Kepteni Maxwell Mahama wa Jeshi la Ulinzi la Ghana enzi za uhai wake.
KEPTENI
Maxwell Mahama wa Jeshi la Ulinzi la Ghana, Jumatatu iliyiopita aliuawa
na wananchi wa eneo la Denkyira-Obuasi kwa kupigwa mawe na kuchomwa
moto asubuhi wakati akifanya mazoezi ya kukimbia. Inasemekana wananchi hao walimwua askari huyo wakidhani ni jambazi kwa kuwa alikuwa na bastola.
Mwili wa Askari huyo ukitolewa kwenye gari.
Waziri
wa Ulinzi nchini humo, Dominic Nitiwul, alisema serikali inafanya
uchunguzi wa mauaji hayo yanakanganya hususan kwa vile marehemu alikuwa
na silaha.
Nitiwul alisema kwamba iwapo watu wengepiga kelele za “mwizi” ni dhahiri angewashambulia kwa risasi kwani angejua atauawa.
“Lakini inaonekana aliuawa kimyakimya bila kupigiwa kelele za mwizi. Au walimvamia bila ya yeye kujua,” alisema waziri huyo.
Waziri wa Ulinzi nchini humo, Dominic Nitiwul.
Waziri
huyo ameongeza kwamba jeshi limepeleka maofisa 35 wa kuungana na kundi
la upelelezi. Hata hivyo, polisi, wanasema wanashindwa kufanya upelelezi
kutokana na kusakamwa na wanajeshi waliojaa huko.
Post a Comment