Mkurugenzi wa Shirika la Ndege ATCL Ahukumiwa Jela
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemhukumu aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mataka na mwenzake Elisaph Mathew, aliyekuwa Kaimu Ofisa Mkuu Kitengo cha Fedha cha ATCL kwenda jela miaka sita kila mmoja au kulipa faini ya jumla ya Sh. Milioni 70 (Milioni 35 kila mmoja).
Mbali na adhabu hiyo, mahakama pia imewaamuru watuhumiwa hao kulipa hasara waliyoisababishia ATCL katika ununuzi wa magari chakavu 26 ambayo ni dola za Marekani 143,442.75 sawa na Sh. Milioni 322.
Aidha mahakama hiyo imemuachia huru William Haji ambaye aliyekuwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Ndani za ATCL.

Post a Comment