ad

ad

KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA - 04



“Mzoa taka mama, simi sijui anataka nini mama, kwani leo kuna takataka humu ndani, mimi sijaziona,” alisema sana mlinzi…

“Wewe hujaziona kwani we ndiyo mzalisha taka? Hebu mfungulie.”

Mlinzi alifungua geti haraka sana, mzoa taka akaingia huku akiwa amebeba fuko la Rambo mgongoni…

“Karibu kijana wangu…”

“Asante mama, shikamoo…”

“Asante sana. Karibu pita.”

Mzoa taka alizama ndani ya geti akimfuata mama. Nyuma yake, mlinzi alikuwa akimwangalia kwa jicho baya ile mbaya…

“Mama mi nina wazo,” alisema mlinzi…

“Liweke wazi…”

“Hilo dude la taka lingejengwa nje…”

“Si jukumu lako,” alijibu mama Joy.

Mlinzi aliumia sana moyoni. Aliamini mzoa taka ana jambo na bosi wake, haiwezekani usiku kucha ampe mapenzi motomoto tena kitandani kwa mumewe, kisha asubuhi hiyo aanze kumgeuzia kibao na kuongea naye kama vile siku nyingine za nyuma. Alimezea lakini akaweka kitu moyoni.

Mama Joy alimshika mkono mzoa taka na kwenda naye nyuma ya nyumba ambako kuna dude la taka…

“Hivi kijana wangu unaitwa nani vile..?”

“Kofu…”

“Kofu..?”

“Ndiyo…”

“Kofu nani?”

“Kofu Nduche…”

“Mbona jina lako limefanana sana na la mlinzi wangu yule..?”

“Yeye anaitwa nani?”

“Fuko…”

“Sasa mama Fuko ni sawa na Kofu..?”

“Eee, Fuko ukiigeuza na kuanzia kwa mbele si unapata Kofu…”

“Eee, kweli. Basi ndiyo hivyo.”

Walipofika kwenye dude la taka, mzoa taka alichungulia ndani ya dude na kukutana na taka kidogo sana…

“Leo hamna kitu mama…”

“Wewe shida yako nini, si nakupa hela yako ya kuzolea…au?”

“Sawa,” alisema mzoa taka huku akianza kuingiza sehemu ya mwili kwenye dude hilo kwa lengo la kuchota takataka kidogo zilizokuwepo.

Mama Joy alimsogelea Kofu na kumshika kiuno kisha akamvuta. Jamaa alichomoka, akasimama akimwangalia mwanamke huyo…

“Vipi, leo hutaki?” aliuliza mama Joy huku akiwa amelegea macho kama aliyekula kungu manga…

“Sijui wewe…”

“Mimi niko tayari,” alisema mama Joy…

“Hata mimi, lakini leo nimechoka sana…”

“Umechokeshwa na nini?”

“Sijatia kitu tumboni tangu nimeamka.”

“Hilo tu, twende huku,” mama Joy alimshika mkono mzoa taka na kwenda naye hadi jikoni kwake…

“Kuna nini?”

Mfanyakazi wa ndani akafunua sufuria moja…

“Kuna hili pilau, halafu kuna nyama imeshaiva, ila kwenye friji kuna mikate na maandazi, keki zipo mezani, chapati zipo kwenye hotpot, lakini kama utataka samaki wa kukaanga wapo tayari kwenye friji ni wa kupasha moto tu…”

“Mh! Mwenzetu umetaja vitu vingi hadi nimesahau vya kwanza…mpe huyu maziwa na pilau,” alisema mama Joy. Alijua kwa kazi ya kuzoa taka mchana kutwa na kama toka ameamka hajatia kitu tumboni, alitakiwa chakula kizito kidogo…

“Kaa pale kwenye kiti.”

Mzoa taka alikaa akisubiri kifungua kinywa hicho ambapo moyoni alisema atakula mpaka kukomba sahani na akitoka pale ni mpaka kesho yake, fedha yote ya siku hiyo atakwenda kununulia bangi na kupiga viroba kwa wingi.

Mama Joy alikwenda chumbani kwake, akabadili nguo. Alivaa taulo akaingia bafuni kuoga. Alipotoka, alivaa khanga mbili, moja alijizungusha kupitia kwenye nido zake, nyingine kupitia kiunoni.

Akatoka kwenda jikoni ambako alimkuta mzoa taka yuko katikati ya mlo wa pilau na maziwa kwenye kikombe kikubwa…

“Vipi, changamka upate nguvu…”

“Sawa mama…”

Mama Joy naye alichukua kikombe na kujimiminia maziwa peke yake…

“Nikupe na nini mama?” aliuliza mfanyakazi…

“Hapana, maziwa yanatosha sana.”

Ukimya ulitawala jikoni, mzoa taka alikuwa akiendelea kupata ‘brekfasti’ yake, mama Joy alikuwa bize na maziwa yake huku mfanyakazi naye akijihudumia mwenyewe.

Mzoa taka alitangulia kumaliza kila kitu…

“Hebu muongeze mgeni maziwa na pilau,” alisema mama Joy lakini mzoa taka aligoma. Ilikuwa lazima agome hata kama anavuta bangi. Maana wavuta bangi wanasifika kwa kula sana, lakini pale alipewa maziwa kwenye kombe kubwa, pilau kwenye sinia na si sahani…

“Mimi nimeshiba sana…”

“Ongeza japo kidogo, we mwanaume bwana,” alisema mama Joy…

“Hapana mama, kesho.”

Mama Joy naye alitelekeza kikombe chake chenye maziwa na kutoka na mzoa taka hadi kwenye dude la taka…

“Sasa, si tayari umeshiba?”

“Nimeshiba sasa…teh! Teh! Teh!” alicheka mzoa taka huyo huku jasho jembamba la shibe likimchuruzika kuanzia kichwani.

Mama Joy alimsogelea mpaka akamkumbatia, akampiga busu. Mzoa taka naye akamrudishia kwa busu. Mama Joy akaenda mbele zaidi, akaomba denda licha ya kwamba kinywa cha mzoa taka huyo kilikuwa kikitoa harufu ya sigara.

“Mwee, ulimi wako una kajoto kazuri,” alisema mama Joy huku akimung’unya mate ya mzoa taka huyo ambaye mwenyewe alikuwa akijiuliza ni kwanini mwanamke huyo mwenye mume tajiri ameangukia kwake tena mchafumchafu asiye na thamani mbele za watu.

Aliwaza jinsi wanawake mitaani wanavyomkataa kwa sababu ya uchafu wake na mibangi anayovuta…

“Mm…au mganga wake alimwambia atembee na mwanaume mchafumchacfu nini?” alijihoji mwenyewe.

Mama Joy, licha ya kulala na kuamka na mlinzi wake, lakini muda huo alijikuta akichemka kwa kutaka penzi tena.

Alimshika mzoa taka na kumlaza pembeni ya dude la taka, akamvua nguo, akavua na zake, wakaanza ligi ya mapenzi huku mwanamke huyo akimiminika wingi wa maneno ya mahaba.

Mlinzi, yaani Fuko alihisi kuna kitu kinachoendelea kwenye dude la taka kwa vile toka bosi wake huyo alivyomshika mkono mzoa taka na kuzama naye maeneo hayo hakurejea tena, hakujua kama mzoa taka alipelekwa hadi jikoni akala pilau na maziwa.

Alisukuma geti kulifunga lote kisha akaanza kutembea kuelekea kwenye dude la taka, aliamini atakutana na fumanizi japo akili nyingine ilimwambia endapo atawafumani kweli ajue na kibarua kitakuwa kimeota nyasi.

Upande mwingine alijua hawezi kufukuwa kwa sababu ishu si kikazi ila wivu wa kimapenzi…

“Itakuwa alale na mimi halafu mzoa taka kaja anampapatikia vile, lazima kuna kitu wanakifanya,” alisema moyoni mlinzi.

Alipotokea kwa mbali alianza kuona miguu minne ikiwa imefungana pamoja, akashtuka…

“Si nilisema mimi,” alisema moyoni. Miguu hiyo ilikuwa ikipishanapishana kwa kuingiliana kwa staili mbalimbali. Mlinzi aliweza hata kujua miguu ya mzoa taka ni ipi na ya tajiri yake ni ipi.

Alichofanya, alikimbilia jikoni kwa mfanyakazi wa ndani…

“Dada nanihii, nenda kwenye dude la taka haraka sana ukaone…”

“Kuna nini kwani Fuko..?”

“Nimekwambia we nenda, husikii…”

“Sasa nitakimbilia sehemu kutazama kitu ambacho sikijui, pengine nikikiona nitaogopa je?”

“Shauri zako,” alisema mlinzi na kutoka.

Nyuma, mfanyakazi huyo aliamua kwenda kwenye dude la taka huku akili yake ikiwa haiwazi atakutana na kitu gani.

“Ha..!” alishtuka sana mfanyakazi huyo ambaye kiumri alikuwa amempita mama Joy.

Mama Joy naye alishtuka kusikia hamaki ya mfanyakazi wake, akamsukuma mzoa taka kisha yeye akasimama haraka sana huku akihema kwa kasi…

“Mama…” alisema yule mfanyakazi…

“Mama nini? Unasemaje kwanza?”

Mfanyakazi alikimbilia ndani huku akilia. Kwake yeye kitendo alichokiona alikichukulia kama nuksi au mkosi, pia alihisi kujidhalilisha nafsi kwani hakukitegemea..

“Yaani bosi! Anazini na mtoto mdogo yule! Tena mchafuuu! Mh! Ama kweli dunia imekwisha! Loo!” mfanyakazi huyo alisema hayo moyoni mwake.



***



Mama Joy, baada ya kumwona mfanyakazi wake amekimbia, alihisi heshima kubwa amepata…

“Mimi naona twende chumbani kwangu, hapa wala siko huru, kama ameanza kuja huyu anaweza kutokea mwingine,” mama Joy alimwambia mzoa taka…

“Chumbani mwako! Kitandani?” mzoa taka alishangaa na kumuuliza…

“Kwani kuna nini?”

Wakati mama Joy anamwambia mzoa taka kwani kuna nini, alishamshika mkono na kwenda naye kupita kwenye mlango mdogo wa nyuma ambapo si rahisi kuonwa na mtu.

Mlinzi pale getini alikwenda tena kwa kunyata hadi akafika eneo ambalo kuna nguzo nene, akasimama ili ajipange tena kwenda jirani na dude la taka…

“Safari hii nikiwakuta bado wanazini nawafumania, nitamwambia bosi habari hii nitamwambia mume wake akirudi safari, najua hatataka,” alisema moyoni mlinzi.

Alishangaa sana kutowakuta pale chiji ya dude la taka, akabaki kutumbua macho pima huku akijiuliza ni wapi wawili hao wanaweza kuwa wamekwenda kumalizia kula ‘uraha’ wao…

“Au wamekwenda choo cha nje kule? Haiwezekani! Labda wamekwenda kule nyuma kabisa,” alisema huku akienda nyuma ya nyumba ambako pia hakuwakuta…

“He! Au wameingia ndani kabisa?”

Alikwenda jikoni, akamkuta yule mwanamke wa kazi amekaa kwenye kiti huku akilia…

“Nini tena? Amekufokea?”

“Mh! Siwezi kulia kwa kufokewa na tajiri wangu wa kazi hata siku moja, ila mimi nimemshangaa sana bosi, yule kijana ni mchafu sana halafu sijui anavuta bangi. Lakini eti yeye amelala naye kama mpenzi wake! Unajua sijawahi kusikia achilia mbali kuona,” alilalama mwanamke wa kazi…

“Kwani uliwakutaje?” mlinzi aliuliza…

“Wako ‘kazini’…”

“Walipokuona?”
ITAENDELE SIKU YA KESHO

No comments

Powered by Blogger.