Matokeo Ya Marekani Live: Donald Trump 244, Clinton 209
Trump ashinda jimbo la Montana
Mgombea
wa Republican Donald Trump ameshinda jimbo la Montana. Jimbo hilo lina
kura 3 za wajumbe. Clinton sasa ana jumla ya kura 104 za wajumbe na
Trump 140.
Trump 'ana nafasi nzuri' - New York Times
Gazeti
la New York Times, ambalo limekuwa likiunga mkono Hillary Clinton,
linasema mfumo wake wa kompyuta kwa sasa unabashiri uwezekano wa Trump
kushinda kuwa 53%.
Louisiana kwenda kwa Trump
ABC News wanakadiria kwamba Donald Trump atashinda jimbo la Louisiana.
Jimbo hilo limepigia kura mgombea wa Republican katika chaguzi nne mtawalia lakini waliunga mkono Bill Clinton mwaka 1992 na 1996.
Jimbo hilo huwa halichukuliwi kama ngome ya Republican kama yalivyo majimbo mengine jirani.Jimbo hilo lina kura nane za wajumbe.
Jimbo hilo limepigia kura mgombea wa Republican katika chaguzi nne mtawalia lakini waliunga mkono Bill Clinton mwaka 1992 na 1996.
Jimbo hilo huwa halichukuliwi kama ngome ya Republican kama yalivyo majimbo mengine jirani.Jimbo hilo lina kura nane za wajumbe.
Clinton mshindi Connecticut, kwa mujibu wa ABC
Hillary
Clinton ameshinda jimbo la Connecticut, ngome ya chama cha Democratic
ambapo amejishindia kura saba za wajumbe, kwa mujibu wa ABC News.
Clinton sasa ana kura za wajumbe 104 na Trump 129.
Trump mshindi jimbo la Arkansas
Trump anakadiriwa kushinda jimbo la Arkansas kwa mujibu wa ABC News. Jimbo hilo lina kura sita za wajumbe.
Kwa kura za wajumbe, sasa Trump ana 129 na Clinton 97
Kwa kura za wajumbe, sasa Trump ana 129 na Clinton 97

Post a Comment