ad

ad

USIKU WA KIGODORO - 17


ILIPOISHIA: “Ni kweli faza, tena ilikuwa ndoa halali kabisa kwa wakati ule.”
“Unaposema ilikuwa ndoa halali kabisa kwa wakati ule una maana gani?”
SASA JIACHIE MWENYEWE…

Nina maana wakati nafunga naye ndoa sikujua kama ana mume mwingine kabla yangu. Ila baada ya kutokea lililotokea ndiyo nimejua kumbe nilikuwa siko sawasawa,” alisema James na kuashiria ukomavu wa busara.
“Vema sana, sasa nilichotaka ni hicho, kwamba bwana James atambue kuwa ndoa haikuwa yake, kaingilia. Lakini pia napenda nijua kwako Semi, uko tayari kumsamehe mkeo? Maana kwa upande wake ameshalijua kosa lake na ndiyo maana alikuja kutubu kwangu na nikamfanyia maombi.”
“Kusema kweli baba paroko nampenda sana mke wangu lakini alichokifanya sijakubaliana nacho, nahisi ni zaidi ya usaliti. Kwa hiyo kusema nimsamehe hapana,” alisema Semi kwa sauti ya upole kabisa.
Lina alianza kudondosha machozi huku akionekana uso umevimba. Eg yeye, moyoni alisema…
“Kama anachomoa si James ajichukulie mke tu!”
“Kwa hiyo unataka kuniambia kwamba haupo tayari kwa ndoa?” aliuliza padri.
“Ndiyo, sipo tayari,” Semi alisisitiza.
Padri, Eg, Lina na James wakaangaliana huku nyuso zao zikionesha mshangao mkubwa lakini Semi hakuonesha kushangazwa na mishangao yao.
Ukimya ulitawala kwa muda, padri ndiye akaukata kwa kuuliza…
“Kuna mwenye nyongeza?”
James alikataa kwa kutingisha kichwa, Eg akataka kusema lakini akaacha, Lina yeye ni machozi tu. Semi midomo ilimchezacheza kwa hasira.“Basi sawa, nifunge kikao. Lina, pole sana, mimi sina jinsi tena, mumeo kaamua hivyo,” alisema padri huku akisimama.
James alikuwa wa kwanza kuondoka baada ya kumpa mkono paroko huyo, Semi akasimama, naye akampa mkono paroko na kuondoka, Lina na Eg walibaki. Lina kilio kama kawa huku akisema…
“Faza, ina maana kweli sina ndoa tena?”
“Ndoa ipo, maana alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitengue, ila mumeo hataki kuishi na wewe. Mimi nilichojifunza kwake ni kwamba bado ana hasira ya tukio, ngoja atulie lakini na wewe mwombe sana Mungu,” alisema padri.
“Ni kweli kabisa Lina, shemeji bado hayuko sawa. Unajua jambo lenyewe zito,” alisema Eg huku akitangulia kuondoka mbele ya Lina ambaye bado alikuwa anamwaga machozi.
Je, unajua nini kilitokea hapo? Usikose kusoma kwenye Gazeti la Risasi, Jumatano ijayo.
Mama Kisamvu, mtoto Muhogo, ni shiida!

Samahani, sijui mwenzangu unaitwa nani?”
“Juliana Anold.”
“Unaishi wapi?”
“Ilala.”
“Ilala kubwa, Ilala gani?”
“We tambua ni Ilala,” alijibu Juliana huku akimwangalia kijana aliyekuwa mbele yake kwenye foleni ya benki akimuuliza.
“Oke, mimi naitwa Bitungu, naishi Temeke, lakini Ilala huwa nafikafika sana ndiyo maana nikataka kujua wewe unaishi Ilala gani?”
“Mimi naishi Ilala tu.”
“Oke, tuyaache. Una boifrendi?”
“Ninaye ndiyo.”
“Anaishi wapi?”
“Temeke.”
“Temeke ipi?”
“Temeke tu.”
“Mh! Oke, tuyaache hayo, naweza kupata namba ya simu?”
“Ya huyo boifrendi wangu au?”
“Ya kwako, boifrendi wako mimi ya nini?”
“Nitajie zako, nitakubip,” alisema Juliana kwa sauti yenye utulivu maana ni eneo la benki.
Bitungu alimtajia Juliana namba zake za simu, baada ya hapo wakaendelea kutembea kwenye foleni.
Juliana ndiye aliyeanza kuhudumiwa, alipotoka akampa mkono wa bai kijana huyo huku akichia tabasamu la ‘nakuacha’.
***
“Juli,” mama yake alimwita siku ya pili yake tangu mrembo huyo kukutana na Bitungu…
“Natoka mara moja, lakini nitachelewa kurudi.”
“Hivi mama, kila siku unapenda kutoka muda huu, kurudi unachelewa mpaka unagombana na baba huwa unakwendaga wapi kwani?”
“Wee mtoto, acha maswali yako. Unapatia wapi ubavu wa kuniuliza maswali kama hayo mimi mama yako?”
“Nisamehe mama.”
“Tena koma kabisa, usirudie tena.”
***
“Baby, unajua nilikumisi sana? Hatujaonana tangu lini?” mama Juliana alimwambia mpenzi wake ambaye ni dogodogo.
Lina na Eg walitoka, ilibidi Lina aende nyumbani kwa Eg kuishi huko ambapo baada ya wiki mbili alipokea barua kutoka mahakamani ikimtaka afike kwa tarehe aliyopangiwa bila kukosa akiwa analalamikiwa na James.
Lina alifika tarehe hiyo akiwa na Eg, wakamkuta James amejaa tele. Malalamiko ya James kwa Lina mahakamani hapo ni kuamua kufunga ndoa batili na James huku akijua ana mume halali na hivyo kumsababishia hasara na kumchanganya akili mwanaume huyo.
Lina alikana mashitaka na kesi inaendelea huku Semi naye akimfikisha kwenye mahakama nyingine akidai talaka, nako kesi bado inaendelea. Kesi zote zimemkalia vibaya Lina, anakabiliwa kutoa talaka kwa Semi na kuamriwa kulipa gharama alizozitoa James kwa ajili ya ndoa yao.
Ama kweli, kabla ya kutenda fikiri kwanza, ikibidi hata mara saba mpaka kumi au kushirikisha watu wenye hekima zaidi yako.

MWISHO.

No comments

Powered by Blogger.