ad

ad

YANGA YAIFUATA SIMBA FA CUP

Simon Msuva wakishangilia na Paul Nonga moja ya magoli ya leo dhidi ya Friends Rangers
Yanga imefanikiwa kutinga raundi ya 16 bora ya michuano ya Azam Sports Federation Cup kufuatia ushindi wa goli 3-0 dhidi ya Friends Rangers inayoshiiki ligi daraja kwanza. Mchezo huo umechezwa leo January 24 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
Niyonzima leo alikuwa sehemu ya kikosi cha Yanga kilichocheza dhidi ya Rangers mchezo wa FC Cup
Niyonzima leo alikuwa sehemu ya kikosi cha Yanga kilichocheza dhidi ya Rangers mchezo wa FC Cup
Simon Msuva amefunga magoli mawili kwenye mchezo huo. Goli la kwanza amelifunga dakika ya sita akiunganisha kwa kichwa krosi ya Issoufour Bubacar kabla ya kuzama tena wavuni kupachika bao la pili kwa shuti kali dakika ya 24 akiitendea haki pasi ya Paul Nonga ambaye leo amepoteza nafasi lukuki za kufunga kwenye game hiyo.
Paul Nonga leo ameshindwa kupachika mabao kutokana na nafasi alizopata
Paul Nonga leo ameshindwa kupachika mabao kutokana na nafasi alizopata
Matheo Anthony alikamilisha ushindi wa Yanga kwa kufunga bao la tatu dakika ya 51 baada ya kuiweka kambani krosi ya Salum Telela.
Rangers 3
Friends Rangers walijitahidi kucheza vizuri lakini walizidiwa mbinu na uzoefu na wachezaji wa Yanga kwenye mchezo wa leo. Rangers walitengeneza nafasi kadhaa lakini safu ya ushambuliaji iliyokuwa ikiongozwa na Good Hamis akishirikiana na Eleciter Mpepo haikufua dafu mbele ya ukuta wa Yanga uliotengenezwa na Vicent Bossou pamoja na Pato Ngonyani.

Yanga wanaungana na Simba, Toto Africans, Ndanda FC, ambao walishinda kwenye mechi zao za jana wakati Friends Rangers wao wameaga rasmi mashindano hayo kwa msimu huu.

No comments

Powered by Blogger.