Askari JWTZ Walionusurika Shambulio la DRC Wanaendelea Vizuri – Pichaz
KUFUATIA wanajeshi 14 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ),
waliouawa katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wakati
wakilinda amani kushambuliwa na waasi kuuawa huku wengine 44
wakijeruhiwa na mmoja wao kutojulikana alipo, picha za majeruhi wa tukio
hilo zinaoshesha wanaendelea vizuri.
Kiongozi wa Mkuu wa Walinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa Duniani,
Jean-Pierre Lacroix amewatembelea ma kuwasalimia Askari Majeruhi wa JWTZ wanaopatiwa matibabu nchini Congo na Uganda baada ya shambulio hilo.
Miili ya wanajeshi waliouawa kwenye shambulio hilo iliagwa juzi Desemba, 14 mwaka huu katika Viwanja vya ulinzi vilivyopo makao ya jeshi yaliyopo Upanga jijini Dar es Salaam.
Wanajeshi waliouawa ni Hamad Haji Bakari, Chazil Khatibu Nandonde, Idd Abdallah Ally, Juma Mossi Ally, Ally Haji Ussi, Pascal Singo, Samwel Chenga, Deogratius Kamili, Mwichumu Vuai Mohamed, Hassan Makame, Issa Mussa Juma, Hamad Mzee Kamna, Salehe Mahembano na Nazoro Haji Bakari.
Askari hao 14 walifariki dunia katika mapigano na waasi wa kikundi cha ADF nchini DRC, huku 44 wakijeruhiwa na mmoja akipotea baada ya kambi yao kuvamiwa eneo la Mashariki mwa nchi Desemba 7 wakati wakitekeleza majukumu ya ulinzi wa amani.
Miili ya wanajeshi waliouawa kwenye shambulio hilo iliagwa juzi Desemba, 14 mwaka huu katika Viwanja vya ulinzi vilivyopo makao ya jeshi yaliyopo Upanga jijini Dar es Salaam.
Wanajeshi waliouawa ni Hamad Haji Bakari, Chazil Khatibu Nandonde, Idd Abdallah Ally, Juma Mossi Ally, Ally Haji Ussi, Pascal Singo, Samwel Chenga, Deogratius Kamili, Mwichumu Vuai Mohamed, Hassan Makame, Issa Mussa Juma, Hamad Mzee Kamna, Salehe Mahembano na Nazoro Haji Bakari.
Askari hao 14 walifariki dunia katika mapigano na waasi wa kikundi cha ADF nchini DRC, huku 44 wakijeruhiwa na mmoja akipotea baada ya kambi yao kuvamiwa eneo la Mashariki mwa nchi Desemba 7 wakati wakitekeleza majukumu ya ulinzi wa amani.
Post a Comment