ad

ad

Ofisi ya Kamishna Mkuu TRA Yavunjwa, Kompyuta Mbili Zaibiwa


Watu wasiojulikana  wamevamia  na  kuvunja  ofisi  ya  kamishna Mkuu wa Mamlaka  ya  Mapato  Tanzania (TRA) na kuiba kompyuta  na  vifaa vingine.

Habari tulizozipata ambazo zimethibitishwa  na Polisi kanda maalumu  ya  Dar  es  Salaam zinasema miongoni mwa kompyuta zilizoibiwa  ni  ile  iliyokuwa  inatumiwa  na  Dr Philip Mpango  alipokaimu nafasi ya  Kamishna mkuu wa TRA  kabla ya kuteuliwa  kuwa  Waziri  wa  Fedha

Kwa mujibu wa chanzo hicho,huenda kompyuta hiyo ikawa na taarifa muhimu kuhusu ukwepaji wa kodi  na  sakata  la  makontena  Bandarini.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu  Ya Dar es salaam,Simon Sirro amesema tayari jeshi hilo  linawashikilia  watu  wanne  kwa  uchunguzi  zaidi

Siro  alitaja  vitu  vilivyoibwa  katika  ofisi  hiyo  kuwa  ni  Kompyuta  mbili, Televisheni  moja  na  King'amuzi.

Alisema  wanaoshikiliwa  ni  walinzi  wawili  kutoka  kampuni  ya  Suma JKT ambao  walikuwa  zamu  usiku huo, Katibu Muhtasi  pamoja  na  Karani  wa  Ofisi  hiyo.

Hata  hivyo, Mkurugenzi  wa  Elimu kwa Mlipa  Kodi TRA, amekanusha  kutokea  kwa  tukio  hilo  akisisitiza  lilikuwa  ni  jaribio  la  wezi  kutaka  kuvunja  ofisi  hiyo.

Kayombo  alisema  hakuna  wizi  wowote  uliotokea  katika  jaribio hilo  kwa  sababu  hawakufanikiwa  kuingia  ndani.Alisema  mali zote ziko salama  na  suala  hilo  limeripotiwa  polisi  kwa  uchunguzi  zaidi.

No comments

Powered by Blogger.