ILIPOISHIA
“Manka
kwa nini ulinitenda?”
“Kivipi
mpenzi?”
“Vitu
hivi mbona hukunipa mwanzo?”
“Mpenzi
vilikuwa havijaungwa, hata vya chukuchuku havikuiva.”
“Hapana...hapana...sikubali.”
“Hukubali
nini tena mpenzi?”
“Siwezi
kula nisishibe heri nisipewe.”
“Mateja
leo utakula mpaka utasaza nipo kwa ajili yako.”
“Na
baada ya leo?”
“Mi
nipo tu.”
“Hapana..hapana
...lazima nikuoe.”
“Na
mchumba wako?”
“Wewe
ndiye uliyekuwa mchumba wangu.”
“Kama
nilikuwa mchumba wako kwa nini uliniacha?”
Huwezi kuamini wakati tukizungumza hivyo
kilimo kiliendelea huku Mateja akishinda kukaa chini kama kakalia moto.
TUSAPOTI KWA KUTEMBELEA HILI TANGAZO
“Vipi?”
Nilimuuliza huku nikimtazama usoni kwa jicho lilililegea kama mtu mwenye
usingizi mzito.
“Mm..mm..mmh,”
Mateja aligugumia kama dume la panya kwenye ghala la mahindi.
Baada
ya muda maskini mateja machozi yasiyo na kilio yalimtoka, niliyahifadhi
hakugusa chini.
“Asante
Manka...asante mpenzi.”
Mtoto
wa kike sifa hazikunivimbisha kichwa niliuchukua mpini na kuurudisha kwenye
jembe kilimo kiliendelea. Mmh, kweli kila kiumbe na sehemu zake, kurudisha
mpini kwenye jembe kulikuwa kama kumtupia samaki majini. Mateja alikuja juu
kama moto wa kifuu kila nilipotaka kumtuliza ndivyo raha zilivyogonga kila kona
ya mwili na kujikuta nikiwacha autawale mchezo.
Nilifika
kipindi duniani nikawa sipo mbinguni sipo nikawa naelea kati, nakiri sikujua
kilichokuwa kikiendelea zaidi ya kuhisi kama mtu kanivua nguvu zote mwilini
kilichoendelea sikujua. Niliposhtuka nilijikuta nimelala pembeni ya Mateja
ambaye alikuwa hajitambua kwa usingizi mzito.
Kilinichonishangaza
kujikuta sote tumo ndani ya shuka moja, nilijiuliza inawezekana Mateja ndiye
aliyenifunika. Nilipotaka kunyanyuka nilihisi kama kizungungu nilijirudisha
kulala. Wakati nataka kufumba macho nilisikia naitwa.
“Manka...Manka,”
niliposikiliza vizuri niligundua ni Bi Shuu.
“Abee.”
“Amka
ujimwagie maji.”
“Sina
nguvu.”
“Jitahidi
hivyo hivyo.”
Nilijinyanyua
kwa kuzilazimisha miguu ikiwa haina nguvu, nilijizoazoa na kwenda kujimwagia maji, Bi Shuu maji
alikwisha yapeleka bafuni. Nilioga maji yaliyokuwa ya baridi sijui aliyatoa
kwenye friji. Baada ya kujimwagia maji mwili ulichangamka kidogo, hapo ndipo
nilipoanza kuisikia njaa.
“Manka
kamuamshe na mwenzako naye akajimwagie maji ili mle pamoja”
“Kwa
saa ngapi sasa”
“Saa
sita kasoro.”
“Mtume!”
Nilikwenda
kumuamsha Mateja aliyekuwa akikoroma ilionekana kalinyekarinde lilimpeleka puta
na kujikuta akipoteza nguvu nyingi. Inawezekana kabisa alijua ni yule Manka wa
mwaka 47 na kuingia kichwa kichwa matokeo kanyolewa bila maji.
Kila
nilipomtikisa alionekana yupo hoi kwa kugeuka kama umekufa, niliendelea
kumtikisa.
“Mateja..Mateja.”
“Mmh.”
“Amka.”
“Niache
nilale kidogo.”
“Najua
umechoka, amka ujimwagie maji upate nguvu.”
“Manka
naomba nipumzike nimechoka sana.”
“Matejaaaa,
hebu amka.”
Nilimwambia
huku nikimshika mkono na kunyanyua, alinyanyuka na kukaa kitako kitandani.
Akiwa kama mtu aliyekunywa pombe ambayo ilikuwa bado kichwani, aliinama mkono
mmoja alishika kitandani na mwingine kichwani. Sikutaka kumpa nafasi nilimsimamisha
na kumfunga upande wa kanga.
Huwezi
kuamini nilivyokuwa nimechoka bila kuelekezwa na Bi Shuu nisingeweza kuyafanya
yale. Maji ya baridi niliyojimwagia ndiyo yaliyonipa nguvu, nilimshika mkono
mpaka bafuni ambako nilikuta tayari Bi Shuu ameisha tayarisha maji ya baridi.
Kwa
kuwa nilijua ubaridi wa maji Mateja
atauogopa nilipomtoa kanga nimwagia kwa kumshtukiza kama makopo mawili. Japo
alilalamika lakini alinieleza kweli maji yale yameupa tena nguvu mwili wake.
Alimuongeza maji mengine na kuufanya mwilini wake uchangamke zaidi.
Alipomaliza
kujimwagia maji ya baridi tulirudi ndani, sikuamini macho yangu kukuta Bi Shuu
amekwisha andaa chakula mezani kukiwa na kila kitu. Muda wa Mateja kujimwagia
maji, yeye aliutumia kuandaa chakula. Yaani sijui niseme nini, nimekutana na
watu wengi lakini Bi Shuu kiboko.
Japo
usiku ulikuwa mkubwa lakini mama wa watu hakulala alikwenda sambamba na mimi.
Kilichonishangaza baada ya mtinange na kupitiwa usingizi nilijiuliza yeye
alikuwa wapi? Kama sisi tulilala kwa zaidi ya masaa matatu yeye muda huo
alikuwa anafanya nini?
Mateja
baada ya kuona nilimsikia akisema.
“Manka
umejuaje kama nina njaa, maana hapa nahisi tumbo jeupe.”
Kwa
vile na mimi nilikuwa na njaa tulivamia wote mezani kukishambulia chakula
kilichokuwa kimepikwa kwa ustadi wa hali ya juu na Bi Shuu. Tukiwa mezani baada
ya kufunua kawa lililikuwa na maneno RAHA YA MUWASHO UKUNWE . Ajabu ya Mungu
kawa lile lilionekana jipya halijawahi kutumika, baada ya kulifunua harufu
nzuri ya chakula ilijaa puani mwetu. Nilimnawisha mikono kisha nilimkaribisha
kama nimepika mie.
“Karibu
mpenzi.”
“Asante,’”
Mateja alijibu huku akijipakulia kwenye sahani yake, wakati anaweka kijiko cha
kwanza nilisikia kitu kikigongwa dirishani. Ilionesha kuna kosa nimefanya.
Nilinyanyuka haraka huku nikisema.
“Samahani
dear nakuja,” nilitoka nje na kukutana na Bi Shuu.
“Vipi
Bi Shuu?”
“Manka
nilikueleza nini?”
“Kuhusu
nini?”
“Mwanaume
kama mtoto asiguse kitu kazi yote ifanye wewe.”
“Ulikuwa
una maana gani?”
“Asijipakulie,
mpakulie ikiwezekana hata vijiko vya awali mlishe kisha mwache ale mwenyewe.”
“Nimekulewa,”
nilimjibu bila kusubiri maelezo mengine kumuwahi Mateja asijipakulie zaidi.
Nilipofika nilikuta ndio anataka kuongeza kijiko cha tatu. Nilikidaka kijiko na
kusema.
“Mpenzi
kwa nini usumbuke wakati nipo.”
“Aah,
si kila kitu ukifanye.”
“Hapana
wewe ni mgeni wangu, kila kitu mimi ndiye dereva.”
“Haya
mama.”
Nilimpakulia
chakula cha kiasi kisha nilimuwekea mchuzi na kipande cha ndizi, tonge la
kwanza nililikusanya kisha nilimlisha huku nikiweka mkono chini ya kidevu
kuzuia punje ya wali isianguke. Baada ya kulisha nilimsubiri atafune ili
nimuongeze tonge lingine nami nianze kula. Baada ya kutafuna kwa muda
nilimsikia aliguna kitu kilichonitisha na kuwa na wasi wasi huenda chakula si
kizuri.
“Vipi
mpenzi?”
“Mmh,
chakula kitamu kweli kweli, sijawahi kula chakula kitamu kama hiki, kama
nikikuoa na kula hivi kila siku nitenenepa mlangoni nitakuwa sipiti.”
“Asante
mume wangu,” nilijibu makusudi, moyoni niliisifia kazi nzuri ya Bi Shuu.
“Manka,”
Mateja aliniita huku akivuta glasi ya maji iliyokuwa pembeni.
“Abee.”
“Manka
mbona leo naona kama nipo ndotoni?”
“Kivipi?”
“Mbona
siku za nyuma hukunifanyia mambo kama haya, mapenzi ya ukweli na chakula kitamu
kweli kweli.”
“Vimeungwa.”
“Una
maana gani?”
“Mateja
mimi ni Manka mpya.”
“Una
maana gani?”
“Ulichokiona
kazi kubwa ya Bi Shuu.”
“Bado
umeniacha njia panda Bi Shuu amefanya nini?”
Nilimuelezea
bila kumficha kazi kubwa ya Bi Shuu kuniunga na leo kuvionjwa akaviona vitamu.
“Upo
hapo baba?”
“Mmh,
nimekubali kweli aliomba likizo yenye mafanikio.”
“Basi
habari ndio hiyo.”
Baada
ya chakula tulirudi kuoga tena kisha tulipanda kitandani kulala hakuna
aliyekuwa na hamu na mwenzake tulipeana migongo mpaka asubuhi. Mlio wa dirisha
uliniamsha toka kwenye usingizi mzito, jicho langu lilitua kwenye saa ya
ukutani kunionesha ni saa kumi na moja alfajiri.
Nilijinyanyua
kivivu na kwenda hadi mlangoni kumsikiliza Bi Shuu alitaka kunielaza nini,
nilifungua mlango huku nikifikicha macho kutokana na kuzingirwa na usingizi
ulioambatana na uchovu wa mwili. Nilikumbuka usiku wa jana nilitumia nguvu
nyingi ili kumuonesha Mateja mimi ni nani.
Nakumbuka
kuna kipindi niliona kama chini nachochewa kuni jinsi moto ulivyokuwa ukiwaka.
Lakini nilikumbuka maneno ya Bi Shuu sifa kubwa ya mwanamke kwa mwanaume ni
uvumilivu na kutokukubali kushindwa mapema hata siku ya kwanza unapotaka
kuandika CV.
Baada
ya kufungua mlango nilikutana na Bi Shuu akiwa na upande wa shuka.
“Shikamoo
Bi Shuu.”
“Marahaba
mama Shughuli.”
“Mmh!
Bi Shuu jina gani tena hilo.”
“Kwani
uongo shughuli unaiweza, mwana wewe temea chini.”
“Aii
jamani,” nilijikuta nikiona aibu kwa kujua kila nilichokifanya Bi Shuu alikiona
‘live’ bila chenga.
“Sasa
Manka sicho nilichokuamshia, vipi ushampa cha alfajiri?”
“Kipi
hicho?”
“Ooh,
kweli hili sikukuelekeza, raha ya mapenzi ukilala na mwanaume mpe cha asubuhi
ili kiwachangamshe, kijasho kikiwatoka mkaoge mjiandae kwenda kazini.”
“Si
tutachoka sana.”
“Uchoke
nini, hiyo sawa na kuzimua baada ya kulala na hang over asubuhi ukizimua
unajiona sawa hata uzito wa kichwa unapotea sawa na kupata cha asubuhi.”
“Mmh!
Sawa wacha basi nifanye hivyo.”
Niliagana
na Bi Shuu na kurudi ndani, Mateja alikuwa bado amelala nilimshtua kwa kumpa
mshikemshike wa kuvamia shamba lake kwa kuufukua muhogo taratibu kitu kilichomshtua
kunikuta nipo shambani na tayari muhogo
nilikuwa nimeisha ufukua upo mkononi.
“Vipi
mpenzi?” aliniuliza kwa sauti ya usingizi.
“Kawaida
tu.”
“Niache
nilale nimechoka.”
“Kumekucha
mpenzi tunazimua kisha tunakwenda kuoga.”
ITAENDELEA KESHOOOOOOOOOOO
Post a Comment