ad

ad

MATATIZO YA UZAZI KWA AKINA MAMA


Akina mama wana matatizo mengi, mojawapo  kubwa linalowasumbua ni tatizo la kutokushika ujauzito.
Mwanamke kushindwa kupata ujauzito kwa kipindi cha ndani ya mwaka mmoja au zaidi ya mwaka  mmoja wakati mwanaume na mwanamke wanakutana kwa muda unaotakiwa na bila kutumia njia za kuzuia mimba ni tatizo.

Kuna aina mbili ya tatizo hili moja hujulikana  zaidi kwa jina la primary infertility. Hii humaanisha  kuwa mwanamke hajawahi kushika ujauzito maishani mwake.


Pili ni  secondary infertility,  hii humaanisha kuwa aliwahi kupata  mimba lakini ikashindikana kupata nyingine, na ya tatu ambayo  hutokea mara chache  kama asilimia 20 hujulikana  kama fecundability ambapo mwanamke anakuwa na uwezekano wa kupata mimba ndani ya mzunguko mmoja wa hedhi.

Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 80 ya wanandoa  hupata ujauzito bila ya kuwa na tatizo lolote kutokana na matakwa yao ambapo ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wakiwa  wanakutana mara kwa mara kimwili kati ya mara nne hadi tano kwa wiki na bila kutumia kinga  basi huweza kupata ujauzito bila tatizo lolote.

Asilimia 10 ya wanandoa huweza kufanikiwa kupata mimba kwa kipindi cha miaka miwili ndani ya ndoa na asilimia 10 zilizobaki haiwezekani kabisa kushika  ujauzito kwa kipindi cha zaidi ya miaka 2 ndani ya ndoa bila kutumia njia ya kuzuia ujauzito.

Vichocheo vinavyosababisha kutunga kwa mimba vipo vingi kama vile afya ya mbegu za mwanaume kuwa na uwezo  wa kukimbia sehemu za juu ukeni karibu  na shingo ya kizazi  pia mbegu  za mwanaume  ni lazima zibadilike na ziweze kuogelea  haraka kupitia  kwenye shingo ya kizazi.

Lazima kuwepo na upevushaji  wa mayai na mirija ili iwe na afya njema  na isiwe na tatizo  la kusafirisha yai.Mbegu ziwe na uwezo wa kuungana na yai  na kusafiri kutoka kwenye mirija kwenda mji wa mimba na yai lililoungana na mbegu  lazima lisafiri kwa muda wa siku nne hadi tano ili lifike  kwenye mji wa mimba

Itaendelea wiki ijayo.

No comments

Powered by Blogger.