PLUIJM AMPIGIA SALUTI COUTINHO
BAADA ya kiungo wa Yanga, Andrey Coutinho, raia wa Brazil, kufanikiwa kufumania nyavu mara mbili katika mchezo wa Kombe la Mapinduzi dhidi ya Polisi Zanzibar, kocha mkuu wa timu hiyo, Hans van Der Pluijm, amefunguka kuwa kiwango cha mchezaji huyo kipo juu kwa sasa.

Pluijm alianza kwa kumuweka benchi kiungo huyo kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam, lakini michuano ya Kombe la Mapinduzi imemuamsha.Coutinho alifanikiwa kuifungia timu yake mabao mawili kati ya manne waliyofunga katika mchezo wa Kombe la Mapinduzi dhidi ya Polisi Zanzibar.
Akizungumza Pluijm amefunguka kuwa amefurahishwa na uwezo unaoonyeshwa na Mbrazili huyo kwani amekuwa akibadilika kila siku.“Coutinho ni mchezaji mzuri na amekuwa akielewa vyema maelekezo yangu.
“Hakika kwa sasa anaonyesha kiwango kizuri sana uwanjani na kila siku amekuwa akionyesha mabadiliko makubwa,” alisema Pluijm.
Pluijm alianza kwa kumuweka benchi kiungo huyo kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam, lakini michuano ya Kombe la Mapinduzi imemuamsha.Coutinho alifanikiwa kuifungia timu yake mabao mawili kati ya manne waliyofunga katika mchezo wa Kombe la Mapinduzi dhidi ya Polisi Zanzibar.
Akizungumza Pluijm amefunguka kuwa amefurahishwa na uwezo unaoonyeshwa na Mbrazili huyo kwani amekuwa akibadilika kila siku.“Coutinho ni mchezaji mzuri na amekuwa akielewa vyema maelekezo yangu.
“Hakika kwa sasa anaonyesha kiwango kizuri sana uwanjani na kila siku amekuwa akionyesha mabadiliko makubwa,” alisema Pluijm.
Post a Comment