ILIPOISHIA
“Mbona
hivyo mama yangu”
“Kazi
gani ya kutoka saa moja asubuhi kurudi saa tano za usiku?”
Mmh,
makubwa nimekuwa mtoto mdogo wa kuwa chini yake kwa kila kitu. Nilijua uchawi
wa Bi Shuu ni nini, niliinama na kuchukua mkoba wangu na kufungua. Nilihesa
nyekundu tano na kumpa.
“Za
nini?”
“Katumie
tu”
“Za
kodi?”
“Walaa,
nimekutunuku tu mama yangu.”
“Kweli!?”
“Kweli
unafili uliyonifikiza madogo”
Bi
Shuu alifurahi na kunikumbatia na kusahau aliyobwatuka muda mfupi, baada ya
kunipandisha na kunishusha alisema.
“Weee
mwana kulikoni”
“Kaa
chini nikupashe kazi imekuwa kaziiiii”
“Usiniambie”
“Habari
ndiyo hiyo shilingi moja kwa sekunde ndio mpango”
“Wacha
wee leo Mchaka kawa mzaramu”
“Umenifundisha
wewe, ngoja nikaoge nikupashe upashike”
Nilimuacha
Bi Shuu chumbani kwangu akizirudia kuzihesabu pesa nilizompa mimi nikaenda
kujimwagia maji.
Nilipotoka
kuoga nilimkuta akinisubiri kwa hamu kubwa.
“mmhu,
hebu nipe raha”
“Bi
shuu nitakueleza yote kesho”
“Mwana
wee siwezi kulala mpaka unipe siri ya rangi nyekundi kupendeza na kusikitisha”
Huku
nikijifuta maji nilimueleza yote bila kumficha hata moja, mwisho wa yote
nilielezea masikitiko yangu ya bahati ya kupendwa na mkosi wa kuachwa.
“Bi
Shuu, japo nimepata lakini wasiwasi wangu sichelewi kumwagwa”
“Kwani
una tatizo gani?”
“hata
silijui hakuna hata mwanaume mmoja aliyenieleza tatizo langu”
“Mmh,
kuna umuhimu wa kulifanyia kazi”
“Siamini
kama tatizo langu litaisha”
“Hebu
kila ukiwa na huyu bwana msikilie na muulize an apenda nini chochote usimnyime”
“mmh,
Bi Shuu wanaume wengine waharibifu ukimchekea anakuharibu”
“Sio
unavyo fikiria’
“Kuna
nini wanaume wanacho taka zaidi ya kuwaharibu wanawake, sijazaa babu wee cha
kuwekewa matambala”
“Sina
maana hiyo si wote wana penda mchezo huo.”
“mmh,
nitamsikiliza”
“Sasa
mwana wee lala nakuomba muheshimu mpenzio kama Mungu wako huoni muda si mrefu
nasi tutatembelea gari”
“Ndicho
ninachokiomba, sijui yatakuwa yale yale.”
“Basi
mwali lala usingizi unono.”
“Nawe
pia Bi shuu”
Bi
Shuu aliniaga na kuondoka na kuniacha nikimalizia kujifuta maji ili nilale.
******
Siku
ya pili wakati namalizia kujipodoa kabla ya kwenda kujifusha udi kwa Bi Shuu
simu ya Mateja iliingia, niliipokea na kuzungumza naye.
“Haloo
ma’ Sweet.”
“Ooh,
ma honey girl.”
“Ni
mimi, mhu baba nipe habari naona simu za asubuhi asubuhi?”
“Aah,
kawaida ila kuna dereva nimemtuma atakupitia muda si mrefu.”
“Hakuna
tatizo Sweet.”
Baada
ya Mateja kukata simu, kwa vile nilikuwa tayari nimeisha jipodoa nilikwenda
chumbani kwa Bi Shuu. Kabla ya kuingia nilikutana na moto uliokuwa ukinukia
vizuri, harufu ya asubuhi ile ilikuwa zaidi na ya jana yake
Niliingia
na kumkuta akiweka udi kwenye kitezo, aliponiona alitabasamu na kusema.
“Haya
mwali jifushe uwahi kazini.”
Niliinama
na kufunikwa shuka ili moshi wote wa harufu nzuri uishie kwenye nguo na
mwilini, baada ya muda alifunua shuka na kuninusa kama mbwa anayesaka chakula
jaani. Asikuambie mtu Bi Shuu havumi lakini yumo, mtu mzima lakini ovyooo.
“Umevaa
kufuri gani?” Bi Shuu aliniuliza swali ambalo sikufikiria kuniuliza.
“Nyeupe.”
“Hebu
nione.”
Mmh,
makubwa nilinyanyua gauni na kuiona nilikuwa nimevaa kufuli la mikanda
‘Bikini’.
“Mwali
ndio nini?” Bi Shuu alishtuka.
“Mbona
umeshangaa?”
“Unakwenda
kwenye starehe au kazini?”
“Kazini.”
“Sasa
mbona umevaa kufuri kama unakwenda kwenye kilimo cha mihogo.”
“Babu
weee kwenda na wakati.”
“Acha
ushamba vaa kufuri la kawaida, hilo kufuri unalivaa siku unayokutana na mpenzi
ukitoa nguo tu akiona anaingia kimuhemuhe.”
Mmh,
sikutaka kubishana naye nilirudi hadi chumbani kubadili kufuri, wakati namaliza
kuvaa honi ya gari ilipigwa nje nilijua
mtu aliyetumwa kunifuata amefika. Nilikimbilia chumbani kwa Bi Shuu
kumuaga.
“Bi
Shuu naondoka.”
“Umebadili
kufuri?”
“Ndiyo.”
“Hebu
nione.”
Nilinyanyua
tena gauni na kunitazama, nilikuwa nimevaa ya kawaida tena ya rangi nyekundu,
alipoiona alisema.
“Ewaaa,
sasa hapo ndipo nilipopataka.”
“Basi
nawahi kuna mtu ananisubiri hapo nje katumwa na mzee,” nilisema huku
nikiteremsha gauni ili niwahi nje.
“Wee
Manka ndio nini?”
“Vipi
tena Bi Shuu mwenzio nachelewa kazini.”
“Hebu
jifushe na hiyo kufuri linukie.”
Nilirudi
haraka na kuchutama kwenye kitezo kwa kulitanua gauni langu moshi wote uingie
chini. Baada ya kufanya yote niliyoelekezwa na Bi Shuu nilimuaga kwa kumbusu
kisha nilipitia mkoba wangu na kutoka nje. Nilimkuta gari likinisubiri,
niliingia kwenye gari na gari liliondoka.
“Mambo?”
“Poa,
sijui yako?”
“Hata
mimi ipo poa.”
Safari
iliendelea hadi ofisini, nilipofika nilipita moja kwa moja hadi ofisini kwa
Mateja, alivyokuwa ameisha ingia ofisini. Baada ya kufungua mlango wa ofisi
niliingia huku nikiachia tabasamu pana na kutanua mikono yangu, Mateja
aliponiona alizunguka meza yake kunipokea. Tulikutana katikati na kukumbatiana.
Tuliporomosheana
mabusu moto moto huku tukigandisha midomo kwa muda na kubadilisha mate.
“Mmh,
tosha,” nilisema huku nikijitoa mikononi kwa Mateja.
“Mhu,
za nyumbani?”
“Mmh,
mzuri sijui kwako?”
“Kwangu
ilikuwa ngumu kidogo kutokana na kuwa na wakati mgumu baada ya kukuota tupo
pamoja niliposhutuka nilijikuta nipo peke yangu.”
“Pole
sana, basi ndio ufanye haraka kunichukua.”
“Kwa
mateso ya jana kuna umuhimu wa kufanya hivyo.”
“Basi
mengine baada ya kazi.”
“Haya
mama, mimi niseme nini.”
Nilimbusu
tena na kurudi kuendelea na kazi yangu, baada ya kukaa kwenye kiti nilijikuta
nikikumbuka jinsi bosi wangu Mateja alivyochanganyikiwa na mimi.
Nilimbusu
tena na kurudi kuendelea na kazi yangu, baada ya kukaa kwenye kiti nilijikuta
nikikumbuka jinsi bosi wangu Mateja alivyochanganyikiwa na mimi. Pamoja na
furaha ile bado wasiwasi wangu ulikuwa nini hatima yangu kwake, nitaendelea
naye au ndiyo atanitosa kama waliotangulia.
ILIPOISHIA
Wazo
la awali lilikuwa kuomba msaada kwa Bi Shuu ili niweze kumdhiniti. Niliendelea
na kazi zangu kama kawaida, muda wa mchana tulikwenda kula pamoja kama wapenzi
wasiojificha.
Siku ile baada ya kurudi nyumbani aliniomba
tuwe wote usiku wa siku ile, sikumkatalia kwa vile ndiye aliyekuwa mmiliki wa
mwili wangu. Usiku alinipitia na
kuondoka kwenda kulala naye mpaka asubuhi, kaonja kaona tamu sasa anataka kula
kabisa. SASA ENDELEA.....
Ni
kweli nilifurahi kulala na Mateja mpaka asubuhi kuonesha jinsi gani
alivyopagawa kwangu, lakini usiku kwangu ulikuwa wa karaha sana yaani mambo
nisiyoyapenda ya kusumbuana wakati wa mapenzi yalijirudia tena. Nilishindwa
kumkatalia kwa vile alikuwa bosi wangu
kwa kuogopa kufukuzwa kazi na maisha ya kutangatanga yalinichosha. Usiku
mzima kugeuzwa kama chapati ooh geuka hivi, lala hivi fanya hivyo, basi kero
mtindo mmoja. Nilijiuliza bila kunisumbua vile hawezi kukidhi haja zake, mpaka
kunakucha nilikuwa nimekasirika mtoto wa kike kila kona ya mwili iliniuma
hayakuwa mazoezi bali adhabu ya mapenzi.
Asubuhi
Mateja alifurahi sana na kuniahidi kabla ya yote kukibadili chumba changu kwa
kuninunulia sofa za nguvu, alinipa pesa nyingi za kutumia na kunirudisha
nyumbani. Huwezi amini nilipofika nyumbani nilimkuta Bi Shuu akinisubiri,
kutokana na uchovu nilimsalimia na kuingia ndani nijilaze.
Kabla
sijabadili nguo na kuvaa kanga nyepesi Bi Shuu aliingia.
“Mankaaaaa,”
aliniita kimbea.
“Unasemaje
Bi Shuu,” nilimuuliza huku nikimuangalia jicho zito la usingizi.
“Mmh,
sikuwezi.”
“Kwa
nini Bi Shuu?”
“Mambo
yako mazito.”
“Mmh
kawaida tu, vipi ushakunywa chai?”
“Nilikuwa
nakusubiri wewe.”
“Mimi
kwa sasa hivi siwezi nimechoka sana.”
“Eeeeh
Manka weee, mlikuwa mnakomoana.”
“Wee
Acha tu,” niliona kama ananichelewesha kulala kutokana na umbea wake wa utu
mzima. Nilivuta pochi na kutoa noti kadhaa za kumi kumi na kumpatia Bi Shuu
bila kuzihesabu.
“Za
nini?”
“Za
kwako.”
Bi
Shuu alichanganyikiwa na kunivamia kwa furaha na kujitahidi kunibeba japo uzito
wangu ulikuwa mkubwa. Kweli pesa sabuni ya roho Bi Shuu alipagawa na kuniona
kama malaika niliyetumwa kuja kumpa furaha ya asubuhi ile.
“Bi
Shuu niache nipumzike.”
“Mwali
weee lala, tena utakutana nimekuandalia chakula kizuuuri.”
Bi
Shuu alitoka na kuniacha nikimalizia kuondoa nguo mwili kisha kuchukua kanga
nyepesi kisha kujitupa kitandani. Nililala kwa muda wa saa zaidi ya nane
kutokana na uchovu wa mbilinge za Mateja usiku kucha.
Majira
ya jioni Mateja alifanya kweli kwa kuleta sofa za nguvu kitu kilichofanya Bi
Shuu kunipa chumba kikubwa cha nyumba kubwa. Niliamini ule ulikuwa mwaka wangu
wa mimi kurudi katika maisha ya kutanua. Niliamini muda si mfupi lazima niwe na
gari langu mwenyewe.
Baada
ya kukipamba chumba changu na kupendeza Bi Shuu aliniweka chini na kunipa somo.
“Manka
Mungu akupe nini, ukishikwa shikamana mwali wee.”
“Hata
mimi najua Bi Shuu.”
“Unaonekana
mwanzo ulikuwa ukifanya makusudi mbona sasa hivi mwanaume kapagawa muda si
mrefu utakuwa dunia ya wenye nazo.”
“Ndio
maana yake.”
“Basi
Manka nitakuongezea vikorombwezo akigusa amenata.”
“Usiniambie!”
“Kwanini
wazee wenzangu pamoja na umri wangu wakionja wanapagawa itakuwa wewe ukioga
maji yanatelemka.”
“Tena
kweli ufanye haraka maana ameisha tangaza ndoa.”
“Basi
hiyo kazi niachie.”
Mateja
alinipigia simu kuwa siku ile angekuja kulala ili jumatatu twende kazini pamoja
nami sikumkatalia. Kweli usiku alikuja kulala kwenye chumba changu kilichokuwa
na hadhi kubwa kwa mtu yoyote. Kama
kawaida ya usiku wa jana yake yalijirudi ya kusumbuliwa lala hivi geuka hivi
fanya hivi, basi taabu mtindo mmoja.
Na
siku ile nilivumilia lakini moyoni nilijisemea siku nyingine nitampasha kweli
wake hawezi kunigeuza kama mwanasesele na kunichezea apendavyo. Nikajikuta siyachukia mapenzi na kuyaona
kwangu ni karaha na si starehe, mwanaume alikuwa akipanda juu ya mnazi hashuki
mpaka nahisi kichefuchefu.
Niliamini
kabisa alitaka kunikomoa kwa vitu alivyonipa, kwangu sikuona mapenzi zaidi ya
mateso. Uvumilivu uliponishinda nilianza kuwa mkali kwa kumgomea kwa usumbufu
wake kwa kumueleza makavu kuwa sitaki kama hawezi kifo cha mende tuache.
Mateja
alinielewa na kustarehe bila usumbufu, nilishangaa kumbe anaweza kukwea mnazi
bila kujifunga kamba za miguu. Kilichonishangaza ndani ya mapenzi yetu
yaliyochukua miezi minne, Baadhi ya
mambo yalianza kutoonesha dalili zozote za kutimiza ahadi yake.
Siku
zilivyozidi kwenda mbele ndivyo uhusiano na Mateja ulivyozidi kulega, hata kuwa
pamoja baada ya kazi ikafutika kila muda alionekana yupo bize. Kitendo cha
kutokuwa karibu na Mateja kilimshtua sana Bi Shuu kwani hata vizawadi navyo
vilikatika. Siku moja aliniweka chini na kuniuliza.
“Manka
kulikoni?’
”Hata mimi sijui.”
“Manka
kila siku hujui wakati unaharibu.”
“Bi
Shuu unanilaumu bure.”
“Hivi
kama na huyu atakuacha unafikiri utampata nani?”
“Bi
Shuu nimejitahidi kwa kila ulilonifundisha nililifanya lakini matokeo yake ndio
hayo lazima kuna mkono wa mtu.”
“Manka
kuna kitu gani alichokipenda Mateja hukumpa?”
“Mmh,
kila kitu nimempa.”
“Kweli?”
“Kweli
kabisa, nikudanganye ili iweje.”
“Sasa
itakuwa nini?”
“Hata
mimi sijui, huu utakuwa ni mkosi tu”
“Basi
naomba kesho ukienda kazini niitie Mateja.”
“Mmh,
sijui kama atakuja, lakini nitafikisha ujumbe.”
Siku
ya jumatatu nilikwenda kazini kama kawaida huku nikifikilia jinsi ya kufikisha
wito kwa Mateja wa kuitwa Bi shuu. Hakuwa Mateja niliyekuwa namfahamu.
Ilionesha mapenzi yalikwisha kabisa. Kila alipoingia ofisini alinisalimia
lakini hakuna kilichoendelea.
Nilipomuuliza
alinijibu kwa kifupi “Nipo bize,” nilijikuta nikiiona kazi ngumu kama si Bi
Shuu ningeacha kazi kutokana na kujiona sina thamani tena kwa Mateja. Siku moja
roho iliniuma sana baada ya msichana mmoja kuingia ofisini kwa Mateja bila
kumuulizia kwangu kama ilivyokuwa kwa wateja wengine.
Niliacha
kazi zangu na kumfuata ndani, nilipoingia ofisini mbona lilinishuka mtoto wa kike. Niliwakuta
wamekumbatiana na Mateja huku midomo yao ikiwa imegandiana. Nilitamani ardhi
ipasuke inimeze, nilisimama kama sanamu nisijue cha kufanya, machozi yalinitoka
bila kizuizi, pamoja na kuniona hawakushtuka ndio kwanza walizidisha kutomasana
kimahaba. Niliona wazi kabisa penzi langu na Mateja limefika ukingoni.
Nilirudi
ofisini kwangu na kukaa chini kazi ilikuwa chungu nilijikuta nikilia peke
yangu, nilitamani kuondoka niiache kazi. Lakini niliyakumbuka maneno ya Bi Shuu
kuwa siku zote penzi tamu ni lile lisilo sukumwa ninalosukumwa lina kasoro.
Nikiwa
nimeinama nafuta machozi nilishtushwa na sauti ya Mateja.
“Manka.”
Bila
kuitika nilinyanyua uso kumuangalia huku kitambaa kikiwa karibu na macho kufuta
machozi. Mateja alikuwa amesimama mbele ya meza yangu akiwa ameshikana kimahaba
mmoja alimshika mwenzake mkono shingoni na mwanaume kiunoni.
“Vipi
mbona unalia?” Mateja aliniuliza kwa kunikujeli, sikumjibu niliendelea kufuta
machozi.
“Manka
huyu ndiye mke wangu mtalajiwa.”
Sikumjibu
niliinama chini na kulia kilio cha kwikwi ambacho Mateja na mpenzi wake
hawakukijali. Niliwasikia wakiondoka, niliwasindikiza kwa macho mpaka
walipotoweka, baada ya kutoweka machoni mwangu nilijikuta nikijiuliza nalia
nini kwani tukio lile halikuwa la kwanza upande wangu kutendewa.
Ni
kweli lazima moyo uniume kutokana na ahadi nzuri za Mateja ambazo nilijua
zitanibadilisha katika maisha yangu. Ndoto yangu ya mchana ya kumiliki gari na
nyumba iliyeyuka kama bonge la mafuta katika kikaango cha moto. Baada ya muda
Mateja alirudi na kunipita kuingia ofisini kwake bila kunisemesha jambo lolote.
Nilikumbuka
wito niliopewa na Bi Shuu wa kwenda kuzungumza naye juu ya matatizo yangu, kila
nilipotaka kumwambia moyo ulisita na kuamua kuipotezea tu. Muda wa kutoka nilijikuta
nikijikaza kike na kumueleza.
“Samahani
bosi.”
“Bila
samahani,” Mateja alinijibu kistaarabu.
“Bi
Shuu alikuwa anakuita.”
“Bi
shuu naye ana shida gani tena?”
“Hata
sijui.”
“Mmh,
yule bibi na umri wake yuko vile wakati wa usichana wake alikuwaje?”
“Mmh,
sijui.”
“Basi
mwambie nitamtembelea wikiendi.”
Jamani
kauli ya Mateja ilinipa matumaini labda atarudisha moyo wake, siku zote
nilimuamini Bi Shuu kwa maneno yake matamu yaliyojaa misemo nahau na methani
ili kumlainisha mtu.
“Jamani
bosi kwa nini usiende leo?”
“Manka
nipo bize sana atanisamehe, lakini mwambie sijamdharau nitaitikia wito wake.”
ITAENDELEA SIKU YA KESHO
Post a Comment