ad

ad

Isabela Ajazwa ‘Kitumbo Ndii’

MSANII wa filamu na muziki Bongo, Isabela Mpanda amejazwa kitumbo ndii na sasa amekuwa akijificha ili watu wasiuone ujauzito wake huo. 

Isabela ambaye aliwahi kuapa kwamba hayupo tayari kuzaa nje ya ndoa tena, kwani tayari ana watoto wawili, chanzo kinaeleza ujauzito wake wa sasa unakadiriwa kuwa na umri wa miezi sita huku aliyempa ujauzito huo akimficha.


“Isabela ana mimba kubwa tu na amekuwa akijificha na mara nyingi akiwa anatoka anavaa nguo kubwa ambazo zinaficha tumbo sijui anaona aibu kwa vile aliapa kwamba hatazaa tena nje ya ndoa au vipi? Ngoja niwatumie picha zake mumuone,” kilisema chanzo hicho.


Alipotafutwa Isabela alisema; “Hayo ni mambo yangu binafsi sitaki kuyazungumzia sana, nyie subirini mumuone mtoto, kuhusu kusema kwamba sitazaa nje ya ndoa tena ni maneno tu na ndiyo tunatakiwa tuwe na akiba ya maneno.”

No comments

Powered by Blogger.