo ndiyo yalikuwa maisha yake na hata alipoambiwa na Keith kwamba hakutakiwa kutoka, kwake yalikuwa mateso makubwa.
“Haiwezekani! Siwezi kukaa na mwanaume mmoja, kwani kanioa? Yeye mbona ana familia yake, lazima nitoke,” alisema Fareed huku akionekana kutokukubaliana na kile kilichokuwa kikiendelea.
Ndivyo alivyofanya, baada ya wiki moja huku akiwa amempa Godfrey mahaba mazito akaamua kuondoka na kuelekea Dubai. Hakuwa ameaga, alimtoroka kwani kitu alichokuwa akikiangalia ni kwa namna gani angeweza kuifurahisha roho yake.
Huko Dubai alikwenda kuonana na bilionea mwingine, Saed ambaye alikuwa akimsumbua sana kwenye simu. Walipoonana kwa mara nyingine, wakaelekea kitandani ambapo huko wakafanya mambo yote na kukumbushiana siku ya kwanza walipokuwa wameonana.
Hakutaka kuwasiliana na Keith, mwanaume huyo alimpigia sana simu kutaka kuzungumza naye lakini hakupokea, alinyamaza kimya na hata zile meseji alizokuwa akitumiwa, nazo hakuzijibu japokuwa aliziona na kuzisoma.
Akili na mawazo yake yalikuwa kwa Bilionea Saed tu ambaye hakuwa msiri, alimchukua Fareed na kumtamulisha kwa baadhi ya marafiki zake na kuwaambia kwamba alikuwa mpenzi wake wa kufa na kuzikana. Hilo lilimpa furaha Fareed kwa kuamini kwamba angeishi milele na mwanaume huyo.
Marafiki wa Saed nao hawakutaka kukubali, kwa kuwa Fareed alionekana kuwavutia tena huku kwa nyuma akianza kutuna na kifua kuonekana, hawakutaka kumuacha, walichokifanya ni kuanza kummendea kitu ambacho kilimfurahisha kwani akili yake ilifikiria fedha kuliko mapenzi.
Alipokea meseji nyingi kutoka kwa wanaume mbalimbali, wote walimtaka kimapenzi. Hakuwa mchoyo, alikubali kufanya nao na hivyo kukutana nao sehemu yoyote waliyotaka na kuwaridhisha.
Ndani ya mwezi mmoja akatembea na marafiki kumi wa Saed, hakuwa akijua, alipokuwa naye alikuwa akimsifia kwa marafiki zake kumbe ndiyo haohao waliokuwa wakimbadilikia kila alipowapa kisogo.
Wakati mwezi wa pili ulipokatika, ndipo akaingia kwenye umbo rasmi la kike, alikuwa na muonekano kama wa wanawake wengine, alikuwa na kifua kikubwa, wowowo, mavazi ya kile, alijitahidi kuibadilisha sura yake kwa kuipaka sana poda, akaseti nywele zake, kwa kifupi alikuwa mwanamke kamili isipokuwa sehemu za siri ambapo alishindwa kuibadilisha.
“Hivi huyu mpumbavu Keith anaendelea kunisubiri au? Asahau! Mimi siwezi kuwa na bwana mmoja. Kwanza ukila ugali kila siku utachoka, siku nyingine kula wali, ukiuchoka, kula pilau, nalo ukilichoka, nyonya koni,” alijisemea huku akiirambaramba midomo yake kama mwanamke aliyepewa ahadi ya kukutana na mwanaume kwenye nyumba ya wageni.
Wakati yeye akifikiria hayo yote, upande wa pili Keith alikuwa na hasira kali, hakuamini kama kweli Fareed alikuwa amemtenda kiasi hicho na wakati alikuwa ametumia kiasi kikubwa cha fedha kumgharamia.
Hakukubali, moyo wake ulijaza ghadhabu nzito na alikuwa tayari kufanya lolote lile kumshughulikia mwanaume huyo.
Alimtafuta, aliwaagiza vijana wake kila kona hapo Los Angeles kumtafuta na kumleta kwake. Vijana hao wakafanya kazi usiku na mchana, wakazunguka katika Cassino mbalimbali lakini hawakuweza kumuona. Hawakuishia hapo, wakazunguka kwenye miji mingine lakini napo hawakuweza kumuona kitu kilichowapa maswali mtu huyo alikuwa wapi.
“Tumemtafuta sana! Hatujamuona!” alisema kijana mmoja.
“Sawa. Ngoja nimpigie wakala wake,” alisema Keith na kumpigia simu Asteria, alitaka kufahamu mahali alipokuwa Fareed ili amuue, hata mapenzi aliyokuwa akiyataka, yakamtoka, hakuwa radhi kuona mtu aliyemgharamia akimchukua mwanaume mwingine.
“Na akisema yupo Tanzania tu, namfuata na kumuua hukohuko!” alisema Keith na kumpigia simu mwanamke huyo. Kwa kuwa Fareed hakumwambia kuhusu kumtoroka Keith, wala kumwambia kwamba alikuwa bwana wake mpya, mwanamke huyo akamwambia kwamba alikuwa Dubai akila maisha na bilionea Saed, maneno yaliyomchoma mno Keith.
“Yaani anakula maisha na mwanaume mwingine. Sasa atanitambua,” alisema Keith! Hapohapo akawapigia simu vijana wake. Alitaka kuzungumza nao, mezani kulikuwa na jambo moja tu. Kumteka Fareed na kumuua.
***
Huko Dubai maisha yalikuwa ni ya raha kabisa, Fareed hakuishia kwa wanaume hao tu, alichokuwa akikiangalia kilikuwa pesa tu. Siku zikakatika huku akiendelea kupata fedha, alilala katika mahoteli makubwa na ya kifahari ambayo alipangiwa na mabwana zake.
Alisahau kabisa kama kulikuwa na shida katika dunia hii, alifurahia kwa kuwa aliona kwamba hakukuwa na kitu alichoshindwa kukifanya kwa sababu alikuwa na pesa ya kufanya kitu chochote kile.
Baada ya wiki mbili akapigiwa simu na mwanaume mmoja, alikuwa mwanaume wa Kizungu aliyemwambia kwamba alitaka kuonana naye, mwanaume huyo alijitambulisha kwa jina la Mickey Downford.
Kwanza Fareed hakutaka kukubali, lilikuwa jambo gumu kukutana na mwanaume huyo, alihisi kwamba hakuwa na fedha za kumpa kwani yeye aliwazoea mabwana wa Kiarabu ambao walikuwa radhi kutoa kiasi chochote cha pesa ili kupata wanachokihitaji.
Kwa kipindi cha wiki nzima Mickey alikuwa akiomba kuonana na Fareed lakini alikuwa akikataa na wakati mwingine alimwambia kwamba hakuzoea kutembea na Wazungu, yeye aliwapenda Waarabu tu.
“Lakini nina pesa!” alisema Mickey kwenye simu.
“Nitaamini vipi?”
“Subiri! Nipe namba yako ya benki,” alisema Mickey na hivyo kupewa namba hiyo.

9

Ndani ya dakika kumi, simu ya Fareed ikalia kuonyesha kwamba kulikuwa na ujumbe, haraka sana akaichukua na kuangalia, ilikuwa ni meseji kutoka katika huduma ya kibenki ambayo ilimwambia kwamba alikuwa amepokea kiasi cha dola elfu hamsini, zaidi ya milioni mia moja na nusu kwa fedha za Kitanzania.
Akakaa chini, hakuamini kile alichokuwa amekiona, hakujua kama alitumiwa na mwanaume ambaye alimpuuzia kila alipomwambia kwamba walitakiwa kuonana. Kiasi hicho kilikuwa kikubwa sana kwake, kwa kawaida aliwatoza wanaume kiasi cha dola elfu moja mpaka elfu mbili, kitendo cha kupewa kiasi kikubwa cha fedha kilimchanganya. Wakati akiwa kwenye hali ya furaha, Mickey akampigia simu.
“Nadhani umeona mabadiliko kwenye akaunti yako!” alisema Mickey.
“Nimeona mpenzi!”
“Huo ni mwanzo. Na nimekupa kiasi kidogo kwa sababu tu huniamini!” alisema Mickey.
Kichwa cha Fareed kilichanganyikiwa, hakuamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa amemtumia kiasi kikubwa cha fedha. Hapo ni kwamba hawakuwa wamekutana na kuzungumza, hawakulala kitandani alimgawia kiasi hicho cha fedha, kama angemfanyia kama wengine angepata kiasi gani?
Alipojiuliza, akajikuta akianza kuvutiwa na Mickey. Hakutaka kubaki hotelini, haraka sana anawasiliana na mwanaume huyo kwa miadi ya kuonana na kumwambia kwamba walitakiwa kuonana sehemu tulivu, katika ufukwe wa Kite uliokuwa Magharibi mwa mji huo.
Ndani ya saa moja, tayari Fareed alifika mahali hapo. Alikuwa akiangalia huku na kule akimtafuta mwanaume aliyekuwa amepanga naye miadi ya kuonana.
Baada ya dakika kadhaa, akaliona gari la kifahari, Bugatti la watu wawili likifika mahali hapo. Alilikodolea macho, lilikuwa gari la gharama kubwa na ilionyesha kwamba mtu aliyekuwa humo ndani hakuwa wa mchezomchezo kuhusu masuala ya pesa.
Mlango ukafunguliwa, ukafunguka kwa kwenda juu na mwanaume mmoja aliyevalia suti kuteremka. Watu wote waliokuwa katika ufukwe huo walikuwa wakimwangalia, hawakuamini kama kijana mdogo aliyeteremka ndiye aliyekuwa akiendesha gari hilo la kifahari.
“Mmh! Kuna watu wana hela bwana!” alijisemea Fareed, hakuwa amejua kwamba mwanaume huyo ndiye alikuwa Mickey aliyekuwa akimsubiri.
Moja kwa moja Mickey akaifuata meza ya chakula iliyokuwa katika eneo la kulia chakula, akachukua simu yake na kumpigia Fareed kwa ajili ya kumpa taarifa kwamba alikuwa amefika.
“Mbona sikuoni?” aliuliza Fareed.
“Unaliona hilo gari lililosimama hapo ufukweni?”
“Ndiyo! Hili la kifahari?”
“Yaap!”
“Sasa wewe upo wapi?”
“Umemuona dereva aliyeteremka?”
“Ndiyo!”
“Huyo ndiye mimi!”
“Ndiye wewe? Unaendesha Bugatti?”
“Yeah! Naomba unifuate! Bila shaka unajua hapa nilipokuja kukaa,” alisema Mickey na kisha kukata simu.
Fareed hakuamini, alimdharau mwanaume huyo lakini kumbe alikuwa bilionea mkubwa tu. Wakati anapiga hatua kuelekea kule kulipokuwa na meza ile, macho yake hayakuacha kuliangalia gari lile, lilimpagawisha na kujiona kama yeye ndiye mmiliki halali.
Alipofika katika meza hiyo, kitu cha kwanza Mickey akasimama na kumkumbatia. Ilikuwa vigumu kuamini kama mtu huyo alikuwa mwanaume kwani alivalia gauni refu, kilemba na nyuma alijazia kwani zile sindano alizokuwa amechomwa zilifanya kazi vizuri na hata kifua chake kilijaa.
“U mzuri sana,” alisema Mickey huku akimkumbatia Fareed.
“Nashukuru sana mpenzi!” alisema Fareed, akatoa tabasamu la kike na kutulia kwenye kiti.
Walizungumza mambo mengi huku Mickey akimwambia kwamba alikuwa bilionea kutoka nchini Australia na alifika hapo kwa ajili ya mambo yake ya biashara ila alipomuona klabu siku za nyuma ndizo zilimpagawisha na kuitafuta namba yake ambayo kwa maelezo yake alimwambia kwamba aliinunua kutoka kwa mtu kwa dola elfu mbili.
“Jamaniiiii!”
“Ndiyo ukweli!”
Walizungumza mambo mengi mno huku muda wote Mickey akizungumza kama bilionea mkubwa. Walichukua saa moja, walipomaliza, wakaelekea katika Bugatti ile, wakaingia na kuondoka mahali hapo.
Njiani, Fareed alipagawa mno, moyo wake ulijuta kutofahamiana na mwanaume huyo tangu kitambo kwani alikuwa mzuri wa sura na kubwa zaidi ni kwamba alikuwa na pesa kitu kilichokuwa ugonjwa wake mkubwa kama mtu aliyezaliwa benki.
Wakafika hotelini, Mickey hakutaka kuwa na haraka, aliamini kwamba huyo alikuwa wake hivyo alichokiifanya ni kumuacha huku akimpa dola elfu mbili na kuondoka zake pasipo kufanya kitu chochote kile.
Fareed alichanganyikiwa, alipoingia hotelini, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mwanaume huyo tu. Hakuamini kama kweli alikuwa amefanikiwa kuwa na mtu aliyekuwa na pesa, ambaye hakuwa mchoyo kama alivyokuwa Mickey.
Akaanza kuwa msumbufu, kila wakati alikuwa akimpigia simu mwanaume huyo na kumuuliza alikuwa akiendeleaje, alitaka kuonana naye na kumpa haki yake na si kutumia pesa zake tu.
“Tutaonana tu mpenzi kabla sijarudi Australia! Utakuwa na nafasi usiku wa leo nikufuate twende klabu?” aliuliza Mickey.
“Yeah! Tena nitakuwa mpweke sana. Naomba uje kunichukua mpenzi!” alisema Fareed.
“Sawa. Nitakuja!” alisema Mickey na kukata simu.
Usiku huohuo Mickey akafika hotelini hapo, hakutaka kuchelewa, akamchukua Fareed na kuondoka naye. Walizungumza kama wapenzi, aliongea kama mwanamke na hata mapozi aliyokuwa akiyafanya pale kitini alipokaa alikuwa kama mwanamke.
Saa 8:12 usiku Mickey akamrudisha Fareed hotelini na kisha kuondoka zake. Njiani, hata kabla hajafika katika hoteli aliyochukua chumba, akachukua simu yake na kupiga upande wa pili ambapo baada ya sekunde kadhaa, ikapokelewa.
“Umefikia wapi?” iliuliza sauti ya upande wa pili.
“Kila kitu kipo poa. Kama itawezekana basi kesho tumuue,” alisema Mickey.
“Haina shida. Waambie wenzako kesho mfanye hayo mauaji! Au subiri mpaka nije. Kesho jioni nitaingia, nitahakikisha namuua kwa mkono wangu,” alisema mwanaume upande wa pili na kisha kukata simu.
***
Keith hakutaka kubaki nchini Marekani, aliamini kwamba kwa namna moja au nyingine ilikuwa ni lazima Fareed afe kama alivyokuwa amepanga hivyo ilikuwa ni lazima aondoke na kuelekea Dubai.
Njiani, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mwanaume huyo, aliuumiza moyo wake vilivyo, alitumia kiasi kikubwa cha fedha kumlea lakini kama kunguru vile alishindwa kufugika kabisa.
Aliamua kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kumuua ili kuupa furaha moyo wake. Wakati mwingine aliiona ndege ikienda taratibu sana, alitamani hata kuiongezea kasi kwani ilikuwa ni lazima afike mapema, amuue Fareed na kurudi zake nchini MArekani.
Baada ya saa zaidi ya ishirini, ndege ikatua uwanja wa ndege ambapo moja kwa moja akaondoka na kuelekea hotelini. Akawasiliana na Mickey, kijana wake aliyempa kazi ya kufanya mauaji na kumwambia kwamba ilikuwa ni lazima waonane hotelini na vijana wenzake kwa ajili ya kupanga ni kwa namba gani wangeweza kufanya mauaji hayo.
Ndani ya dakika ishirini, vijana wote walikuwa hotelini humo. Akazungumza nao na kuwaambia mipango iliyokuwepo, wakajadili ni kifo cha namna gani mwanaume tata huyo alitakiwa kufa, wakakubaliana kwamba ilikuwa ni lazima abakwe, aingizwe kwenye boti, iende katikati ya bahari huku akiwa amefungwa miguu kwa jiwe kubwa kisha kufa hukohuko.
“Sawa. Wewe endelea kuwasiliana naye,” alisema Keith.
Hapo akawa na amani moyoni mwake, Mickey hakuwa na hofu alijua kwamba Fareed hawezi kutoka mikononi mwake hivyo ilikuwa ni lazima kufanya kama alichoambiwa.
Ili kumtia mshawasha Fareed, siku hiyo alizima simu siku nzima kitu kilichomnyima raha Fareed na kumpigia kila wakati lakini simu haikuweza kupatikana.
Ilipofika saa moja usiku na Fareed kupiga simu, ikawa inaita, mapigo yake ya moyo yakawa juu, hakuamini kama kweli simu hiyo ilikuwa hewani. Alikumbuka Mickey, hakujua kama mwanaume huyo alikuwa mtu mbaya aliyetaka kumuua baada ya kumbaka yeye na wenzake.
Kitendo cha Mickey kupokea simu, Fareed akaanza kuongea kwa sauti ya kulialia kwani alitaka abembelezwe sana, apozwe kama mwanamke aliyekuwa akihitaji faraja kutoka kwa mwanaume aliyekuwa akimpenda kwa dhati.
“Nisamehe mpenzi! Nilikuwa sehemu fulani hivi,” alisikika Mickey kwenye simu.
“Nimekukumbuka jamani! Mpaka nikataka nijiue kwa ajili yako,” alisema Fareed kwa sauti yake ya kuwapagawisha wanaume.
Wakazungumza mengi na mwisho wa siku wakakubaliana kwamba lingekuwa jambo jema kama wangekutaka katika Klabu ya Dubai Night kwa ajili ya kuburudika na kuzungumza mengi. Hiyo ilikuwa furaha kwa Fareed kwani kitu pekee alichokuwa akikitaka kwa kipindi hicho ni kuonana na mwanaume huyo tu.
“Nakuja bebi!”
“Sawa.”
10


Akakata simu. Akaelekea bafuni na kujiandaa. Siku hiyo alijiapiza kwamba ni lazima alale na Mickey kwani kama asingefanya hivyo basi kungekuwa na watu ambao wangemfuata na kulala naye kisha kumsahau yeye.
HAkutaka kuona hilo likitokea. Alichukua dakika kumi kuoga, akatoka bafuni na kisha kuanza kujipaka losheni na kujipulizia marashi yake ya Kizenji, alipomaliza, akavaa taiti iliyombana hasa iliyokuwa na rangi nyeusi, akakibusti kifua chake na kisha kupaka wanja sehemu nyusi zake alizokuwa amezinyoa na kumalizia na kujipata lipstiki mdomoni.
Alipojiangalia kwenye kioo, yeye mwenyewe akajitamani, siku hiyo alitoka chicha, alikuwa akivutia na aliamini kwa kila mwanaume ambaye angemuona, kusingekuwa hata na mtu mmoja ambaye angegundua kwamba alikuwa mwanaume kwani alikuwa na muionekano wa kike kwa asilimia mia moja.
Akatoka mpaka nje ya hoteli ambapo ndani ya dakika chache, Mickey akafika mahali hapo na kumchukua. Ndani ya gari kila mmoja alionekana kuwa na furaha tele. Ilikuwa vigumu kumgundua Mickey kwamba alikuwa na mpango mchafu kwani kwa jinsi alivyokuwa akitabasamu, ilionekana kabisa hakukuwa na tatizo lolote lile.
HAwakuchukua muda mrefu wakafika klabu ambapo wakateremka na kuelekea ndani. Humo, Fareed alionekana kama kuchanganyikiwa, alikuwa akicheza kila wimbo uliokuwa ukipigwa na kila alipotaka kunywa, alikwenda sehemu ya kununulia vinywaji na kunywa kwani alikuwa na mtu mwenye pesa.
Wakati hayo yote yakiendelea, vijana wa Keith walikuwa humo ndani, walikuwa wakifuatilia kila kitu, walimwangalia, wao wenyewe walihisi kwamba alikuwa mwanamke kwa jinsi alivyokuwa amejiremba na kuonekana mrembo kupita kawaida.
Muziki uliendelea mpaka iipofika saa tisa ambapo wakatoka huku Fareed akiwa amechoka kupita kawaida. Wakaingia ndani ya gari na kuondoka mahali hapo.
Wala hawakuchukua mwendo mrefu, Mickey akasimamisha gari pembezoni mwa barabara ambapo hakukuwa na mwanga mkali na kisha kuteremka, Fareed alishangaa, naye akateremka kwa kuhisi kulikuwa na kitu lakini hata kabla hajafanya kitu chochote kile, gari moja likasimama, wanaume wawili waliokuwa na miili mikubwa wakateremka, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumfuata, wakamkamata na kumziba mdomo kisha kumuingiza ndani ya gari lao na kuondoka.
Fareed aliogopa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendela, hakujua wale watu walikuwa wakina nani na kwa sababu gani walikuwa wamemteka kama walivyofanya.
Wakati akijiuliza hilo, mwanaume aliyekaa pembeni ya dereva akageukia kule nyuma na kumwangalia Fareed, walipogonganisha macho, akashtuka baada ya kugundua kwamba alikuwa Keith.
“Keith…” aliita Fareed.
“Yes my love!” (ndiyo mpenzi wangu) alisema Keith huku akitoa tabasamu.
“What are you doing?” (unafanya nini?)
“I just want to play a game! A nice one, it is Flecks of Blood,” (ninataka tucheze mchezo! Mchezo mzuri, unaitwa Michirizi ya Damu) alijibu Keith huku akiwa kwenye tabasamu pana.
Safari iliendelea, Fareed alikuwa na hofu kubwa moyoni mwake, alijua kabisa kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake, hakutegemea kuona mwanaume huyo akimfuatilia mpaka huko.
Akaanza kuomba msamaha kwa kuamini kwamba angesamehewa lakini hicho hakikuwa kipindi cha kusamehewa bali kilikuwa kipindi cha kuuawa kwa kile alichokuwa amekifanya.
Gari likaondoka na kuelekea katika ufukwe wa Kite, huko, tayari kulikuwa na boti waliyokuwa wameiandaa ambayo ingewapeleka mpaka mbali kabisa kwa ajili ya kumtosa baharini, na hawakutaka kabisa mwili wake uonekane, hivyo walikuwa na jiwe ndani ya boti ile kubwa.
Wakateremka na kuingia ndani ya boti na safari ya kuelekea katikati ya bahati kuanza. Njiani, kila mtu alikuwa akimwangalia Fareed kwa macho yaliyojaa tamaa, kwani kwa jinsi alivyokuwa, ilikuwa vigumu sana kumuacha hivihivi.
Hapo ndipo walipoanza kumbaka kama walivyokubaliana. Fareed alisikia maumivu makali, alikuwa akilia huku akitaka kuachwa lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa radhi kumuachia.
Aliendelea kubakwa mpaka akahisi mwili ukikosa nguvu, macho yake yakaanza kujaa giza, na hakujua ni kitu gani kiliendelea baada ya hapo.
“Tayari! Mfungeni jiwe,” aliagiza Keith, Fareed akafungwa jiwe kubwa na kisha kutupwa baharini. Akaanza kuzama huku akiwa amepoteza fahamu. Walichokifanya wanaue hao, kwa haraka sana wakaondoka mahali hapo huku kila mmoja akiwa na furaha kwani waliamini kwamba kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angeuona mwili wa Fareed.
****
Asteria alichanganyikiwa, hakujua mahali alipokuwa Fareed, alijaribu kumtafuta katika simu yake kwa kuona kwamba angempata na kuwasiliana naye kwa ajili ya biashara lakini mwanaume huyo hakupatikana.
Hakujua alikuwa wapi, aliangalia kwenye WhatsApp yake, ilionyesha kwamba mara ya mwisho kwa mwanaume huyo kuwa katika mtandao huo ilikuwa ni wiki moja iliyopita.
Hakujua ni kwa jinsi gani angempata, akajaribu kuwasiliana na Keith na kumuuliza kuhusu Fareed lakini bilionea huyo alimwambia kwamba yeye mwenyewe alikuwa akimtafuta kwani alimuaga kwamba anakwenda Dubai, baada ya hapo hakumuona tena.
Hakumwambia ukweli kwamba alimuua Fareed, alimficha kwa kuhisi kwamba siri hiyo ingedumu milele. Moyoni mwake hakuwa na huruma, kwa kile alichokifanya kwake kilionekana kuwa sahihi kwani kama kuumizwa moyo wake na mwanaume huyo, aliumizwa sana na hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya kumuua bila huruma.
Asteria hakutaka kukubali kuendelea kubaki nchini Tanzania, Fareed ndiye alikuwa biashara yake kubwa, japokuwa alikuwa na wanawake wengine waliokuwa wakijiuza lakini kwa mwanaume huyo ndiye alikuwa soko, aliyempa pesa na kuishi katika maisha ya raha kupita kawaida.
“Nakwenda Dubai!” alisema Asteria.
“Kufanya nini?”
“Kumtafuta Fareed.”
“Kwani bado hujampata?”
“Ndiyo! Wewe umempata?”
“Hapana!”
Alikuwa akizungumza na mmoja wa wasichana waliokuwa wakimfanyia kazi. SIku iliyofuata, hakutaka kubaki nchini Tanzania, akapanga safari na kupaa kuelekea Dubai kwa kuamini kwamba angeweza kumuona huko.
Moyo wake ukaanza kuingiwa na hofu, akahisi kwamba mwanaume huyo alikuwa amekufa na mwili wake kutupwa kwani kwa mtu kama Fareed, jinsi alivyokuwa akipenda mitandao ya kijamii lingekuwa suala gumu sana kukaa hata saa moja pasipo kuingia Facebook, WhatsApp, Beashare au mtandao mwingine wowote ule.
Alipofika Dubai, akaelekea hotelini. Siiku hiyo hakuwa sawa, alipanga kuonana na wanawake wengine ambao walikuwa chini yake, akaonana nao na kuzungumza nao pamoja na kuwauliza kuhusu Fareed lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa akifahamu mahali alipokuwa, kila mmoja alisema kwamba mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni kabla hajakwenda Ubelgiji, baada ya hapo hawakujua alikuwa wapi.
Alikaa Dubai kwa mwezi mzima, hakumuona Fareed na wala hakujua mahali alipokuwa. Akakata tamaa na kuona kwamba tayari mwanaume huyo alikuwa marehemu hivyo kitu pekee alichokuwa akikitaka ni kuiona maiti yake ili ajiridhishe tu.
“Hata nikiiona maiti yake nitashukuru Mungu! Yaani Fareed amekufa? Amekufaje? Mbona hata taarifa sikupewa?” alijiuliza huku akiwa amechanganyikiwa, hakujua kabisa mahali alipokuwa mtu huyo.
Alichokifanya ni kuwasiliana na marafiki zake wengine waliokuwa wakiishi nchini humo na kuwaambia kile kilichokuwa kikiendelea kwamba kulikuwa na ndugu yake ambaye hakujua mahali alipokuwa mpaka muda huo, hao ndiyo waliomshauri kwamba alitakiwa kutembelea katika hospitali mbalimbali kwa ajili ya kumtafuta kwani inawezekana alikuwa amekufa ila mwili wake ulihifadhiwa mochwari.
Hilo lilikuwa wazo zuri, alichokifanya siku iliyofuata ni kwenda katika hospitali mbalimbali lakini kote huko hakuweza kuukuta mwili wa Fareed kitu kilichomfanya kumalizia katika hospitali ya mwisho ya Sultan Idris Medical Center iliyokuwa pembezoni mwa Dubai ambapo haikuwa mbali kutoka baharini.
Alipofika huko akajitambulisha na kitu kilichomfanya kufika mahali hapo. Kwa jinsi alivyokuwa akijielezea, kila mmoja alimuonea huruma hivyo kumchukua na kuondoka naye kuelekea mochwari kwa ajili ya kuitambua maiti ya ndugu yake aliyokuwa akiitafuta.
“Ni tangu lini?” aliuliza daktari.
“Mwezi mmoja sasa umepita sijaweza kumuona.”
“Una uhakika kwamba alikuja Dubai?”
“Ndiyo! Mara ya mwisho kuwasiliana naye alikuja huku,” alijibu Asteria.
Hawakuchukua mwendo mrefu wakafika katika mochwari ya hospitali hiyo na hivyo kuingia ndani. Humo ndani kulikuwa na masanduku mengi ambayo ndani yake kulikuwa na maiti kadhaa huku kukiwa na baridi kali ambalo muda mwingi Asteria alikuwa akitetemeka tu. Wakaanza kuzunguka huku na kule, wakayafungua madroo makubwa na kuangalia ndani kama kulikuwa na maiti ya Fareed.
Walizunguka kwenye madroo mengi lakini hawakufanikiwa kuiona maiti ya Fareed kitendo kilichomfanya kuhisi kwamba mwanaume huyo hakuwa amekufa lakini wakati akijiandaa kutoka ndipo akaambiwa kwamba kulikuwa na sehemu nyingine ya madroo hawakuwa wameangalia hivyo wakaelekea huko.
Walipofika, yakafunguliwa na kuanza kuangalia maiti moja baada ya nyingine. Muda wote mapigo ya moyo wake yalikuwa juu, kila alipopiga hatua alikuwa akitetemeka mno.
Baada ya dakika kadhaa, wakafika katika droo moja kubwa, ndani yake kulikuwa na maiti ya mwanaume mmoja, ilikuwa imefunikwa, haraka sana msimamizi aliyekuwa ndani ya mochwari ile akaifungua maiti ile, macho ya Asteria yalipotua katika sura ya maiti ile, miguu yake ikamlegea, hakuamini kile alichokiona, akashindwa kuvumilia, hapohapo akaanza kulia kama mtoto.
***
Bilionea Keith alikuwa mwenye furaha tele, alichokuwa akikitaka alitekeleza, moyo wake ulikuwa na faraja kubwa, alijona shujaa kwani kitendo cha kuchunwa pesa zake na mtu ambaye baadaye alikuja kumsaliti, kwake ilionekana kuwa dhambi kubwa.
Alikunywa na kuyafurahia maisha yake, kila alipokaa baa na kunywa pombe, akili yake ilikuwa kwa Fareed ambaye alimchukia kupita kawaida. Moyo wake haukujuta hata mara moja, alijipongeza kwa kazi kubwa aliyokuwa ameifanya.
“Mungu mlaze mahali pema peponi,” alisema Keith huku akiinua glasi ya pombe yake juu.
Wiki ya kwanza ikakatika, ya pili ikaingia, hakuacha tabia yake ya kuchukua wanawake. Alikuwa akipenda wanawake kama alivyokuwa akipenda kula. Alikuwa na familia yake, aliipa kila kitu lakini kamwe hakuacha tabia yake ya kulala nje. Alijua kwamba mkewe aliumia sana lakini hakutaka kujali, kwake, kulala na wanawake wengi ndiyo yalikuwa maisha yake.
Akili yake ni kama ilikuwa imevurugwa, wanawake walimpagawisha kupita kawaida. Akili ikaathirika kwa wanawake, hakuwa akifanya kitu chochote pasipo kufikiria ngono.
Alitembea nchi nyingi, huko alilala na wanawake wengi, alitembea nao pasipo kuhofia kitu chochote kile. Wakati akiwa katika harusi ya rafiki yake iliyokuwa ikifanyika nchini Malaysia, ndipo akakutana na msichana mrembo, mwenye sura yenye mvuto, msichana huyo mweusi aliyekuwa raia wa Nigeria akatokea kumpagawisha kupita kawaida.
Hakutaka kuchelewa, moyo wake ulichanganyikiwa, kwa jinsi alivyomwangalia mwanamke yule, alisikia damu yake ikizunguka kwa kasi kubwa katika mishipa yake.
Hakutaka kuchelewa, kwa haraka sana akamsogelea, alipomfikia, akamsalimia, msichana huyo alipoitikia, sauti yake ikamuingia mpaka moyoni mwake, ikaivuruga akili yake, tabasamu lake likamburuza vilivyo.
“You look very beautiful,” (unaonekana mrembo sana aiseee) alisema Keith huku akiachia tabasamu pana.
“You too my babyto…” (wewe pia mpenzi wangu) alijibu msichana huyo huku akitoa tabasamu pana, Keith alipoangalia meno, akagundua kwamba msichana huyo alikuwa na mwanya mdogo, huo ndiyo ulikuwa ugonjwa wake mkubwa.
“My name is Keith from Los Angeles…” (naitwa Keith kutoka Los Angeles…) alijitambulisha harakaharaka huku akimpa mkono.
“Maria Ogabugu from Lagos…” (Maria Ogabugu kutoka Lagos…) alijibu msichana huyo huku akimpa mkono. Walipogusana tu, Keith akahisi kama akipigwa na shoti ya umeme. Kwa kifupi, kwa Maria, alikufa na kuoza, hakutaka kuambiwa chochote kile.
“I like Africa…” (naipenda sana Afrika) alisema huku akiachia tabasamu pana.
****
Ulikuwa ni msimu wa joto kali Mjini Dubai, katika kipindi hicho watu wengi waliokuwa wakiishi huko waliondoka na kuelekea katika nchi nyingine kutokana na hali hiyo kuwatesa sana.
Nyuzi joto ambayo kila siku iliwaonyesha kwamba ni nyuzijoto 34 ilibadilika mpaka kufika nyuzijoto 42. Hali ilitisha na hata wale waliokuwa ndani ya nyumba zao, muda wote ni viyoyozi tu ndiyo vilivyokuwa vikiwapuliza.
Katika kipindi hichohicho cha joto kali ndicho kipindi ambacho hakukuwa na mwezi angani, baharini kulikuwa na giza, hata wale wavuvi ambao walikuwa wakiondoka kwenda kuvua, hawakwenda mbali, kwa kutumia taa zao, samaki walifuata mwanga na kuwavua kirahisi zaidi.
Katika kipindi hichohicho cha joto kali na giza kubwa baharini ndicho kilikuwa kipindi ambacho mvuvi maarufu wa samaki, mzee Ahmedi El Saadat aliuchukua mtumbwi wake na kwenda baharini kwa ajili ya kuvua samaki kama alivyokuwa akifanya siku nyingine.
Alipofika mbali, akashusha nyavu zake na kuanza kusubiri samaki. Alikaa mahali hapo, siku hiyo kulikuwa na giza kubwa, siku hiyo ilionekana kuwa ya tofauti kwake kwani alikuwa na hofu moyoni mwake mpaka wakati mwingine akahisi kwamba kungekuwa na tatizo lingetokea mahali hapo.
Alikaa kwa nusu saa, ghafla akaanza kuisikia boti kubwa ikienda kule alipokuwa. Alishtuka, alihisi wale walikuwa watu wabaya ambao walitaka kumfanyia kitu kibaya mule baharini, boti ile ya kifahari ilikwenda na kusimama mbali kabisa ambapo ghafla akawaona watu wakitoka huku wakiwa na mtu mwingine aliyekuwa akilia kuomba msamaha.
Aliogopa, akajua kwamba hao hawakuwa watu wazuri hata kidogo, alibaki akiwaangalia, hakujua walitaka kufanya nini, kwa jinsi mtu yule alivyokuwa akilia, aligundua kwamba lengo kubwa lililowafanya kufika mahali hapo lilikuwa ni kumuua tu.
Huku akiwa haamini macho yake, watu wale wakaanza kumbaka mtu waliyekuja naye, aliumia moyoni mwake, moyo wake ukajawa na hasira, alitamani sana kuwafuata na kupambana nao, alijua ni kwa jinsi gani Mungu aliyekuwa akimwabudu alikataza vitu kama hivyo, alisaga meno lakini akajificha zaidi kwani alijua kwamba kama angefanya chochote na kuonekana, basi angeuawa kama kupoteza ushahidi.
Kitendo cha kumbaka Fareed kilichukua dakika nyingi mpaka alipozimia ambapo wakamchukua, wakamfunga kamba ngumu iliyokuwa na jiwe kisha kumtupa baharini na kuondoka mahali hapo.
Alisubiri mpaka wafike mbali ndipo akajitosa baharini. Hakutaka kuona mtu huyo akifa mbele ya macho yake, moyoni mwake alijisikia hukumu nzito hivyo ilikuwa ni lazima amsaidie kwa nguvu zote kumuokoa kwenye kifo kilichokuwa kikimsubiri.
Akazama kwenye maji huku akiwa na kisu chake alichokuwa akikitumia kuparuria samaki. Alipofika chini na kumulika kwa tochi yake, akafanikiwa kumuona Fareed akiwa chini kabisa, amenasa kwenye tope huku akiwa hajitambui kabisa.
Akamfuata mpaka pale alipokuwa na kuanza kuikata kamba ile ambayo wala haikumletea ubishi sana, ikakatika na kisha kumchukua na kuanza kwenda naye juu.
Alifanikiwa, alipofika kwenye boti yake ndogo, akamchukua na kumuweka kisha kuanza kumtoa maji yaliyoingia mwili mwake. Hilo lilionekana kumsaidia, alipomaliza, akawasha boti na kuondoka, hata kuendelea kuvua samaki mahali pale, hakutamani tena.
Alipofika ufukweni, akalifuata gari lake ambalo kila siku alikuwa akija nalo na kulipaki sehemu, akamuingiza Fareed na kuondoka mahali hapo huku akiwa anapiga dua kimoyomoyo kama kumtaka Mungu amponye mtu aliyekuwa naye, hakumfahamu ila moyo wa huruma ulimuingia na kuamua kumsaidia kwa moyo mmoja.
Alipofika nyumbani akamuingiza ndani na kumlaza kitandani. Kichwa chake kilikuwa na mawazo tele, alikuwa akijiuliza kuhusu Fareed, alikuwa msichana au mvulana.
Alikuwa na muonekano wa kike, ila alipoiangalia vizuri mikono yake, akagundua kwamba alikuwa mwanaume, sasa mwanaume gani aliyekuwa na muonekano huo?
Alijazia kwa nyuma, alikuwa na kifua kikubwa, matiti yaliyosimama, kwa kifupi alichanganyikiwa na hakujua kuhusu mtu huyo, kwake, alikuwa na maswali mengi yasiyokuwa na majibu yake.
Hiyo ilikuwa siku ya kwanza, akamvua nguo na kumwangalia sehemu za siri, yeye mwenyewe alichanganyikiwa, alikuwa na muonekano wa msichana mrembo lakini kumbe sehemu zake za siri zilikuwa ni za mwanaume.
“Huyu ni nani?” alijiuliza.
Mkewe akaingia chumbani humo, akamfuata mumewe na kumuuliza kuhusu mtu huyo. Hakumficha, alimwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea, jinsi alivyowaona watu wabaya wakimtupa baharini kwa lengo la kumuua, lakini kwa kuwa aliwaona, akaenda kumuokoa akiwa amezamishwa ndani ya maji.
“Alhamdulilah!” alisema mkewe huku akiangalia juu na kuinua mikono yake kama ishara ya kumshukuru Mungu.
Hapo ndipo alipoanza kupata matibabu, katika kipindi chote hicho, mke wa mzee aliyekuwa Ahmedi hakuwa akijua kama mtu aliyepelekwa nyumbani kwake na mumewe alikuwa mwanaume, alikuwa na muonekano wa asilimia mia moja wa kike.
Aliharibika vibaya kwa nyuma, mzee Ahmedi aliligundua hilo lakini hakutaka kumwambia mke wake, alikuwa kimya huku wakati ambao mwanamke huyo hakuwepo nyumbani, alichukua nafasi hiyo kumtibu nyuma kulipoharibika vibaya.
Waliendelea kumuhudumia nyumbani hapo mpaka siku mbili baadaye aliporudiwa na fahamu. Kitu cha kwanza kabisa baada ya kufumbua macho ni kuanza kuangalia huku na kule, alishangaa mahali alipokuwa, hakukumbuka chochote mpaka alipotulia kwa dakika kadhaa na kukumbuka kile kilichokuwa kimetokea kabla ya kuwa mahali hapo.
Moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama kweli Keith alimfanya hivyo, moyo wake uliumia, alitakiwa kuuawa lakini aliokolewa na mwanaume huyo mvuvi ambaye alimwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea.
Fareed hakutaka kuondoka nyumbani hapo, alitulia, wiki moja baadaye alipojisikia afadhali, akaaga na kuondoka zake kurudi nchini Tanzania. Moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, kifua chake kikajaa kisasi, hakukuwa na kitu kilichomuumiza kama kubakwa na vijana wa Keith ambaye hakuridhika na kutaka kumuua.
Alipofika nchini Tanzania, ndani ya Jiji la Dar es Salaam, akaelekea nyumbani kwake ambapo huko akampigia simu Asteria, baada ya kusikia sauti ya Fareed hakuamini, akamwambia kwamba angekwenda nyumbani hapo kuzungumza naye, alitaka kujua ni kitu gani kilitokea.
Ndani ya dakika thelathini tu mwanamke huyo alikuwa ndani ya nyumba hiyo, alimkumbatia Fareed, hakuamini kama mwanaume huyo alikuwa hai, alijua kwamba alikufa.
“Nilikufuata mpaka Dubai,” alisema Asteria.
“Ikawaje?”
“Nilikwenda hospitali na kuonyeshewa miili mingi. Niliiona maiti ya Ashura ndani ya kabati kubwa mochwari,” alisema Asteria maneno yaliyomshtua Fareed.
“Ashura?”
“Ndiyo! Nilishtuka sana, sikuamini macho yangu. Fareed, iliniuma sana. Hebu niambie na kwako ni kitu gani kilitokea?” aliuliza Asteria huku akimwangalia Fareed.
“Ni mambo makubwa yaliyonitokea. Hakika nitamchukia Keith maisha yangu yote,” alisema Fareed huku akimwangalia Asteria.
“Kuna nini tena?”
ITAENDELEA KESHO HAPA HAPA....KUMBUKA KUSHARE NA MARAFIKI ZAKO

No comments

Powered by Blogger.