ad

ad

DANCE 100 WAPEWA SOMO NA BASATA‏

 
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu,akiongea na vijana wanaoshiriki katika robofainali ya  Dance 100 wakati wa semina iliyoanandaliwa na EastTV kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la sanaa(BASATA) shindano hilo limedhaminiwa na Vodacom Tanzania ambapo vikundi 16 vimeingia robo fainali itakayoanza Agosti 23 na kikundi kitakachoshinda katika shindano hilo kitajinyakulia kitita cha shilingi milioni 5.
 
Washiriki wanaoshiriki katika robofainali ya  Dance 100 wakiwa katika picha ya pamoja na majaji wa shindano hilo Queen Darleen na Super Nyamwela wakati wa semina iliyoanandaliwa na EastTV kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la sanaa(BASATA) shindano hilo limedhaminiwa na Vodacom Tanzania ambapo vikundi 16 vimeingia robo fainali itakayoanza Agosti 23 na kikundi kitakachoshinda katika shindano hilo kitajinyakulia kitita cha shilingi milioni 5.
 
Mmoja wa Majaji wa shindano la Dance 100,Super Nyamwela akisalimiana na washiriki wa shindano hilo walioingia robofainali wakati wa semina iliyoanandaliwa na EastTV kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la sanaa(BASATA) shindano hilo limedhaminiwa na Vodacom Tanzania ambapo vikundi 16 vimeingia robo fainali itakayoanza Agosti 23 na kikundi kitakachoshinda katika shindano hilo kitajinyakulia kitita cha shilingi milioni 5.
 
Washiriki wa shindano la Dance 100 wanaounda kundi la Wazawa crew toka Temeke jijini Dar es Salaam wakipitia mkataba wakati wa semina iliyoanandaliwa na EastTV kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la sanaa(BASATA) shindano hilo limedhaminiwa na Vodacom Tanzania ambapo vikundi 16 vimeingia robo fainali itakayoanza Agosti 23 na kikundi kitakachoshinda katika shindano hilo kitajinyakulia kitita cha shilingi milioni 5.
 
Washiriki wa shindano la Dance 100 wanaounda kundi la Best Love toka Temeke jijini Dar es Salaam wakipitia mkataba wakati wa semina iliyoanandaliwa na EastTV kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la sanaa(BASATA) shindano hilo limedhaminiwa na Vodacom Tanzania ambapo vikundi 16 vimeingia robo fainali itakayoanza Agosti 23 na kikundi kitakachoshinda katika shindano hilo kitajinyakulia kitita cha shilingi milioni 5.
 
Waratibu wa shindano la Dance 100 kutoka kushoto Bhoke Egina na Happy Shame wakihakiki ujazaji wa mikataba ya washiriki wa shindano hilo wakati wa semina iliyoanandaliwa na EastTV kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la sanaa(BASATA) shindano hilo limedhaminiwa na Vodacom Tanzania ambapo vikundi 16 vimeingia robo fainali itakayoanza Agosti 23 na kikundi kitakachoshinda katika shindano hilo kitajinyakulia kitita cha shilingi milioni 5.
Na Mwandishi Wetu
WASANII wa vikundi 16 vilivyoingia hatua ya robo fainali ya mashindano ya 'Dance 100%' yaliyoandaliwa na EATV na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, wametakiwa kuwa wabunifu zaidi katika kucheza mitindo mbalimbali kama wanavyofanya wasanii wa nchi za nje.
Hayo yamesemwa leo/ jana na mmoja wa  majaji wa shindano hilo, Hassan Mussa (Super Nyamwela) wakati wa semina iliyokuwa ikitolewa na Baraza la sanaa la Taifa(BASATA) jinsi ya kuwapiga msasa wasanii walioingia robo fainali ya mashindano hayo.
Mussa alisema ni wakati wa kila dansa kuwa mbunifu kama wanavyofanya wasanii wa nje  na kuacha kung'ang'ania mtindo mmoja.

"Wasanii wenzangu inabidi twende na wakati, tujitahidi kuwa wabunifu wa mitindo badala ya kukalia tu mtindo mmoja maana kuna mitindo mingi ambapo tukiwa wabunifu tutaweza kufaidika nayo katika kutufikisha mbali zaidi katka tasnia yetu,"alisema Mussa.

Naye mratibu wa mashindano hayo, Happy Shame alisema semina hiyo imeandaliwa ili wasanii wa vikundi 16 vilivyoingia robo fainali waweza kuelezwa vigezo vinavyotumika kuwapata washindi na pia kuwafahamu majaji.
Shame alisema semina kama hiyo itakuwa ikifanyika kila hatua inayoendelea ili kuwafanya washiriki kuwa kitu kimoja na pia kuwapa uelewa zaidi wa mashindano hayo.

Alisema hatua ya robo fainali ya mashindano hayo itafanyika Agosti 23,mwaka huu kwenye ukumbi wa Don Bosco Oysterbay na washiriki wa vikundi sita wataaga rasmi huku washiriki wa vikundi 10 wakiingia nusu fainali.
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu alisema lengo la kudhamini mashindano hayo ni kwa ajili ya kuwapatia ajira vijana kupitia katika tasnia hiyo.Nkurlu alisema ni vema na makampuni mengine yakaiga mfano huo wa kuwakomboa vijana kwa kuwapatia ajira kupitia kwenye vipaji vyao.
"Ni vema tukaisapoti serikali katika suala zima la ajira kwa vijana na ndiyo maana tumeamua kudhamini mashindano haya,"alisema Nkurlu.
Naye Afisa Matukio wa Basata, Kurwijira Maregesi aliwaasa washiriki  wote kuhakikisha vikundi vyao vinasajiliwa ili kuweza kikidhi viwango vya kufanya kazi kimataifa na kudumu badala ya kuwa vikundi vya mashindano tu.
Mwisho.

No comments

Powered by Blogger.