ad

ad

Waziri Lukuvi Azindua Mji Wa Kisasa Arusha

Na Nahmoud Ahmad Arusha
Waziri wa ardhi , nyumba na maendeleo ya makazi William Lukuvi amewaagiza viongozi wa halmashauri na majiji nchini kuharakisha utoaji wa vibali vya ujenzi na kuachana na urasimu unaosababisha kuwepo kwa ujenzi holela .

Lukuvi aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza katika uzinduzi wa nyumba  kumi za  mfano za mradi wa mji wa kisasa wa  Safari City  zilizopo Mateves sambamba  na kutoa hati miliki kwa wanunuzi 100 wa kwanza wa viwanja zinazotekelezwa na shirika la nyumba la taifa (NHC) .

Alisema kuwa kumekuwepo na ucheleweshaji mkubwa wa vibali vya ujenzi unaosababishwa na wahusika wenyewe na hivyo kupelekea wananchi hao kujenga kiholela kutokana na wananchi hao kuchoka kusubiri.

Aidha kufuatia hali hiyo alimwagiza mkuu wa mkoa wa arusha Mrisho Gambo kufanya ukaguzi wa mafaili ya vibali vya ujenzi na kuweza kugundua idadi ya watu ambao hawajapatiwa vibali vyao mpaka sasa hivi.

“Unajua idadi kubwa ya wananchi wanaojenga kiholela sio kwamba wamevunja sheria bali wanafanya hivyo kwa ajili ya ucheleweshaji wa vibali kwa hiyo hatua hiyo inasababisha pia kuchelewa kutoana na kusubiri kwa muda mrefu bila kupata jibu lolote”aliongeza Lukuvi.

Awali mkurugenzi mkuu wa shirika la nyumba la taifa Nehemia Mchechu alisema kuwa mradi huo wa kitovu cha mji wa kisasa wa safari city jijini hapa una ukubwa wa hekari 559.4 na ni sehemu ya miji iliyopangiliwa kitaalamu na kwa kuzingatia sheria za mipango miji.

“Mradi huu ulibuniwa na shirika la nyumba kwa lengo la kupunguza uhaba wa makazi kwenye jiji hili ambapo tumetenga maeneo kwa ajili ya waendelezaji kujenga sehemu za biashara,burudani ,utalii,hospitali, elimu,huduma za kijamii kama vile polisi,na zimamoto lakini pia yapo maeneo ya wazi kwa ajili ya michezo na mapumziko”alisema Msechu.

Aidha Mchechu aliziomba taasisi kuunga mkono maagizo aliyoyatoa raisi kwa halmashauri na taasisi zinazohusika kuhakikisha kuwa zinaweka miundombinu  yote muhimu katika maeneo yanayohitajika kuendelezwa na NHC ili kuweza kupunguza gharama za nyumba zinazojengwa
Powered by Blogger.