ad

ad

MH! MISSED CALL YA SHEMEJI! - 02



ILIPOISHIA
Usiku wa siku hiyo, Beka na mke wake, Aisha walitofautiana chumbani, ikawa zogo…
“Mimi nataka nikisema unisikilize, siyo kujibishanajibishana, we mwanamke vipi?”
“Vipi kwani vipi, wewe mwanaume vipi?
ENDELEA KIVYAKO…
(PUNGUZO LA BEI TUSAPOTI KUTEMBELEA TANGAZO CHINI  LI - CLICK UJIONEE)
Dada wa Aisha, alisikia malumbano hayo kupitia chumbani anakolala, akashtuka na kukaa kitandani ili asikilize kwa undani.
“Kwani ina maana mimi sichoki siyo? Kila siku, kila siku utadhani chakula bwana,” alisikika Aisha akisema.
Dada mtu alijisikia vibaya sana kwani alijua kilichokuwa kimetawala malumbano yao ni masuala ya unyumba kama si ndoa…
“Sasa huyu mdogo wangu, kama amefikia hatua ya kusema hivyo kwa mumewe, ndoa si itamshinda! Mke anaweza kweli kusema maneno kama hayo kwa mumewe? Kwa hiyo anataka mumewe achukue uamuzi gani sasa? Akitoka nje ya ndoa maneno, ooo… nasalitiwa! Kumbe yeye mwenyewe ndiye chanzo.”
***
Asubuhi iliyofuata, dada mtu aliamka mapema, akaenda sebuleni kama ilivyo kawaida yake, akakaa na kuwasha Tv kuangalia vipindi mbalimbali, mara akatokea Beka.
“Za asubuhi shemeji?” alisalimilia Beka huku akionesha uso usiokuwa sawa tofauti na kawaida yake ya kupenda kumtania shemeji yake huyo.
“Salama shemeji, pole…ee! Umeamka salama?” dada wa Aisha alijichanganya hapo, lengo lake aseme umeamkaje, akajikuta anatoa pole kwa sababu mawazo yake yalikuwa kwa lile tukio la usiku.
“Nimepoa shemeji,.” Alisema Beka, shemeji yake akashangaa kuona mwenye pole ameikubali bila kuuliza ni pole ya nini.
Hiyo ilimpa nguvu dada mtu kuuliza zaidi…
“Kwani shemeji nini kimetokea?”
“Aah! Shemeji mdogo wako wakati mwingine siyo.”
“Kafanyaje?”
“Unajua….”
Beka alipoanza kusema tu, alisikia mlango wa chumbani unafunguliwa, ina maana Aisha anatoka, akasema…
“Shem nitakusimulia baadaye.”
“Poapoa!”
***
Ni kweli Aisha ni mdogo wa Ime, lakini hudhani ni mapacha kwani udongo uliotumika kumuumba Ime ni wa aina yake, pengine ni huo wanaouita mfinyanzi kwani kwa macho haikuwa rahisi kumjua nani mkubwa, nani mdogo.
Mbaya zaidi walifanana hata sura na maumbo, tena umbo la Ime usiseme, alifungasha kwelikweli, kwa vile tu alichakazwa na maisha magumu ya kwa mume wake alikotoka.
Ila yeye pia alijaliwa weupe kumzidi mdogo wake Aisha, sasa kama angekuwa na maisha ya mjini na kutumia yale ‘mambo yetu’ huenda weupe wake ungefanana na wa Mchina kama si Mzungu achilia mbali Mwarabu.
***
Aisha alitoka, akamkuta dada yake anawekaweka vitu sawa sebuleni huku akifuatilia matangazo kwenye Tv…
“Shikamoo dada.”
“Marhaba, umeamkaje Aisha?”
“Salama tu, naona unapangapanga!”
“Ah! Usingizi unaisha mapema sana mdogo wangu, mawazo kibao.”
“Usiwaze sana dada, nimekwambia we ishi hapa, kwani tatizo lako nini?”
“Najua, lakini mtu kwake mdogo wangu.”
“Imeshindikana sasa, utalazimisha dada?”
“Lakini kweli mdogo wangu.”
Aisha alipita kwenda jikoni kisha akaenda uani na kumalizia na chooni kuangalia usafi ulivyofanywa na msichana wa kazi.
Mumewe alirudi ndani akiwa ameshaoga, alijiandaa akatangulia kutoka kwenda kazini…
“Shem, mimi nawahi kibaruani, baadaye.”
“Baadaye shemeji yangu, uniletee matunda bwana.”
“Sawa shemeji.”
Aisha yeye alicheka tu kisha akamtania mume wake…
“Na mimi baby uniletee matunda.”
“Sawa.”
Ndani ya moyo, dada yake alipata tabu sana kwani alijiuliza kama Aisha anasema vile asubuhi wakati usiku alitoka kumwekea ngumu mumewe kuhusu tendo la ndoa ni sahihi? Aliona si sahihi wala si sawasawa kwa mwanamke mwenye akili zake timamu kichwani.
Alihisi mdogo wake ameacha maadili waliyofundishwa na wazazi wao  na kushika yake ambayo yametawaliwa na ubabe na kutokuwa na adabu ndani ya nyumba.
Alitamani sana kummbwatukia mdogo wake lakini moyoni akasema kwa sababu shemeji yake alimwambia atamsimulia baadaye hivyo ni muhimu kusubiri muda ufike ili amsikie ndipo aone uwezekano wa kuzungumza na Aisha.
***
Siku hiyo, Beka alirejea nyumbani saa kumi na mbili jioni. Sebuleni alimkuta shemeji yake…
“Ohoo, karibu mume wangu, pole kwa kazi jamani?”
“Nimekaribia mke wangu, nashukuru sana kwa kunipa pole kwa kazi,” alisema Beka huku akiachia mfuko mkubwa wa rambo uliokuwa ukipokelewa na shemeji yake huyo.
Alifikia kukaa kwenye kochi, akavua viatu, soksi na kuhema kidogo kisha akaulizia kama mke wake alisharudi…
“Mke mwenzio amerudi?”
“Bado, tena kanipigia sasa hivi, kasema akichelewa, nianze kuchambua mchele maana kuna foleni,” alisema shemeji huyo akipeleka jikoni ule mfuko ambao ndani yake mlikuwa na matunda.
“Ni kweli kuna foleni sana.”
Shemeji alipoona Beka ndiyo amewahi kufika kuliko mkewe, aliamini ndiyo wakati muafaka wa kumsikia alichotaka kumwambia…
“Shemeji,” aliita dada wa Aisha huku akikaa…
“Yes shemeji…”
“Asubuhi uliishia kuniambia utaniambia, ni nini kwani shemeji?”
“Ah! Shemeji mdogo wako anazinguaga sana. Basi tu! Hivi unaweza kuamini kwamba wakati mwingine inapita wiki tatu hataki kunipa unyumba? Ni akili hizo?”
“Kweli?”
“Kabisa.”
TUNAOMBA SAPOTI YA KUJIUNGA NASI FACEBOOK LIKE HAPA
 
“Ah! Aaaa! Madai yake?”
“Si ya msingi…”
“Kwamba..?”
“Anakuwa amechoka!”
“Na..?”
“Anajua yeye.”
“Mh!” aliguna dada mtu huyo huku akimwangalia shemeji yake kwa macho ya huruma…
“Sasa ina maana unaishije shemeji?”
“Kivipi shemeji?” 
 
Aaaa! Masuala fulani…”
“Kama..?”
“Kamaa…aaa…da! Yaani inapotokea mmegombana kama wanandoa inakuaje usiku, anakuchia uhuru au anabana?”
“Mh! Shemeji we acha tu, mdogo wako ananibania sana. Si inapotokea tumegombana tu, hata kama hatujagombana. Kwa kawaida yeye mpaka ajisikie…
“Mbaya zaidi shemeji, hata inapotokea mimi naumwa halafu yeye anataka ananilazimisha, lakini kwa upande wake sivyo.”
“Da! Jamani, Aisha ameipatia wapi hiyo tabia? Sisi hatujalelewa hivyo, ndiyo maana hata siku ya harusi kama unakumbuka shemeji, baba aliongea sana, alimwambia akaishi na mumewe kwa jinsi alivyolelewa…
“Tena shemeji kama utakumbuka vizuri, baba alisema kusalitiwa ndani ya nyumba kunatokana na mke mwenyewe, ndiyo kama hivi. Sasa kwa mfano ukitaka kumsaliti hapa atasema wewe si mwaminmifu? Si yeye mwenyewe ndiye atakuwa chanzo?”
“Ni kweli shemeji, labda uongee naye mdogo wako.”
“Akha! Niongee naye nini? Yeye si mtoto, anajua maisha, anajua kila kitu, mtoto ukimnyima chakula ndani akienda kula kwa majirani utamsema?”
“Huwezi kumsema shemeji!”
“Huwezi kabisa, maana wewe ndiye tatizo,” alishadadia dada wa Aisha.

Beka akaendelea kulalamika…
“Unajua shemeji ilifika mahali nikasema afadhali ningekuoa wewe, maana kama unakumbuka wewe ndiye ulikuwa wa kwanza kuonana na mimi nilipokuja kule kikazi, ndiyo nikasikia ulikwenda likizo na ulikuwa una mume.”
“Wewe kama mimi shemeji, hata wakati wa matatizo na mume wangu nilisema moyoni afadhali ningeolewa na wewe, unaonekana ni mtulivu, mvumilivu na mwingi wa busara kama siyo hekima.”
Mara mlio wa gari ulisikika kwa nje, Aisha alikuwa amerejea…
“Shemeji huyo mwenye mji amerudi, baadaye basi shemeji,” alisema dada wa Aisha kwa sauti ya kuiba asisikike huku akiwa amesimama…
“Sasa shemeji mazungumzo yetu bado lakini, nipe namba ya simu…”

Nitakupa kiaina,” alisema dada mtu huyo huku akitokomelea chumbani kwake kwa mwendo wa haraka kama vile alikuwa hataki akutwe akiwa laivu na shemeji yake.
“Za saa hizi?” Aisha alimsalimia mumewe…
“Salama tu, za huko?”
“Huko poa kiasi chake, lakini si sana.”
“Kwa nini?”
“Nimechoka sana, leo mambo yalikuwa mengi sana mume wangu.”
Wakati Aisha anatumia neno ‘mume wangu’, Beka akakumbuka jambo aliloongea na shemeji yake…
“Akha! Niongee naye nini? Yeye si mtoto, anajua maisha, anajua kila kitu, mtoto ukimnyima chakula ndani akienda kula kwa majirani utamsema?”

Huwezi kumsema shemeji.”
“Pole sana mke wangu,” alidakia Beka huku moyoni akisema…
“Ningekuwa mumeo kweli ungekuwa unaninyanyasa kitandani?”
“Nimeshapoa mume wangu! Dada yuko wapi?”
“Nadhani chumbani kwake.”
“Amelala?”
“Sijui, lakini alikuwepo.”
“Au anaumwa?”
“Nimekwambia sijui mke wangu.”
Aisha alipita hadi chumbani kwa dada yake akamkuta amelala kitandani lakini si usingizi…
“Dada shikamoo.”
“Marahaba, pole na majukumu mdogo wangu.”
“Nimepoa, ulikula mchana?”
“Aaah! Nilikula sana, tena nilishiba haswa sidhani kama usiku nitakula.”
“Kwa nini usile? Yaani kula mchana ni sawa na kula usiku? Mbona kila mlo unajitegemea.”
“Tatizo shibe mdogo wangu.”
“Hamna bwana dada, usiwe hivyo, lazima ule hata siku shemeji akikuona ajue kweli ulikuwa ukitunzwa na mdogo wako.”
Wakacheka, Aisha akatoka huku dada yake akimwangalia kwa nyuma na kusema moyoni…
“We cheza na mume tu, siku moja utajikuta unalia kilio cha mbwa, mdomo juu, masikio walu, mjini hapa! Ohoo!”
Aisha alikwenda kubadili nguo, alipotoka alikaa sebuleni na mumewe Beka wakizungumza na mambo mawili matatu kisha akaenda jikoni kuanza maandalizi ya chakula cha jioni.
***
Kule chumbani, baada ya kuondoka Aisha, dada mtu aliwaza kitu…
“Hivi, mimi na shemeji tutamaliza salama kweli? Mbona kama viashiria fulani si vizuri? Ina maana na yeye…mh! haya, tupo hapa,” alisema moyoni akiwa amekaa kitandani na kujiinamia kwa mawazo…
“Lakini kwa mfano sasa, imetokea mambo yamekwenda mwisho wake yamekuwa mambo, itakuaje? Nikubali? Noo! Siwezi kumkubalia shemeji yangu, yule ni mume wa mdogo wangu wa damu moja…
“Lakini sasa anamtesa mumewe, anamnyima haki yake ya ndoa, anasema mpaka apende yeye, ikitokea akapenda mume yeye hataki majanga.”
***
Jikoni na sebuleni ni mbali kidogo, dada mtu alitoka chumbani kwake akaenda kuungana na mdogo wake jikoni kwa ajili ya maandalizi ya chakula.
Ndipo alipokumbuka kwamba, aliahidi kutoa namba yake ya simu kwa shemejiye, hivyo akaenda chumbani kwake na kuchukua kalamu na karatasi akaiandika namba hiyo na kukikunja kile kikaratasi na kutembea nacho hadi sebuleni, akamtupia shemeji yake na kuondoka zake kurudi jikoni.
“Majangaa…majangaa…mbona majangaaa…mbona majangaa…,” aliimba dada mtu huyo, mdogo wake akapokea…
“Ndoa nifunge mimi, fungate niende mimi, mume umchukue wewee…kuolewa niolewe mimi, mahari nitolewe mimi, mume uite wewe,” alidakia Aisha huku akicheka…
“Majangaa…majangaa…mbona majangaa,” aliendelea kuimba dada mtu kwenye eneo la kibwagizo cha wimbo huo kisha wote wakacheka sana, ghafla dada mtu akasema...
ITAENDELEA SIKU YA KESHOOOOOOOOOO

No comments

Powered by Blogger.