ad

ad

USIKU WA KIGODORO - 05



ILIPOISHIA: Wakati mazungumzo yakiendelea, mume wa Lina alifunga breki nje ya nyumba ya Eg na kupiga honi ana shida na mke wake huyo…
“Pii pii piii!”     
JIRUSHE MWENYEWE SASA…
Eg ndiye aliyechungulia nje baada uya kusikia honi ya gari, akashtuka sana na kusema…
“Ha! Lina, shemeji Semi…”
“Kweli?”
“Mungu tena, amesimamisha gari hapo nje.”
“Mungu wangu, sasa?”
“Hata sijui! Kwani amefuata nini huku?  Au ametonywa ishu nzima?”
“Hapana, atakuwa ana shida na mimi. Lakini sasa nimeshavaa itakuaje? Si ataniona nimekuwa rasmi sana kuliko huyo niliyemsingizia?”
“Na kweli.”
Semi alipiga tena honi, Eg akatoka. Lina alivua gauni la kitchen party na kuvaa alilokwenda nalo kisha naye akatoka. Ndugu na marafiki wa Eg nao wakafuata hadi kwenye gari…
“Shem mambo?” alisalimia Eg…
“Poa, mzima wewe?”
“Mimi mzima. Karibu sana.”
“Asante sana.”
“Huyu ndiye shemeji kwa Lina?” ndugu mmoja wa Eg aliuliza akiamini Semi ndiye bwana harusi mtarajiwa…
“Eee, ndiyo huyu.”
“Oo! Karibu sana shemeji…sisi leo mambo yatakwenda vizuri kabisa ukumbini…bibiye atapendeza kupita kawaida,” aliropoka yule ndugu bila kujua kwamba anakaribia kulipua bomu.
Kilichosaidia ni kwamba, maneno yake yalifunga ufahamu wa Semi kwani kule kusema sisi leo mambo yatakwenda vizuri, Semi alijua ni sherehe ambayo mkewe alishamwambia ipo.
Kule kusema bibiye atapendeza kupita kawaida hakukumfanya Semi ahisi kitu kwani ni kweli mke wake alitoka nyumbani na gauni zuri la kitenge ambalo alisema atalivaa kwenye kitchen party ya rafiki yake, ubaya uko wapi sasa!
“Sawa jamani, nawatakia sherehe njema, nimekuja kumpa maagizo huyu, mimi nakwenda Morogoro nikichelewa nitarudi kesho.”
“Sawa mume wangu,” alisema Lina. Mwanamke mmoja akadakia…
“We, bado hajawa mume wako, atakuwa mumeo ukishafunga naye ndoa.”
Lina na Eg walishtuka sana kwa kauli hiyo, walijua sasa mambo hadharani lakini katika hali isiyotarajiwa, Semi akajibu…
“Tufunge ndoa mara ngapi? Shemeji Eg hujawaambia nini?” akawasha gari na kuondoka huku akicheka.
Mambo yalikuwa mambo, mkorogano ulitawala kila aliyesema, aliyesikia alitafsiri vingine kabisa.
Hata yule mwanamke aliyejibiwa kwamba ‘tufunge ndoa mara ngapi?’
alijua ameambiwa kwa kutaniwa kwani alijua ile kitchen party ya Lina, muoaji mwenyewe ndiye yule. Na Semi naye alijua yule mwanamke ameuliza kwa sababu ya ugeni, hajui kama Lina yupo kwenye ndoa ndiyo maana akamwambia Eg, ‘shemeji Eg hujawaambia nini?’
***
Lina aliendelea kujipamba, magari mawili ya kukodi yakafika kwa ajili ya kupelekwa ukumbini.
Shamrashamra ukumbini zilinoga kama si kuvutia, kwani kila kitu kilikwenda sawasawa. Lina pamoja na kwamba alitegemea michango lakini yeye mwenyewe kwa kupitia kwenye mfuko wa James alichangia fedha kwa kiasi kikubwa na kusababisha bajeti kwenda ilivyopangwa.
Shughuli ilikuwa nzuri, waalikwa walikula la kunywa na wakasaza huku kila mmoja akimpongeza Lina.
Lakini muda mwingi wa sherehe hiyo, Lina alipenda kuinamisha kichwa ili kukwepa macho ya watu akiamini pengine kuna ambaye atakuwa anamjua. Mbali na macho ya watu, awali kabisa Eg alishawatangazia waalikwa kuachana na kupiga picha kwa kutumia kamera za kwenye simu zao. Na wala hakukuwa na mpiga picha aliyekodishwa.
Baada ya shughuli hiyo, Lina alikwenda kulala kwa Eg baada ya kumpigia simu mume wake na akamwambia hatarudi toka Morogoro.
Usiku Lina alianza kuchati na James…
“Baby sherehe ilikuwa nzuri sana, nimemaliza kazi bado kwako ndoa wikiendi ijayo.”
“Niko fiti baby, mipango yote tayari. Tutakwenda fungate wapi baby?” aliuliza James swali lililomuumiza sana Lina kwani alijua kwenda fungate ni kubumbulua mambo kwa mume wake, atamuaga anakwenda wapi!”
“Popote pale my dear,” alijibu Lina.
Kama wangekuwa wanaongea kwa sauti angeshangaa kusikia sauti ya Lina inazungumza kwa unyonge wa hali ya juu.
“Basi niachie mimi, nitachukua hoteli nzuri sana tena kubwa ya hapa mjini. Au unataka twende nje ya mji kama Zenji?”
“Noo! Hata hapa Dar panatosha sana my love.”
Walichati mpaka saa tisa kasoro lakini muda mwingi akili ya Lina ilikuwa haipo sawa. Kuna wakati alitamani hata kufunguka lakini alishindwa kwa sababu walishafika mbali na angesababisha mawazo ya James kuamini kwamba  wanawake ni wabaya sana.
Siku ya ndoa ndiyo ikafika sasa, Lina alikuwa anajiandaa kivyake na James kivyake walikubaliana wakutane kanisani na kuungana kuingia ndani kwa ibada ya ndoa.
 “Uko wapi Lina?”
“Kwa dada, ndiyo tunataka kutoka kwenda saluni my dear.”
“Lina usinitibue, kwa dada saa hizi wakati unajua kanisani tunatakiwa saa nane kamili mchana, sasa uende saluni saa sita hii utamaliza muda gani? Kanisani utakuja saa ngapi na ndoa itafungwa saa ngapi au hutaki tufunge ndoa Lina?”
“Nitamaliza mapema tu.”
Mara Lina akakata simu…
“Khaa! Yaani Lina kanikatia simu mimi? Ana maana gani?” alijiuliza James. Alipopiga tena iliita bila kupokelewa…
“Afadhali isingepatikana ningesema chaji imeisha, sasa hapokei ana maana gani?” James aliendelea kuwaza…
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

No comments

Powered by Blogger.