JERRY SILAA: NATAKA TUMSOMESHE DOREEN KABUCHE MASTERS ILI KUPATA WATAALAM
Meya wa manispaa ya Ilala Mhe. Jerry
Silaa asubuhi ya leo alipatwa ugeni ofisini kwake kutoka kwa Doreen
Kabuche ambae ni mwanafunzi pekee kwa mwaka huu aliyekuwa best student
udsm kwa kupata GPA 4.8 kwenye shahada adimu Ya takwimu bima.
Mhe.
Jerry Silaa amewaambia waandishi wa habari kuwa, mwaka 2011 Doreen
Kabuche alimaliza Kidato cha sita Benjamin Mkapa na kuwa best female
student walimuita na akamzawadia laptop yenye thamani ya shilingi
Milioni moja na nusu…
“Mwaka huu amekuwa best student udsm
kwa kupata GPA 4.8 kwenye shahada adimu Ya takwimu bima. Nataka
tumsomeshe Masters ili kupata wataalam wataoangalia mifuko yetu ya
pension. Tuache kulalamikia utendaji mbovu wakati hatusomeshi wataalam” alisema Mhe. Jerry
Post a Comment