ad

ad

VITA AZAM NA GOR MAHIA NANI KUTAWAZWA MFALME KAGAME CUP LEO

Habari One



Leo ndio Leo Fainali ya Kombe la Kagame kati ya  Azam FC dhidi ya Gor Mahia ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,

Azam FC yenye beki imara ambayo haijaruhusu hata bao moja mpaka hatua hii imeingia fainali baada ya kupata ushindi dhidi ya KCCA kwa bao 1-0 huku Gor Mahia ikiwa imeingia fainali baada ya ushindi dhidi ya timu ngumu ya Al Khartoum.

Hii ni mara ya pili kwa Azam FC kuingia fainali ya Kagame, mara ya kwanza ikiwa ni 2012 ambapo ilifungwa na Yanga iliyokuwa ikifundishwa na Tom Saintfiet ambaye sasa ni kocha wa timu ya taifa ya Togo.
Powered by Blogger.