JAMANI DADA MARTHA...LOOH!-2

ILIPOISHIA
“Yaani simuelewielewi, anaingia bandani, anatoka, anaingia, anatoka, ila poa tu, akiingia tena nafunga banda...”
JIACHIE KIVYAKO SASA...
“Martha...Martha...anaonekana ni mwanamke mwenye kujitambua. Inaonekana ameshaumizwa sana sasa machale yanamcheza namna ya kumkubali mtu,” alisema moyoni Roi akiwa amelala anaangalia juu...
“Da! Iko siku lakini...naweza kusema atakuwa wangu lakini kumbe ana mwingine ndiyo maana anaingia na kutoka.”
***
Kwa upande wake, Martha kule kwake alikokuwa alikuwa amelala huku akiwaza...
“Mh! Roi bwana. Anaonekana ananitaka, lakini mimi siwezi kwa kweli. Nimeshalizwa sana tu. Wanaume wa siku hizi ndivyo walivyo,” alisema moyoni Martha, akajikuta akishika simu na kumtumia meseji Roi...
“Baba!”
Roi alikuwa anaangalia muziki kupitia runinga, meseji ya Martha ikaingia, akaisoma...
“Nikwambie kitu baba?”
Roi aliachia tabasamu, akaamini kwamba anachotaka kukisema Martha ni kwamba amekubali wawe na uhusiano, akamjibu...
“Niambie baby wangu...”
“Unanipenda?”
“Sana!”
“Kweli?”
“Kweli kabisa.”
“Mimi naomba...tena naomba sana baba, tuwe kaka na dada.”
Roi alikuwa peke yake lakini aliguna kwanza, akaangalia kulia na kushoto kama aliyeamini kwamba, kuna mtu anamwona alivyong’onyea...
“Sawa,” alijibu Roi meseji kwa ufupi sana...
“Loo! Asante God...sasa naweza kuwa huru na wewe kama kaka yangu...nakupenda sana kaka, nitakuheshimu na kukuthamini. Nimetokea kukupenda sana Roi, amini hivyo.
“Kifupi mimi sina kampani yoyote ile, wewe ndiyo utakuwa kampani yangu kama kaka.”
“Usijali sista...hata mimi nakupenda sana kama dada yangu, nitakuheshimu na kukuthamini,” alijibu Roi.
Baada ya hapo, waliagana kwa ajili ya kulala...
“Bro, usiku mwema, Mungu akulinde...”
“Na wewe sista. Mungu akutangulie, ulale salama chini ya ulinzi wake.”
“Asante kaka...”
***
Kulikucha, Martha ndiye alikuwa wa kwanza kumtumia meseji Roi...
“My love bro.”
Mlio wa meseji ndiyo uliomwamsha Roi kutoka usingizini, akaisoma meseji hiyo na kuijibu...
“Yes darling sista.”
“Umeamkaje my sweethaert kaka?”
“Niko vizuri my baby sister. Wewe je?”
“Mimi pia...niko njiani bro nakwenda job. Leo tunaweza kuonana?”
“Hakuna tabu sista.”
“Oke...basi kazi njema na wewe bro wangu, nakupenda sana.”
“Nakupenda sana pia sista.”
***
Jioni walipomaliza kazi, walikwenda kukaa baa ya Ground Pub! Waliipenda pub hiyo kwa sababu ilikuwa inauza pweza na supu yake ‘mchuzi wa pweza’ na wakazi wengi wa Jiji la Dar walipenda kwenda kukaa hapo jioni.
Wakiwa hapo, Martha alimtumia meseji Roi...
“Sweetheart bro!”
Roi baada ya kuisoma meseji hiyo alianza kuweweseka akitingisha kichwa na kuachia tabasamu. Kuitwa sweetheart bro alihisi mwili kusisimka kimahaba..!
“Duu! Huyu Martha huyu...sijui! Huu ni usista kweli au kuna lingine?” alijiuliza mwenyewe, akamjibu...
“Darling sista!”
“Wapi?”
“Nipo hapa Ground Pub Sinza...wewe je?”
“Mimi ndiyo natoka. Je, tunakutana?”
“Yes! Njoo hapa, si unapajua?”
“Yes! Nikifika hapo?”
“Ukifika nipigie.”
Roi alipomaliza kuzungumza na Martha aliwaambia wenzake...
“Jamani...jamani...sikieni...”
“Vipi?” walimuuliza...
“Kuna mgeni wangu anakuja hapa, anatokea Kariakoo.”
“Ni shemeji yetu au?” aliuliza Julio...
“Acha maswali mengi wewe, mtamuona hapahapa akifika.
Lakini Roi akatumia nafasi ile kuwasimulia kisa chake na msichana huyo. Aliwasimulia ishu yote kuhusu Martha walivyokutana, walikofikia na wanakoelekea...
“Aaah! Mtu kama huyo bwana ngumu sana kumwelewa. Hapo unatakiwa kujiongeza katika kila neno lake. Pengine yeye yupo siriasi kwamba anataka wewe uwe kaka yake halafu wewe unawaza mapenzi, utamboa” alisema Julio...
“Hakuna, huyo ameshaingia laini, hapo Roi ni wewe tu,” alisema Pauli wakiwa tayari wapo kwenye moja baridi, moja moto.
Walibadilishana mawazo kuhusu Martha mpaka wakafikia hatua ya kuachana na mazungumzo hayo, wakahamia kwenye mambo mengine.
Baada ya nusu saa, simu ya Roi iliita...
“Jamani huyo, ameshafika...halooo sista...”
“Ee... nimefika hapa barabarani.”
“Ngoja nimtume mhudumu akufuate.”
“Poa.”
Roi alimpa simu yake mhudumu mmoja wa baa hiyo aende nayo barabarani...
“Ukifika pale piga namba hii, utakutana na dada mgeni wangu mmoja mlete hapa,” alisema Roi, mhudumu akaondoka na simu.
Baada ya dakika mbili, mhudumu aliongozana na Martha mpaka alipokaa Roi na marafiki zake. Kazi ikawa, Martha akae wapi sasa? Akae kwenye kiti cha jirani na kaka yake, Roi au?
Post a Comment