Lulu Diva: Namuogopa Baraka Kama Ukoma
Lulu Abassi ‘Lulu Diva.
Akizungumza na Wikienda, Lulu Diva
alisema kuwa Baraka alimpelekea Nay umbeya na kumtangazia ubaya kwa
sababu waliwahi kuingia kwenye uhusiano lakini yeye aliamua kuachana
naye kwa sababu aliona hawatafika mbali.
“Baada ya kuachana na Baraka, alianza
kunitangazia ubaya kwa Nay kuwa sifai, kisa kikiwa ni kumpiga chini
hivyo namuogopa kama ukoma,” alisema Lulu Diva.
Baraka alipotafutwa alimkana Lulu Diva kuwa hajawahi kuwa naye na wala hapendi kumzungumzia.
Chanzo: GPL
Post a Comment