ad

ad

‘SOMETIMES’ UONGO UNAHITAJIKA KWENYE MAPENZI!

  KILA kukicha kunaibuka mambo mapya. Katika ulimwengu wa mapenzi kila siku lazima uwe mwanafunzi ili uweze kuboresha uhusiano wako. Ukiacha ubongo wako uingize vitu vipya ni rahisi kubadilika na kuwa wa kisasa zaidi.
 
Somo la leo linashangaza kidogo lakini ni vizuri kama tukijifunza. Tumezoea kusikia kuwa uongo ni kitu kibaya katika maisha ya mwanadamu – ni kweli. Uongo si mzuri lakini katika uhusiano na mapenzi, wakati mwingine unanafasi na unaboresha sana uhusiano.
Kwa kawaida uongo unakatazwa kuanzia kwenye mafundisho ya dini na hata katika jamii. Mtu muongo si mwaminifu. Hakubaliki.
Hata mwanasiasa ambaye ni muongo, wapigakura wake hawamchagui tena atakaporudi mara ya pili; kwa nini? Kwa sababu aliwaongopea.
Hiyo ni kweli kabisa, lakini hapa katika Let’s Talk About Love nataka kukupa kitu kipya kabisa ambacho hujawahi kukipata mahali popote; uongo mtamu!
Ndiyo! Kuna uongo mzuri tena wenye faida na utakaokusaidia kukuza upendo wako kwa mwenzi wako. Ni suala la kukubali kujifunza tu. Karibu darasani tujifunze...
 
UDANGANYIFU
Rafiki zangu, sitaki kueleweka vibaya katika hili lakini kama nilivyosema mwanzo, uongo si kitu kizuri kwenye jamii. Mtu anayedanganya hakubaliki. Kwa tafsiri ya haraka, mwongo si mwaminifu.
Haaminiki kwa sababu ni rahisi kutunga mambo ambayo hayapo na akayatengenezea mazingira yakaonekana ni ya kweli. Huyu hafai hata kidogo. Lakini rafiki zangu, katika uhusiano upo uongo ambao unakubalika kama nilivyosema.
Nasema unakubalika maana una lengo la kutengeneza uhusiano, kuufanya uendelee kuwa na nguvu na si kuupoteza.
Huo ndiyo uongo unaokubalika. Kabla sijaenda mbele zaidi hebu twende tukaone kwanza tofauti ya uongo mzuri na mbaya halafu tutaendelea na darasa letu.
 
UONGO MZURI
Haikubaliki hata mara moja kumdanganya mpenzi wako kuhusu taarifa zako muhimu. Nasema hivyo kwa sababu utakuta mwingine anafanya kazi mahali fulani, lakini kwa sababu ya kutaka ukubwa anadanganya kwamba anafanya kwenye taasisi fulani kubwa.
Huo ni ulimbukeni ambao hauna maana. Mweleze mwenzi wako ukweli, ukifanya hivyo atakuwa anajua yupo na mpenzi wa namna gani. Una sababu gani ya kumdanganya mwezi wako?
Wapo wanaodanganya wanatoka katika familia zenye uwezo mkubwa kifedha, huku wengine wakijipachika majina ya koo maarufu ili waheshimiwe na wapenzi wao, huo ni utumwa, mbaya zaidi kuna siku ukweli unajulikana halafu unabaki na aibu zako.
Ndugu zangu, katika maisha ya kila siku ni vyema ukawa mkweli kwa watu muhimu wanaokuzunguka hasa mtu ambaye unatarajia awe mwezi wa maisha yako. Utaficha mpaka lini wakati kuna siku atagundua ukweli? Kuwa mkweli.

UONGO MZURI
Naam! Upo uongo ambao unakubalika rafiki zangu. Unajua kuna baadhi ya mambo ukiyasema kwa usahihi kama yalivyo yanaweza kuleta athari kwenye uhusiano, ndiyo maana nimesema kwamba upo uongo unaokubalika.
Inawezekana umefanya kitu ambacho hakimpendezi mpenzi wako, ama kwa kujua au kutokujua, lakini baada ya kuhisi labda amegundua na kukuuliza, unakataa. Ukikubali kwa kitu ambacho hakipendi inaweza kusababisha penzi kuvunjika.
Unabaki kuwa uongo mzuri kwa sababu kwanza una lengo la kulinda penzi, lakini pia hauna madhara kwa mpenzi wako. Huo ndiyo uongo mzuri ninaouzungumzia hapa.
 FUNGUA ubongo wako sasa, maana muda wa kujifunza kuhusu uhusiano na mapenzi umewadia. Huwezi kukwepa kujifunza, ukifanya hivyo utabaki na mawazo yaleyale kila siku.
 
Inawezekana kwa uelewa wako kuna mambo ambayo unayafahamu kuhusu mapenzi, lakini kwa kuwa mdau wa kona hii, unaongeza kitu kingine kipya kila siku.
Naam! Sasa nipo tayari kuendelea na mada yetu iliyoanza wiki iliyopita. Nazungumzia juu ya uongo wenye manufaa kwenye mapenzi. Rafiki zangu, nilipata wakati mgumu sana kwa kupokea changamoto mbalimbali kutoka kwa wasomaji wangu baada ya sehemu ya kwanza ya mada hii wiki iliyopita.
Nilibadilishana mawazo na wengi kwa kadiri muda ulivyoruhusu, lakini mwisho wa yote niliwashauri kwamba wavute subira hadi leo katika mwendelezo wake ambapo nina majibu ya maswali yote.
Hebu sasa twende tukaone uongo ambao unakubalika na hauna madhara zaidi ya kujenga uhusiano. Rafiki zangu, kuna wakati ukweli unaweza kuharibu!

WENZI WALIOTANGULIA
Nani amewahi kuwa mkweli kwa mpenzi wake mpya kuhusu idadi ya mapatna aliowahi kutoka nao kimapenzi?
Hebu anza na wewe mwenyewe? Jiulize, tangu umeanza mapenzi umetoka faragha na wanaume/wanawake wangapi? Je, upo tayari kumtajia mpenzi wako?
Umewahi kufanya hivyo? Rafiki zangu, kati ya mambo ambayo yanaudhi sana katika mapenzi ni pale mpenzi anapogundua kwamba mwenzi wake ni jalala, yaani ametoka na wapenzi wengi kabla yake.
Wengi wanatamani sana kusikia kwamba wao ni wa pili au tatu, vinginevyo akutane na mwanamke ambaye bado hajaanza kabisa mambo ya mapenzi. Rafiki zangu, tuwe wakweli, kumwambia mpenzi wako kwamba umeshatoka kimapenzi na wanaume hamsini, ni sawa na kumtangazia kwamba wewe ni mhuni uliyeshindikana.
Hata kama ni kweli umetoka na idadi hiyo, akikuuliza ipunguze, mwambie yeye ni mwanaume wako wa nne! Wa kwanza, alikutoa usichana ukiwa mwanafunzi, baada ya hapo ukaachana naye kabisa na mapenzi.
 
Mwingine ulikutana naye chuo, ukamuacha baada ya kugundua kwamba alikuwa akipenda kukutumia tu, wa tatu ulifuma meseji ya mapenzi kwenye simu yake ukaamua kumuacha, yeye ni wa nne!
Mwanaume huyo atajisikia fahari sana kuwa na mwanamke mwenye namba ndogo ya wanaume aliotembea nao, ingawa moyoni mwako unaujua ukweli, lakini inabidi udanganye ili kulinda penzi lako. Tupo pamoja jamani?

UGOIGOI FARAGHA
Ukiwa na mpenzi wako, si ajabu katika mazungumzo yenu ya kawaida, akakuuliza kuhusu uwezo wako wa kucheza ‘ligwaride’ muwapo faragha. Kwa bahati mbaya kuna rafiki wenye matatizo ya hapa na pale faragha.
Baadhi ya wanawake husumbuliwa na tatizo la maumivu wakati wa tendo, kuchelewa kufika mshindo na hivyo kuachwa njiani au kupoteza hamu ya tendo.
Wanaume wao husumbuliwa na tatizo la kufika mshindo mapema, kushindwa kurudia tendo na kuchoka mapema wakati mwenzake akiwa bado angali anamuhitaji.
Kimsingi matatizo makubwa hapa husababishwa na utayari wa kisaikolojia, maandalizi duni n.k. Unapozungumza na mwenzako kuhusu hili, hutakiwi kumpa taarifa za kweli.
Zipo athari kadha wa kadha za kuwa mkweli juu ya matatizo uliyonayo katika eneo hili. Kubwa zaidi, unajiongezea tatizo, maana utakuwa unaingia uwanjani ukiwa unajua kabisa kwamba mpinzani wako anajua udhaifu wako hivyo ni rahisi kukushinda!
Matatizo ya aina hii hutibiwa zaidi na mtu mwenyewe, kugundua udhaifu wake na kuufanyia kazi. Kama umegundua kwamba unapata maumivu wakati wa tendo, ni wazi kwamba maandalizi si ya kutosha, dawa yake hapo ni kutumia muda mwingi katika maandalizi kabla ya kuanza kazi yenyewe.
Kueleza tatizo lako moja kwa moja, kutamfanya mwenzako awe na mawazo, akiamini kwamba ama hutaendana na kasi yake, hatakufurahisha au utamuacha njiani. Kwa mtazamo huo ni rahisi sana kufikiria kuachana na wewe ili akatafute anayeendana naye.

CREDIT: Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Saikolojia ya Uhusiano.

No comments

Powered by Blogger.