ROSE NDAUKA ASEMA UCHUMBA WAKE NGANGARI
Stori: Gladness Mallya
MWIGIZAJI nyota wa filamu, Rose Ndauka ameibuka na kukanusha vikali uvumi uliozagaa kuwa uchumba wake na Malick Bandawe umevunjika na kusema siyo kweli kwani bado upo ngangari kuliko kawaida.
Mwigizaji nyota wa filamu Bongo, Rose Ndauka akipopzi.
Akistorisha juzikati, mwigizaji huyo anayeishi na
mchumba wake huyo, alisema uvumi huo hauna msingi kwa sababu asubuhi ya
siku hiyo (Jumatatu) alikuwa amemnyooshea nguo alizovaa wakati akielekea
kazini kwake.
Rose Ndauka akiwa na mpenzi wake Malick Bandawe.
Awali, kulikuwa na madai ya kuwepo kwa mtafaruku baina ya wawili hao
na kudaiwa kuachana kutokana na mmojawapo kulala nje siku tatu, kitendo
kilichochochewa na kuonekana kwa Rose akiwa peke yake wakati wa fainali
za kumtafuta msanii chipukizi zilizofanyika katika ukumbi wa Mlimani
City wiki iliyopita.

Post a Comment