Taifa Stars kujipima na Harambee Stars
TIMU ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars imepanga kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Kenya, Harambee Stars Mei 29, mwaka huu jijini Nairobi.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Kenya (FKF) zimekubaliana kuwepo kwa mchezo huo wa kirafiki, utakotumika kama sehemu za maandalizi kwa timu zote.
Kikosi cha Taifa Stars kinachonolewa na Kocha Mkuu, Charles Mkwasa kinatarajiwa kuingia kambini mwezi ujao, mara baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu Bara ili kujiandaa na mchezo huo wa kirafiki kabla ya kuwakabili Misri.
Stars pia itacheza na Nigeria Septemba mwaka huu wakati Kenya inajiandaa na mechi dhidi ya Congo kati ya Juni 3 hadi 5, mwaka huu mchezo wa Kundi E la kufuzu michuano hiyo.
mwisho

Post a Comment