ad

ad

KARDASHIAN AAJIRI MTAALAM AMPUNGUZE KILO SABA ALIZOONGEZEKA


Mwanamitindo na mwigizaji  wa Marekani, Kim Kardashian akiwa na mtaalam huyo ameajiriwa ili amfundishe jinsi ya kupika chakula bora zaidi.
MWANAMITINDO na mwigizaji Kim Kardashian wa Marekani anasemekana ameongezeka uzito wa kilo 15 na hivyo amemwajiri mtaalam ambaye amempa jukumu la kuhakikisha uzito huo wa ziada unaondoka.
Mtaalam huyo ameajiriwa ili amfundishe jinsi ya kupika chakula bora zaidi kwa ajili ya familia hiyo akiwemo mtoto wake wa kike mwenye umri wa miezi 19 aitwaye North.
Kim Kardashianakiwa katika pozi.
Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 34 na mke wa mwanamuziki maarufu Kanye West, alisema: “Nimeanza kutafuta mtaalam wa mambo ya chakula kwani ninakula bila mpango.  Nimeanza kula chakula bora na kufanya mazoezi ili kubadili mtindo wa maisha yangu hususan sasa ambapo nina mtoto.  Ninataka kujua nini cha kupika na jinsi ya kupika chakula bora.”
Alipoulizwa iwapo anapanga kupata mtoto wa pili, alisema: “Ninatarajia jambo hilo.  Tunajaribu na tunaombea jambo hilo litokee.  Hivi sasa sina ujauzito lakini hivi sasa nimeongezeka kilo 15.”

No comments

Powered by Blogger.