JAMANI DADA MARTHA LOOO!-24
“Wewe usiwe mjinga. Pesa za kupanga za nini? Usipokee. Unachotakiwa kufanya wewe ni kung’ang’ania kuishi kule kwake. Mwambie wewe utakuwa unaishi kule yeye na Martha waishi hapa. Kwa hiyo akitoka kazini anakufuata kule. Mnajirusha halafu midamida anakuja huku,” alisema mmoja wa wanawake hao.

SASA ENDELEA MWENYEWE...
Mama Anna alikubaliana na ushauri huo kwani kwake aliuona kama ni wa kuweza kumfikisha kwenye ndoa kabisa na kumpiku Martha.
***
Martha na Roi waliwasili nyumbani hapo, usiku wa saa tatu. Waliwakuta wapangaji wapo nje bado wakipiga domo licha ya kibaridi cha mbali.
Macho ya Martha yalitua kwenye sura ya mama Anna, akakasirika kwa mbali. Kilichomshtua zaidi Martha ni gauni alilovaa mama Anna muda huo ndiyo lilelile ambalo aliambiwa na muuza duka kwamba, mwanamke aliyeingia na Roi ndani alikuwa amevaa...
“Inawezekana kweli mama Anna alikuwa amekwenda kule kwa Roi lakini labda hakukaa sana akatoka ila yule kijana wa dukani hakumwona ndiyo maana alijua bado yupo,” alisema moyoni Martha...
“Jamani za leo?” alisalimia Roi akiwa nyuma ya Martha wakiingia ndani...
“Nzuri tu za kwako shemeji?”
“Salama za kazi shemeji?”
“Salama za kazi honey?” alijibu mama Anna kwa sauti ya chini kiasi kwamba, Martha alijua amezungumza kitu kwa sauti ya chini ambayo hakuisikia hali iliyompa dukuduku kubwa sana...
“Baby,” Martha alimuita Roi wakiwa wameshazama ndani kwao...
“Yes! Niambie...”
“Mimi nahisi huyu mwanamke huyu...mama Anna ana jambo na wewe lakini sijalijua. Ila nalifanyia kazi.”
“Jambo kama lipi?”
“Kuna jambo. Mfano, hapo wakati tunaingia wenzake wamekusalimia. Hata yeye amekusalimia, lakini kuna maneno f’lani ameyasema naamini siyo salamu na ameyasema kwa sauti ya chini sana.”
“Mh! Mimi sijui kwa kweli. Labda ana mambo yake mwenyewe,” alijibu Roi huku moyoni akiujua ukweli.
***
Ilikuwa saa nne usiku, Martha akiwa anapiga pasi sebuleni, Roi yuko chumbani. Nje, usawa wa dirisha la sebuleni kwa Martha, alikaa mama Anna peke yake. Alikuwa akichati na Roi kule chumbani.
Alichokishangaa Martha, simu ya Roi ilipotoa mlio wa meseji, baada ya dakika kadhaa, simu ya mama Anna kule nje nayo ilitoa mlio wa meseji.
Martha alishtuka, hasa baada ya kubaini kuwa, milio hiyo ya meseji ilikuwa ikipokezana kusikika. Kwamba, unapolia wa simu ya Roi, baada ya muda unadakia wa simu ya mama Anna...
“Mh!” aliguna Martha, akaacha kupiga pasi, akasimama kusikilizia kwa umakini zaidi...
“Titiri...titiri...” huo ulikuwa mlio wa simu ya Roi...
“Titiiiti...” huo ulikuwa mlio wa simu ya mama Anna.
Martha aliingia chumbani, akampiga jicho moja Roi, akamwona akiweka simu juu ya dressing table...
“Baby, nataka kumpigia simu bro, lakini kumbe simu yangu sijaweka salio, niazime ya kwako nimpigie,” alisema Martha...
“Mh! Hata yangu haina salio, chukua elfu mbili hii ukanunue vocha,” aliwahi kusema Roi, Martha akaanza kushtuka. Aliamini Roi alikuwa akichati na mama Anna nje.
Alikwenda dukani kununua vocha, wakati anarudi alisimama chini ya mti wenye giza na kumwangalia mama Anna anavyoongea na simu huku akicheka...
“Teh! Teh! Mimi ni mashine baby...tena nakwambiaje? Siku akijua naamini patachimbika. Lakini mimi wala simuogopi,” alisema mama Anna huku akicheka.
Akaendelea...
“Duu! Baby, mfano pale kwako. Mimi miguu yote ilinyong’onyea, nikajua tumekwisha! Loo!”
Martha alipojitokeza, mama Anna alishtuka, akapunguza sauti huku akisema...
“Basi tufanye kesho baby wangu, usiku mwema.”
Martha alipita bila kusema kitu kwa mama Anna, akazama ndani na kumpa Roi vocha ya buku, akabaki na ya buku kuingiza kwenye simu yake.
***
Ilikuwa saa saba usiku, Martha alichelewa kupata usingizi kwa mawazo kuhusu kutaka uhakika wa kuwepo kwa mawasiliano kati ya mama Anna na jamaa yake, Roi...
“Hivi kama ni kweli nichukue hatua gani?” alijiuliza moyoni Martha...
“Na yale mazungumzo ya kwenye simu ya mama Anna muda ule mbona ni kama alikuwa akiwasiliana na Roi?”
Ghafla alipata wazo, alitoka kitandani huku macho yake yakitua kwa Roi. Alipobaini anauchapa usingizi mzito, aliifuata simu yake, akaichukua na kwenda nayo sebuleni.
Aliikuta simu hiyo haina ‘password’ kwa hiyo akaingia ndani moja kwa moja kwenye kiboksi cha meseji...
“Baby, unajua wakati tunaongea ghafla akatokea demu wako, ndiyo maana nikakuaga.”
Meseji hiyo ilitoka kwa mama Anna kwenda kwa Roi. Martha aliishiwa nguvu, nusura aanguke. Akaendelea kusoma nyingine...
“Basi usiku mwema baby. Nimekumisije jamani!”
Roi naye akajibu...
“Mimi je? Natamani kesho ifike haraka tukutane unikate kiu yangu. Lala salama mpenzi wangu nikupendaye.”
Martha alisimama, akamwomba Mungu kwanza kisha akajipa moyo na ujasiri wa hali ya juu. Akatuma meseji kwa mama Anna...
“Baby...”
Ingawa ilikuwa usiku sana, Martha akaamini atajibiwa, lakini hakujibiwa, akatuma nyingine...
“Jamani baby, naomba nije kwako basi, nimekumisi kweli mwenzio.”
Dakika zilikatika, hakupata jibu. Akazifuta meseji zake hizo mbili na kuamua kurudi chumbani kulala. Alitamani sana kumwamsha Roi ili ambane kuhusu meseji hizo lakini akajivumilia. Aliirudisha simu mahali alipoichukua na kulala.
***
Kulikucha, Martha aliamka na kuanza kufanya kazi za ndani lakini siku hiyo hakumwamsha Roi mpaka alipoamka mwenyewe.
Roi, kabla hajatoka kitandani, aliichukua simu na kuangalia meseji, akakutana na meseji ya mama Anna ikiomba radhi...
“Baby samahani, ulipotuma meseji usiku nilikuwa nimelala fofofo mwenzako. Halafu uliposema umenimisi unataka kuja ulikuwa unamaanisha au utani tu? Bibiye ungemwachaje kitandani peke yake?”
Je, nini kilitokea? Ili kuyajua yote hayo, tukutane inayofuata Jumamosi.

SASA ENDELEA MWENYEWE...
Mama Anna alikubaliana na ushauri huo kwani kwake aliuona kama ni wa kuweza kumfikisha kwenye ndoa kabisa na kumpiku Martha.
***
Martha na Roi waliwasili nyumbani hapo, usiku wa saa tatu. Waliwakuta wapangaji wapo nje bado wakipiga domo licha ya kibaridi cha mbali.
Macho ya Martha yalitua kwenye sura ya mama Anna, akakasirika kwa mbali. Kilichomshtua zaidi Martha ni gauni alilovaa mama Anna muda huo ndiyo lilelile ambalo aliambiwa na muuza duka kwamba, mwanamke aliyeingia na Roi ndani alikuwa amevaa...
“Inawezekana kweli mama Anna alikuwa amekwenda kule kwa Roi lakini labda hakukaa sana akatoka ila yule kijana wa dukani hakumwona ndiyo maana alijua bado yupo,” alisema moyoni Martha...
“Jamani za leo?” alisalimia Roi akiwa nyuma ya Martha wakiingia ndani...
“Nzuri tu za kwako shemeji?”
“Salama za kazi shemeji?”
“Salama za kazi honey?” alijibu mama Anna kwa sauti ya chini kiasi kwamba, Martha alijua amezungumza kitu kwa sauti ya chini ambayo hakuisikia hali iliyompa dukuduku kubwa sana...
“Baby,” Martha alimuita Roi wakiwa wameshazama ndani kwao...
“Yes! Niambie...”
“Mimi nahisi huyu mwanamke huyu...mama Anna ana jambo na wewe lakini sijalijua. Ila nalifanyia kazi.”
“Jambo kama lipi?”
“Kuna jambo. Mfano, hapo wakati tunaingia wenzake wamekusalimia. Hata yeye amekusalimia, lakini kuna maneno f’lani ameyasema naamini siyo salamu na ameyasema kwa sauti ya chini sana.”
“Mh! Mimi sijui kwa kweli. Labda ana mambo yake mwenyewe,” alijibu Roi huku moyoni akiujua ukweli.
***
Ilikuwa saa nne usiku, Martha akiwa anapiga pasi sebuleni, Roi yuko chumbani. Nje, usawa wa dirisha la sebuleni kwa Martha, alikaa mama Anna peke yake. Alikuwa akichati na Roi kule chumbani.
Alichokishangaa Martha, simu ya Roi ilipotoa mlio wa meseji, baada ya dakika kadhaa, simu ya mama Anna kule nje nayo ilitoa mlio wa meseji.
Martha alishtuka, hasa baada ya kubaini kuwa, milio hiyo ya meseji ilikuwa ikipokezana kusikika. Kwamba, unapolia wa simu ya Roi, baada ya muda unadakia wa simu ya mama Anna...
“Mh!” aliguna Martha, akaacha kupiga pasi, akasimama kusikilizia kwa umakini zaidi...
“Titiri...titiri...” huo ulikuwa mlio wa simu ya Roi...
“Titiiiti...” huo ulikuwa mlio wa simu ya mama Anna.
Martha aliingia chumbani, akampiga jicho moja Roi, akamwona akiweka simu juu ya dressing table...
“Baby, nataka kumpigia simu bro, lakini kumbe simu yangu sijaweka salio, niazime ya kwako nimpigie,” alisema Martha...
“Mh! Hata yangu haina salio, chukua elfu mbili hii ukanunue vocha,” aliwahi kusema Roi, Martha akaanza kushtuka. Aliamini Roi alikuwa akichati na mama Anna nje.
Alikwenda dukani kununua vocha, wakati anarudi alisimama chini ya mti wenye giza na kumwangalia mama Anna anavyoongea na simu huku akicheka...
“Teh! Teh! Mimi ni mashine baby...tena nakwambiaje? Siku akijua naamini patachimbika. Lakini mimi wala simuogopi,” alisema mama Anna huku akicheka.
Akaendelea...
“Duu! Baby, mfano pale kwako. Mimi miguu yote ilinyong’onyea, nikajua tumekwisha! Loo!”
Martha alipojitokeza, mama Anna alishtuka, akapunguza sauti huku akisema...
“Basi tufanye kesho baby wangu, usiku mwema.”
Martha alipita bila kusema kitu kwa mama Anna, akazama ndani na kumpa Roi vocha ya buku, akabaki na ya buku kuingiza kwenye simu yake.
***
Ilikuwa saa saba usiku, Martha alichelewa kupata usingizi kwa mawazo kuhusu kutaka uhakika wa kuwepo kwa mawasiliano kati ya mama Anna na jamaa yake, Roi...
“Hivi kama ni kweli nichukue hatua gani?” alijiuliza moyoni Martha...
“Na yale mazungumzo ya kwenye simu ya mama Anna muda ule mbona ni kama alikuwa akiwasiliana na Roi?”
Ghafla alipata wazo, alitoka kitandani huku macho yake yakitua kwa Roi. Alipobaini anauchapa usingizi mzito, aliifuata simu yake, akaichukua na kwenda nayo sebuleni.
Aliikuta simu hiyo haina ‘password’ kwa hiyo akaingia ndani moja kwa moja kwenye kiboksi cha meseji...
“Baby, unajua wakati tunaongea ghafla akatokea demu wako, ndiyo maana nikakuaga.”
Meseji hiyo ilitoka kwa mama Anna kwenda kwa Roi. Martha aliishiwa nguvu, nusura aanguke. Akaendelea kusoma nyingine...
“Basi usiku mwema baby. Nimekumisije jamani!”
Roi naye akajibu...
“Mimi je? Natamani kesho ifike haraka tukutane unikate kiu yangu. Lala salama mpenzi wangu nikupendaye.”
Martha alisimama, akamwomba Mungu kwanza kisha akajipa moyo na ujasiri wa hali ya juu. Akatuma meseji kwa mama Anna...
“Baby...”
Ingawa ilikuwa usiku sana, Martha akaamini atajibiwa, lakini hakujibiwa, akatuma nyingine...
“Jamani baby, naomba nije kwako basi, nimekumisi kweli mwenzio.”
Dakika zilikatika, hakupata jibu. Akazifuta meseji zake hizo mbili na kuamua kurudi chumbani kulala. Alitamani sana kumwamsha Roi ili ambane kuhusu meseji hizo lakini akajivumilia. Aliirudisha simu mahali alipoichukua na kulala.
***
Kulikucha, Martha aliamka na kuanza kufanya kazi za ndani lakini siku hiyo hakumwamsha Roi mpaka alipoamka mwenyewe.
Roi, kabla hajatoka kitandani, aliichukua simu na kuangalia meseji, akakutana na meseji ya mama Anna ikiomba radhi...
“Baby samahani, ulipotuma meseji usiku nilikuwa nimelala fofofo mwenzako. Halafu uliposema umenimisi unataka kuja ulikuwa unamaanisha au utani tu? Bibiye ungemwachaje kitandani peke yake?”
Je, nini kilitokea? Ili kuyajua yote hayo, tukutane inayofuata Jumamosi.
Post a Comment