Mastaa walioingia kwenye mapenzi na kufikia hatua ya kufunga ndoa na mashabiki wao
Kanye West na Kim Kardashian.
Kanye Omar West,rapper,producer na fashion designer alikua shabiki mkubwa wa mwanamitindo Kim Kardashian kabla ya kuwa nae kwenye mahusiano hasa ukizingatiwa kuwa rapper huyu ni mbunifu wa mitindo hivyo inadaiwa Kim Kardashian alikua chaguo la Yeezy ambae wakati anafanya mipango ya kumnasa Kim mwanzoni mwa mwaka 2013,tayari Kanye alikua mpweke kwani alikua ametengana na aliekua mpenzi wake Amber Rose hivyo ikawa rahisi kumnasa mrembo huyo kutoka kwenye familia ya Kardashian girls ambapo walifunga ndoa rasmi mwaka 2014 na wamefanikiwa kupata watoto wawili,binti pekee Nort West na Saint West.
Mariah Carey na Nick Cannon.
Muigizaji,rapper,mchekeshaji,Radio & Tv Host Nick Cannon alikua shabiki mkubwa wa mwanamuziki Mariah Carey kabla ya wawili hao kujikuta kwenye mahaba mazito.Mara kadhaa Nick Cannon alijikuta akionyesha hisia zake pale alipokua akizungumzia nyimbo za mrembo huyo au akimtazama akiperfom ambapo alifunga nae ndoa April 30 mwaka 2008 na kufanikiwa na kuzaa nae watoto wawili ambao ni binti Monroe Cannon na Moroccan Scott Cannon.
Wiz Khalifa na Amber Rose.
Mwanamuziki na modal Amber Levonchuck maarufu kama Amber Rose alikua shabiki kubwa wa rapper Wiz Khalifa kabla ya wawili hao kuamua kufunga ndoa mnamo mwaka 2013.Hata hivyo ni kama wawili hao walijikuta kwenye mapenzi bila kujuna kwa undani tabia zao kwani licha ya wawili kufanikiwa kuzaa mtoto pekee wa kiume Sebastian Taylor Thomas walitengana rasmi mwaka 2014.
Katie Holmes na Tom Cruise.
Kwa wale wapenzi wa filamu nadhani watakumbuka vituko vya mwigizaji nguli Tom Cruise kwenye filamu inayofahamika kama “Mission Impossible”,hali iliyopelekea warembo wengi kutamani kuwa kwenye mahusiano na staa huyu wa Hollywood akiwemo muigizaji Katie Holmes ambae kwa wakati huo alikua shabiki mkubwa wa Cruise ambapo licha ya kufanikiwa kuonja penzi la Tom Cruise hadi kufikia hatua ya kufunga nae ndoa November 18,2006 na kuzaa nae binti pekee Suri Cruise,hatimae walitengana na kupeana talaka rasmi mwaka 2012.
Mchekeshaji,muigizaji na mtangazaji wa redio Russell Edward Brand,ambae ni raia wa Uingereza alikua shabiki mkubwa wa mwanamuziki Katy Perry ambapo alifanya kila aliloweza kuhakikisha anamtia mrembo huyo kwenye himaya yake ambapo mpango wake ulifanikiwa na wawili hao wakafunga ndoa mwaka 2010 ila mahusiano yao hayakudumu kwa muda mrefu kwani walipena talaka mwaka 2012 huku walitupiana vijembe ambapo Kety Perry alimtuhumu Russell kuwa msaliti kwa kuchepuka na warembo wengine.

Post a Comment