KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA - 10

ILIPOISHIA
Mara mlango uligongwa…”
“Nani..?”
“Mimi,” aliitikia mlinzi…
“Unasemaje?” mama Joy alimuuliza baada ya kufungua mlango. Hakuwa na shaka kwamba aliyegonga ni mumewe kwa sababu alijua hawezi kutoka ofisini baada ya kutokuwepo kwa siku mbili…
“Mzoa taka amekuja bosi, nimwambieje?”
“Mwingize ndani, anisubiri kule nyuma kwenye dude la taka.”
Mama Joy alifunga mlango kwa nguvu, akamrudia Bonny…
“Sasa mpenzi wangu wakati wa kukupa zile laki mbili umefika, umesikia..?”
“Nashukuru sana.”
Mama Joy aliliendea kabati lake la nguo na kutoa laki mbili, Bonny akaziona…
“Hizi hapa.”
Lakini kabla ya kumpa alimshika na kumvutia kwake, wakagongana vifua, mama Joy akatumia nafasi hiyo tena kumwomba denda Bonny, kijana kinywa kikafunguka na kukaa wazi, ulimi wa mwanamke huyo ukapita zake na kuanza kutalii huku ukitoa joto la mahaba…
“Mmm…” aliguna mama Joy, akaguna sana, Bonny akajikuta mikono yake ikimshika mama Joy kwenye mabega na kumvutia kwake, wakakumbatiana kwa sana…
“Mmmm…” Bonny aliiga kama mama Joy. Wakiwa wanaendelea na kulana denda, Bonny alifanikiwa kuziona zile laki mbili kwenye mkono wa kulia wa mama Joy, hapo akazidi kusisimka. Alianza kuamini kwamba, kama atamshikilia mwanamke huyo atakuwa msaada wake mkubwa kila akirudi toka chuo.
Miguu yao ilichoka kusimama, wakajikuta wakiangukia kitandani. Bonny hakujali umama, akamvua nguo lakini zake hakutaka kuvua, akamchezesha gwaride la haraka.
Mama Joy alimsifia sana Bonny, akamwambia anapenda aone kifua chake kikiwa kazini kinafananaje, Bonny akashuka kitandani na kuvua nguo zote, wakabaki walivyozaliwa. Gwaride likaendelea.
Mama Joy alipata ushindi wa kwanza na wa pili huku alipokuwa akiusaka wa tatu, akauupata sambamba na kijana huyo.
***
Jikono mlinzi na Helena walikuwa wakimteta bosi wao huyo…
“Kwanini amekuwa hivi siku hizi? Zamani hakuwa hivi…”
“Ooo, we unajuaje, niulize mimi ninaye shinda ndani, we si unawaona wageni wakiingia na kutoka tu,” alisema Helena, akaongeza…
“Tena nadhani we umeanza kubaini hilo baada ya kupewa nafasi ya kula tunda, lakini huyu mwanamke hajatulia hata kidogo, ni mzinzi mkubwa, sijui anajisikiaje? Hana aibu wala haya, ameumbwa vibaya…”
“Mh! Kwa kweli, pengine malezi ya kwao, maana kuna watu wamelelewa vibaya katika maisha na ndiyo wanaokuwa na tabia hii…”
“Kulelewa vibaya kivipi, ina maana wazazi wake walikuwa wakimwambia awe mzinzi..?”
“Hapana, utakuta mzazi hajali bintiye akitoka na kurudi hata saa sita usiku, unadhani anakuwa wapi kama si kwa wanaume..?”
“Ni kweli lakini.”
Mara, walisikia mlango wa chumbani ukifunguliwa, mlinzo akakimbia kurudi kwenye lindo lake…
“Bosi amesema nenda kamsubiri kwenye dude la taka, lakini ujue mzee mwenye nyumba yupo hapa mjini…”
“Yupo ndani..?”
“Nimekwambia yupo mjini, hujui Kiswahili..?”
“Sasa mbona unawake kaka..?”
“Lazima niwake, iko siku moja utanaswa kama mwizi wewe, malaya wa kiume we…”
“Kha! Bosi hayo matusi yanatokea wapi tena?”
“Acha wewe, ondoa kelele zako hapa, ala!”
“Usinikoromee, we nyanda wa geti tu, huna tofauti na mimi, tena afadhali mimi Napata nafasi wa kuja kujirusha na bosi wako…”
“Nani hajajirusha naye?”
“Ina maana hata wewe tayari..?”
“Achilia mbali mimi, hivi saa hizi yuko ndani na kijana naye anajirusha kama wewe na mimi.”
Mara, mama Joy na Bonny alitokea na kuwakuta mlinzi na mzoa take wamesimama getini…
“Nyie vipi hapo..?”
“Hakuna kitu bosi, nilikuwa namwelekeza huyu aende kwenye dude la takataka kama ulivyosema…”
“Mama,” mzoa taka aliita…
“Unasemaje kijana wangu..?”
“Huyo nani..?”
“We unamtakia nini?”
“Mh! Isije kuwa kama mimi..?”
“Kama wewe kivipi..?”
“Mpenzi wako…”
“Ha!” alihamaki Bonny kumsikia mzoa taka akisema maneno yenye dalili kwamba ni mpenzi wa mwanamke huyo…
“Usijali sana Bonny, huyu kijana anakujaga kuzoa takataka humu ndani kwangu…”
“Pii…piii,” honi ya gari ililia getini…
“Nani huyo?” aliuliza mama Joy…
“Bosi, si wote tuko ndani?” alijibu mlinzi huku akikimbilia geti dogo kwanza…
Alifungua na kuchungulia nje, akaliona gari la baba Joy…
“Bosi…bosi mzee kaja…”
“Pipii…piii…”
“Mh! Hebu fungua, hakuna jinsi,” alisema mama Joy. Mzoa taka baada ya kusikia mwenye gari nje ni mume wa yule mwanamke, alitimua mbio kuelekea kwenye dude la taka, akazamisha fuko lake kwenye dude lile kisha na yeye akapanda na kuzama bila kujali harufu.
Geti lilifunguliwa, baba Joy akaingia na gari mpaka kwenye sehemu anayoegesha, akashuka akiwa amekazia macho Bonny…
“Shikamoo baba Joy…”
“Marhaba Bonny, hujambo bwana…”
“Sijambo…”
“Za siku..?”
“Nzuri…”
“Upom, sijakuona siku nyingi, siku hizi nasikia upo chuo aliniambia mzee wako…”
“Eee, nipo chuo.”
“Sawa, karibu sana.”
“Asante, nilikuja kusalimia sasa naondoka,” alisema Bonny lakini kwa sauti ya kutetemeka kwa wasiwasi…
“Ni vizuri, umekuwa baba sasa, naona hata sauti imeanza kutoka ya kutetemeka.”
Baada ya Bonny kuondoka na geti kufungwa, baba Joy alimkazia macho mkewe…
“Kuna fundi atakuja kuchukua gari hili akatengeneze…Fuko fungua geti nataka kutoka na hilo gari analolitumia mama Joy.”
Geti lilifunguliwa, baba Joy akahamishia vitu vyake, hasa brifkesi kwenye gari jingine aina ya Land Cruiser V8 na kuondoka zake bila kuongeza kitu kwa mkewe wala mlinzi…
“Fuko funga geti,” alisema mama Joy. Aliondoka na kumfuata mzoa taka kule alikokimbilia ambapo hakumuona. Alishindwa kumuita kwa jina kwa sababu alishamsahau jina…
“Huyu atakuwa amekwenda wapi?”
Mzoa taka kule ndani ya dude la taka alisikia dalili za mtu kutembeatembea, aliwaza ni mume wa mwanamke anayefanya naye mapenzi. Na alijua anamsaka yeye, sasa ili kujilinda aliinua kichwa kidogo na kuchungulia…
“Ah!” alijikuta akishangaa hivyo baada ya kumwona mama Joy…
“Siii,” alimwita maana alikuwa amempa mgongo akielekea kona nyingine ya nyumba.
Mama Joy aligeuka na kumwona mzoa taka, akaachia tabasamu laini…
“Wewe umezamaje humo ndani..?”
“Nimezama tu mwenyewe, si unajua tena kujiokoa…”
“Haya toka tuongee sasa, maana pale ulimuulizia yule kijana ni nani, yule kijana anaitwa Bonny, ni kijana wa nyumba ya tatu tu hapo mbele, familia yake na familia yangu ni kama marafiki wakubwa sana, alikuja kunisalimia,” alisema mama Joy baada ya mzoa taka kutoka katika dude la kuzolea taka…
“Mbona mlinzi wako alisema yeye ni kama mimi…”
“Yule mlinzi hana akili nzuri, sisi wenyewe tumemgundua baada ya kuanza kazi, hapa tulipo tunatafuta mlinzi mwingine,” mama Joy aliamua kumsilibia Fuko akiamini hata yeye Fuko maneno yake alilenga kumharibia.
Mama Joy kwa wakati huo hakuwa anahitaji penzi, Bonny alishamgalaza kila mahali, mwili ulikuwa umechoka kama mtu aliyetoka kufanya mazoezi ya viungo…
“Kwa hiyo sasa?” aliuliza mzoa taka…
“We zoa taka zako nenda uje kesho, mimi nataka kulala sasa, mwili wote unauma.”
“Unauma kwa sababu gani..?”
“Mzee wako usiku alinikamua sana…”’
“Siyo yule kijana..?”
“Nimekwambia yule kijana ni mtoto wa jirani, hujaamini tu…”
“Sawa, lakini sasa mimi leo nimekuja nina shida moja…”
“Shida gani..?”
“Nataka kupanga chumba Manzese…”
“Kwa hiyo unataka pesa za pango..?”
“Eee…”
“Tena itakuwa afadhali, kule nikija tunajificha zetu. Ni shilingi ngapi?”
“Elfu sitini…”
“Kwa siku moja?” aliuliza kwa mshangao mama Joy…
“Hapana, kwa miezi sita…”
“He! Ina maana kuna wenye nyumba wanaochukua kodi ya miezi sita..?”
“Manzese wapo wengi, kama huyu ninayekwambia.”
Mama Joy alimtaka mzoa taka asuburi palepale alipo. Aliingia ndani na kutoka na shilingi laki moja na elfu ishirini…
“Hizi ni kwa ajili ya mwaka mmoja…”
“Eh! Atakubali..?”
“Ina maana huwa hawakubali kupokea fedha ya mwaka mzima, ajabu!”
Mzoa taka alizipokea, akaondoka akiahidi kurudi na majibu kesho yake.
***
Usiku wa siku hiyo, mama Joy na mumewe wakiwa kitandani, mazungumzo yao yalikuwa hivi…
“Mama Joy…”
“Abee,” mama Joy licha ya kuitika lakini pia mapigo ya moyo wake yalikwenda kwa kasi, haikuwa kawaida ya mumewe kumwita hivyo usiku wakiwa wamelala.
Hata pale ilipotokea mume anataka haki yake ya tendo la ndoa alimshika mahali na kumwonesha ishara kwamba alitakiwa kugeukia upande wa pili sasa…
“Hivi unavyoamini wewe ni mke wa mtu..?”
“Naamini hivyo, kwani vipi baba Joy…”
“Mimi siamini…”
“Kwa kutumia kigezo gani..?”
“Leo sitakamwabia natumia kigezo gani, ila kesho au keshokutwa nitakwambia na utakijua tu.”
Mama Joy alionesha dalili za kumdharau mume wake, akageukia ukutani na kunyamaza kimya.
Baba Joy alilala akiangalia juu, yaani chali, viganja vya mikono aliviweka kwenye mto na kuegemeza kisogo chake hapo.
Alikuwa akiamini mkewe ana uhusiano na mzoa taka na aliendelea kuamini kwamba, jana yake aliporudi kutoka Arusha kijana huyo alifichwa au alitolewa nje ya nyumba hiyo kwa staili ya kikomandoo…
“Lakini kama ni hivyo, tatizo liko getini, lazima…”
“Dawa hapa ni moja tu, kumwaga ‘mapesa’, nimmwagie pesa mlinzi, nimmwagie pesa Helana, wao ndiyo watakuwa wakinipa hatua kwa hatua kwa sababu lazima wanajua,” aliwaza moyoni mwake baba Joy, hata alipopitiwa na usingizi hakujua zaidi ya kujikuta ameamka kumekucha lakini akiwa amechoka sana...
“Leo lazima kila kitu kiwe wazi,” alisema akitoka chumbani akiwa na pajama mpaka jikoni ambako alimkuta Helena akifanya usafi…
“Hujambo Helena…”
“Sijambo bosi, umeamkaje?”
“Mimi mzima. Eee, nina shida na wewe, lakini iwe siri ya sisi wawili…”
“Ipi tena hiyo bosi?” aliuliza Helena. Akilini aliwaza kwamba, neno litakalotoka kwenye kinywa cha baba Joy ni…
“Mimi nimetokea kukupenda sana, sasa kwa sababu mama Joy analeta mambo ya kijinga naomba sana uwe mpenzi wangu, lakini tufanye kwa siri.”
Lakini kilichotoka kinywani mwa baba Joy ni hiki…
ITAENDELEA SIKU YA KESHO
Post a Comment