ad

ad

Ibaada ya Kuaga Mwili wa Mume wa Zari, Ivan Ssemwaga

Mwili wa Ivan ukiwasili kanisani hapo kwa ajili ya kuaga
MWILI wa aliyekuwa mume wa Zarina Hassan, Ivan Semwanga ambao ulifika Kampala jana kutoka Afrika Kusini, leo umepelekwa katika Kanisa la Mtakatifu Paul la Namirembe jijini Kampala kwa ajili ya kupewa heshima za mwisho kwa ndugu na marafiki.
Mwili wa marehemu ukiingizwa kanisani
Watu mbalimbali maarufu walikuwepo kanisani hapo kwa ajili ya ibada maalum, miongoni mwao akiwemo mfanyabiashara Godfrey Kirumira, Aidah Nantaba, na Waziri wa Nchi wa Habari na Teknolojia ya Mawasiliano.

Semwanga aliyeacha watoto watatu atazikwa kesho Jumanne nyumbani kwao wilaya ya Kayunga.
Zari akifunua jeneza lenye mwili wa marehemu mumewe
Semwanga alifariki katika Hospitali ya Biko Academy iliyoko jijini Pretoria nchini Afrika Kusini alipokuwa akitibiwa matatizo ya moyo.

No comments

Powered by Blogger.