ad

ad

KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA - 05



“Wako ‘kazini’…”

“Walipokuona?”

“Mama akamsukuma yule kijana, halafu akaanza kunijia juu, mimi nikaondoka,” alisema mfanyakazi wa ndani huku akiangaliaangalia nje kwa tahadhari kubwa…

“Mama huyu…”

“Lakini we Fuko, mbona na wewe umelala kwa bosi usiku wa kuamkia leo?”

“Si ndiyo hapo sasa hata mi mwenyewe najiuliza, kwanini alale na mimi halafu alale na mzoa taka? Usikute ni mambo ya kishirikina,” alisema mlinzi…

“Kwani wewe ulikuwaje hadi mkalala kitandani na kuzini?”

“Alinitongoza..!”

“Alikutongoza..?”

“Sasa wewe dada unavyoona mimi naweza kumtongoza huyu bosi, nitaanzia wapi kwanza? Au unadhani mzoa taka alimtongoza? Huyu mama ni mtaalam wa kutongoza, huenda hata mumewe alimtongoza.”



***

Mama Joy alimtumbukiza chumbani kwake mzoa taka ambaye alifikia kushangaashangaa chumba kilivyo kikubwa na vitu vingi…

“Mh! Si nitachafua hapa leo?” ndani ya moyo wake aliamini hivyo…

Alimshika kijana huyo na kumuegemeza kifuani kwake huku akimwambia maneno matamu ya mahaba…

“Mpenzi wangu, nataka nikiachana na wewe leo nisitamani mwanamke mwingine mpaka ipite wiki moja, sawa?”

“Sijakulewa.”

“Nasema hivi, tukipanda kitandani sasa hivi ufanye mambo mazuri sana, nataka tukimaliza leo nisiwe na hamu ya mwanaume mpaka wiki moja ipite.”

“Sawa.”

Mama Joy alimvua nguo mzoa taka na kubaki na ‘kufuli’ tu, kisha akavua na za kwake. Alitangulia kupanda kitandani, mzoa taka akafuatia akiwa na wasiwasi, hamu ya mapenzi hakuwa nayo kama ilivyokuwa kule nje kwani mazingira ya chumba na alivyo yeye vilikuwa vitu viwili tofauti…

“Sijui ananisema mi mchafu sana,” aliwaza…

“Sasa mbona jogoo mwenyewe hawiki, una nini?” aliuliza mama Joy huku akijaribu ‘kumtoa’ jogoo kwenye banda ili aende nje akawike, lakini wapi!

“Kijana, una nini mpenzi wangu, mbona hivi..?”

“Hata mi sijui, lakini tungeenda kule nje kwenye majani ndiyo kuzuri…”

“Mimi nje siwezi, we si umeona hali ilivyokuwa kule nje, kwani tatizo lako nini?”

“Sina uhuru na humu chumbani kwako, kuko kama ikulu bwana…”

“Umewahi kufika ikulu wewe?”

“Si wanasemaga kuzuri sana…”

“Sasa ikulu hakuna wafanyakazi wa kufanya usafi?”

“Mi sijui, lakini bado naogopa sana…”

“Unamuogopa mume wangu..?”

“Hapana, ila ntachafua…”

“Nini..?”

“Mashuka yako, mi sijaoga toka juzi ilee.”

“Wala usijali, mfanyakazi yupo atafua mashuka, we tulale hapahapa, lakini fanya nilivyokwambia, nikomeshe kabisa leo,” alisema mama Joy huku akipeleka mkono kwenye jogoo la mzoa taka huyo.

Kwa mbali, alianza kuwika kwani mzoa taka alihakikishiwa amani yake.



***

Fuko na mfanyakazi wa ndani walitoka kiaina kwenda kuwachungulia wawili hao kule nje, wakawakosa…

“Ha! Watakuwa wamekwenda wapi?” aliuliza mlinzi…

“Hawa wamekwenda chumbani. Hakuna sehemu nyingine wanayoweza kwenda zaidi ya huko,” alijibu mfanyakazi.





***

Baba Joy alikuwa amemaliza mambo yaliyompeleka Arusha, sasa alikuwa amekaa kwenye mgahawa akibadilishana mawazo na wenyeji wake…

“Unajua bwana, mwanamke siku zote anatakiwa kujitambua. Ukikuta mwanamke hajitambui ujue kazi unayo we mwanaume…” alisema mmoja wa wenyeji hao aitwaye Molleli…

“Ni kweli. Wanawake wa sasa wengi hawajijui. Utakuta mwanamke mke wa mtu lakini bado anapenda magenge, anapenda makundi, anataka awe anatoka na marafiki zake. Halafu ogopa sana mke wa mtu akiwa anapenda kuwa na ukaribu na vijana vijana…”

Baba Joy aliguna hapo. Akakumbuka jinsi mkewe alivyo na ukaribu na mzoa taka kiasi cha kumkaribisha ndani kwake hata giza likiwa limeingia.

Palepale alichukua simu yake iliyokuwa mezani na kumpigia simu mlinzi…

“Hujambo Fuko..?”

“Sijambo bosi, shikamoo…”

“Marhaba, mama Joy yupo..?”

“Yupo bosi…”

“Na nani..?”

“Unasema..?”

“Nakuuliza yupo na nani..?”

“Nani mama..?”

“We una akili kweli? Unadhani nakuuliza kuhusu nani..?”

“Nimekujibu bosi, nimesema mama yupo…”

“Yupo na nani..?”

“Unasema?”

Baba Joy alikata simu kwa hasira. Lakini akili ikamwambia kuna kitu ndiyo maana mlinzi anajibu maswali yote kasoro hilo tu! Aliisachi namba ya mkewe, akampigia.



***

Mama Joy alikuwa akimbembeleza mzoa taka akubali kulala kitandani na aondoe mawazo kwani ndiyo yanayomfanya jogoo ashindwe kuwika….

“Haa! Mume wangu huyo anapiga…

“Haloo…”

“Uko wapi wewe..?”

“Nani mimi..?”

“Unaniuiliza swali gani hilo..?”

“Niko nyumbani…”

“Na nani..?”

“Nani mimi..?”

“Mama Joy…”

“Abee…”

Baba Joy alikata simu. Alianza kuhisi kitu kikubwa zaidi. Akampigia mfanyakazi wa ndani…

“Za safari bosi..?”

“Njema, upo nyumbani..?”

“Ndiyo bosi…”

“Mama je..?”

“Yupo bosi…”

“Yupo na nani..?”

“Nani mama..?”

“Hivi nyiye hapo nyumbani pana nini leo..?”

“Kwa nini bosi..?”

“Mbona hammalizi kujibu badala yake mnauliza maswali… nimekuuliza mama je, yupo hapo nyumbani? Badala ya kunijibu unaniuliza na wewe ‘nani mama?’” alifoka baba Joy…

“Samahani sana bosi, mama yupo na mgeni wake…”

“Mgeni gani…?”

“Kijana mmoja hivi…”

“Huyo kijana we unamjua..?”

“Namjua bosi, anakujaga kuzoa taka...”

“Kumbe ni yule mzoa taka siyo?” aliuliza baba Joy huku akisimama kwenda kuongelea pembeni maana aliona pale siri zake zitakuwa nje…

“Ndiyo bosi…”

“Wako wapi muda huu..?”

“Naona wapo…ooooo, wapo sebuleni bosi…”

“Yaani huyo mzoa taka anakaa sebuleni kwangu..!”

Moyoni mfanyakazi huyo alisema…

“Ungejua wako chumbani kabisa, ungepaa na ndege utue Dar ufumanie.”

“Haya, asante sana,” baba Joy akakata simu. Alisimama kwa muda, kisha akampigia tena mfanyakazi huyo…

“Haloo bosi…”

“Sasa sikia, akiwa anatoka huyo mbuzi nibip…”

“Sawa bosi.”

Baada ya kukata simu, mfanyakazi huyo wa ndani alimwangalia mlinzi…

“Unajua bosi amejua..?”

“Hata mimi kaniuliza hivyohivyo. Nilishikwa na kigugumizi kama wewe mwanzo,” alisema mlinzi…

Mzoa taka na mama Joy walitumia dakika kama ishirini kule chumbani. Wakati wanatoka, mama Joy alitangulia mbele akifuatiwa na mzoa taka kwa nyuma.

Walizunguka kwenda kwenye dude la taka, mzoa taka akachukua fuko lake akasindikizwa hadi getini. Alichopewa na mwanamke huyo anakijua mwenyewe.

Mfanyakazi wa ndani alipogundua hilo alimbip baba Joy, naye akapiga haraka...

“Bosi wametoka tayari,” mfanyakazi alisema kwa sauti ya chini sana…

“Mama Joy kamsindikiza mpaka wapi?” baba Joy aliuliza huku akiinua mkono wa kushoto juu na kuutingisha ili aweze kusoma saa…

“Kamfikisha getini tu…”

“Haya, sasa sikia, mimi nitarudi kesho, nikifika mjini sitakuja nyumbani mpaka huyo mwanaharamu aje, kwani si anakujaga kila siku?”

“Ndiyo bosi.”

“Haya, nashukuru sana ee..?”

“Sawa bosi.”

Baada ya kukata simu, mama Joy alitokea jikoni…

“We mbona unaongea kwenye simu kwa kunong’ona sana, unaongea na nani?”



“Shangazi yangu anasema anaumwa sana bosi…”

“Sasa kama shangazi yako anaumwa ndiyo uongee kwa kunong’ona..?”

“Anasema hajisikii vizuri bosi…”

“Khaa! Sasa asipojisikia vizuri yeye ndiyo inakufanya wewe uongee kwa kunong’ona..?”

“Nisamehe mama…”

“Hapa nyumbani kwangu karibu nitawaachisha kazi watu maana nahisi kama mmeanza kunifanyia ushushushu kwenye nyumba yangu, mimi sitaki,” alisema mama Joy akiwa amesimama huku amemshikia kiuno. Akaendelea…

“Unanichimba siyo?”

“Sikuchimbi bosi…”

“Ulikuwa unaongea na nani? Maana najua siyo shangazi yako…”

“Shngazi bosi, kweli tena…”

“Nikikwambia unipe simu nione nitakuta namba ya shangazi yako..?”

“Ngoja mama nikwambie ukweli…”

“Niambie…”

“Kuna mzee mmoja wa nyumba ya tatu hapo, huwa ananitaka. Ndiye amekuwa akinipigia simu kila mara. Sasa hivi amenipigia anasema kama sina kazi niende tukale japo denda, sasa nilikuwa namuuliza denda ni nini..?”

“Sasa ulikuwa unanificha nini..?”

“Nilijua utakasirika bosi…”

“Nikasirikie nini?”

“Utajua kumbe naachaga kazi nakwenda kukutana na wanaume nje.”
ITAENDELEASIKU YA KESHO

No comments

Powered by Blogger.