ad

ad

Malaika ashtua Mashabiki kwa picha zake Mbili za ngono



MSANII wa muziki anayefanya poa Bongo na Mamtoni, Diana Exavery ‘Malaika’ hivi karibuni aliwashtua mashabiki wake baada ya kupiga picha mbili za kingono, kitu ambacho hawakukitarajia kutoka kwake. 

Picha hizo ambazo ni kinyume na maadili ya Kitanzania zinamuonesha binti huyo aliyejaaliwa kuwa ni figa matata akiwa ameacha wazi sehemu ya kufua chake baada ya kuvaa nguo ambayo ni kama hakuwa amevaa kitu. Awali, staa huyo alitupia picha moja mtandaoni ikiwa imeacha wazi eneo lake hilo nyeti lakini inadaiwa baada ya watu wake wa karibu wanaojiheshimu kuiona, walimjia juu na hivyo kuamua kuiondoa haraka. 

Lakini wakati akiiondoa mtandaoni picha hiyo, Ijumaa lilifanikiwa kuinasa picha nyingine ambayo ‘hata kwa dawa’ gazeti hili lisingethubutu kuitumia bila kuiziba (angalia iliyopo ukurasa wa mbele). Baada ya picha hizo kuvuja, mwandishi wetu alifanya jitihada za kumtafuta Malaika kupitia simu yake ya mkononi ili azitolee ufafanuzi picha hizo lakini hakuweza kupatikana mara moja. 

Mbali na picha hizo, Malaika ambaye hivi karibuni alikuwa akifanya shughuli zake za kimuziki nchini Marekani aliwahi kupiga picha akiwa amevaa nguo ya ndani na kuacha wazi sehemu kubwa ya makalio yake, mazingira yaliyomfanya ‘ale za chembe’ na akidaiwa kuwa anatumia fursa hiyo kutafuta kiki.

No comments

Powered by Blogger.