BEYOND LOVE- (ZAIDI YA MAPENZI) SEHEMU YA 20 MPAKA YA 39
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond Love -21
Tom au Papaa Bill kama alivyojulikana na wengi
amekuwa tajiri mkubwa sana nchini Tanzania, pamoja na utajiri wake amejikuta
akiwa mtu wa starehe kupita kiasi. Hakuona tabu kutumia fedha nyingi katika
sterehe. Alidhamini Bendi nyingi za muziki jijini Dar es Salaam kwa kutumia
fedha ili kulinda heshima yake!
Siku moja katika uzinduzi wa Albamu mpya ya Kigingi
Music Band, ndani ya Ukumbi wa 56 Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Tom
alikutana na kitu ambacho kiliuvuruga
ubongo wake kwa muda! Macho yake yalikutana na msichana mrembo sana !
Huyu ni Mayasa, binti wa Mbagala jijini Dar es
Salaam, anayejua kila aina ya utundu. Tom akaapa kuondoka naye, hakujua kama
Mayasa naye alikuwa akimtega.
Je, nini kitatokea? Tom ataondoka na Mayasa? SONGA
NAYO.....
Tom alibaki kimya kwa nukta kadhaa akizidi
kumkodolea macho Mayasa ambaye kwa wakati huo vituko ilikuwa sawa na kiitikio
kwenye nyimbo za Muziki wa Kizazi Kipya! Alihisi mapigo ya moyo wake
kubadilika, alishasahau kwamba alikuwa jukwaani na alitakiwa kuwatambulisha
wanamuziki wapya kutoka nchini Congo . Mayasa alishajua udhaifu wa Tom,
alichokifanya ni kugeuka nyuma kisha akaanza kutembea kwa mwendo wa madoido
akiacha sehemu kubwa ya miguu yake mizuri ikionekana kwa nyuma.
“Duh! Jamani hivi huyu mwanamke yupo katika dunia
hii hii ya siku zote au ameshuka? Huyu lazima nitumie fedha zangu,” Papaa Bill
akawaza kisha kwa taabu akajitahidi kuanza kuzungumza kwenye kipaza sauti.
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
“Samahanini sana kwa ukimya wa muda mfupi uliojitokeza, unajua nilikuwa nawaza ni kiasi gani tutakuwa na mashabiki wengi katika hii bendi yetu, wanamuziki niliokuja nao kutoka Congo ni wakali sana na bila shaka watafurahia mazingira ya Tanzania .
“Mimi sitakuwa na mengi sana ya kuzungumza, acha
nimpishe Kiongozi wa Bendi, Abuu Sekidevi awakaribishe ili wapenzi wa bendi
yetu wawaone,” Tom au Papaa Bill akasema kisha akakabidhi kipaza sauti kwa Mc
wa siku hiyo.
Watu wakashangalia sana . Abuu ambaye alikuwa ndiye
Kiongozi wa Bendi, akapewa kipaza sauti na kuwakaribisha wanamuziki wapya
kutoka Congo . Walishangiliwa sana .
“Kuna binti alikuwa amesimama pale, mzuri-mzuri hivi, mweupe sana ni wa wapi?”
Tom akamuuliza Jomba ambaye alikuwa mpambe wake.
“Yupi?”
“Alikuwa amesimama pale na wenzake!”
“Amevaa nguo za rangi gani?”
“Gauni jepesi!”
“Aaah! Nilimuona, vipi kwani?”
“Kanidatisha!”
“Kakudatisha?!”
“Ndiyo mkubwa, sasa ustaarabu unakuwaje?”
“Kwa mara ya kwanza nakuona ukianza kuzungumzia
wanawake wa nje ya mkeo!”
“Ni kweli lakini leo nimezidiwa, lazima nikubali,
sina ujanja!”
“Sasa vipi unamtaka?”
“Tena haraka sana !”
“Nipe dakika kumi tu!”
“Kweli?!”
“Nkuhakikishia!”
“Poa kaka, nakuaminia!”
“Ni kazi ndogo sana kwangu, msubiri sasa hivi
anakuja kukaa na wewe meza moja, hayo mambo mengine nakuachia wewe!”
“Mambo gani tena?”
“Kumuimbisha!!”
“Sitazungumza kitu, fedha itanisaidia!”
“Nakuamini kaka!”
Jomba akaondoka akiwa anatembea kwa mbwebwe sana ,
alikuwa na uhakika wa kurudi na Mayasa, siyo kwa sababu anajiamini, bali
alikuwa anamfahamu vizuri sana Mayasa. Siku zote msichana huyo alijua fedha na
siyo mapenzi ya kweli.
Hakutembea sana , akakutana na Mayasa akiwa na
kampani yake, akasimama mbele yao . Akatabasamu. Mayasa hakupata shida sana
kujua kuwa Jomba alikuwa mpambe wa Papaa Bill. Alichokifanya na yeye ni
kutabasamu.
“Mambo vipi warembo?” Jomba akasalimia.
“Poaaaaa....” Wote wakaitikia.
“Naona mpo!”
“ Kama unavyotuona!”
“Samahani mrembo, naweza kuzungumza na wewe
kidogo?” Jomba akamwambia Mayasa.
“Kuna nini tena?”
“Nisikilize kwanza, mbona unakuwa na wasiwasi kiasi
hicho?”
“Siyo wasiwasi, ni vyema nikajua hata dondoo
kwanza!”
“Ni ujumbe wako!”
“Poa!” Mayasa akakubali. Wakaenda pembeni
kuzungumza.
“Unamfahamu Papaa Bill?”
“Namsikia, kwani vipi?”
“Amesema nikuite!”
“Anataka nini?”
“Mtoto wa kike vipi? Mbona unakuwa na mashaka,
twende umsikilize anasemaje?” Jomba akamwambia Mayasa ambaye hakubisha zaidi.
Wakaongozana hadi kwenye meza aliyokuwa amekaa Papaa Bill.
Tom alipomuona alichanganyikiwa, kwanza hakuamini
kabisa kwamba Jomba alifanikiwa kumleta Mayasa. Msichana huyo akakaa kwenye
kiti akitabasamu kwa manjonjo ya kimahaba.
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
“Karibu mrembo!”
“Athante!” Mayasa akaitikia akijitahidi kuubana
ulimi wake kwa mapozi ya kimahaba.
“Unatumia kinywaji gani?”
“Wine!”
“Sawa mwite Mhudumu akuletee!”
Muda mfupi baadaye Muhudumu alifika ambapo
alimletea Mayasa wine aliyokuwa akiihitaji. Wakaanza kunywa pamoja. Papaa Bill
alijikuta akishindwa kuzungumza kitu. Baadaye Mayasa akamwomba Papaa Bill,
awaite marafiki zake ili wajumuike pamoja.
“Wako wapi?”
“Kulee!” Mayasa akasema akisonza kidole chake
kuonyesha mahali marafiki zake walipo.
“Nenda kawaite hakuna tabu!”
“Hapana!” Jomba akadakia.
“Kwanini?” Papaa Bill akauliza akiwa na hofu sana .
“Acha niende nikiwalete mwenyewe. Si wale
niliokukuta nao?”
“Ndiyo!”
“Acha nikawalete!”
“Poa!” Wakakubaliana.
Jomba akaondoka na kwenda moja kwa moja kuwaita
wale marafiki zake na Mayasa. Muda mfupi baadaye, wakafika pale na kuketi
pamoja, wakaagiza vinywaji na kunywa pamoja.
“Unajua muda wote huo tumekaa pamoja hapa, lakini
hatujafahamiana!” Tom akasema akitabsamu.
“Lakini sisi tunakufahamu!”
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Naitwa nani?”
“Papaa Bill a.k.a
Nyamihela!” Mayasa akasema.
“Hamjakosea, lakini mimi siwafahamu!”
“Kabla hatujakuambia majina yetu, huyu rafiki yako
anaitwa nani?”
“Labda mwenyewe aseme!” Tom akajibu.
“Mimi ni Jomba warembo!”
“Mjomba?!” Mayasa akauliza akitabasamu.
Siyo Mjomba, nimesema Jomba!”
“Ooh! Hapo sasa nimekupata...miye naitwa Mayasa,
hawa marafiki zangu ni Angela na Monalisa!”
“Vizuri sana
, sasa tunaweza kuendelea kuburika hadi tutakapotosheka!” Tom au Papaa Bill
alisema akitabsamu.
Kama Tom alivyosema, kilichofuata baada ya pale
ilikuwa ni kula na kunywa kwa kasi ya ajabu sana . Muda ukazidi kwenda, wakiendelea
kunywa na kula, hadi ilipofika usiku wa saa tisa na nusu. Wakati huo Tom
alikuwa ameshachangamka! Hakuwa na aibu aliyokuwa nayo awali.
“Mayasa....” Tom akaita.
“Abee!” Sauti ya Mayasa ilisikika, ilimchanganya sana Tom ambaye hakumini kama alikuwa akiisikiliza sauti ya Mayasa.
Kwa hakika mapenzi yalishauteka moyo wake,
alishindwa kuelewa ni kwanini alijikuta akimpenda Mayasa kiasi kile. Tom
akazama katikati ya dimbwi la mawazo, akasahau kwamba alikuwa akizungumza na
Mayasa.
“Papaa nakusikiliza...” Mayasa akamzindua Tom
katikati ya mawazo.
“Sorry kuna kitu kilikuwa kinanichanganya kidogo!”
Papaa Bill akasema.
“Ni nini?”
“Mambo ya biashara zangu!”
“Pole, lakini watu kama
nyie ni lazima muwe hivyo!”
“Ni kweli kabisa!”
“Enheee....nakusikiliza!” Mayasa alionekana kuwa na
hamu sana na
alichokuwa akitaka kuzungumza Tom.
“Hebu tusogee pembeni kidogo!”
“Sawa!” Wakasogea pembeni kwenye mwanga hafifu.
“Sikiliza Mayasa, sina sababu ya kuzungumza maneno
mengi, mimi nina pesa na nimezunguka kila mahali, lakini sijawahi kukutana na
mwanamke mzuri kama wewe, amini kwamba
nimetokea kukupenda ghafla sana
. Tafadhali naomba unipe moyo wako, nakupenda sana !” Tom akasema kwa hisia kali sana za mapenzi.
“Papaa unasema kweli?” Mayasa akasema akimtizama
Tom kwa macho yaliyojaa matamanio ya mahaba.
“Niamini!”
“Papaa, unajua nyie wenye pesa, hamuwezi kuvumilia
kuwa na mwanamke mmoja, akitokea mwanamke mwingine mzuri zaidi yangu, unaniacha
na kwenda naye.” Mayasa akasema.
“Siyo Papaa Bill, mimi ni wa tofauti kabisa na matajiri
wengine unaowajua!”
“Kweli unanihakikishia sitaumia?”
“Nakuhakikishia!”
“Sawa!” Tom akamsogelea Mayasa wakakumbatiana.
Kitu cha ajabu ni kwamba, Mayasa alionekana kama alikuwa na uhusiano na Tom kwa muda mrefu sana . Haraka aliusogeza
ulimi wake ndani ya kinywa cha Tom, wakaanza kubadilishana mate!
“Bill nakupenda sana !”
“Hata mimi pia, sasa baby sioni kama
kuna sababu ya kuendelea kuwepo hapa, twende zetu!” Tom akasema.
“Kwenda wapi?”
“Kupumzika!”
“Ni mapema sana
Papaa Bill!”
“Hapana Mayasa, leo ni siku yetu, naomba tutumie
usiku huu kufungua ukurasa mpya wa mapenzi!” Tom akazidi kumshawishi Mayasa.
“Sawa!” Mayasa akamjibu.
“Ahsante sana
dear!”
Wakashikana mikono na kwenda walipokuwa wamekaa
rafiki zake Mayasa na Jomba, wakawaaga.
“Jomba tutaonana kesho, mimi naondoka na mrembo
wangu, stareheni salama!” Tom akasema akitoa noti ishirini za elfu kumi-kumi.
“Hizi zitawasaidia kwa ajili ya vinywaji na nauli!”
“Poa kaka!” Jomba akashukuru.
Tom akamshika mkono Mayasa na kwenda zao hadi alipoegesha
gari lake, wakaingia. Tom akawasha gari,
wakaondoka maeneo ya Kinondoni. Walikuwa wanaelekea Ubungo katika moja ya
hoteli nzuri ya kifahari. Tom alipanga kumsaliti mkewe Mariam kwa mara ya
kwanza. Alilemewa na mapenzi mazito kwa Mayasa.
“Nitahakikisha natumia kila njia awe wangu wa moja
kwa moja, hapo ndipo nitakapopata nafasi ya kuchuma ninavyotaka. Nani ampende
huyu mjinga? Shida yangu ni mali
tu, na wala siyo mapenzi!” Mayasa aliwaza wakiwa njiani kuelekea hotelini.
Je, nini kitatokea? Mayasa atafanikiwa kumteka Tom
na kuchuma mali
zake kama anavyotamani? Usikose
Beyond Love- 22
Hata hivyo, Mayasa anajisemea moyoni mwake kwamba, hana
mapenzi na Tom na anajihakikishia kutumia kila njia ili aweze kuchuma sehemu ya
utajiri wake. Je, atafanikiwa? Nini nkitatokea? SONGA NAYO...
Tom haamini kama msichana
aliyekaa pembeni yake ndani ya gari lake alikuwa Mayasa. Hata yeye
alijishangaa, kwani hakuwahi kupenda kama alivyompenda Mayasa. Msichana huyo
alimwingia akilini mwake kwa kasi ambayo hata yeye mwenyewe alishindwa kupata
majibu kila alipojiuliza.
“Yaani sijawahi kupenda
katika maisha yangu kama ninavyompenda Mayasa, huyu mwanamke ameniingia hadi
mimi nashangaa, sijui kuna nini bwana? Lakini hata hvyo ni mzuri sana, naamini
uzuri wake ndiyo unanizuzua.” Tom
akawaza wakati akiwa anashuka katika bonde lililopo eneo la Mkwajuni, Barabara
ya Kawawa, akiifuata barabara inayoelekea Magomeni.
“Papaa...” Mayasa akaita.
“Vipi baby?”
“Naona kama una mawazo, kuna
nini?”
“Hapana, hakuna tatizo, nipo
sawa kabisa!”
“Nahisi kuna kitu unajaribu
kunificha!”
“Hapana...”
“Sawa kama hakuna kitu lakini
nahisi kama kuna kitu kinakuchanganya akilini mwako, au unamuwaza mkeo?”
“Nimuwaze mke wangu wakati
nipo na wewe?”
“Kwani haiwezekani?”
“Nitakuwa mwanaume wa ajabu
sana.”
“Kwanini unasema hivyo Papaa
Bill?”
“Kama nilikuwa naona
ananifaa, ananitosha, ananiridhisha, ananivutia kwanini nihangaike kukusumbua?
Lakini kwasababu kuna mapungufu katika maeneo kadhaa ndiyo maana nimeona wewe
unaweza kusaidia kuziba hayo mapengo!”
“Kwahiyo mimi nipo na wewe
kwa sababu ya kuziba mapengo tu?!”
“Hapana...amini kwamba
nimekupenda lakini wakati huo huo, tambua kwamba nina mke. Wewe utakuwa na
nafasi yako kwangu na yeye atakuwa na nafasi yake, pia ni vizuri kila mmoja
akaheshimu nafasi ya mwenzake....hasa wewe...”
Tom alimwambia Mayasa akionyesha hana masihara kabisa na kilichokuwa
kikitoka kinywani mwake.
Pamoja na usaliti ambao
alikuwa anataka kumfanyia mkewe Mariam, lakini moyo wake ulikuwa na maumivu
makali sana. Hakutaka Mariam wake adharauliwe kwa sababu ya mwanamke wa nje,
tena aliyekutana naye Club.
Tom akaendesha gari kwa kasi
alipofika Morocco, kwenye makutano ya Barabara ya Uzuri na Kawawa ambayo alikuwa
anaitumia, alikata kulia na kuifuata Barabara ya Uzuri hadi Sinza Kijiweni
ambapo alikata kushoto kufuata Barabara ya Shekilango.
Kasi ya gari ilikuwa ni ile
ile, alibadilisha gia kila baada ya muda, hakuona haja ya kupunguza mwendo
kwenye matuta ya barabarani, alikuwa akipita kwa mwendo ule ule. Alipofika
kwenye mataa ya Shekilango, akakata kulia akifuata Barabara ya Morogoro ambapo
aliendesha gari hadi kwenye mataa ya makutano ya Barabara za Morogoro, Sam
Nujoma na Mandela, hapo alikata kushoto akiifuata Barabara ya Mandela.
Hakufika mbali sana, kabla ya
kufika River Side, akaingiza gari ndani ya geti jekundu, katika hoteli moja
nzuri sana. Moja kwa moja wakaenda hadi Mapokezi wakipitia mlango maalum,
akalipia chumba na kiupandishwa ghorofa ya nne kwenye chumba chake.
“Karibuni sana.” Mhudumu
akasema.
“Tunashukuru lakini zingatia
maadili ya kazi yako.” Tom akamwambia.
“Kwanini unasema hivyo bosi?”
“Nafikiri unanifahamu
vizuri!”
“ Ndiyo....”
“Ni nani?”
“Papaa Bill!”
“Sasa sitaki mtu yeyote ajue
kuwa nimelala hapa, nenda na hilo kichwani mwako!”
“Naheshimu na kuzingatia sana
maadili ya kazi yangu!”
“Usiku mwema!”
“Nawe pia.”
Tom aitumia muda mwingi sana
kumwangalia Mayasa ambaye alikuwa na sura na umbo la kuvutia sana. Msichana
hoyo, akipita sehemu yoyote ambapo kuna mwanaume asiye na matatizo yoyote
katika via vyake vya uzazi basi lazima asisimke.
“Hebu simama.” Tom akamwambia
Mayasa.
Mayasa akasimama.
“Zunguka nyuma!” Tom
akamwambia huku akitabasamu na kutingisha kichwa. Mayasa akafanya hivyo.
“Sasa simama upande upande!”
“Kwani vipi?”
“Nataka kukuona vizuri!”
“Kwani hukuniona?”
“Ndiyo maana nimesema
vizuri.”
“Sawa bwana!” Mayasa
akageuka, safari hii alikuwa akigeuka kwa mapozi, huku akipandisha gauni lake
na kuacha miguu yake wazi, ambayo ilianza kupandisha presha yake ya mapenzi.
“Hakika wewe ni mwanamke
mrembo sana, sema chochote unachotaka nikupe ili kuonyesha mapenzi yangu
kwako!” Tom akamwambia Mayasa akitabasamu.
Mayasa akamfuata mahali Tom
alipokuwa amekaa, akakaa na kupandisha mguu wake mmoja juu ya miguu ya Tom. Tom
akahisi shoti ya umeme ikipita mwilini mwake. Mayasa alikuwa mwanamke
aliyemchanganya sana ubongo wake.
Akasogeza kinywa chake karibu
kabisa na sikio la kuume la Tom, kisha akaanza kuzungumza kama anamnong’oneza;
“Ni kweli unanipenda Papaa?”
“Kwanini huniamini?”
“Siyo kama sikuamini Papaa!”
“Sasa kumbe nini?”
“Kama nilivyokuambia kule
Club, wewe ni mwanaume tajiri na maarufu, kila mtu anakufahamu, nitawezaje kuwa
na wewe kama sitanyang’anywa?”
“Mimi ndiyo mwamuzi, na ni
mimi ndiye niliyekupenda. Ndiyo maana nimekuwambia chagu chochote utakacho
nikupe ili kuonyesha penzi langu la kweli kwako!”
“Sawa, naona itakuwa vizuri
sana kama ukinihamisha nyumbani!”
“Una maana gani?”
“Naishi na wazazi wangu na
umri wote huu ni aibu sana, kwanza nina wadogo zangu wawili wa kike na wote
wanaishi na mabwana zao, nimebaki mimi tu, nyumbani kwahiyo naona itakuwa vyema
kama utanipangishia chumba!”
“Chumba au nyumba?”
“Utakavyoona mwenyewe Bill”
“Acha nikutafutie nyumba
nzima, kuhusu samani za ndani niachie mimi, kila kitu utakikuta ndani ya
nyumba!”
“Nitafurahi sana Papaa Bill!”
“Anza kufurahi kuanzia sasa!”
“Sawa mpenzi wangu.” Mayasa
akasema akicheka kwa sauti kubwa sana.
“Nilitaka kusahau, unataka
maeneo gani?”
“Utakayoona yanafaa!”
“Chagua mwenyewe!”
“Kinondoni au Mwananyamala.”
“Basi nipe muda mfupi sana,
haitazidi mwezi mmoja!”
“Sawa baby!” Baada ya hapo,
lugha ya Kiswahili haikutumika tena.
Hata hivyo lugha
iliyozungumzwa badala ya Kiswahili haikuwa Kiingereza, Kifaransa wala lugha
nyingine yoyote ambayo hutumika kama njia ya mawasiliano duniani. Walikuwa
wakizungumza lugha ya mapenzi!
*******
Pamoja na kwamba Tom alikuwa anapenda sana
starehe, haikuwahi kutokea hata siku moja, akaacha kurudi nyumbani. Siku hiyo
hadi kufikia saa tisa na dakika zake za usiku, Mariam alikuwa hajamtia machoni
mwake mumewe.
Siku zote alikuwa mtu wa
starehe sana lakini alipompigia simu alipopokea na kumweleza mahali alipo na
wakati mwingine hadi muda aliokuwa akitarajia kurudi nyumbani. Siku hiyo
ilikuwa tofauti sana, simu ya Tom ilikuwa haipatikani ka bisa!
“Masikini mume wangu, sijui
atakuwa amekumbwa na balaa gani tena, siyo kawaida yake kuwa hajarudi nyumbani
hadi muda huu, mbaya zaidi hata simu yake haipatikani,” Mariam akawaza akiwa
amejilaza kwenye sofa kubwa sebuleni akiwa hoi kwa uchovu akimsubiria mume wake
bila mafanikio.
Mapenzi yao sasa
yalibadilika, hayakuwa sawa na ilivyokuwa awali, mara nyingi Mariam aliishia
kulala mwenyewe nyumbani akiwa hana la kufanya. Hata alipotaka kutafuta kazi,
Tom alikataa akidai kuwa uwezo wa fedha alionao, haumruhusu yeye kufanya kazi,
kwani ana uwezo wa kumuachia fedha za matumizi kila siku bila matatizo.
Hakupata usingizi hadi
asubuhi akiwa yupo sebuleni akimsubiria mumewe, hadi kufikia saa mbili za
asubuhi, Tom alikuwa hajafika nyumbani, mawazo yakazidi kumjaa akilini mwake.
“Lazima nifanye jambo la
ziada hapa, natakiwa kwenda kutoa taarifa Polisi kwanza!” Mariam anawaza kisha
akaamua kwenda kubadilisha nguo haraka na kutoka nje.
Akiwa ndiyo kwanza, amewasha
gari, anasikia honi ikipigwa mlangoni. Mlinzi anafungua mlango, gari la Tom
linaingia na kuegeshwa pembeni. Mariam haamini macho yake. Alitegemea kumuona
Tom akiwa na huzuni kutokana na matatizo aliyohisi kuwa nayo, lakini alishuka akiwa na tabasamu pana.
Mariam akashuka garini, akiwa
ameyatuliza macho yake kwa Tom ambaye hakuonekana kuwa na chembe ya wasiwasi.
Akaingia ndani na kumuacha Mariam akiwa amesimama nje, ni jambo ambalo
lilichukua muda mrefu sana kuaminika akilini mwa Mariam.
Mariam akamfuata Tom ndani,
macho yake yakianza kupatwa na unyevunyevu na kubadilika rangi na kuwa mekundu.
Akamkuta Tom akiwa amejilaza kwenye sofa kubwa.
“Vipi Tom mume wangu?”
“Salama, za tangu jana?”
“Mimi ndiyo natakiwa
kukuuliza wewe!”
“Ooooh! Hivyooeh....mimi
mzima, sina matatizo!”
“Lakini ulilala wapi?!”
“Kitandani!”
“Hayo ndiyo majibu gani Tom?”
“Nimekwambia nimelala
kitandani!”
“Eti?”
“Hujasikia au hujapenda?
Halafu we’ mwanamke...naona sasa unataka kunipanda kichwani, tafadhali naomba
uniache, usipende kufuatilia sana mambo yangu!” Tom akasema kwa sauti kubwa
iliyoonyesha kujaa hasira.
Mariam hakuwa na kitu kingine
cha kuzungumza zaidi ya kwenda kujifungia chumbani, alichokifanya huko ilikuwa
ni kulia akiamini alikuwa anapunguza hasira zake.
Tom ameshaanza kubadilika, sasa ameanza tabia ya kulala
nje na anarudi nyumbani bila woga kwa mkewe.
Beyond Love- 23
Upande wa pili, Mariam
anakuwa na wasiwasi sana kutokana na mume wake kutorejea nyumbani, usiku mzima
anaweweseka sebuleni akilia. Asubuhi Tom anarejea lakini alipoulizwa kwanini
hakurejea nyumbani alitoa majibu ya hovyo.
Mariam hakuwa na kitu
kingine cha kufanya zaidi ya kurudi chumbani na kuanza kulia. Je, nini
kitatokea? SONGA NAYO...
Machozi ya Mariam yalikuwa na thamani kubwa, thamani hiyo ilitokana na
kipimo cha mapenzi kilichokuwa ndani yake! Alimpenda sana Tom wake, lakini
badiliko la tabia yake lilimkosesha raha moyoni mwake.
Mariam hakuwa na amani, alishindwa kuelewa ni shetani gani aliyemwingia
mumewe na kumbadilisha kiasi kile. Hadi wakati huo hakuwa na uhakika kama
aliyemjibu majibu machafu kiasi kile alikuwa Tom wake aliyemfahamu siku zote.
“Sasa amezidi! Amefikia hatua ya kulala nje, Tom kwanini unanitesa lakini?”
Mariam alisema maneno hayo huku akilia kwa uchungu, chumbani alipokuwa
amekimbilia.
Hasira zilipomzidi Mariam, alijikuta akizidisha kilio, jambo lililomuudhi
sana Tom ambaye haraka alitoka na kwenda chumbani kumfuata kwa lengo la kumpa
kipigo.
“Pumbaaaafu....hapa siyo Klinik, umeelewa? Naomba unyamaze haraka sana!”
“Sinyamazi.”
“Unasema?”
“Sinyamazi Tom, niache nilie hasira zangu ziishe. Unanitesa sana Tom lakini
sasa umeona ili kunidhibitishia kwamba ni kweli hunipendi, umeamua kulala nje
kabisa, sasa nina thamani gani kwako mimi?!”
“Hivi wewe mwanamke, nimekuoa au umenioa?”
“Tumeoana!” Mariam akajibu kwa kujiamini huku akifuta machozi machoni
mwake.
Hakujua ni kiasi gani lilikuwa jibu baya kwa Tom. Alimwangalia kwa jicho la
hasira kisha akamsogelea polepole huku akitetemeka kwa hasira zilizoonekana
dhahiri.
“Hivi, hii jeuri unaipata wapi wewe mwanamke? Nakuuliza wewe...hii jeuri
unaipata wapi?”
“Tom mpenzi wangu, kukuliza ulilala wapi imekuwa jeuri?”
“Hata kama, mimi ni mwanaume na nina mambo mengi, na kama nilikuwa
nahangaika na biashara zangu, utajuaje?”
“Ni lini uliwahi kulala nje Tom, kama kuchelewa ulikuwa unanipa taarifa,
iweje kwenye kulala nje ushindwe kuniambia?”
“Kwahiyo kila ninachokifanya lazima nikuambie siyo?”
“Mimi kama mkeo, natakiwa kufahamu hayo yote, kumbuka uliahidi nini siku ya
ndoa, kumbuka Tom mume wangu!”
“Hata kama, lakini nimekuambia kuwa nina kazi nyingi na ndizo nilizokuwa
nahangaika nazo, nilitegemea ungenipokea na kunipa pole, lakini mwenzangu ndiyo
kwanza unaanza ugomvi!”
“Lakini simu zilikuwa hazipatikani!”
“Ziliisha chaji!”
“Hapakuwa na njia nyingine ya kunijulisha Tom!”
“Lakini mbona umeshikilia sana hilo jambo? Kitu kidogo unataka kiwe
kikubwa?”
“Natetea uhai wangu Tom, hivi unafikiri kama ukizoa maradhi huko na
kuyaleta hapa nyumbani itakuwaje kama siyo kuniua?”
“Unasemaje wewe mwanamke? Yaani mimi ni ukimwi? Sasa naona upole wangu
unaniponza, unataka kunipanda kichwani sasa!” Tom akasema hayo huku akivua
mkanda wake wa suruali.
Kilichofuata baada ya hapo ilikuwa ni kipigo cha nguvu, ambapo pamoja na
Marim kuomba msamaha Tom aliendelea kumpiga!
“Nisamehe mume wangu utaniua, naomba msamaha, tafadhali
Tom...nakufaaaaa...” Mariam alipiga kelele lakini Tom aliendelea kumpiga mpaka
hamu yake ilipoisha akaamua kuachana naye.
******
BAADA YA MIEZI SITA
Mapenzi ya Tom na Mayasa yalizidi kushamiri huku mateso, manyanyaso na
matusi kwa Mariam yakiwa ni vitu vya kawaida kila kukicha! Tom alibadilika
sana, akawa hasikii wala haambiwi kwa Mayasa.
Kama ni mapenzi basi yalitakiwa kutafutiwa jina lingine maana katika penzi
la wawili hao yalikuwa makali zaidi ya neno lenyewe! Walikuwa kama kumbikumbi,
kila mahali walikuwa pamoja.
Tom alishindwa kuelewa kwanini alijikuta akizidisha mapenzi kwa yule
mwanamke kwa kasi ambayo hata yeye mwenyewe hakujua ilipotokea. Alimuona Mariam
kama kinyaa mbele yake, hakuwa na muda wa kukaa na Mariam hata kujadili kuhusu
mambo mbalimbali ya familia yao.
Muda mwingi alikuwa na Mayasa, Tom hakujua siri ya kumpenda zaidi Mayasa,
kulikuwa na kitu kilichosababisha mapenzi kati yao kuongezeka! Mayasa alikwenda
kwa Mtalaamu wa Kienyeji ambaye alimuwekea mambo yote sawa! Tom alikuwa mkononi
mwa Mayasa na hakuwa na uwezo wa kufurukuta kwa namna yoyote ile! Alikuwa kama
bendera ambayo siku zote huwa inafuata upepo.
Siku moja Tom akiwa na Mayasa mjini, Tom alijikuta akifanya jambo la hatari
sana. Baada ya kupungukiwa na fedha, waliamua kwenda kwenye mashine ya kutolea
fedha ya CRDB Tawi la Azikiwe na kumtuma Mayasa aende akachukue pesa.
“Sasa nitawezaje wakati sifahamu namba zako za siri?”
“Hilo tu, nitakupa!”
“Lakini ni vizuri ukaenda mwenyewe, mambo ya pesa hasa akaunti ni siri ya
mhusika mpenzi wangu! Hebu shuka kwenye gari uende ukachukue pesa, acha uvivu
wako!” Mayasa alimwambia Tom lakini alikuwa anamtania kwani alikuwa anajua
kwamba dawa ndizo zilizokuwa zikifanya kazi.
“Wewe ni mpenzi wangu siyo?” Tom akauliza.
“Hata hili gari linajua hivyo.”
“Umejibu vizuri sana, sasa sina haki ya kukutuma?”
“Unayo!”
“Namba za siri za hiyo kadi ni 1343, nenda katoe laki tano haraka!”
“Sawa baba, isiwe ugomvi!” Mayasa akasema kisha akatoka kwa mwendo wa
maringo kuelekea kwenye mashine.
Tom alibaki hoi akikodolea macho makalio ya Mayasa, yaliyokuwa yanavutia
sana. Watu waliomwona akipita, walishindwa kuzuia hisia zao na kujikuta
wakimtimzama kwa macho ya matamanio.
Ilibaki kidogo Mayasa azimie baada ya kuona fedha zilizokuwa kwenye akaunti
ya Tom, pamoja na kwamba alikuwa anafahamu Tom alikuwa na fedha nyingi sana,
lakini hakuwahi kufikiria kwamba akanuti yake ingekuwa na fedha nyingi kile.
Akaunti ya Tom ilikuwa na zaidi ya bilioni thelathini, hata hivyo alikuwa
na akaunti nyingine katika Benki za NBC na Barclays ukiachilia mbali akaunti
nyingine zilizokuwa nje ya nchi. Mayasa akachukua kiasi kile cha fedha na kurudi
kwenye gari.
“Umefanikiwa?”
“Ndiyo!”
“Twende!” Tom akawasha gari na kuondoka na Mayasa, safari yao iliishia
katika moja ya Hoteli za sasa iliyokuwa ufukweni mwa Bahari ya Hindi.
Wakiwa huko Mayasa alikumbushia ahadi ya kupangishiwa nyumba, aliyoahidiwa
na Tom.
“Haraka ya nini? Subiri kwanza!”
“Lakini dear nitaendelea kukaa Mbagala hadi lini? Sina hadhi ya kukaa kule
tena!”
“Ni kweli lakini nimekuambia subiri mpenzi wangu, nakuandalia kitu cha
maana na muda mfupi baadaye utafurahia!”
“Tutaona!” Walikula raha huko usiku mzima.
******
Wiki mbili baadaye Tom alimpigia simu Mayasa na kutaka wakutane kwa ajili
ya kumpatia zawadi nzuri sana aliyoiandaa kwa ajili yake.
“Kwani we’ uko wapi?” Mayasa akamwuliza.
“Uwanja wa nyumbani 56 Club!”
“Mimi nipo Mwananyama, acha nichukue taxi mara moja nakuja hapo sasa hivi!”
“Nakusubiri mpenzi wangu!” Muda mfupi baadaye Mayasa akafika.
Bila kupoteza muda Tom akamwambia Mayasa aingie kwenye gari. Akaingia.
Wakaangaliana kwa pamoja na kuachia matabasamu mapana sana usoni mwao.
“Leo ni siku ya furaha katika penzi letu, nataka kukuonyesha kwamba
nakupenda, nakuthamini, nakuheshimu na nataka kuwa na wewe katika siku zote za
maisha yangu!”
“Mbona unanitisha mpenzi, kuna nini?”
“Usijali, fumba macho yako, halafu nitakufunga kitambaa cheusi kisha
nitakufungua baada ya kufika mahali zawadi ilipo, sawa?”
“Hakuna shida mpenzi wangu!” Tom akatoa kitambaa na kumfunga Mayasa usoni,
kisha akaondoa gari.
Safari yao iliishia Kinondoni B, karibu kabisa na Shule ya Sekondari Biafra
ambapo kulikuwa na nyumba nzuri ya kifahari iliyokuwa na kila kitu ndani! Nje
ya nyumba hiyo, kulikuwa kumeegeshwa gari mpya aina ya Toyota Rav 4 la rangi la
Buluu, ukoka ukiwa umechukua nafasi kubwa pamoja na bustani nzuri iliyokuwa
pembeni ya bwawa la kuogelea.
Tom alipoegesha gari lake, akafungua mlango na kumtaka Mayasa atoke. Baada
ya hapo akamfungua kitambaa usoni mwake na kumpa funguo mbili, moja wa gari na
mwingine wa nyumba.
“Huu ni funguo wa nyumba yako, na huu ni wa gari lako, lile pale. Kuanzia
leo, hii ni nyumba yako, ina kila kitu ndani, furahia maisha mpenzi wangu!” Tom
akasema akitabasamu.
Mayasa hakuweza kuelewa kama yaliyokuwa yakitokea yalikuwa ni ndoto au
tukio la kweli. Akamwangalia Tom huku akitetemeka kwa furaha, midomo yake
ikaanza kutingishika!
“Ni nyumba ya kupanga au...” Tom hakumuacha Mayasa amalizie sentesi hiyo,
akamkatisha.
“Nimeinunua na hati yake hii hapa, nimekuwa nikifanya ukarabati na kuifanya
ya kisasa kwa miezi sita sasa, hii ni nyumba yako....mali yako!” Tom akamwambia
Mayasa akitabasamu.
Tayari macho ya Mayasa yalishajaa machozi, akamsogelea Tom na kumkumbatia
kwa nguvu, mabusu motomoto mashavuni mwa Tom yalitawala.
“Nimeamini unanipenda Tom!”
“Tena sana, kuliko hata Mariam!”
“Kweli?”
“Nakuhakikishia!”
“Leo ni siku ya furaha ya penzi letu, ili niamini vizuri kama kweli
unanipenda, twende tukalale nyumbani kwako, hapo utanifanya nione unanithamini
na kunipenda na humpendi mkeo!” Mayasa akasema akiwa ameyatuliza macho yake
usoni mwa Tom.
Maneno yale yalizunguka kwenye ubongo wa Tom zaidi ya mara kumi bila kupata
jibu la kumpa Mayasa.
“Tom, nahitaji jibu lako mpenzi wangu!”
Tom akafungua kichwa chake, macho yake yakitizama chini huku akionekana
kuwa na mawazo mengi sana yaliyomkumba ghafla. Kila alipotaka kuzungumza
alionekana kusita.
Beyond Love – 24
Katika hali ya
kushangaza sana, Mayasa anamwambia Tom akubali kwenda kulala nyumbani kwake, pamoja
na kwamba alikuwa akifahamu kwamba ana mke. Linakuwa jambo zito sana kwa Tom,
lakini Mayasa anaendelea kumng’ang’aniza.
Je, atakubali? Nini
kitatokea? Ssa SONGA NAYO...
Kama ni mtihani, huu ulikuwa mkubwa kuliko yote kwa Tom! Pamoja na kumpenda
sana Mayasa, lakini kitendo cha kumwambia akalale naye nyumbani kwake kilikuwa
cha udhalilishaji mkubwa kwa mkewe wa ndoa Mariam.
Ni kweli Tom alikuwa katika mtihani mzito sana na hakuweza kufungua mdomo
wake kusema chochote, hadi dakika mbili baadaye, Mayasa alimtingisha kwa nguvu
na Tom kurejewa na kumbukumbu zake vizuri. Ni kama hakuwepo mahali pale.
“Mbona umenyamaza?”
“Unasema?”
“Mbona upo kimya, nahitaji jibu lako!”
“Najua Mayasa, lakini fahamu kwamba umenipa mtihani mkubwa sana!”
“Mtihani mkubwa kivipi?”
“Mayasa!” Tom akaita.
“Nakusikia mpenzi wangu!”
“Huoni kuwa huo ni mtihani mkubwa sana kwangu?”
“Labda nikuulize swali kabla ya kujibu lako!”
“Endelea...”
“Unanipenda?”
“Mayasa mpenzi wangu, hata wewe unaweza kunisaidia kujibu!”
“Pengine ninalo jibu, lakini yawezekana jibu nililonalo mimi ni tofauti na
fikra zako!”
“Hapana...unavyowaza ndivyo nilivyo!”
“Kwahiyo sasa nikuambie ninavyowaza jibu yako?”
“Ndiyo!”
“Utaniamini?”
“Kwanini nishindwe?”
“Tom hunipendi, hunipen...” Mayasa akasema akilia.
Tom hakutaka kuyaona machozi ya Mayasa, haraka akaanza kumfuta machozi yake
na kumbembeleza anyamaze.
“Niache nilie Tom, ni haki yangu!”
“Haki ya kuli? Kivipi?”
“Napenda nisipopendwa!”
“Usiseme hivyo mpenzi wangu, mimi nakupenda sana!”
“Kama unanipenda kwanini unanifanyia hivi?”
“Kumbe yote haya niliyoyafanya huoni thamani yake?”
“Sina maana hiyo, nataka udhihirishe penzi lako kwangu mbele ya mkeo,
nataka mkeo afahamu kwamba yupo unayempenda zaidi, ambaye ni mimi. Kwanini
unanitesa kiasi hicho Tom?” Mayasa alikuwa akizungumza kwa hisia sana huku
machozi yakimtoka machoni mwake.
Tom hakujua kilichokuwa akilini mwa Mayasa, alifanya yote hayo kwa sababu
alikuwa akihitaji Mariam afukuzwe ili aweze kuzitawala vizuri mali za Tom, hiyo
ndiyo iliyokuwa ndoto yake siku zote. Kuchota mali za Tom ingewezekana kama
Mariam angeondoka ndani ya nyumba ya Tom na hatua ya kwanza kwake ilikuwa ni
kwenda nyumbani kwa Tom na kulala pale.
Aliamini kwa kufanya kungemchukiza Mariam na kuamua kundoka zake kwenda
kwao. Wazo lake lilikuwa zuri sana ingawa hakujua ni kiasi gani lilikuwa sumu
kwa mwenzake.
Ukimya wa mrefu ukapita, wote wakiwa hawazungumzi chochote hadi Tom
alipoamua kuanzisha mazungumzo.
“Nina swali moja kwako!”
“Uliza!”
“Unanipenda?”
“Saaana!”
“Sasa sikiliza, mimi ni mwanamke na wewe ni mwanaume, sawa?”
“Ndivyo ilivyo!”
“Wewe una nafasi yako kama mke na mimi nina nafasi yangu kama mume ni
kweli?”
“Hujakosea kitu!”
“Lakini pia unakubali kwamba, mwanaume ndiye kichwa cha nyumba?”
“Hata kwenye maandiko ipo!”
“Sasa mimi kama mumeo, kichwa cha nyumba, msemaji wa mwisho, naomba
unielewe kwamba, kwa leo haitawezekana kwenda kulala nyumbani, lakini naweza
kulala na wewe hapa kwa ajili ya kuizundua nyumba, umenielewa?” Tom akasema kwa
kujiamini sana ingawa alitarajia kukutana na jibu la kukataliwa.
Kinyume na matarajio yake, Mayasa alimsogelea Tom na kukumbatia kwa nguvu,
kisha akausogeza mdomo wake karibu kabisa na wa Tom, akautoa ulimi wake haraka
na kuutumbukiza kinywani mwa Tom. Wakaanza kufurahia mapenzi.
“Nimekuelewa mpenzi wangu, hakuna shida!”
“Nami nimefurahi sana kwa uelewa wako mpenzi wangu, naona sasa umekuwa na
unatambua nafasi ya mwanaume katika mapenzi.” Tom akasema akishangulia ushindi
moyoni mwake.
“Ahsante mpenzi wangu!” Maneno hayo yalitoka kinywani mwa Mayasa lakini
moyoni ilikuwa ni tofauti kabisa; “Huna ujanja wewe, nakulea-lea kwanza, lakini
kuna siku utaingia mkenge tu.”
Tom akamshika mkono Mayasa, wakaingia ndani. Macho ya Mayasa hayakuwa
tayari kuamini kilichokuwa mbele yake, ilikuwa sebule nzuri ya kisasa yenye
kila kitu cha maana!
Kwanza kulikuwa na seti ya masofa mazuri, chumba maalumu cha chakula
(dinning room), jokofu kubwa, redio kubwa, luninga na deki yake na kila aina ya
anasa.
Hayo yangekuwa makazi mapya ya Mayasa baada ya kuishi muda mrefu katika
maisha duni huko Mbagala. Hakuamini macho yake, kama kweli Tom alikuwa
amedhamiria kumjengea nyumba nzuri nzuri kiasi kile. Macho yake yalizunguka
kila kona ya sebele ile ya kisasa yakitizama vitu vizuri vilivyokuwepo.
“Ahsante sana mpenzi wangu, siamini macho yangu!” Mayasa akasema akimwaga
machozi kama mvua.
“Amini, amini mpenzi wangu, wewe ndiye niliyekuchagua kutoka moyoni
mwangu!”
“Nakuamini mpenzi!”
“Sasa twende nikakuonyeshe bed room!” Tom akamwambia na kumshika mkono
kisha wote kwa pamoja wakaongozana hadi chumbani.
Huko Mayasa ndiyo alishindwa kuelewa namna gani atakavyotoa shukrani zake.
Kilikuwa chumba kikubwa, kizuri na chenye kila kitu! Kwanza kulikuwa na kabati
kubwa la nguo, kitanda kikubwa cha futi sita kwa sita ambacho kilitengenezwa
kwa kutumia ngozi, meza ya vipodozi pamoja na vikorobwezo kibao!
Choo na bafu vyote vilikuwa ndani, kukiwa na bomba la maji ya mvua ambayo
hutoka ya moto, baridi na ya mchanganyiko! Kilikuwa chumba cha kisasa sana.
Mayasa akamwangalia Tom, kisha akajikuta hisia zake za mapenzi zikimpanda sana,
akamsogelea na kumtupia kitandani. Kilichoendelea huko ilikuwa ni shughuli
nzito iliyomalizika baada ya saa moja.
Wote wakiwa na furaha wakatoka na kwenda nje kuogelea katika bwawa la
kuogelea. Hakika yalikuwa maisha ya kifahari sana, kila kitu kilikuwa kipya kwa
Mayasa. Siku hiyo hawakutoka kabisa, kila kitu kilikuwa ndani. Vyakula vyote
vilikuwa kwenye majokofu.
Walipomaliza Tom alijipumzisha nje, wakati Mayasa akiendelea kupika chakula
ndani. Mayasa alijiona mshindi katika maisha mchezo ule hatari wa
kuisambaratisha ndoa ya watu.
“Haya ndiyo maisha, lakini mambo bado, nitahakikisha ananyooka, mimi ndiyo
Mayasa mtoto wa mjini, niliyezaliwa, kukulia na kusomea katika jiji la
wanjanja, jiji la Dar es Salaam,” Mayasa alijisemea moyoni mwake wakati akipika
chakula cha usiku.
Baadaye walikula na kulala usingizi wa mapenzi mazito.
******
Macho ya Mariam yaliganda katika saa ya ukutani iliyokuwa ikionyesha kuwa
ilikuwa imeshatimia saa 7:55 usiku! Zilibaki dakika tano tu, kabla ya kufika
saa 8:00, muda ambao kwa hakika, wanandoa wengi huwa katika harakati za
kutafuta watoto!
Mariam alikuwa sebuleni akiwa anamsubiria mume wake bila mafanikio. Machozi
yake sasa yalikuwa ya kawaida. Vituko na mateso kutoka kwa mumewe vilizidi,
hakuona kama alikuwa na thamani kwa mumewe tena. Siku zote alikuwa wa kumangwa
na kutukanwa kuwa yeye mgumba, neno lililomuuma sana.
“Kwahiyo kwasababu sijashika mimba ndiyo
anichukie kiasi hiki? Tom hanitendei haki, ananinyanyasa!” Mariam
alisema kwa sauti kubwa na kuamua kwenda chumbani kulala, hapakuwa na matumaini
ya Tom kurejea.
Asubuhi ya saa 4:30, gari la Tom lilikuwa likipiga honi nje, mlinzi
akafungua na Tom akaingiza gari na kuegesha mahala pazuri. Akashuka na kuingia
ndani. Alipokutana na Mariam sebuleni, hakuonyesha kama kuna kosa alilokosea,
akamsalia katika hali ya kawaida kabisa.
“Umeamkaje Mariam?!” Tom akamsalimia huku akielekea chumbani.
“Salama!” Mariam alipojibu, Tom akaongeza mwendo kwenda chumbani.
Mariam hakuweza kuvumilia zaidi, akamfuata nyuma nyuma hadi chumbani.
Hakuwa na ukali kwa mume wake, akamwacha akavua nguo na kwenda bafuni,
aliporudi ndipo alipomwomba kuzungumza naye.
“Lakini mume wangu, kwanini umebadilika tabia kiasi hiki? Kila siku unalala
nje, kwanini lakini?” Mariam akamwuliza Tom.
“Mazungumzo yenyewe ndiyo haya?”
“Ndiyo, kwani unaona ni madogo mume wangu?”
“Makubwa, tena makubwa sana!”
“Sasa una mpango gani?”
“Wa kuendelea kulala nje kila siku!”
“Naomba usifanye hivyo Tom wangu, unajua ninakupenda sana!”
“Hata mimi nakupenda sana, lakini kipo kinachokifanya nilale nje, sasa kama
unataka nianze kulala nyumbani, basi niruhusu niwe nakuja na kinachokifanya
nilale huko nje!”
“Hilo ni jambo dogo sana kwa mtu anayempenda mpenzi wake kama mimi. Hakuna
tabu, nimekuruhusu!”
“Kweli?”
“Niamini mpenzi wangu!” Wakakumbatiana kwa furaha.
Siku nzima Tom alishinda nyumbani akiwa na mkewe, tena akijitahidi kumpa
haki ya ndoa kwa kikamilifu, lakini jioni akamuaga Mariam kuwa anatoka kidogo.
“Unakwenda wapi tena?”
“Kuchukua hicho kinachonifanya nisilale nyumbani karibu kila siku!”
“Sawa!” Mariam alijibu akitabasamu.
******
Mariam alichukulia maneno ya Tom kama utani, hakujua kama mwenzake alikuwa
akimaanisha alichokuwa akikizungumza. Tom alipoondoka, moja kwa moja alikwenda
nyumbani kwa Mayasa ambaye alimkuta akitizama luninga sebuleni.
“Njoo chumbani nina habari njema mpenzi wangu!”
“Habari njema? Kuhusu nini tena?”
“Jiandae tuondoke!”
“Tunakwenda wapi?”
“Nimesema jiandae twende!” Ndani ya dakika kumi tu, Mayasa alikuwa
ameshamaliza kuvaa na walikuwa njiani wakielekea nyumani kwa Tom, ingawa Mayasa
alikuwa hajui.
“Tunakwenda wapi lakini?”
“Leo tunaenda kulala kwangu, nataka Mariam ajue nina akili na nilifunga
naye ndoa kwa bahati mbaya, wewe ndiye unayefaa kuwa mke wangu wa ndoa na siyo
yeye!”
“Sijakusikia vizuri, umesema tunaenda wapi?”
“Nyumbani kwangu!”
“Nakupenda sana Tom, kweli sasa umeamua kudhihirisha penzi lako kwangu,
naomba ukanyage mafuta sawasawa tumuwahi huyo mwehu wako!” Mayasa alimwambia
Tom kwa sauti iliyojaa mahaba mazito, kweli Tom akafuata maagizo aliyopewa na
Mayasa, akakanyaga mafuta kisawa-sawa.
Alikuwa anamuwahi Mariam, hakika alidhamiria kumuumiza.
Beyond
Love- 25
Masikini
Mariam, hajui kilichokuwa kikimjia! Tom anakwenda kwa Mayasa na kumpa habari
hizo njema, ambapo Mayasa anakuwa haamini kabisa alichosikia. Tom
anamhakikishia kwamba, alichosikia kilikuwa yakini na kwamba walikuwa
wanakwenda kulala nyumbani kwake.
Je,
nini kitatokea? SONGA NAYO...
M
|
ayasa
alikuwa akishangilia ushindi moyoni mwake, alijiona mwenye akili kuliko
kawaida. Alimshukuru sana
mganga wake kimoyomoyo, akiamini ndumba zilikuwa zinafanya kazi ipasavyo.
“Huu
ni mwanzo mzuri sasa, naamini kila kitu kitakwenda sawa, utajiri wa Papaa Bill
utakuwa wetu na siyo wake.
“Halafu
inaonekana hicho kimwanamke chake hakijui mapenzi, sasa ngoja nimuonyeshe mji,
mimi ndiyo mtoto wa mjini bwana!” Aliwaza Mayasa akimtizama machoni Tom.
“Tom...”
Mayasa akaita.
“Nakusikiliza
mpenzi wangu!”
“Nimeamini
kwamba unanipenda sana,
wewe ni mwanaume wangu wa maisha na sasa najihakikishia kuwa na wewe siku zote
za maisha yangu.”
“Ni
kweli kabisa, usiwe na wasiwasi Mayasa wangu, yaani mpaka najuta kumfahamu
Mariam, sijui kwanini nilikutana na yule mjinga-mjinga, yaani nina mkosi wa
ajabu sana,
simpendi yule mwanamke hata chembe!”
“Pole
sana, lakini
mimi nipo kwa ajili ya kukupa furaha katika maisha yako, usiwe na wasiwasi
mpenzi wangu, kila utachokitaka kwangu utakipata, sawa sweetie wangu?!” Sauti
ya mahaba ilimtoka Mayasa, tena kwa kutokea puani.
Tom
alikiri kwamba mwanamke yule alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuufanya moyo wake mateka. Hakuwa na la
kufanya zaidi ya kukubali kuwa katika himaya ya mapenzi ya Mayasa.
“Naweza
kukuliza!” Mayasa akamwuliza Tom.
“Maswali
mangapi?”
“Moja
tu!”
“Uliza.”
“Nataka
kujua tutalala wapi?”
“Una
swali la nyongeza?”
“Hapana.”
“Umesema
unataka kujua mahali tutakapolala?”
“Ndiyo!”
“Hilo tu?”
“Kwani
dogo?”
“Ok!
Vizuri sana,
acha nikujibu kwa vitendo!”
Alichokifanya
Tom ni kuchukua simu yake kisha kubonyeza namba za Mariam, ikaita na baada ya
muda ikapokelewa. Tom akaweka sauti ya juu ‘loud speaker’ kisha akaanza
kuzungumza naye.
“Vipi
Tom mume wangu?”
“Salama
mama, habari za hapo nyumbani?”
“Nzuri,
sijui wewe?”
“Mie
ni mzima wa afya njema!”
“...ah
Tom wangu, kama kuna siku umenifurahisha ni
leo, yaani umenipa raha sana!”
“Kweli
eh?!”
“Saaana,
halafu naomba uwahi, usiku wa leo utakuwa kwa ajili yetu, nitakuonyesha mambo
zaidi ya mchana!”
“Sawa
mpenzi, hakuna shida, umepika nini?”
“Chakula
chako ukipendacho!”
“Nini?”
“Bunia!”
“Kama siyo ndizi samaki, basi itakuwa ugali samaki!”
“Ni
ugali samaki mpenzi wangu, mboga za majani na mtindi, najua leo utajilamba sana!”
“...hasa
kama samaki wenyewe watakuwa sato!”
“Ni
lini nimekupikia samaki wengine tofauti na sato?”
“Utakuwa
mlo mzuri sana
kwangu!”
“Basi
uwahi Tom, angalau tuoge pamoja!”
“Hakuna
tabu, lakini nitakuwa na mgeni, sasa ni vizuri kama
utaandaa kile chumba cha wageni vizuri!”
“Hilo tu mume wangu, labda
useme lingine!”
“Na
chakula chake pia!”
“Hakuna
shida!”
“Basi
baadaye mpenzi wangu!”
“Sawa...mwaaaaaaa....”
“Mwaaaaaa...”
baada ya mazungumzo hayo kwenye simu, Mariam alimuangushia busu mwanana Tom
ambaye naye alijibu kisha akakata simu.
Baada
ya hapo akamgeukia Mayasa akamwangalia kwa jicho lililojaa mahaba, huku
akitabasamu kwa furaha. Alikuwa akishangilia ushindi!
“Nadhani
umesikia kila kitu!”
“Sina
la kuongeza mpenzi wangu, sasa moyo wangu mweupeeeee!”
“Leo
ni siku yake, atajuta kukutana na mimi, mwanamke ananing’ang’ania utafikiri
aliambiwa mwanaume nipo peke yangu? Nimeshafanya kila aina ya vituko lakini
hasikii, sijui ni mwanamke wa aina gani yule?”
“Kwanza mwanamke gani mgumba? Subiri nikuzalie watoto
haraka-haraka, upate warithi wa mali
zako!” Mayasa akadakia.
Ilikuwa
kauli ambayo ilimsisimua sana
Tom, kuambiwa kwamba angezaliwa mtoto, tena haraka-haraka kulimpa faraja sana moyoni mwake, akawa
na matumaini ya kuwa baba baadaye.
“Umenifurahisha
sana Mayasa,
hakuna kitu ninachokitamani kama kuwa baba,
unanifanya nijisikie vizuri sana,
ahsante sana
mpenzi wangu, ahsante!”
“Tena
nipe muda mfupi tu, kutoka sasa!”
“Tutaona!”
“Sasa?”
“Nini
tena?”
“Tunakwenda
moja kwa moja nyumbani au tunapitia mahali kwanza?”
“Wewe
unaonaje?”
“Nilikuwa
naona ingekuwa vizuri zaidi kama tutapitia
mahali tuzungumze zaidi kwanza, kabla ya kwenda nyumbani. Nafikiri muda mzuri
ni kuanzia saa tano au sita za usiku!”
“Tufanye
saa saba!”
“Sawa,
twende wapi?”
“Corner
Bar!”
“Sawa!”
Safari yao ikabadilika, wakaenda moja kwa moja Corner Bar, iliyopo Sinza,
Afrika Sana, jijini Dar es Salaam.
******
Furaha
iliyokuwa moyoni mwa Mariam, haikuwa rahisi kuelezeka, alimuona kama Tom wake alikuwa mpya kabisa, sasa alikuwa na imani
kwamba Mungu wake alikuwa ameshamsikia na yake yalikuwa majibu.
Hakuwa
na chembe ya hisia tofauti na hizo, hakujua kama
muda huo, Tom alikuwa na mwanamke Bar, tena alikuwa akipanga kwenda kulala naye
nyumbani kwao. Hilo
halikuweza kuchukua nafasi kabisa katika moyo wake.
Alichokifanya
ni kuhakikisha anamridhisha mumewe ipasavyo siku hiyo, kitu cha kwanza kabisa
kufanya ilikuwa ni kupika chakula kizuri sana
ambacho mumewe alikuwa akikipenda sana,
ugali sato! Kitu kingine alichokifanya ni kuhakikisha chumba chao kinakuwa
kisafi kuliko zote, baada ya hapo akafanya usafi katika chumba cha wageni.
Alipomaliza
maandalizi yote hayo, akakaa sebuleni akimsubiria kwa hamu kubwa sana mumewe ambaye mpaka
wakati huo, saa 2:00 za
usiku, wakati taarifa ya habari ya Kituo cha Televisheni cha ITV ikianza,
alikuwa hajafika!
Saa
moja ikaondoka, ya pili, tatu na hatimaye ilifika saa 6:00 za usiku, Tom akiwa bado hajafika, hapo
ndipo alipoanza kupatwa na wasiwasi ambapo aliamua kumpigia simu. Hata hivyo
simu yake haikupatikana!
Hakuingia
chumbani, akabaki pale pale sebuleni akimsubiria mumewe kwa shauku kubwa! Saa
saba kasarobo za usiku, honi ilisikika getini, Mariam hakuwa na mashaka kwamba
aliyekuwa mlangoni alikuwa mumewe. Mlinzi akafungua geti, Tom akaingia ndani na
kuegesha mahala pazuri.
Akafungua
mlango na kushuka garini, kisha akazunguka upande wa pili na kumfungulia
Mayasa, akashuka.
“Karibu
nyumbani mpenzi!”
“Ahsante
sana.”
“Twende.”
“Tangulia.”
Wakaongozana moja kwa moja, hadi ndani.
Mariam
akawapokea kwa furaha sana,
hakujua kilichokuwa nyuma ya pazia. Tofauti na matarajio yake, Tom alipita moja
kwa moja na Mayasa hadi katika chumba anacholala yeye na Mariam kila siku.
Mariam
akashindwa kuelewa kilichokuwa kikiendelea, kuna wakati alikuwa akifikiria
labda mumewe aliamua kumfanyia mzaha. Alidumu sebuleni kwa dakika mbili tu,
sebule haikukalika tena, akaondoka na kuwafuata chumbani. Dakika mbili zilikuwa
nyingi sana kwa
Tom na Mayasa.
Aliwakuta
wakiwa kama walivyozaliwa, huku wakicheza
michezo ya kimahaba bila wasiwasi!
“Tom!!!”
“Mariam!?”
“Nini
unafanya na huyu mwanamke huku chumbani kwetu?”
“Sitaki
kuamini kama macho yako yamepoteza uwezo wa
kuona kiasi hiki!” Tom akasema kwa sauti tulivu sana, ambayo ilionekana dhahiri kabisa
alidhamiria.
“Toooom...”
“Yes
Mariam!”
“Umeona
haifai kufanya uchafu wako huko nje, na sasa umeniletea hapa nyumbani kabisa!”
Sauti ya Mariam sasa, ilianza kukata-kata, huku machozi yakifanana kabisa na
maji machoni mwake.
“Lakini
ukiona hivi ujue hutakiwi, kwanini unang’ang’ania? Mwanamke gani wewe, hata
shepu huna, hebu ona wenzako tulivyojazia...hivi wakati wazuri tunaumbwa, we’
ulikuwa wapi mwenzetu? Hebu toka utuachie nafasi tujinafasi!” Mayasa akasema,
akimtizama Mariam kwa dharau sana.
Wakati
huo Mayasa alikuwa akijitingisha-tingisha akiwa kama
alivyozaliwa. Mapigo ya moyo wa Mariam yaliongezeka kasi kuliko kawaida,
akahisi kizunguzungu na kuanguka chini kama
gunia la mchele.
“Haaaaah,
Mariam?!” Tom akapiga kelele.
“Wa
nini, mwache afe!” Mayasa akasema.
“Lazima
tumsaidie!”
“Sasa
amua kuwa na mkeo au mimi!” Mayasa akasema akianza kuvaa nguo zake tayari kwa
kuondoka.
“Usifaye
hivyo Mayasa, lakini tunatakiwa kumsaidia!”
“Inaonekana
bado unampenda huyo mkeo, sasa baki naye!” Sasa Mayasa alikuwa anatoka nje ya
chumba kile.
Tom
hakutaka kuruhusu jambo lile litokee, akamfuata na kumrudisha chumbani, pamoja
na kwamba moyo wake ulikuwa ukimuuma sana, lakini kwa kumridhisha Mayasa, Tom
akaamua kumburuza Mariam hadi sebuleni kisha akarudi chumbani kulala na Mayasa.
Hadi wakati huo, Mariam alikuwa hajazinduka.
Beyond Love- 26
Baada ya mzozo wa muda
mrefu kati ya Tom na Mariam, kuhusu tabia ya
Tom kulala nje, hatimaye Tom anamweleza Mariam kwamba kuna kitu
kilichomsababisha alale nje na kama angekuwa tayari aje nacho nyumbani!
Bila Mariam kuelewa
kwamba alikuwa anakaribisha matatizo, akakubali. Tom anakwenda nyumbani kwake
na Mayasa, anamfukuza Mariam chumbani kwake na kulala na Mayasa. Mariam
anapatwa na mshtuko na kuanguka mlangoni.
Tom anamburuza hadi
sebuleni na kumwacha huko kisha anarudi chumbani kulala na Mayasa. Je, nini
kitatokea? Kwanini Tom anamchukia Mariam kiasi hicho? Anza sasa KUSONGA NAYO...
Kitendo cha Tom kukubali kumuacha Mariam akiteseka sebuleni na kwenda
chumbani kulala na Mayasa, kilimfurahisha sana Mayasa, alijiona mwanamke
mshindi ambaye ana nguvu ya ushawishi. Hali ilikuwa tofauti sana na Tom, yeye
moyoni mwake alikuwa mwenye uchugu mwingi sana, ingawa ni kweli alikiri kwamba
Mayasa alikuwa moyoni mwake zaidi kuliko Mariam.
“Umenifurahisha sana mpenzi wangu, sasa naamini kweli unanipenda kwa
mapenzi ya dhati, wewe ndiye mwanaume wa maisha yangu, siwezi kukuacha hata
siku moja!” Mayasa akasema akimkumbatia Tom aliyekuwa anaonekana dhahiri hana
furara aliyokuwa nayo awali.
Jambo hilo liligundulika haraka sana na Mayasa, alijua wazi kwamba Tom hakuwa
na furaha aliyokuwa nayo awali, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa hakulipenda,
siku zote alitaka kuibuka mshindi, kupotea kwa furaha ya Tom, kwa kiasi kikubwa
kulimaanisha ushindi wake ulikuwa katika hati hati za kutoweka.
Ni jambo ambalo Mayasa alipingana nalo siku zote, kwake kulikuwa hakuna
kitu kinachoitwa kushindwa, ushindi ndiyo kitu pekee ambacho kilikuwa na maana
kubwa katika maisha yake, akili yake iliwaza ushindi pekee, bila kujali njia
ambayo ushindi huo ungepatikana!
Alimwangalia Tom kwa jicho la hasira, kisha mkono wake akaupeleka moja kwa
moja hadi kwenye sidiria yake alipokuwa amefunga hirizi yake na kuiminya kwa
nguvu!
“Una nini Tom?” Mayasa akauliza kwa ukali sana.
Tom hakujibu!
“Hivi, nazungumza mwenyewe?”
“...hapana...” Tom akajibu kama alikuwa ametokea katika usingizi mzito.
“Bali?”
“Mbona upo hivyo?”
“Vipi Mayasa?”
“Umeniitaje?!”
“Mayasa!”
“Yaani umefikia hatua unaniita Mayasa?”
“...samahani mpenzi wangu, nilipitiwa kiudogo, unasemaje mpenzi wangu?”
“Inaonekana bado unampenda huyo mkeo, kama ndivyo ni bora uniambie niondoke
zangu, sikulazimishi kuwa na mimi!”
“Hapana, kwani kuna nini?”
“Mbona sioni uchangamfu wako? Hukuwa hivyo Tom, naona una mawazo ya mkeo!”
“...hapana...nani? mariam? Mimi...ah no! Labda siyo Thomas, siwezi kabisa
kuwa na mwanamke mbovu kama yule, tena sijui nilikutana naye usiku au vipi?
Tena usikumbushe kuhusu hilo lijanamke, hebu tuzime taa tulale...” Tom
akajikuta akiropoka bila kujua maneno yale yalitokea wapi.
Kwa Mayasa ulikuwa ushindi ambao alikuwa akiutegemea siku zote. Kama ni
barabara, basi hiyo ilikuwa imenyooka! Hapakuwa na kitu kingine zaidi kupanda
kitandani na kulala usingizi wa kiutu uzima!
***
Kila alipojaribu kuvuta kumbukumbu juu ya watu waliokuwa mbele yake,
hakuweza kuwajua kabisa. Hilo halikuwa na maana sana kwake kwa wakati huo,
lakini kwanini waliamua kumtesa na kumnyanyasa ndiyo jambo ambalo lilimnyima
kabisa raha.
Huyu ni Tom, akiwa katikakati ya wanaume sita waliokuwa wamejazia vyema
vifuani mwao, wakimwangalia kwa hasira huku wakimhakikishia kifo!
“Lazima ufe, we bweha!” Mmoja wa wanaume wale walioonekana kuwa na hasira
sana akauliza.
“Nimefanya nini lakini?”
“Utajua mwenyewe, jiulize ni nani ambaye una ugomvi naye!”
“Ugomvi?”
“Ndiyo, ugomvi...ni nani ambaye huna maelewano naye?”
“Mbona naishi na watu vizuri sana!”
“Hata hivyo, hiyo siyo kazi yetu, tunachojua sisi ni kukuua tu na hiyo
ndiyo kazi yetu ambayo tumelipwa kuifanya, hayo mambo mengine hatuna haja
nayo!”
“Msiniue tafadhali!”
“Tutakuua tu lazima, hakuna kitu cha kubadilisha ukweli huu, lazima ufe.”
Mtu mwingine ambaye alionekana kama ndiye mkuu wa wengine alisema kwa hasira.
Tom alishindwa kuelewa mahali pale palikuwa ni wapi na alifikaje? Alijaribu
kuwaza kama kuna mtu alikosana naye, lakini hakumuona. Ghafla akashangaa
amepoteza fahamu, alipozinduka baadaye, alikuwa katika katikati ya pori nene,
mbele yake kukiwa na shimo kubwa, akiwa amezungukwa na wale vijana wenye silaha
mikononi mwao.
Tom alikuwa amefungwa kamba mikono yote na miguu na hakuw ana uwezo wa
kufanya jambo lolote. Tom alitetemeka sana.
“Naombeni mnisamehe tafadhali!”
“Hatuwezi kukusamehe, lakini tutafanya jambo moja kwa ajili yako!” Kiongozi
wa lile kundi akasema.
“Ni nini?’
“Tutakuonyesha picha ya mtu ambaye ametuagiza tukuue!”
“Sawa, naombeni nimuone!” Tom akasema akiwa na hamu kubwa sana ya kujua ni
nani ambaye aliamua kufanya njama za kumuua.
“...ambaye anataka ufe ni huyu hapa...halafu acha kufuatilia maisha ya
watu...kufa salama...” Yule mtu akamwambia akimwonyesha ile picha.
Macho ya Tom hayakuwa tayari kuamini mtu wake wa karibu, mpenzi wake wa
kweli ambaye aliamua kuachana na mkewe kwa sababu yake ndiye aliyekuwa akitaka
auawe. Ilikuwa picha ya Mayasa. Tom akachanganyikiwa.
“Mayasa, nooooooooo.....” Tom akapiga kelele.
Katika hali ya kushangaza sana, wale wakaanguka mmoja mmoja baada ya
kupigwa risisi kama mvua miilini mwao. Tom hakuweza kugundua ni nani
aliyewapiga risasi. Ghafla akashangaa kumuona mtu mbele yake akiwa amevaa
kininja, akijifunika hadi usoni.
Mtu huyo akaanza kuvua zile nguo za Kininja, kisha akavua ile kofia
iliytofunika hadi uso wake, hapo ndipo Tom alipogundua alikuwa ni Mariam. Tom
akashtuka sana.
“Mariam?!”
“Ndiyo ni mimi ninayekupenda, ambaye penzi langu halina mashaka kwako,
nakupenda Tom ndiyo maana nimekuja kukuokoa...” Mariam akasema akitokwa na
machozi kama mvua.
“Siamini macho yangu...Mariam....”
“Ni mimi!”
“Marimuuuuuuuuu....” Tom akapiga kelele kwa sauti ya juu sana. Muda huo huo
akazinduka usingizini, alikuwa amelala kitandani na Mayasa, hapo ndipo
alipogundua kwamba alikuwa ndotoni.
Ilikuwa ndoto ya ajabu sana, hakuweza kujua maana ya ile ndoto. Alipogeuza
macho yake kumwangalia Mayasa, alimkuta akiwa anakoroma usingizini, akawasha
taa na kunyanyuka polepole kitandani, kisha akaizima taa na kutoka hadi
sebuleni kwenda kumfuata Mariam.
Moyo wake ulimuuma sana kumkuta Mariam hadi wakati ule hajazinduka,
alichokifanya ilikuwa ni kumbeba hadi chumba cha wageni na kumlaza kitandani,
akamfunika shuka na kumwekea chandarua. Moyo wake ulikuwa kama umepigwa ganzi,
alishindwa kulewa ilikuwaje hadi akamchukia Mariam kiasi kile.
“Nashindwa kuelewa kwanini inakuwa hivi, ni kweli mimi siyo wa kwanza kuwa
na mwanamke wa nje, lakini mbona mimi namfanyia mke wangu vituko kiasi hiki?
Kuna nini lakini?” Tom akajikuta akijiuliza maswali mfululizo kichwani mwake
bila kupata majibu yakinifu.
Akiwa anamwangalia Mariam aliyekuwa amelala pale kitandani kwa huruma,
akashangaa mtu akimgusa mgongoni.
“Hivi we’ mwanaume una nini? Hutosheki? Umeona uje na huku?”
“Ah! Mayasa?!”
“Ndiyo mimi, unashangazwa na nini?”
“Samahani mpenzi wangu?”
“Imekuwaje tena?”
“Ah, hakuna kitu.”
“Unafanya nini hapa?”
“Nimeamua kumleta Mariam huku.”
“Kwanini?”
“Mbu zilikuwa zinamng’ata sebuleni.”
“Una uhakika hakuna zaidi ya hivyo?”
“Ndiyo, hakuna kitu.”
“Kwanini hukuniaga?”
“Sikuona sababu ya kukusumbua.”
“Haya twende chumbani.” Mayasa akamuamrisha Tom ambaye hakubisha.
Mayasa alikuwa mbabe kupitiliza, alikuwa na kitu kilichomfanya awe na jeuri
aliyokuwa nayo, nguvu za giza alizokuwa akizitumia zilikuwa zinafanya kazi
vyema bila ya Tom kugundua chochote. Walipofika chumbani, kazi ilikuwa moja tu,
kupeana mapenzi motomoto hadi asubuhi.
Hawakulala tena, Tom hakuwa na kumbukumbu za Mariam tena, kichwani mwake
kulikuwa na mtu mmoja tu, Mayasa. Alimuona mwanamke mzuri kuliko kawaida.
“Nakupenda sana Mayasa!” Tom akamwambia.
“Una uhakika?’
“Ndiyo, nakupenda sana, huoni mambo niliyokufanyia?”
“Mambo gani?”
“Nimekujengea nyumba nzuri, nimekupa gari na kila kitu utakacho nakupa,
hiyo haitoshi kukufanya uamini kwamba nakupenda?”
“Haitoshi!!!”
“Unataka nifanye nini tena, sema chochote nitafanya!”
“Kweli?”
“Ndiyo, nakupenda sana na sitaki kukufanya uumie kwa ajili yangu!”
“Nataka umfukuze Mariam hapa nyumbani, tuishi kwa furaha!”
“Na kule kwako?”
“Nitaweka mpangaji, nataka kuishi na wewe hapa!”
Tom hakuwa na jibu.
*******
Jicho lake la kuume ndilo lilikuwa na kwanza kufumbuka, kisha likafuata la
upande wa kushoto. Taratibu kumbukumbu zikaanza kumrejea Mariam. Kilikuwa
chumba ambacho siyo alichokuwa akilala siku zote. Akapiga jicho kila upande na
kujaribu kuvuta kumbukumbu zaidi, akatambua kwamba ni kweli siyo chumba
anacholala siku zote.
Akakumbuka vyema kwamba kilikuwa chumba cha wageni, tena alichokiandaa
jioni yake kwa ajili ya mgeni ambaye Tom alimwambia angekuja naye. Kufikia
hapo, akakumbuka kila kitu. Alikuwa amelala katika chumba cha wageni. Hakuweza
kukumbuka aliingia vipi na muda gani. Akaamka kichovu na kupiga hatua za
taratibu kuelekea chumbani kwake.
Alipofika mlangoni, akasikia kelele za mahaba zikitokea chumbani. Walikuwa
ni Tom na Mayasa wakipeana maraha chumbani. Mariam akachanganyikiwa, lilikuwa
tukio la udhalilishaji sana. Mariam akachungulia kupitia tundu la ufunguo
lililokuwa mlangoni, alichokiona humo ndani hakifai kuandikika hapa! Akaanza
kulia.
“Tom mume wangu, ni nini unafanya na huyo mwanamke wako? Kwanini unakuwa
hivi lakini? Yaani umeshindwa kufanya uchafu wako huko nje, unakuja kunifanyia
hapa nyumbani, tena chumbani kwetu, katika kitanda ninacholala na
wewe...Tom...Tom...Tom...kwanini unafanya hivi lakini?!” Mariam akapiga kelele
akilia kwa uchungu.
Muda mfupi baadaye mlango ulifunguliwa, Mayasa akatoka akiwa amevaa upande
wa kanga, tena kanga yake mwenyewe, uso wake ulikuwa umejaa makunyanzi,
akamsogelea na kumzaba kibao kikali sana shavuni mwake.
“Koma kuharibu starehe za watu, ungekuwa na maana angenileta hapa? Huna
jipya, mwanamke hujui mapenzi zaidi ya kufua na
kupika, unafikiri kwa mtindo huo ataacha kutafuta mtoto wa mjini
anayeweza kumpa raha kama mimi? Na utalijua jiji na mitaa yake...” Mayasa
akasema akibenua midomo yake.
Uso wa Mariam ulilowana kwa machozi, alishindwa kuelewa kwanini mateso yale
yalikuwa kwake tu na siyo kwa mwingine.
“Halafu Mariam uwe na adabu, naomba usijaribu kumsumbua mpenzi wangu, nenda
kalale chumbako kwako kule!” Tom naye akatoka na kumwambia Mariam.
Mariam alihisi alikuwa ndotoni, lakini ukweli ni kwamba haikuwa ndoto, kila
kilichokuwa kikitokea katika maisha yake kilikuwa yakini kwa maana ya yakini
haswa.
Beyond Love- 27
Yote haya yanasababishwa na mwanamke mmoja hatari sana,
Mayasa! Huyu ni mtaalamu wa kwenda kwa waganga ambao walimtengeneza Tom na
kumsahau kabisa Mariam. Sasa Mayasa ameshaingia nyumbani kwa Tom huku Mariam
akilala katika chumba cha wageni. Mariam haamini kinachotokea katika maisha
yake. Hajui hatma yake. Nini kitatokea katika maisha yake? SONGA NAYO...
Masikio ya Mariam yalikuwa
hayataki kuamini yalichosikia wakati macho yake yakikataa katakata kukubaliana
na kilichoonekana kupitia tundu la funguo, mambo yaliyofanyika chumbani
yalikuwa mazito sana. Alishindwa kuelewa ni kosa gani kubwa alilomfanyia Mungu
kiasi cha kumpa adhabu kubwa kiasi kile.
Ilikuwa lazima afikirie kitu
cha kufanya, mawazo pekee yasingeweza kutosha kukabiliana na tatizo lililokuwa
mbele yake. Alijua kitu kimoja moyoni mwake, kwamba alikuwa anampenda sana Tom,
na mambo yote yaliyokuwa yakitokea ni juhudi za shetani kutaka kumharibia mume
wake.
“Mungu ni wewe peke yako
ndiye mwenye uwezo wa kunisaidia tatizo hili, naomba msaada wako baba, sina
uwezo peke yangu, nisaidie mwanao...” Mariam aliomba moyoni mwake machozi
machoni mwake yakitiririka.
Mara akapata wazo jipya,
aliona ni bora aendelee kumuomba Tom abadili mawazo yeke. Aachane na huyo
mwanamke kwani yeye ndiye mkewe wa ndoa aliyekuwa kwa ajili yake.
“Tom mume wangu, kwanini
unanitesa kiasi hiki? Ni kosa gani nililokufanyia lakini mume wangu mpenzi?
Kumbuka ahadi yako siku ya ndoa Tom, kumbuka!” Mariam alisema akitokwa na
machozi.
“Huna kosa Mariam...” Tom
akajibu akiwa chumbani.
“Sasa kwanini unanitenda
hivi?”
“Huna mvuto mtoto wa kike,
ndiyo maana ameona awe na mimi mwenye mvuto.” Mayasa akajibu.
“Sijakuuliza wewe!”
“Kumbe umemuuliza nani?”
“Mume wangu!”
“Unachekesha sana wewe, hivi
Tom ni mumeo kweli wewe?”
“Kwani mume wa nani?”
“Yupo na nani chumbani? Hivi
angekuwa anakuthamini angekulaza chumba cha wageni? Ameona huna jipya ndiyo
maana amekususa, mwanamke usiye na haya, unayesubiri kutupiwa mabegi nje?!
Kwani huoni kuwa hutakiwi humu ndani? Si uondoke...” Mayasa alisema maneno hayo
macho makavu akiwa hana woga hata kidogo, alimchukia Mariam kuliko kitu
chochote.
Mariam alikuwa ni kama
anaharibu mambo yake, wazo la kwamba yeye ndiye aliyemwingilia mwenzake
nyumbani kwake halikupata nafasi kabisa akilini mwake. Aliona kama Mariam ndiye
aliyekuwa akimwingilia yeye.
Mariam alilia kwa uchungu
mwingi sana, aliamini machozi yake pengene yangemuuma Tom na kubadilisha uamuzi
wake, lakini ilikuwa tofauti kabisa, Tom alikuwa kimya chumbani akila raha na
Mayasa, hakuonyesha kujali hata kidogo thamani ya chozi la Mariam.
Maisha yaliendelea kwa mtindo
wa Mariam kulala chumba cha wageni na Tom kulala na Mayasa huku Mariam
akishurutishwa kufanya kazi zote za nyumbani. Ni kama alikuwa mfanyakazi wa
ndani! Kazi kubwa ya Mariam ilikuwa ni kusali, akimuomba Mungu wake amsaidie.
Maisha yalikuwa ya shida sana.
Afya ya Mariam ikaanza
kuzorota, kila siku kwake ilikuwa ni kilio. Tom hakuonyesha kujali, Mayasa
alikuwa ndiye kila kitu nyumbani kwake, alipanga na kutoa amri ya kila jambo
ndani ya nyumba. Usiku mmoja Mariam hakulala kabisa, alitumia kuwaza maisha
yake, kwa muda wa miezi mitatu aliyovumilia, hakuna hata siku moja ambayo Tom
alionyesha dalili za kubadilika tabia wala msimamo wake.
Tom alizidi kuwa mkali kwake
na hakutaka kushirikiana naye kwa chochote, Mariam hakuona kama kuna sababu ya
kuendelea kuteseka kwa mwanaume ambaye alikuwa hana mapenzi na yeye tena.
Akapanga nguo zake usiku huo kwa safari ya kuondoka asubuhi yake. Alishachoshwa
na vituko vya Tom.
*****
Saa kumi na mbili asubuhi,
Mariam alikuwa ameshajiandaa kuondoka. Akiwa na begi lake la nguo, alikwenda
hadi mlangoni mwa chumba cha Tom na Mayasa na kugonga. Alitumia muda wingi sana
kugonga bila kufunguliwa.
“Nani?” Tom akauliza kwa
ukali.
“Ni mimi!” Mariam akajibu kwa
sauti ya unyonge sana.
“Sawa wewe, lakini nani?”
“Mariam!”
“Unataka nini asubuhi yote
hii? Kwanini unatuharibia starehe zetu?”
“Samahani, sina nia mbaya!”
“Shida yako ni nini?”
“Nimekuja kukuaga Tom, naenda
kwetu, nakuacha uendelee kuishi na mwanamke wako ambaye umeona anafaa kuliko
mimi!”
“Siyo kwamba nimeona anafaa
kuliko wewe, bali ndiyo uweli wenyewe ulivyo. Sasa unaondoka sasa hivi au
baadaye?”
“Nimekuja kukuaga sasa hivi
naondoka!”
“Hakuna neno wasalimie wote,
waambie Tom au Papaa Bill sasa anakula bata na mtoto mzuri Mayasa!”
Mariam hakujibu tena, akaanza
kulia akivuta mabegi yake kwenda nyumbani kwao.
Kwa Mariam ilikuwa siku mbaya sana ambayo kwa hakika isingeweza kufutika
katika maisha yake, lakini kwa Mayasa na Tom, ilikuwa siku nzuri sana kwao,
kwani walikuwa wanaachiwa uhuru wa kufanya kila kitu wanachotaka kwa nafasi!
*****
“Vipi tena mwanangu? Mbona hivyo?!”
“Mama acha tu!”
“Nini?”
“Matatizo!”
“Matatizo gani? Mbona
sikuelewi?”
Mariam hakuweza kujibu kitu
tena zaidi ya kulia. Mama yake akamfuata huku naye machozi yakimtoka, lakini
kabla hajamfikia, Maram alianguka chini na kupoteza fahamu.
“Mungu wangu, mwanangu ana
nini jamani? Nini kimempata tena jamani?” Mama yake na Mariam alipiga kelele,
muda huo huo baba yake Mariam akatoka ndani.
“Vipi kuna nini?”
“Mariam amekuja
analia...kaanguka chini kabla hata sijajua kinachomsumbua!”
“Amesema ana tatizo gani?”
“Hajasema chochote, tumpeleke
hospitalini kwanza, hayo mambo mengine tutajua baadaye!”
“Sawa!”
Hawakuwa na muda wa kupoteza,
wakamwingiza Mariam kwenye gari na kumpeleka katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili. Nusu saa baadaye tayari walishafika hospitalini na Mariam apelekwa
katika chumba cha mapumziko kwanza kwa ajili ya kupewa huduma ya awali.
“Nini kimempata?” Daktari
aliwauliza wazazi wa Mariam.
“Ameanguka ghafla!”
“Kabla ya hapo alikuwa
anaumwa?”
“Kwakweli hatuna uhakika
maana alitokea kwa mume wake asubuhi hii akiwa katika hali hii, inawezekana
amegombana naye!”
“Mmejaribu kumtafuta kwenye
simu?”
“Ndiyo, hapatikani.”
“Ok! Subirini kidogo nje,
acha sisi tufanye kazi yetu!” Daktari yule akasema akiwatizama wenzake ambao
walitingisha vichwa kumuunga mkono alichokizungumza.
Wazazi wa Mariam wakatoka nje
na kuwaacha madaktari wakijaribu kuokoa maisha ya Mariam.
“Sijui atakuwa amepatwa na
nini mwanetu jamani!” Mama Mariam akamwambia mume wake.
“Inawezekana kuna kitu
wamekorofishana na mume wake, maana naona hata afya yake siyo nzuri kabisa.”
“Mungu amsaidie apate nafuu
kwanza, tutazungumza naye baadaye!”
Waliendelea kuzungumza juu ya
afya ya mtoto wao hadi saa moja baadaye, mmoja wa madaktari waliyekuwa
wakimhudumia Mariam alipotoka nje.
“Anaendeleaje sasa?” Mama
Mariam alikuwa wa kwanza kumuuliza daktari.
“Msijali, inabidi mkubaliane
na matokeo, maana hatuwezi kubadili kitu kilichopo!” Daktari akasema kwa
utulivu sana.
“Dokta sema tu, nini
kimetokea?”
“Punguzeni wasiwasi kwanza,
tulieni...”
Beyond Love- 28
Anapelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya
matibabu ambapo anaingizwa katika chumba cha wagonjwa wa awali kwa ajili ya
kupatiwa huduma ya kwanza.
Ghafla daktari anatoka nje, uso wake ukionekana kuwa na
jambo lililotokea. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO mwenyewe...
Mwili wa mama yake na Mariam
ghafla ulikuwa kama umemwagiwa maji ya baridi, alishahisi lazima mwanaye
atakuwa amekubwa na matatizo makubwa sana, kitu pekee ambacho kilizunguka
ubongoni mwake ilikuwa ni kiifo! Kwa vyovyote vile uso wa daktari yule
ulisomeka kwamba taarifa zilizokuwa zikiwajia baadaye zilikuwa za msiba.
Machozi kama maji yalianza
kutiririka ghafla machoni mwa mwanamke huyo ambaye uso wake ulishajaa
makunyanzi. Machozi yake yalisbabisha hata baba yake na Mariam naye apatwe na
wasiwasi mkubwa sana. Hisia za mwanaye alikuwa marehemu ziliutawala moyo wake
kwa kasi ambayo hata yeye hakujua ilipotokea!
“Dokta kuna nini, mbona
unatutisha?” Baba yake na Mariam akauliza akiwa na wasiwasi mwingi sana moyoni
mwake.
“Sema tu, kama mwanangu
amekufa, hakuna jambo jipya hapo na wala huna haja ya kujaribu kutuficha!”
“Hapana wazee wangu, hebu
tulieni kwanza, hakuna jambo baya lililotokea, na kwa hakika tunahitaji sana
msaada wenu katika tatizo hili!”
“Tatizo gani?”
“La binti yenu!”
“Sawa, kwani amekufa?”
“Hapana...Mariam ni mzima na
kwa bahati nzuri ameshazinduka sasa, lakini kuna jambo limejitokeza ambalo
ndilo lililosababisha nije kuwaona kwanza!”
“Ni nini dokta?” Mama Mariam
alikuwa wa kwanza kuuliza kwa sauti iliyojaa wasiwasi mwingi sana.
Angalau sasa tabasamu la baba
yake na Mariam sasa lilianza kuonekana, uso wenye makunyanzi ulianza kupotea
taratibu na nuru kuanza kushamiri katika nyuso za wazee hawa ambao kwa hakika
walikuwa na mapenzi mazito sana kwa mtoto wao.
“Enhee dokta, tatizo ni
nini?”
“Binti yenu baada ya
kuzinduka tu, ametaja jina la Tom, tena akipiga kelele akidai kwamba
anamnyanyasa sana. Sasa sijui kama mnamfahamu huyo Tom!”
“Ndiyo tunamfahamu!”
“Ni nani?”
“Mumewe!”
“Ameachana naye?”
“Hapana, wanaishi pamoja ila
leo asubuhi hii ndiyo amekuja nyumbani lakini kabla ya kuzungumza chochote
tukashangaa amepoteza fahamu kwa inavyoonekana watakuwa wamekwaruzana kidogo!”
“Ok! Sasa hatua gani
mmekwishachukua kama wazazi?”
“Kubwa ambalo kwetu sisi
lilikuwa la maana zaidi ilikuwa ni kuhangaikia afya ya binti yetu kwanza,
ingawa pia tumejaribu kumpigia mwenziye simu lakini hapatikani!” Baba yake na
Mariam alisema.
“Ok! Poleni sana!”
“Tunashukuru, nini
kinaendelea kwa muda huu?”
“Mariam itabidi abaki hapa
hospitalini kwa siku tatu zaidi, tunahitaji kuwa naye karibu sana kwa kipindi
hiki, anahitaji ushauri wa Kisaikolojia na baadaye tutawapa taratibu za
kuzungumza naye kwa ukaribu zaidi ili kuweka haya mambo sawa!”
“Tunashukuru sana dokta,
tunaweza kumuona?”
“Hakuna shida, lakini
tunashauri msimuulize maswali magumu sana kwa kipindi hiki ambacho anaonekana
kuwa na mawazo sana akilini mwake, msalimieni na mumpe pole tu, tafadhali
msimuulize mambo magumu sana. Akili yake kwasasa inahitaji kupata wasaa wa
kupumzika!”
“Hakuna tabu dokta!”
Dakika mbili baadaye wazazi
wa Mariam walikuwa wameshaingia katika chumba kile ambapo walimkuta Mariam
akiwa amelala juu ya kitanda, macho yake yakiwa yamejaa machozi.
“Mama....baba....” Mariam
aliita akionekana kuwa na majonzi sana.
“Mwanangu, pole sana
mama...utapona mama usijali!” Mama yake Mariam alisema akimwangalia mwanaye
aliyekuwa ametulia kitandani.
Hakuwa na uwezo hata wa kukaa
mwenyewe. Mariam alitia huruma sana, muda huo mama yake alipata nafasi ya
kuweza kugundua kwamba Mariam alikwa amedhoofu sana, afya aliyokuwa nayo,
haikuwa yake ya siku zote. Mariam alikuwa amepungua sana.
“Ahsante mama, lakinia
alichonifanyia Tom kinauma sana mama yangu...nimevumilia lakini nimeshindwa!”
“Amekufanyia nini?” Baba yake
Mariam akadakia.
“Tom ameamua kuwa na mwanamke
mwingine sasa!”
“Umejuaje?”
“Anaishi naye pale nyumbani,
mwanzoni alikuwa anafanya siri, lakini sasa ameweka kila kitu wazi, kaamua kuja
naye nyumbani na ni muda mrefu sasa mimi nalala chumba cha wageni, Tom
amebadilika, ananichukia sana sasa hivi!”
“Usijali mwanangu, kila kitu
kinapangwa na Mungu, binadamu hatuwezi kupanga mambo mama, na hata kama
tukipanga Mungu mwenyewe ndiye mwenye uwezo wa kubadilisha, kitu cha msingi
kwako kwa sasa ni kutuliza akili yako na kumwachia Mungu kila kitu! Yeye ndiye
atakayejua kitu cha kufanya, atakupigania na kukufanya huru tena, mkabidhi yeye
kila kitu na maisha yako yatakuwa mapya mwanangu. Mungu ni kila kitu mama,
asikudanganye mtu mwanangu!” Mama yake
Mariam alihakikisha anamuweka sawa mwanaye ili aweze kukabiliana na tatizo
alilokuwa nalo.
“Lakini mama, hamuwezi
kuzungumza naye, nampenda sana Tom wangu mama, nampenda Tom, nitawezaje kuishi
bila yeye?”
“Sawa, acha tujaribu kwanza,
lakini nakusihi tuliza akili yako mama, afya yako imezorota sana mwanangu,
kumbuka sisi wazazi wako tupo na tunakupenda sana, hatutaweza kukubali tukuache
uteseke, sawa mama?” Mama Mariam alizungumza kwa sauti ya upole iliyojaa
mapenzi mazito.
“Sawa mama, lakini lazima
mjaribu kuzungumza na Tom kwanza!”
“Sawa, usijali!”
Baada ya hayo, wazazi wa
Mariam wakatoka nje ya chumba kile na kuwaacha Madaktari wakiendelea kumtibu
Mariam.
******
“Karibuni sana, sijui
mnamuhitaji nani?” Ilikuwa sauti ya Mayasa ambayo ilitokea puani huku ikiwa na
sifa zote za ushangingi.
“Mwenye nyumba!” Mama yake na
Mariam akasema kwa sauti tulivu sana.
“Hivi nyie ni kina nani?”
“Siyo kazi yako binti,
nahitaji kuonana na mwenye nyumba!” Mama Mariam akasisitiza.
“Unajua nawashangaa sana,
haiwezekani nyie mkawa wageni wa hapa halafu mnashindwa kujua kuwa mimi ndiyo
mama mwenye nyumba!” Mayasa akasema kwa nyodo za wazi kabisa.
Ilikuwa kauli kali ambayo
ilimnyomnyong’onyesha sana mama Mariam na mumewe.
“Sikiliza binti, tunahitaji
kuonana na Tom!” Baba Mariam akasema kwa sauti ya ukali.
“Oh! Tom, sasa mtaingia ndani
au nimuite hapa nje?”
“Mwite huku nje, tutazungumza
naye hapa hapa!”
“Nimwambie ni akina nani?”
“Wageni wake wa kibiashara!”
“Ok!” Mayasa akaondoka na
muda mfupi baadaye, Tom akaja akiwa ameongozana na Mayasa.
“Mnataka nini kwangu?” Tom akauliza
kwa ukali sana.
“Unasemaje?” Baba yake Mariam
akauliza kwa sauti iliyojaa mshangao mkubwa.
“Kwani masikio yako umeweka
pamba? Kwanza ondokeni kwangu, sina muda wa kupoteza kuzungumza na nyie,
mnanipotezea muda wangu wa kustarehe na mpenzi wangu!”
“We’ Tom umechanganyikiwa?
Hujui kuwa sisi ni wakwe zako? Tumekuletea taarifa muhimu, mwenzako amelazwa
Muhimbili!”
“Mwenzangu ndiyo nani?”
“Mariam!”
“Mariam siyo mwenzagu, siwezi
kuishi na mwanamke kama yeye, mwenzangu ni Mayasa! Huyu mnayemuona hapa ndiye
mke wangu ambaye ninampenda kuliko kitu chochote katika maisha yangu, sihitaji
kusikia habari nyingine tofauti na Mayasa wangu. Nawaomba mtoke kwangu!” Tom
alisema maneno hayo huku akibamiza geti na kufunga kwa komeo.
Mama Mariam na mumewe
wakabaki wanaangaliana, machozi machoni mwao ndiyo faraja pekee ambayo
ingewasaidia kwa wakati huo. Wakaangaliana kwa uchungu, wakasogeleana kisha
wakakumbatiana na kuanza kulia. Walishindwa kuelewa ni mkosi wa aina gani
uliompata binti yao.
“Binti yetu wa pekee Mariam,
kwanini anapatwa na balaa kubwa kiasi hiki, kwanini lakini?!” Baba yake na
Mariam alisema huku machozi yakilowanisha shingo ya mkewe aliyekuwa amelala
kifuani mwake.
“Lakini naamini siyo Tom,
yupo aliye nyuma ya akili zake, ni shetani pekee ndiye anayemsumbua!”
“Mungu adhihirishe utukufu
wake!”
“Amen!” Wakatoka kwa pamoja
wakiwa wameshikana mikono, wakalifuata gari lao, wakaingia na kuondoka
taratibu. Msaada pekee uliobakia ulikuwa ni Mungu pekee.
Beyond Love- 29
Huko wanakutana na balaa juu ya balaa, wanaambulia matusi
na kufukuzwa kama mbwa! Mfariji wao pekee aliyebakia anakuwa ni machozi! Kilio
kinatawala! Machozi matupu. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO...
Haikuwa rahisi kugundua
kwamba kwa muda wote wa robo saa Dk. Joseph Kisanga aliuokuwa akiutumia
kuzungumza na Mariam, alikuwa akizungumza mwenyewe! Dk. Kisanga alikuwa
akizungumza kwa sauti ya taratibu, ukimya wa hali ya juu ukiwa umetawala na
akihakikisha kwamba Mariama anarejea katika hali yake ya kawaida, lakini kumbe
akili ya Mariam haikuwa pale!
Mapenzi yake kwa Tom ndiyo
yaliyokuwa akilini mwake na siyo ushauri wa Dk. Kisanga ambao kwake ulikuwa
sawa na porojo zisizo na maana yoyote. Kilikuwa chumba kimya, chenye mwanga
hafifu, lakini kilichokuwa na hewa ya kutosha iliyozalishwa kwa mashine maalumu
ya kisasa.
Mariam akiwa ameketi kwa
mtindo wa kutazamana na Dk. Kisanga ambaye ni Mtaalamu wa Magonjwa ya Afya ya
Akili na Mshauri wa Mambo ya Saikolojia na Maisha katika ofisi yake hii ambayo
siku zote huwa ni tulivu sana akiwashauri watu wengi hasa waliokata tamaa. Ni
Dk. Kisanga ndiye aliyemsaidia mzee Mallya, mfanyabiashara wa maarufu jijini
Dar es Salaam, aliyetaka kujiua baada ya bohari lake la kuhifadhia mizigo
muhimu kuungua na kumsababishia hasara ya mamilioni ya pesa!
Dk. Kisanga pia ndiye
aliyemshauri msanii maarufu Bisongi ambaye aliathiriwa na dawa za kulevya
lakini baada ya kuzungumza naye akimpa ushauri, akakubali kuacha na kubadilika
kabisa! Naam. Dk. Kisanga ni mshauri maarufu ambaye amejizolea umaarufu mkubwa
sana katika kutoa ushauri na kubadilisha maisha ya watu!
Hali ilikuwa tofauti sana kwa
upande wa Mariam. Ilimchukua muda mrefu sana Dk. Kisanga kugundua kwamba muda
wote huo alikuwa akizungumza peke yake.
“Mariam bila shaka tupo
pamoja!” Dk. Kisanga akasema akimtizama Mariam usoni.
Mariam alikuwa kimya.
“Mariam...Mariam...we,
Mariam...!” Dk. Kisanga akamwita kwa mara nyingine.
“Abee Dokta!”
“Mbona kama haupo hapa?”
“Tupo pamoja!”
“Unakumbuka nilizungumza nini
mara ya mwisho?”
“Ndiyo!”
“Nilisemaje?”
“Ah! Dokta...nakuelewa vizuri
sana!”
“Hapana lazima unisikilize
vizuri Mariam, maisha yako yana thamani kubwa sana, hutakiwi kuyapa mapenzi
kipaumbele zaidi kuliko maisha yako. Ni kweli mapenzi yana umuhimu mkubwa sana
katika maisha yako lakini maisha yako yana thamani zaidi kuliko hayo mapenzi
ambayo kwasasa yamekuwa tatizo kubwa kwako....” Dk. Kisanga aliendelea
kumshauri Mariam kwa muda mrefu sana, akijitahidi kuzungumza naye kwa upole
huku akihakikisha hali ya afya yake inarudi kuwa nzuri.
Mariam alionekana kumsikiliza
Dk. Kisanga kwa makini sana, lakini kilichokuwa kikifanyika kilikuwa ni sawa na
mchezo wa kuigiza, kwani alionekana kumsikiliza kwa umakini mkubwa lakini ndani
ya moyo wake kulikuwa na kitu tofauti kabisa, moyoni mwa Mariam kulikuwa na
maandishi makubwa yaliyosomeka; TOM! Ni yeye tu ndiye aliyekuwa wimbo moyoni
mwake.
“Nimekuelewa Dk. Kisanga,
nashukuru sana kwa kubadilisha maisha yangu, naamini sasa nimekuwa mpya na
nitahakikisha natulia na kuishi maisha yangu bila matatizo wala kumuwaza Tom!”
Mariam alisema kwa utulivu sana.
“Nimefurahi sana kusikia
hivyo, amini kila kitu hupangwa na Mungu, hivyo ni wajibu kuhakikisha yeye
anakuwa nguzo yako namba moja katika maisha yako. Nimefurahi sana Mariam, naona
sasa unaweza kurudi nyumbani, hakikisha unafika hapa hospitalini kuonana na
mimi kila mwezi hadi hali yako itakapokaa sawa.”
“Hakuna tabu Dokta, nashukuru
sana!”
“Ahsante!”
Siku hiyo hiyo Mariam
aliruhusiwa kurudi nyumbani akiwa ameonekana kuwa na nafuu kubwa. Wazazi wake
walifika hospitalini na kumchukua kwenda naye nyumbani. Walikuwa na matumaini
makubwa sana ya mwanao kuwa mpya, walimwamini sana Dk. Kisanga kutokana na
uwezo wake mkubwa wa kushauri.
“Vipi mama, unajisikiaje
sasa?!” Mama yake na Mariam alimwuliza akiwa anatizama usoni.
“Nina nafuu sasa mama!”
“Kweli?”
“Ndiyo mama.”
“Kwahiyo unataka kutuambia
kwamba, sasa hivi hali yako imetengemaa.”
Baba yake akadakia.
Mariam hakuwa na jibu!
Alitulia kimya bila
kuzungumza chochote, ni jambo lililowashtua sana, hawakutarajia kama mwanawo
angekaa kimya kwa muda mrefu kiasi kile, hasa kutokana na ukweli kwamba alikuwa
akionyesha ushirikiano wa kutosha kuanzia mwanzoni.
“Vipi mbona umenyamaza?”
“Kuna tatizo baba!”
“Tatizo? Tatizo gani tena, si
umesema unaendelea vizuri mwanangu?”
“Baba bado mawazo juu ya Tom
yananisumbua na kuna jambo ambalo ni bora kama ningelifanya ili kuepukana na
haya matatizo.”
“Ni nini?”
“Nahitaji kuwa mbali na Dar
es Salaam, mbali na Tom, mbali na Mayasa, mbali na Vyombo vya Habari. Sihitaji
kusikia wala kujua chochote kinachohusiana na Tom, nimechoshwa na mambo yake,
nataka kutulia sasa.” Mariam akasema huku akilia kwa uchungu.
“Mwanangu huwezi kuwakimbia
watu na hata kama unaweza, utawakimbia hadi lini?” Mama yake akadakia.
“Naweza mama, inawezekana
kabisa kuwakimbia, sina jinsi zaidi ya kuondoka hapa Dar es Salaam!”
“Uende wapi sasa, uende wapi
mwanangu?” Baba yake akadakia.
“Nitakwenda kwa bibi!”
“Yupi?”
“Wa Morogoro, acha niende
nikapumzike Matombo!”
“Lini?”
“Kesho!”
“Mbona haraka sana?”
“Kesho ni siku nzuri sana
kwangu, acha nianze kujiandaa!”
******
Mapenzi ya Tom na Mayasa
yalizidi kupamba moto, Tom akawa hashikiki wala hakamatiki, kila kitu ilikuwa
ni Mayasa. Tayari alishamkabidhi kila kitu katika maisha yake. Siri zote za
kibiashara alikuwa ameshampa, namba zote za siri za kadi zake za benki Mayasa
alikuwa anazijua.
Tom alikuwa amechanganyikiwa!
Penzi la Mayasa lilimchanganya sana kiasi kwamba, alikuwa kama chizi mwenye
akili timamu! Hata yeye mwenyewe alishindwa kuelewa ni mapenzi ya aina gani
yaliyokuwa na nguvu kiasi kile. Hata hivyo alipuuza na kuamini kwamba alikuwa
akimpenda sana Mayasa na hapakuwa na kitu kingine zaidi ya hicho.
Kwa upande wa Mayasa ilikuwa
tofauti sana, hata siku moja hakuwahi kuhisi kumpenda Tom, hilo hata yeye
mwenyewe alilikiri moyoni mwake. Kama alikuwa akimpenda, basi ni kwasababu ya
pesa alizokuwa nazo. Aifurahia kuishi maisha mazuri, huku akisiamia miradi
mbalimbali ya Tom iliyokuwa jijini Dar es Salaam na mikoani. Mayasa alikuwa ni
kila kitu.
Mara nyingi alikuwa akikutana
na marafiki zake na kuzungumza nao juu ya mambo mbalimbali ya kimaisha, siku
zote walishindwa kuelewa ni kwanini Tom alimpenda kiasi kile. Siku zote
aliishia kuwaambia kwamba mapenzi yake ya kweli ndiyo nguzo kubwa inayomfanya
aendelee kufaidi maisha mazuri kwa Tom.
“Shosti sema ukweli bwana,
lazima kuna kitu kipo nyuma ya pazia!” Rukia, mmoja wa marafiki zake alimwuliza
Mayasa.
“Zaidi ya penzi langu, nini
kingine?”
“Sema shoga yetu na sisi
tuwatulize wapenzi wetu, haiwezekani Papaa Bill mpaka anafikia hatua ya
kumuacha mkewe kama hakuna kitu kingine nyuma ya pazia!”
“Aaaah! Bwana...kikubwa ni
utaalamu kitandani...haya inatosha sana shoga zangu, nendeni mkajifunze mambo
ya kitandani....tehe...tehe...tehe....” Mayasa alisema akicheka.
“Lakini ni vizuri ukatuambia
ukweli bwana!”
“Sina ukweli mwingine zaidi
ya huo...” Mayasa akazidi kusisitiza. Hakuwa tayari kutoa siri zake za ndani
kiasi kile.
“Sawa shoga yetu lakini nina
ushauri mzuri sana kwa ajili yako. Huwezi kuwa mjinga kiasi hicho, Papaa Bill
ana pesa nyingi sana na tayari anakuamini kwa kiasi kikubwa, lakini kama
hutakuwa makini, unaweza kuachana naye ukawa huna kitu!”
“Kwahiyo?”
“Lazima ufanye kitu fulani,
uwe tajiri!”
“Kitu gani hicho shosti
yangu?”
“KAMA UNATAKA UTAJIRI WA TOM,
HUNA BUDI KUWA NA ROHO NGUMU! UNACHOTAKIWA WEWE KUFANYA NI KUMPOTEZA!”
“Kumpoteza? Unamaanisha
nini?”
“PAPAA BILL ANATAKIWA AFE!”
Rukia akambia Mayasa ambaye alikuwa kimya sana akiwasikiliza.
Lilionekana wazo
lililomchanganya sana akili yake, alitumia kimya kwa muda mrefu sana bila
kuzungumza kitu, lakini baadaye akafungua kinywa chake na kuzungumza; “Wazo
lako ni zuri sana, lakini sasa nitamuuaje? Na watu wakijua?” Mayasa akasema
akitetemeka kwa hofu.
“Acha ujinga Mayasa,
wewe ni mtoto wa mjini, kama ni kweli
unataka utajiri wa Papaa Bill lazima umwondoe duniani, kama upo tayari sema
nikupe njia nzuri ambazo zitakuwa katika mazingira ya usiri mkubwa, yeye afe
akuache na utajiri wako!”
“Nipo tayari, nakusikiliza!”
Beyond Love- 30
Wakati yote hayo yakitokea, rafiki wa karibu wa Mayasa
aliyeitwa Rukia anamshauri amwondoe Tom duniani ili aweze kumiliki mali zote,
kikiwemo kiwanda cha madini cha Tom Minerals Ltd. Je, atafanikiwa? Nini
kitatokea katika maisha ya Mariam? SONGA NAYO mwenyewe...
Pamoja na ushauri wa
kitaalamu alioupata kutoka kwa Dk. Joseph Kisanga, bado Mariam hakuwa katika
hali yake ya kawaida. Hata yeye mwenyewe alijishangaa, hapakuwa na kitu kingine
akilini mwake zaidi ya Tom. Aliamini pasingetokea mwanaume atakayempenda kwa
mapenzi yake yote kama ilivyokuwa kwa Tom!
Kwake Tom alikuwa ni kila
kitu! Kilichomuumiza zaidi ni majibu ya wazazi wake, kwamba Tom aliwafukuza
nyumbani kwake mbele ya mwanamke wake Mayasa, hilo lilimuumiza sana.
Hakika isingewezekana Mariam,
akavumilia kumuona Tom akiendelea kutesa na Mayasa wake, mbele ya macho yake.
Pengine angejifungia ndani, lakini bado angeweza kumuona kwenye magazeti na
hata kwenye luninga akiwa katika shughuli mbalimbali za kijamii.
Tom asingekwepeka kirahisi!
Kitu pekee kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni lazima Mariam aondoke Dar es
Salaam, aende mbali, kijijini, nje ya mji kusipokuwa na Teknolojia ya
Mawasiliano kabisa. Hiyo ndiyo njia pekee ambayo Mariam alikuwa nayo.
“Ni bora niondoke, nihame
kabisa, sina sababu ya kuendelea kuteseka, pengine ilikuwa lazima niteseke,
niumie, nikose amani, lakini haya yote naamini Mungu wa mbinguni anaona na
atanipigania kwa kila hali ili niweze kushindana na haya majaribu,” Mariam
alimwambia mama yake kwa uchungu, muda mfupi kabla ya kuingia kwenye basi, eneo
la Kituo Kikuu cha Mabasi ya Mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam.
“Usijali mwanangu, hakuna
lenye mwanzo linalokosa mwisho, safiri salama mama, msalimie bibi yako.
Hakikisha unatuliza akili yako mama, huna sababu ya kumfikiria mtu mbaya kama
Tom tena katika maisha yako, fungua ukurasa mpya sasa mwanangu!”
“Nashukuru sana mama!”
“Usijali, lakini bado kuna
kitu ambacho ni muhimu sana ukifahamu mwanangu!”
“Kitu gani mama?”
“Maombi! Unatakiwa uombe sana
mwanangu, msaada pekee kwa sasa ambao upo mbele yako ni kuwa karibu na Mungu!
Ukiweza kutimiza hilo itakuwa rahisi sana kushinda majaribu yaliyopo mbele
yako.”
“Ahsante sana mama kwa
ushauri wako, nafikiri unanijua vizuri sana kuhusu hilo mama yangu, nitakuwa
karibu sana na Mungu wangu kwa kila kitu mama...nakuahidi na itakuwa hivyo
kweli!”
“Nimefurahi sana, nakutakia
safari njema!”
“Ahsante sana mama!”
“Halafu kitu kingine
mwanangu, lazima ujue kwamba wewe bado ni mzuri sana, naamini kuna wanaume
wengi ambao wanahitaji angalau kunywa soda na wewe, kwahiyo huna haja ya
kuhuzunika sana!” Mama yake Mariam alisema akitabasamu.
Mariam naye akatabasamu, tabasamu
la ushindi! Ulikuwa ushindi mkubwa sana kwa mama yake na Mariam, tangu
alipoamka asubuhi, hakuwahi kumuona mwanaye akitabasamu, lakini tabasamu lake
la muda ule, tena la ghafla lilikuwa faraja kubwa sana kwa mama Mariam, sasa
alikuwa ana imani kwamba ufumbuzi umepatikana.
“Nafikiri umenielewa
mwanangu!” Tabasamu la mama yake na Mariam, sasa liliongezeka.
“Mama, kwa utani na wewe!!!”
“Siyo utani mwanangu, wewe ni
binti yangu na sina sababu ya kukutania, ninachokuambia ni kitu cha ukweli
ambacho hata wewe utakidhibitisha, kama utaamua kutulia!”
“Ahsante mama, ahsante sana
mama yangu kwa kuona uzuri wangu, lakini uzuri huu mama, ulikuwa kwa ajili ya
Tom!”
“Tom?!” Mama Mariam akauliza
akiwa ameukunja uso wake.
“Ndiyo mama, Tom!”
“Ndiyo hakutaki sasa mwanangu!”
“Najua siyo yeye!”
“Ni nani?”
“Shetani!”
“Hata kama ni shetani, ndiyo
ampe nafasi kubwa kiasi kile? Wakati mwingine shetani huwa anakaribishwa na mtu
mwenyewe, na ndivyo alivyofanya Tom, yeye ameamua kumkaribisha shetani,
unafikiri kwanini asimchezee kama yeye mwenyewe amemruhusu?”
“Usiseme hivyo mama!”
“Kumbe niseme nini Mariam,
niseme nini?”
“Tunatakiwa kumuombea,
naamini kwa kufanya hivyo siku moja atabadilika, niamini mama!”
Mama Mariam hakujibu kitu
zaidi ya kumtulizia macho mwanaye, macho ambayo hayakuweza kuficha hasira na
chuki za wazi alizokuwa nazo dhidi ya Tom.
“Naomba kukuuliza kitu mama!”
“Uliza!”
“Unamwamini Mungu?”
“Ndiyo, hata yeye anajua
hilo!”
“Vizuri, nina swali lingine!”
“Uliza!”
“Kuna mahali popote ambapo
Mungu amewahi kushindwa?”
“Hapana, yeye ni mshindi siku
zote!”
“Basi ataendelea kuwa mshindi
hata katika hili linalonisumbua na kunitesa mama!”
“Aaaamen!”
“Kwahiyo bado naendelea
kukuomba umuombee!”
“Nitamuombea!”
“Nimefurahi kusikia hivyo,
nimefurahi pia kwa wewe kuwa upande wangu. Nakupenda sana mama...nakupenda
sana!”
“Nakupenda pia mwanangu
mpenzi, nakutakia safari njema!”
“Ahsante mama!” Baada ya hapo
mama Mariam aliondoka kwani dakika moja tu, baadaye basi liliondoka kituoni na
safari ya kwenda Morogoro ikaanza.
Mariam aliweza kuwa macho
hadi alipofika Kibaha tu, baada ya hapo alisinzia kabla ya kupitiwa na usingizi
mzito. Hakujua Chalinze walipita muda gani, hata gari lilipoingia kwenye mizani
eneo la Mikese hakujua, alishtuliwa na abiria aliyekuwa ameketi naye siti moja
gari lilipokuwa likiingia katika katika Kituo cha Mabasi cha Msamvu.
“Tumefika sister amka!”
Kijana huyo akamwambia akimtingisha.
“Mmmmh!” Mariam akaitikia
akionekana kuwa na usingizi.
“Tumefika, inaonekana
umechoka sana!”
“Ah! Ni kawaida, siku zote
huwa napenda kulala nikiwa safarini!”
“Unashukia hapa?”
“Hapana, nitakwenda kushukia
mjini!”
“Sawa basi, mimi nashuka
hapa!” Baada ya abiria waliokuwa wakishukia pale Msamvu kuisha, gari likaondoka
na kuingia katikati ya Mji ya Morogoro likawashusha abiria wote, eneo la
Masika.
Mariam akanyoosha moja kwa
moja akifuata barabara iliyokuwa ikielekea katika Kituo cha Daladala
kilichokuwa kituo cha zamani cha mabasi yanayokwenda mikoani. Kwa bahati nzuri
akapata gari la kwenda kwao, tena lililokuwa likikaribia kuondoka. Akaketi siti
ya dirishani akiwa mkimya sana.
Muda mfupi baadaye safari ya
kwenda Matombo ikaanza. Matombo siyo mbali sana kutokea Morogoro mjini, lakini
kwasababu ya ubovu wa barabara na milima, ilimchukua saa mbili na nusu Mariam
kufika kijijini kwao. Aliposhuka kituoni akakodisha baiskeli ambayo ilimpeleka
nyumbani kwa bibi yake, katikati ya mashamba na mapori makubwa, mwendo ambao
uliwachukua saa nzima na nusu njiani.
Hatimaye Mariam alifika akiwa
amechoka sana, bibi yake alipomuona alimkimbilia na kumkumbatia kwa furaha.
Hata hivyo alishangazwa sana na hali ya afya yake ilivyokuwa imezorota! Baada
ya salamu, bibi alianza kuuliza habari za mjini.
“Wazee hawajambo?”
“Wazima kabisa bibi,
wanakusalimia sana!”
“Nimefurahi sana kusikia
hivyo....enheee, vipi wewe na mwenzako?”
Mariam hakuweza kujibu kitu,
ni kama alikuwa amechomwa na chuma chenye moto katikati ya kidonda kibichi!
Machozi yakaanza kumiminika machoni mwake. Akaanza kulia kwa sauti ya chini.
“Vipi, mbona unalia tena?”
Mariam hakujibu zaidi ya
kuendelea kulia, tena safari hii alilia kwa sauti kubwa zaidi ya awali.
“Sema basi mjukuu wangu, kuna
nini? Au amepata matatizo? Niambie mimi ni bibi yako, nitakusaidia!” Kauli hiyo
ya bibi yake ilizidi kumchoma Mariam ambaye sasa alizidisha kilio chake.
Kazi aliyokuwa nayo bibi
yake, ilikuwa moja tu, kumbembeleza!
*******
Kwa muda mfupi sana, roho ya
Mayasa ilibadilika! Roho yake ilikuwa mbaya kuliko hata ya muuza sumu! Mayasa
alikuwa na roho mbaya kuliko kawaida, hata yeye mwenyewe alijishangaa na
alishindwa kuelewa roho hiyo ya paka alipoipata.
Macho yake mawili yalikuwa
yamemuelekea Rukia ambaye kwa mwonekano wake wa nje, haikuwa rahisi kuamini
kwamba anaweza kumshawishi mtu aondoe uhai wa mtu mwingine kirahisi kiasi kile.
Tamaa ya mali ilimvaa, heshima na umaarufu ulikuwa umemtawala moyoni mwake.
Alikuwa tayari kwa lolote.
“Ni kweli upo tayari?” Rukia
akamwuliza akimkazia macho.
“Nipo tayari kwa moyo wangu
wote!”
“Sawa, sasa ipo njia, lakini
lazima uwe makini sana!”
“Nimeshasema nipo tayari kwa
lolote!”
“Hatutaki utusaliti Mayasa!”
“Ni kitu ambacho hakiwezi
kutokea.”
“Tom anatakiwa kufa, ndani ya
mwezi huu, hatutakiwi kuwa na haraka, unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuongeza
mapenzi yako kwa nguvu, mchanganye kimapenzi sana, toka naye mara nyingi, jamii
ione mapenzi yenu na ikiwezekana wadaku waandike, baada ya hapo kazi itafanyika
kiulaini kabisa!”
“Sawa kabisa...” kila mmoja
alimuunga mkono.
“Lakini nina wasiwasi na
jambo moja!” Mayasa akasema akitetemeka, hakuweza kuificha hofu yake.
Rukia akamkata jicho la chuki
lililojaa mashaka, kwa ilivyoonekana, kama Mayasa angeongea jambo lolote
kupingana na uamuzi wake wa awali, basi hatari ambayo ingekuwa mbele yake
asingeisahau hadi atakapoingia kaburini!
Beyond Love- 31
Mariam
anaamua uamuzi mpya, anakwenda kuishi kijijini Matombo, Morogoro, kwa bibi yake
kwa nia ya kukaa mbali na Tom pamoja na vyombo
vya habari. Hakutaka kusikia kabisa habari za Tom. Wakati hayo yote
yakitokea, shetani wa pesa anamwingia Mayasa, anapanga mipango ya kumuua Tom ili
aweze kurithi mali zote!
Je,
atafanikiwa? Vipi maisha ya Mariam huko kijijini Matombo? SONGA NAYO....
K
|
uulizwa
habari za Tom, ilikuwa ni sawa na kumchoma kwa msumari wenye moto, katikati ya
kidonda kibichi kilichokuwa moyoni mwake. Alitegemea kuulizwa na bibi yake juu
ya Tom, lakini siyo mapema kiasi kile. Hata kama asingeulizwa, lazima angesema,
kwani ndiyo sababu hasa iliyomfanya awe kule kijijini.
Moyo
wa Mariam ulimuuma sana, alishindwa kuelewa ni mapenzi ya aina gani aliyokuwa
kwa Tom, aliumizwa zaidi na jinsi alivyokuwa akimpenda kwa moyo wake mtu ambaye
hakuonyesha kushtuka kabisa na penzi lake. Bibi yake alikuwa amemtonesha!
“Nyamaza
mjukuu wangu, lakini lazima unieleze ukweli wa kilichotokea!” Baada ya Mariam
kutulia, bibi yake akamwambia.
“Bibi
kuna matatizo!”
“Ni
nini?”
“Tom
bibi, Tom ameniacha!”
“Amekuacha?””
“Ndiyo
bibi!”
“Sababu?”
“Hakuna!”
“Haiwezekani,
lazima kuna kitu umemuudhi mwenzako, lakini wazee wameshindwa kumaliza huko
nyumbani?”
“Walikwenda
kwake lakini walifukuzwa na Tom na mwanamke wake!”
“Mwanamke
wake? Unataka kusema kwamba Tom ana mwanamke mwingine?”
“Tena
anaishi naye pale nyumbani, mimi nilikuwa nalala chumba cha wageni, baada ya
kuchoshwa na mambo yao, ndiyo nikaondoka kwenda nyumbani, huko napo ndiyo....”
Mariam akamsimulia bibi yake kila kitu, hadi alipofikia hatua ya kulazwa katika
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
“Pole
sana mjukuu wangu, wewe baki hapa nyumbani, pumzika kwanza, utulize akili yako,
mambo mengine yatafuata baadaye, naamini hali yako itarudi kuwa nzuri. Hapa
utakula kambale na mboga za majani na afya yako itarudi kama zamani, sawa
mama?!” Bibi yake akamwambia kwa sauti iliyojaa mapenzi mazito.
“Ahsante
bibi, nimefurahi sana, umenifurahisha sana kwakweli, naanza kujiona mpya sasa.”
“Kama
ndivyo kweli, basi Mungu wa Mbinguni ashukuriwe!”
“Amen!”
Maisha
yaliendelea kijijini kama kawaida, Mariam akiwa anamsaidia bibi yake kazi za
kilimo. Aliyafurahia mno maisha ya pale kijijini, kwani kama alivyotarajia
awali, hapakuwa na mawasiliano ya aina yoyote, kitu ambacho ndiyo haswa alikuwa
akikitegemea.
Afya
yake ikaanza kurejea taratibu hadi ilipotengemaa kabisa, wazazi wake kila
walipokwenda kumtembelea walikuta mabadiliko! Furaha ikarudi katika maisha
yake. Ingawa ilikuwa kazi ngumu sana, lakini alijishangaa aliwezaje kumsahau
Tom, mwanaume ambaye kwake alikuwa sawa na Wimbo wa Taifa!
Alifurahishwa
sana na mabadiliko yake, kwa bahati nzuri bibi yake alishajua kwamba kutaja
jina la Tom ni sawa na kuchochea matatizo aliyokuwa nayo, hivyo hakuthubutu
kutaja jina la Tom katika mazungumzo yao. Siku zote alikuwa akimfundisha maisha
ya kijijini na jinsi wazee wa zamani walivyoweza kuishi maisha marefu kijijini
kutokana na aina ya vyakula wanavyokula.
“Kwahiyo
bibi, unataka kuniambia kwamba hata mimi sasa nitaishi maisha marefu kwasababu
nipo huku?”
“Bila
shaka mjukuu wangu!”
“Lakini
bibi ukiachana na vyakula, ni nini kingine kilichowafanya wazee wa zamani
waishi miaka mingi zaidi kuliko hivi sasa?”
“Mazingira
pia yanachangia, unajua Mariam, huku kijijini kila kitu ni cha asili. Hakuna
kuvuta moshi wa dizeli wala petroli, hakuna mionzi ya minara ya simu, moshi wa
viwandani wala dawa zenye kemikali, hizi ni sababu kubwa sana zilizowafanya
wazee wa zamani waishi umri mrefu!”
“Sasa
naanza kuelewa!”
Mariam
alikubali maisha mapya, akajifunza vitu vipya kila siku. Hakika aliyafurahia
maisha ya kijijini. Aliona ni bora kuishi maisha yale kijijini, kuliko kuishi
Dar es Salaam lakini akiumizwa na kukosa amani ya kuendelea na maisha. Maisha
ya kijijini yalikuwa chaguo lake la kweli na hakuwahi kuyajutia.
********
Kitendo
cha Mayasa kusema kuna jambo lililompa wasiwasi, kilitoa tafsiri tofauti kwa
Rukia. Msichana huyu ni katili na siku zote hakupenda kabisa msaliti katika
mipango yake. Alimwangalia Mayasa kwa jicho la hasira akisubiria azungumze
jambo lolote ambalo ni kinyume na makubaliano yao ili amuadhibu.
Mayasa
akawaangalia wote kwa zamu, kisha akatingisha kichwa kama anayesikitishwa na
jambo ambalo angelitamka.
“Una
nini?”
“Nimeshasema
kwamba kuna jambo linanitatiza kidogo!”
“Sema
ni nini?”
“Hivi
Rukia, askari hawawezi kujua kweli?”
“Labda
uwaambie wewe, tena naomba nikuambie jambo moja, sina muda wa kupoteza zaidi
juu ya jambo hili...ni hivi, leo jioni tutakutana katika kikao cha siri na
vijana tutakaowapa kazi hii!”
“Ni
wapi?”
“Mbezi!”
*******
Kilikuwa
chumba kidogo, lakini nadhifu na kinachovutia, kikiwa na uwezo wa kuhudumia
watu ishirini kwa wakati mmoja. Ndani ya chumba hicho kilichokuwa na kiyoyozi,
kulikuwa na watu sita waliokutana katika kikao cha siri usiku huo.
Watu
hao walikuwa ni Rukia, Mayasa na vijana wanne ambao walikuwa maalumu kwa
kukodiwa kwa ajili ya kufanya mauaji. Wote walikuwa kimya, vinywani mwao,
ukitoka moshi mzito wa sigara ambao wakati mwingine walikuwa wakiutolea puani
na masikioni! Baada ya ukimya wa muda kupita, Rukia aligonga meza kwa nguvu!
“Tumekutana
hapa kwa kazi moja muhimu iliyopo mbele yetu, kama nilivyotangulia kusema
awali, Papaa Bill anatakiwa aondoke duniani, tena ndani ya mwezi huu! Malipo
yenu ni mazuri sana na leo mtapata malipo ya utangulizi!” Alisema Rukia,
akiwatazama wote kwa zamu.
“Hakuna
tabu sister Rukia, nafikiri unatuamini katika michongo hii, sisi hatuna noma,
tupeni cash, tufanye kazi!”
“Hakuna
shida, suala la pesa siyo tatizo kwangu, chukueni hizi kwanza na ninaomba baada
ya wiki mbili Papaa Bill awe na jina lingine! Marehemu nadhani ni jina
litakalomfaa zaidi!” Mayasa alisema akitoa shilingi milioni tano kama fedha za
utangulizi na kuwapatia wale vijana.
“Hakuna
tabu, tunakuhakikishia kazi nzuri baada ya huo muda uliosema.” Mmoja wao ambaye
ndiye aliyepokea zile fedha alisema.
“Kilichobaki
ni utekelezaji tu!” Mayasa akasema.
“Kuhusu
hilo, usijali kabisa, hawa vijana nawaaminia!” Rukia akasema.
“Sawa,
tutaona!” Kikao kikaahirishwa.
******
Alichokifanya
Mayasa ni kuwa karibu zaidi na mume wake kuliko kipindi kingine chochote
walipokuwa wakiishi na Tom. Alijifanya
kumpenda zaidi, kuwa karibu naye zaidi kuliko kawaida. Tom akafurahi sana,
akazidi kumpa siri zake za biashara akiamini alikuwa mke mwema wa maisha yake.
Hakujua
kilichokuwa nyuma ya pazia, laiti kama angejua alikuwa katika hatari ya kufa
wakati wowote, angeachana naye haraka sana, lakini jambo hilo hakulijua kwani
lilikuwa siri kubwa sana. Maisha yaliendelea kama kawaida, Mayasa akiendelea
kuwasiliana kwa karibu na vijana waliopewa kazi ya kumuua Tom na kuelekezekana
kila kitu kwa hatua.
“Nadhani
sasa kila kitu kipo tayari, mnaweza kukamilisha hiyo kazi!”
“Poa
sister, ungependa iwe lini?”
“Kesho
usiku, miye nitakuwa nyumbani, halafu nyie mtamtegea jirani na nyumbani mpaka
atakapoingia, lakini muda wake mara nyingi ni saa mbili na madakika hivi,
lakini haifiki saa tatu!”
“Umesomoka!”
Siku
iliyofuata, kuanzia saa moja na nusu jioni, nyumba ya Tom ilikuwa imezungukwa
na vijana sita wenye silaha, wakisubiria muda atakaorudi! Kama kawaida yake,
saa mbili na robo alikuwa getini akipiga honi mfululizo ili afunguliwe lakini cha ajabu hakuna
aliyetokea kumfungulia!
“Shiiit!
Huyu mwanamke vipi, kwanini hanifungulii, ngoja nishuke nikagonge mwenyewe!”
Tom akasema akifungua mlango wa mbele ili atoke, lakini kabla hajafanya hivyo
akashangaa akihisi kitu cha baridi kikigusa shingoni mwake.
“Tulia
hivyo hivyo, nyoosha mikono yako juu na ufuate maagizo yote tutakayokuambia!”
Alisikia sauti ya mtu ikimuamrisha nyuma yake.
“Kuna
nini tena jamani?”
“Hatubishani,
lakini kama utaleta ubishi wa aina yoyote nakulipua sasa hivi!”
Sekunde
chache baadaye, Tom alikuwa amezungukwa na watu sita waliokuwa wanaonekana
dhahiri kuwa ni watu wa mazoezi. Alishajua kwamba kifo chake kilikuwa
kimekaribia! Isingekuwa rahisi akubali kufa kijinga kiasi kile, alitakiwa
kufanya jambo fulani ili aokoe roho yake.
“Jamani
kama ni pesa au kitu chochote cha thamani mnataka, niambieni niwape lakini
mniachie roho yangu, nawaombeni sana!”
“Hatuna
shida na pesa zako!”
“Sasa
kumbe mnataka nini jamani?!” Tom akasema akitetemeka kwa woga.
“Tunahitaji
roho yako!”
“Roho
yangu?”
“Ndiyo,
unatakiwa kufa Tom!” Tom akachanganyikiwa zaidi.
“Sikilizeni
ndugu zangu, mnajua...” hakupewa nafasi ya kumalizia sentesi yake.
“Hivi
kwanini tunamkawiza?”
“Mlipue!”
Mwingine akadakia.
Hakuna
aliyezungumza tena baada ya hapo, muda mfupi baadaye ulisikika mlio wa risasi.
Wale vijana wakatoweka na kumuacha Tom akiwa ameanguka chini hoi, damu
zikimvuja mwilini. Tom alikuwa hajitambui!
Beyond
Love- 32
Alipopona
akaamua kwenda kupumzika kwa bibi yake, Matombo, Morogoro. Huko nyuma, Mayasa
anapanga mauaji ya Tom. Siku ya tukio Tom alishangaa anapiga honi lakini
hafunguliwi, alipoamua kushuka ili akagonge geti, ndipo alipokutana na mdomo wa
bastola na kuwekwa chini ya ulinzi! Sekunde chache baadaye, Tom alikuwa chini,
akivuja damu baada ya kupigwa risasi!
Je,
nini kitatokea? SONGA NAYO....
M
|
lio
wa risasi ulisikika mara tatu, lakini baada ya hapo muungurumo wa gari
ukasikika. Hiyo ilimaanisha tayari wauaji walikuwa wameshatoweka eneo la tukio.
Ndani ya dakika tatu tu, watu walikuwa wamejaa getini mwa nyumba ya Tom
wakishuhudia Tom alikiwa hajigusi chini, huku damu zikimtoka kwa wigi!
“Mume
wangu oh! Mume wangu jamani...” Mayasa naye alitoka nje na kuanza kulia,
akamlalia Tom, huku akisikilizia mapigo yake ya moyo kuhakikisha kwamba alikuwa
amekufa au lah!
“Nitabaki
na nani miye...Tom wangu jamani...” Mayasa alizidi kupiga kelele.
Watu
walimuonea huruma sana, walijua ni kaisi gani alikuwa anaumia kutokana na
matatizo aliyopata mumewe. Hakuna aliyejua kwamba yote aliyokuwa akiyafanya
ilikuwa ni maigizo tu! Siri hiyo aliijua yeye mwenyewe.
“Lakini
wezi gani wa mapema hivi?’ Mtu mmoja aliyekuwa kwenye tukio lile aliuliza.
“Hata
mimi nashangaa...” mwingine akadakia.
“Mnashangazwa
na nini jamani, kama watu wanaiba kwenye benki mchana inashindikana vipi kwa
muda huu?”
“Lakini
mbona hawajachukua kitu?”
“Hata
mimi nashangaa!”
Kila
mmoja alikuwa anaongea lake, lakini wengi walishangazwa sana na majambazi hao,
ambao hawakuiba kitu chcohote zaidi ya kumdhuru Tom na kuondoka zao. Ilionekana
kuwepo kwa kitu kilichojificha, kitu ambacho hakuna ambaye alikuwa anakijua.
Muda
mfupi baadaye watu walijadiliana na kuamua kumkimbiza Tom katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili. Akalazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Muda wote huo
Mayasa alikuwa analia sana, alionyesha huzuni kubwa, lakini moyoni mwake
alikuwa akitamani sana Tom afe, hilo ndilo lililokuwa akilini mwake.
Kilichoonekana
usoni mwa Mayasa kilikuwa tofauti kabisa na kilichokuwa moyoni mwake. Mayasa
alikuwa na roho mbaya kuliko hata ya
muuza sumu! Aliweka mbele masilahi yake baada ya kifo cha Tom.
“Samahani
Dokta naweza kumuona mume wangu?”
“Hapana,
yupo kwenye uangalizi maalum kwa sasa, tafadhali nenda urudi kesho asubuhi!”
“Lakini
atapona?”
“Tumuombe
Mungu, tutajitahidi kufanya kila tutakaloweza, lakini nguvu za Mungu ndizo
zinazohitajika zaidi katika hili.”
“Ahsante
sana Dokta.”
*****
Kilikuwa
chumba kidogo, kizuri, chenye hewa safi ya kiyoyozi, ndani ya chumba hicho
kulikuwa na vijana wanne na wasichana watatu, hiyo ndiyo ilikuwa Kamati nzima
ya mauaji ya Tom. Wote walikuwa kimya, wakimtizama Rukia ambaye alikuwa ndiye
Kiongozi wa Kamati hiyo. Rukia akapiga meza kwa nguvu!
“Nina
furaha sana, nina furaha kwasababu kazi ambayo tuliwatuma, mmeikamilisha ingawa
siyo kwa kiasi kikubwa!” Rukia alianza kuzungumza.
“Samahani
sister!” Mmoja wa vijana wale akasema.
“Nakusikiliza!”
“Kwanini
unasema siyo kwa kiasi kikubwa?”
“Acha
wasiwasi kijana, nimesema siyo kwa kiwango kikubwa kwakuwa hajafa lakini
nafikiri Mayasa atakuwa na majibu mazuri juu ya hilo kwakuwa yeye ndiye
aliyeenda naye hospitalini!”
“Ni
kweli Rukia, hali yake siyo nzuri, hana dalili za kupona kabisa, hadi sasa hivi
hajazinduka, naona lazima atakufa tu!”
“Ni
kweli kabisa!”
“Na
hilo ndiyo lengo letu.”
“Kikubwa
zaidi kilichotukutanisha hapa ni kuwalipa pesa zenu zilizobakia, lakini kama
tukihitaji msaada wenu baadaye tutawajulisha na tafadhali mtoe ushirikiano.”
“Hakuna
tabu sister Rukia.”
“Sawa..
Mayasa...” Rukia akaita.
“Nakusikiliza.”
“Wapatie
mzigo wao uliobakia.”
Mayasa
hakuwa na kitu cha kuzungumza zaidi ya kuchukua fedha kwenye pochi yake na
kuwakabidhi.
“Tunashukuru
sana kwa msaada wenu, lakini lazima jambo hili liwe siri,” Mayasa akasema.
“Siyo
tu, siri bali kama tutaisikia mahali popote, basi mjue kuwa kifo kitakuwa
jirani zaidi na nyie!”
“Kuhusu
hilo huna sababu ya kuwa na wasiwasi nalo, kwani ni kazi ya kwanza tunafanya na
wewe?”
“Lakini
watu wanabadilika!”
‘Watakuwepo
ila siyo sisi!”
“Nimefurahi
kusikia hivyo!” Baada ya hapo kikao kikaahirishwa.
Siku
iliyofuata, asubuhi na mapema Mayasa alikuwa ameshafika hospitalini, alikuwa
makini sana na Tom, akihakikisha anamhudumia kwa karibu, lakini nia yake ya
moyoni ilikuwa ni Tom afe, alichukia sana kumuona Tom akiwa bado anaendelea
kuwa hai, ingawa alikuwa anapumua kwa msaada wa mashine.
Aliendelea
kuwa karibu na Tom siku zote, hakuna aliyejua kilichokuwa akilini mwa Mayasa,
kilichokuwa kikifanyika ilikuwa ni mchezo wa kuigiza tu, siri ambayo aliitunza
moyoni mwake.
Wiki
moja baadaye hakuona sababu ya kuendelea kumficha mama yake Tom juu ya hali ya
mwanaye. Akafanya mawasiliano haraka, ambapo siku iliyofuata mama Tom alikuwa
ameshafika Dar es Salaam, akipokelewa na Mayasa. Siku zote mama yake Tom,
hakuwa akimpenda Mayasa, lakini kwasababu alishamuomba sana mwanaye aachane
naye na akakataa, hakuwa na sababu ya kuendelea kuingilia mapenzi yao.
“Enhee
vipi hali yake?” Mama Tom aliuliza mara baada ya kufika nyumbani na kuketi
sofani.
“Pumzika
kwanza mama!”
“Hapana,
lazima nijue hali ya mwanangu!”
“Hana
hali mbaya sana mama, lakini kesho asubuhi tutaongozana pamoja kwenda
kumtizama, ila nimewasiliana na daktari wake amesema hali yake sasa siyo mbaya
sana!”
“Fahamu
zake zimesharudi?”
“Bado,
lakini ana nafuu kubwa!”
Mama
Tom alimpenda sana mwanaye, hakuwa tayari kumuona anakufa akiwa mdogo kiasi
kile, kwa maisha ya shida ambayo amekulia, aliamini alipaswa kuendelea kuwa hai
ili ale matunda ya jasho lake.
Kila
alipokumbuka siku aliyotoka kwenye mgodi unaotitia akiwa na madini kwenye mfuko
wake wa salufeti, alitokwa machozi. Kwake Tom alitakiwa aendelee kuyafaidi
maisha! Kufa mapema kiasi kile ilikuwa ni pigo kubwa sana kwake. Mayasa alipata
kazi ya kumbembeleza mama Tom, ambaye hakunyamaza mpaka sauti ilipoanza kukauka
ndipo akanyamza na kupitiwa na usingizi.
Yeye
ndiye aliyemwamsha Mayasa asubuhi, akimkumbusha kuwahi hospitani kumwona Tom.
Walipoingia wodini na mama Tom kumuona mwanaye akiwa amefungwa mashine za
kupumua, alichanganyikiwa! Tom alikuwa na hali mbaya sana na hadi wakati huo
alikuwa hajitambui!
Ghafla
mama Tom akaanza kuhisi kizunguzungu kikali, mwili wake ukaanza kupoteza nguvu
taratibu, kisha akaanguka chini kama mzigo! Muda huo huo akakimbizwa wodini na
kuanza kushughulikiwa. Hata hivyo hali yake ilizidi kuwa mbaya, usiku wa siku
ile ile, mama Tom alifariki dunia!
“Pole
sana dada, mgonjwa ni nani wako?” Daktari aliyekuwa akimhudumia alimwuliza
Mayasa akifikiria jinsi ya kumweleza juu ya kifo cha mama huyo.
“Mama
mkwe wangu, kwani vipi?”
“Kwa
bahati mbaya sana, ameshafariki dunia!”
“Unasema?”
“Usijali
ni mambo ya kawaida ambayo unapaswa kukubaliana nayo, hata kama ukilia, machozi
yako hayataweza kumrudisha mama duniani, zaidi utakuwa unajiumiza mwenyewe.”
“Lakini
kwanini inakuwa kwangu, nina mkosi gani mimi jamani! Mume wangu amelazwa na
mpaka sasa hivi hajarejewa na fahamu, mama naye amefariki, nitakuwa mgeni wa
nani mimi?”
“Usijali
dada yangu, kubaliana na hali halisi, hatuwezi kubadilisha kilichotokea, zaidi
unapaswa kumshukuru Mungu maana ameagiza tushukuru kwa kila jambo.”
“Ahsante
sana Dokta, nashukuru. Acha nikawapashe habari ndugu zetu na kuandaa taratibu
za mazishi.” Mayasa akasema na kuondoka.
“Sawa.”
Mayasa
aliondoka akiwa na mawazo mengi sana kichwani mwake, hakuona sababu ya
kuendelea kuishi nyumbani kwa Tom, alishachuma mali za kutosha kwa kipindi
kifupi sana ambacho Tom alikuwa amelazwa hospitalini. Aliweza kufanya hivyo
kwasababu Tom alikuwa akiweka mambo yake wazi.
Alishachukua
fedha katika akaunti zote na kuziacha nyeupe kabisa, madini yaliyokuwa
yakihifadhiwa chumbani nayo aliyachukua na kuyauza. Hakurudi tena hospitalini
kumuangalia Tom wala kuuchukua mwili wa mama mkwe wake kwa ajili ya mazishi.
Wiki
moja baadaye, kila kitu kilikuwa tayari na kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni
kuondoka nchini, kwenda zake kujichimbia Uingereza. Hilo ndilo lililofanyika,
Mayasa akapanda ndege na kwenda zake Uingereza, akiwa hajui kabisa
kilichoendelea huku nyuma.
******
Maisha
ya kijijini Matombo, yalianza kumzoea Mariam, kama ilivyokuwa nia yake,
kujitenga mbali na mji ili asiweze kujua habari zinazomhusu Tom na Mayasa.
Alifurahia sana kuishi kijijini na aliyapenda maisha ya kule. Hata afya yake
ilianza kuridhisha. Siku moja alitumwa na bibi yake mjini. Alipokuwa akikatiza
eneo la Nunge akaona meza ya magazeti, hakutaka kuisogelea, maana alijua
pengine angekutana na habari za Tom, jambo ambalo hakutaka litokee.
Katika
hali ya kushangaza sana, akajikuta kuna kitu kinamlazimisha kwenda kwenye meza
ile ya magazeti. Baadaye akaamua kwenda, akijipa moyo kwamba hata kama ataona
habari zake, hazitamuuma sana kwasababu tayari ameshaanza kumzoea!
Magazeti
karibu yote ya siku hiyo, yaliandika habari juu ya kifo cha mama yake Tom,
Mariam alihisi kuchanganyikiwa! Macho yake yakatua juu ya gazeti la Ijumaa. Gazeti
hilo lilikuwa limeandika kwa maandishi yaliyosomeka; ...wakati hali ya Papaa
Bill ikizidi kuwa mbaya, MAMA YAKE MZAZI
AFARIKI DUNIA! Chini ya maneno hayo, kulikuwa na maneno mengine
yaliyosomeka; Mwenyewe yupo hoi Muhimbili, bado hajapata fahamu, mkewe
amkimbia...soma habari kamili uk. 2
Zilikuwa
habari mbaya sana kwa Mariam, akajikuta akipoteza nguvu taratibu, giza totoro
likaanza kupita mbele ya macho yake. Akaanguka chini na kupoteza fahamu.
Beyond Love- 33
Magazeti yote
yaliandika, juu ya taarifa za kifo cha mama yake na Tom, huku Tom mwenyewe
akiwa amelazwa! Mariam anapoteza fahamu.
Je,
nini kitatokea? SONGA NAYO...
|
Alishaumia vya kutosha, alishateseka kiasi cha kutosha,
aliamua kuishi kijijini Matombo ili asizidi kuteseka, alitaka kuwa mbali na
maumivu ya mapenzi. Ni kweli alikuwa akimpenda sana Tom, hata moyo wake
ulimhakikishia jambo hilo, lakini ilikuwa lazima awe mbali na matatizo!
Kumpenda mtu si tatizo, lakini kwa Mariam ilikuwa tatizo!
Alikuwa na kila sababu ya kujitenga na matatizo. Hakutaka kuzidi kujipa mateso
ambayo anaweza kuwa nayo mbali.
Mariam hakuwa na penzi la kinafiki, alikuwa na penzi la dhati
ambalo siku zote lilikuwa hai, lakini hakutaka kumwaga machozi tena, hakutaka
kuumia zaidi, lakini kwasababu tayari alishatambua kwamba moyo wake ulimpenda
sana, akaona njia pekee ilikuwa ni kumkimbia!
Pengine ulikuwa uamuzi wa busara, lakini safari yake ya mjini
ya siku hiyo, ilisababisha matatizo makubwa, ikatonesha kidonda kilichoanza
kukauka. Mambo yakawa yale yale! Hakuweza kuvumilia kusoma habari za Tom akiwa
amelazwa hospitalini, tena akiwa hana msaada wowote, mbaya zaidi mama mkwe wake
akiwa amefariki! Hilo lilimuuma sana na kujikuta akianguka chini na kupoteza
fahamu!
Hakuna aliyekuwa na taarifa za Mariam.
“Vipi jamani?!” Mmoja wa watu waliokuwa wamesimama mbele ya
meza ile ya magazeti alisema.
“Siyo suala la kuuliza, kilichobaki hapa ni kumsaidia tu!”
“Lete gari bro,” jamaa mmoja alijitolea kumchukulia na teksi.
“Mshike huko...tusaidiane jamani...” watu wakasaidiana
kumwingiza Mariam kwenye gari na safari ya kwenda Hospitali ya Mkoa wa Morogoro
ikaanza.
Kutoka Nunge hadi Hospitali ya Mkoa, hapakuwa mbali, dakika
tano tu tayari gari lilikuwa limeshaingia ndani ya Jengo la Hospitali hiyo.
Walipofika mapokezi, waliruhusiwa kwenda moja kwa moja Chumba cha Mapumziko,
akapokelewa vizuri na kuanzishiwa tiba haraka.
“Poleni sana jamani,” Dokta akawaambia wale watu waliompeleka
Mariam hospitalini.
“Tunashukuru sana Dokta.”
“Nani anayehusika zaidi na huyu mgonjwa, nataka kufanya naye
mazungumzo kidogo!”
“Kwakweli hakuna!”
“Hakuna?!”
“Ndiyo hakuna daktari!”
“Unamaanisha nini kusema hivyo, kwahiyo kati ya ninyi nyote
hakuna ndugu wa huyu mgonjwa?”
“Hakuna!”
“Kivipi?!”
“Sisi ni wasamaria wema tu, ambao tumeamua kumsaidia baada ya
kumuona ameanguka na kupoteza fahamu!”
“Ilikuwaje?”
“Kwakweli hatujui, lakini ilikuwa ni mbele ya meza ya
magazeti!”
“Basi hakuna tabu, lakini mnaweza kujitolea pia kumsaidia
malipo ya matibabu yake!”
“Hilo halina tabu.”
“Mungu akubariki kwa hilo, acha sisi tuendelee!”
“Sawa, sijui wewe ni dokta nani?”
“Naitwa Dk. Ringo, tena nilisahau kukufahamisha, sijui na
wewe mwenzangu nani?”
“Naitwa Ramsey Muhando.”
“Nashukuru sana kukufahamu.”
“Nami pia.”
Kazi ya kumtibu Mariam ikaanza, huku gharama zote zikilipwa
na Ramsey ambaye alijitolea.
******
“Sikiliza shoga yangu, mimi sijazoea mambo ya nuksi nyumbani
kwangu, kama nilivyokuambia, mama yake Tom amefariki na sitaki kujihusisha na
jambo lolote linalomuhusu yeye!” Mayasa alikuwa akimwambia Rukia katika kikao
chao kilichofanyika usiku, ndani ya hoteli moja ya kifahari katikati ya Jiji la
Dar es Salaam.
“Kwahiyo sasa utafanyaje?”
“Nawaachia watu wa Halmashauri ya Jiji wazike!”
“Lakini huoni kwamba mambo yanaweza kushtukiwa?”
“Kwanini?”
“Magazeti yameshaandika, halafu nyumbani hakuna msiba,
unadhani utaelewekaje?”
“Kila kitu nimeshakamilisha, nimeshauza vitu vyote, fedha
zilizokuwa benki pia nimekomba zote tena kwenye akaunti zake zote, kuna madini
aliyokuwa akiyahifadhi ndani nayo nimeyachukua. Sina kinachonifanya niendelee
kubaki kwenye ile nyumba, waache wenye moyo mwema watamzika, wakikosekana basi,
bahati mbaya!”
“Safi sana, sasa vipi kuhusu mimi, naambulia nini?” Rukia
akamwuliza Mayasa akiwa anamtizama kwa macho yenye kusubiria jambo fulani.
Mayasa hakumjibu kitu, zaidi ya kumwangalia kuanzia chini
hadi juu, ni kama alikuwa akimchambua!
“Twende!” Mayasa akasema.
“Wapi? Mi’ nataka kujua changu!”
“Ndiyo maana nimekuambia twende!”
“Wapi sasa?”
“Nikakupe chako!”
“Ni nini?”
“Surprise!”
“Okay!” Wote kwa pamoja wakaondoka na kushuka chini ambapo
walipanda kwenye gari la Mayasa na safari ya kwenda kusipojulikana ikaanza.
Rukia alikuwa kimya muda wote wa safari, akiwa hajui ni wapi
hasa walipokuwa wakielekea, maswali tele kichwani mwake yalibaki yanazunguka.
Baadaye gari likasimama nje ya geti jeusi, lenye nyumba moja nzuri sana. Mayasa
akapiga honi mfululizo, mlango ukafunguliwa.
Wakaegesha gari kisha Mayasa akamshika mkono Rukia na
kumtembeza kila kona ya nyumba ile. Ilikuwa nyumba ya kisasa iliyokuwa na kila
kitu ndani, bwawa la kuogelea, gari ndogo ya kutembelea, samani ndani na
bustani nzuri sana iliyokuwa nje.
“Sikiliza rafiki yangu...wewe ni rafiki yangu mpenzi,
nakupenda na ninaheshimu sana msaada wako katika kufanikisha zoezi hili,
kuanzia leo hii ni nyumba yako na kila kitu kilichomo ndani.
“Kwa bahati nzuri, hii nyumba nilijengewa na Tom mwenyewe, na
hati zote zina majina yangu, kwahiyo usiwe na wasiwasi kabisa, hapa ni kwako na
kila kilichomo ndani, kuanzia gari na samani zote, kuishi hapa au kuuza ni
hiyari yako!” Mayasa akamwambia Rukia.
Rukia hakutegemea kama angepewa zawadi kubwa kiasi kile,
kwanza alitumia muda mwingi kuwa kimya akijaribu kutafakari kama ni kweli
kilichokuwa mbele yake kilikuwa yakini, Mayasa akampatia hati zote na kumtoa
wasiwasi kwamba pale palikuwa ni nyumbani kwake na alikuwa na uhuru wa kufanya
jambo lolote apendalo.
“Ahsante sana Mayasa shoga yangu, huu ndiyo urafiki wa kweli,
ni wachache sana wanaweza kuwa kama
wewe!”
“Usijali...sasa sijui utaishi hapa au utauza?”
“Nitauza, siwezi kuishi hapa!”
Ndivyo ilivyokuwa, siku iliyofuata nyumba ilitafutiwa mteja
wa chapchap, ikauzwa kwa bei ya kutupwa! Jioni ya siku hiyo hiyo, Mayasa
akaondoka kwenda zake Uingereza. Hakutaka kuendelea kuishi Tanzania tena,
haikuwa sehemu salama kwake!
Hadi wiki moja baada ya mama yake Tom kufariki bila kutokea
kwa ndugu yeyote, mwili huo ulichukuliwa na Halmashauri ya Jiji na kwenda
kuzikwa. Kama kawaida, magazeti yaliripoti kila kitu, haikueleweka ni wapi
Mayasa, mwanamke aliyekuwa akiishi naye baada ya Tom kumuacha mkewe Mariam,
alipokwenda.
Kwakuwa hapakuwa na ndugu mwingine yeyote, mambo yaliendelea
kuwa giza nene, mwenye majibu alikuwa ni Tom ambaye kwa wakati huo ni kama
alikuwa nusu-mfu!
*******
“Toooom....Toom...Tooom, usife, bado nakupenda, bado
nakuhitaji Tom wangu usife...” Ndiyo maneno aliyozungumza Mariam baada ya
kuzinduka siku tatu baadaye katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro alipokuwa
amelazwa.
“Vipi dada yangu, naomba utulie kwanza...tulia...” Ilikuwa sauti
ya muuguzi ambaye alimwita mwenzake mara moja, ambapo alimuagiza akamwite dokta
haraka.
“Afadhali amezinduka, vipi dada unaendeleaje sasa?” Dokta
akamwuliza akiwa anamtizama usoni.
Mariam hakuwa na la kuongea, alianza kushangaa hadi
aliporudisha fahamu vizuri, hapo ndipo Daktari alipomsimulia kila kitu. Bahati
nzuri, Ramsey mmoja wa watu walioshuhudia tukio la yeye kuanguka, ambaye ndiye aliyekuwa akigharamia
matibabu yake, akatokea. Alifurahi sana kumkuta katika hali nzuri. Akamsimulia
kila kitu kilichotokea, Mariam naye hakuficha chochote kuhusu Papaa Bill ‘Tom’.
Alizungumza kila ukweli unaohusu uhusiano wake na Tom. Historia yake
ilihuzunisha sana, haikuwa rahisi kuamini kama msichana mdogo kama yeye aliwahi
kupitia historia ngumu kiasi kile.
“Pole sana dada yangu, sasa nafikiri ni vyema nikurudishe
nyumbani ukapumzike kwanza!” Ramsey akasema.
“Wapi?”
“Matombo, kwa bibi yako.”
“Haiwezekani!”
“Kwanini?”
“Sitaki!”
“Unataka kwenda wapi?’
“Kama ni kweli unataka kunisaidia, kwasasa nataka kwenda
Muhimbili kuonana na Tom, pili kushughulikia mazishi ya mama mkwe wangu!
Nampenda sana mama...nampenda, najua alikuwa akitamani sana niishi na mwanaye,
lakini Tom alimpuuza mama yake. Lazima nionyeshe mapenzi yangu kwake hata kama
amekufa!”
“Sawa nitakusaidia, lakini lazima hali yako itengemae
kidogo!”
“Sawa!”
Siku tatu baadaye, hali ya Mariam ilipokuwa nzuri akaruhusiwa
kutoka Hospitalini. Kama Ramsey alivyoahidi ndivyo alivyofanya, alifika
Hospitalini akiwa amemnunulia nguo mpya na viatu. Mariam akaoga na kubadili
nguo zake kisha wakaondoka na kwenda Msamvu ambapo walipanda basi la Hood kwa
safari ya kwenda Dar es Salaam.
Safari ilikuwa ndefu sana kwa Mariam, lakini hatimaye
walifika Ubungo, Ramsey akakodi teksi iliyowafikisha Muhimbili. Kutokana na
umaarufu wa Tom ‘Papaa Bill’, haikuwa kazi kubwa kufahamu wodi aliyokuwa
amelazwa. Ramsey na Mariam wakaongozana hadi kwenye kitanda cha Tom.
Mariam hakuamini macho yake, Tom alikuwa amelala kimya
kitandani huku akipumua kwa kutumia mashine. Tom alikuwa hajitambui! Mariam
akaanza kulia, hadi muuguzi alipofika eneo hilo na kumwita ofisini kwake.
“Vipi dada, wewe ni ndugu yake na Papaa Bill?”
“Ndiyo!”
“Nani wake?”
“Mume wangu.”
“Mumeo?
“Ndiyo!”
“Wewe ndiye Mariam, tunayekusoma kwenye magazeti?”
“Ndiyo!”
‘Pole sana mdogo wangu, una moyo wa peke yako kwakweli!”
“Ahsante sana sister, vipi maiti ya mama Tom? Nataka
kushughulikia taratibu za mazishi!”
“Pole sana, ni juzi tu alizikwa na Halmashauri ya Jiji baada
ya ndugu zake kutoonekana!”
“What?!” Mariam alitamka maneno hayo, macho yakimtoka.
Hakuwa tayari kuamini alichosikia.
Beyond
Love- 34
Huko
anakutana na habari za kusikitisha sana, anakuta mama yake Tom, ameshazikwa na
Halmashauri ya Jiji, huku hali ya Tom ikiwa mbaya sana. Mariam
anachanganyikiwa.
Je, nini kitatokea? Kwanini Ramsey ameamua
kumsaidia Mariam kwa karibu? SONGA NAYO...
M
|
arehemu
mama Tom alikuwa akimpenda sana Mariam, alimpenda kwa mapenzi yake yote.
Alimfahamu vizuri sana Mariam, wema wake ulikuwa mkubwa sana, alikumbuka kila
kitu alichokuwa akikifanya kwa ajili ya marehemu mume wake.
Alijua
yote hayo yalifanyika kutokana na mapenzi ya kweli aliyokuwa nayo kwa mwanaye!
Hilo pekee lilimfanya ajitahidi kumshauri mwanaye kwa kila hali aachane na wazo
la kutoishi na Mariam. Alishazungumza sana, alionyesha kila dalili ya
kuchukizwa na vitendo vya Tom, lakini kijana wake hakubadilika!
Pamoja
na kwamba Mariam aliamua kwenda kujificha kijijini Matombo kwa ajili ya kukaa
mbali na Tom, lakini hakuwa akimchukia mama yake! Siku alipoona habari kwenye
gazeti la Ijumaa kuwa amefariki dunia, aliona fadhila aliyokuwa akitakiwa
kufanya ni kumzika mama huyo kwa heshima!
Pengine
angeumia sana baada ya kukuta amezikwa na jambo pekee ambalo lingefuata
ingekuwa ni kwenda kutizama kaburi lake na kusoma dua pembeni ya kaburi lake,
lakini sasa ndoto hizo zimezimika kama mshumaa!
Mama
Tom amezikwa na Halmashauri ya Jiji, ni jambo ambalo lilimuumiza sana moyo
wake. Machozi kama maji yakazidi kumiminika machoni mwake.
“Nyamaza
Mariam, huna sababu ya kulia dada yangu, shukuru kwa kila jambo!” Ramsey,
msamaria mwema aliyemsadia kuanzia Morogoro alimwambia.
“Siyo
rahisi Ramsey, ni vigumu sana kaka
yangu!”
“Kwanini....kubali
kilichotokea, unajua hakuna kitakachobadilishwa na machozi yako!”
“Najua,
lakini naamini machozi yangu yatakuwa yanaonyesha kujali kwangu!”
“Kwa
mtu aliyekufa?”
“Ndiyo!”
“Ndiyo
nasikia kwako...lakini Mariam, nyamaza kulia, huna sababu ya kulia kiasi hicho,
utakuwa unajiumiza tu mdogo wangu!” Nesi naye akamwambia Mariam.
“Ahsante!”
“Pole
sana!”
“Nashukuru!”
Sasa Mariam akatulia kidogo.
Ramsey
akamwangalia Mariam aliyekuwa akiendelea kutokwa na machozi mepesi, akachukua
kitambaa chake na kumfuta machozi.
“Kwahiyo
Sister ni nani anayemuuguza Tom kwa sasa?”
“Papaa
Bill?”
“Ndiyo!”
“Hakuna
mtu yeyote anayemhudumia, yupo peke yake!”
“Hali
yake?”
“Kama
ulivyomuona, hali yake siyo nzuri na amepoteza fahamu tangu siku aliyoletwa
hapa!”
“Nini
zaidi kinachomsumbua?”
“Kwani
Mariam ulikuwa wapi hadi usijue yote hayo?”
“Acha
tu dada’ngu, ni stori ndefu lakini fahamu kwamba sijui chochote kinachoendelea,
nitakusimulia baadaye, lakini nafikiri ni vyema ukanieleza.”
“Alivamiwa
na majambazi na kumpiga risasi, kwa bahati mbaya amepooza kuanzia shingoni
kushuka chini, mbaya zaidi hajapata fahamu na anapumua kwa msaada wa mashine!”
“Mungu
wangu!”
“Usijali
Mariam, maadam unajua kuna Mungu, basi huyo ndiye msaada pekee uliobakia kwa
sasa!”
“Nitaendelea
kumuomba yeye siku zote!”
“Amen!”
“Sasa
Mariam, kwahiyo utakuwa ukimuuguza Tom siyo?”
“Ndiyo,
lazima nifanye hivyo!”
“Vizuri
sana!”
Baada
ya hayo, Ramsey na Mariam wakarudi tena wodini kumuangalia Tom, bado hakuwa
amefumbua macho, hali yake ilikuwa mbaya sana. Mariam akamsogelea na kumbusu
mashavuni mwake, kisha akamshika Ramsey mkono na kuondoka naye.
“Tunakwenda
wapi?” Mariam akamwuliza Ramsey.
“Unamaanisha
nini?”
“Namaanisha
tunapokwenda!”
“Mariam
kwani hujui nyumbani kwangu ni Morogoro?”
“Najua!”
“Sasa?”
“Nilikuwa
nataka kujua kama unakwenda huko!”
“Ndiyo
jibu lake!”
“Ramsey
nashukuru sana kwa msaada wako, napenda kukuambia wazi kwamba wewe ni binadamu
kamili, mwenye utu na unayetambua thamani ya ubinadamu. Mungu akubariki sana
kwa hilo, lakini nilikuwa na ombi lingine!”
“Nini?”
“Sitaki
kwenda nyumbani leo, nahitaji kulala hotelini kwa wiki nzima, unaweza
kunisaidia fedha za kulipia pango na chakula kwa muda huo?”
“Hilo
linawezekana, lakini kwanini hutaki kwenda nyumbani?”
“Nataka
akili yangu ipumzike kidogo kwanza, nina mawazo mengi sana Ramsey!”
“Usijali
lakini sioni kama ni busara kukuacha peke yako katika kipindi hiki kigumu,
nafikiri tutafute hoteli kisha nitalipia vyumba viwili, niendelee kukupa
kampani zaidi au unaonaje?”
“Sawa!”
Ndivyo ilivyokuwa, wakaongozana hadi katika hoteli moja nzuri iliyopo Magomeni,
wakalipia na kuingia ndani.
*****
Magazeti
yote ya siku iliyofuata yalikuwa yamepambwa na habari ya Mariam kuonekana
Muhimbili. Yaliandika habari ile kwa undani sana tena yakiwa na picha
mbalimbali zinazomwonyesha Mariam akilia wodini na nyingine akimbusu Tom
aliyekuwa amelala hoi kitandani!
Walielezea
kitendo kile kuwa ni cha kijasiri na kwamba Mariam alikuwa na penzi la kweli.
Habari hizo ziliwafikia wazazi wa Mariam ambao walikasirika sana. Kwanza
walishindwa kuelewa ni kwanini mtoto wao alikuwa anaendelea kumsaidia Tom,
mwanaume ambaye alimtesa, mbaya zaidi aliwatukana hata wao!
“Unaona
mama Mariam, huyu mtoto ana akili kweli?”
“Sijui
amempa nini mwanangu huyu Tom? Huyo mwanamke aliyemuona anafaa, amemkimbia na
nasikia ameuza kila kitu, sasa kipindi cha matatizo ndiyo Mariam awe msaada
kwake, haiwezekani!”
“Haiwezekani
kabisa!”
“Sasa
tutafanyaje?”
“Kilichopo
hapa ni kwenda Muhimbili hadi kwenye wodi aliyolazwa, lazima tutamwona Mariam!”
Wazo hilo liliungwa mkono na wote wawili ambapo waliingia kwenye gari na kwenda
moja kwa moja Muhimbili.
Walipofika
wakaingia katika wodi aliyolazwa Tom, kama walivyokuwa wakitarajia ndivyo
ilivyokuwa. Walimkuta Mariam akimhudumia Tom, machozi mengi yakimtoka. Mama
yake Mariam alipomuona mwanaye alikuwa na hasira sana, akamfuata na kumvuta
pembeni uso wake ukiwa na makunyazi.
“Hivi
we’ mtoto umelogwa? Una akili kweli? Kwani huyu hana ndugu, hana marafiki?
Mabaya yote aliyokufanyia huyaoni? Matusi aliyotutukana sisi wazazi wako
hayakuuma?
“Umelazwa
mara ngapi kwa ajili yake, lakini leo wewe ndiyo unakuwa wa kumsaidia..sasa
sisi kama wazazi wako, tunakuambia toka haraka sana hapo, unatakiwa tuongozane pamoja nyumbani!”
“Najua
nyie ni wazazi wangu, najua kuwa mnanipenda, lakini lazima mzifahamu na
kuheshimu hisia zangu. Mimi nampenda Tom kwa mapenzi yangu yote, siwezi kwenda
na nyie nyumbani nikaamuacha Tom katika hali hii!”
“Unasemaje
wewe mtoto, hivi una akili kweli wewe?” Baba yake Mariam akamwuliza kwa hasira
sana.
“Akili
ninazo tena nyingi sana, lakini penzi langu kwa Tom litaendelea kudumu siku
zote za maisha yangu!”
“Sasa
kama hujatoka kwenye tumbo langu mimi mama yako, endelea kubaki hapa
hospitalini, lakini kama mimi ni mama yako, niliyekuzaa, urudi mwenyewe
nyumbani!” Mama Mariam akasema kwa sauti ya ukali sana, kisha akamshika mumewe
mkono na kutoka nje.
Baba
Mariam alikuwa na hasira sana, hakuweza kuongea neno lolote zaidi ya kuwa
msikilizaji! Baadaye Mariam naye alitoka kwa hasira, akachukua taxi na kwenda
hotelini.
******
Mariam
alipofika hotelini, aliingia chumbani kwake akiwa amechanganyikiwa sana. Kila
alichokifanya aliona kama anakosea! Mawazo mengi yalimchanya kichwani.
Zaidi
ya kufikiria kuhusu wazazi wake ambao walikuwa wanamzuia kumhudumia Tom, lakini
pia aliumizwa na wema wa Ramsey. Hakutaka maumivu tena baadaye, alianza kuhisi
kwamba Ramsey angehitaji kulipwa fadhila.
Hapo
ndipo alipoamua kumpigia simu Ramsey, hakutaka kubaki na mawazo kichwani mwake.
Akachukua mkonge wa simu, kisha akabonyeza namba za chumbani kwa Ramsey, simu
ikaanza kuita, baadaye ikapokelewa na sauti tulivu sana ya Ramsey.
“Yes,
Mariam hapa, naomba uje chumbani kwangu Ramsey!”
“Chumbani
kwako?” Ramsey akauliza kwa mshangao.
“Ndiyo!”
“Kuna
nini?”
“Njoo
tu!” Dakika mbili baadaye Ramsey alikuwa chumbani kwa Mariam akiwa amevaa bukta
na fulana nyepesi, uso wake ukionyesha wazi wasiwasi aliokuwa nao.
“Kuna
nini dada Mariam?”
“Nataka
kujua kwanini unanifanyia yote haya?”
Ramsey
hakuwa na jibu la haraka. Aliangalia juu, kisha akarudisha macho yake chini
kabla ya kuyatuliza usoni mwa Mariam.
“Unasema?”
Ramsey akauliza.
“Kwanini
umekuwa mwema kwangu kwa kiasi kikubwa namna hii?”
Ramsey
alikuwa kimya.
Beyond Love- 35
Huko anakutana na habari za kusikitisha sana! Anakuta mama
yake Tom, ameshazikwa na Halmashauri ya Jiji huku hali ya Tom ikiwa mbaya sana.
Anaamua kumhudumia Tom kwa moyo wote, lakini wazazi wake wanapingana naye,
wakidai kuwa hakuwa mwanaume mwenye mapenzi ya kweli kwani alimtesa sana.
Mariam anaachana na wazazi wake na kurudi hotelini ambapo
alikutana na Ramsey, anamlazimisha amwambie ni kwanini aliamua kumsaidia kwa
kiwango kikuwa kiasi kile. Haijulikani nia ya yeye kuuliza swali hilo.
Je, nini kitaendelea?
SONGA NAYO...
Ramsey aliendelea kuwa kimya,
katika siku ambazo alishangazwa sana na Mariam basi ni pamoja na siku ile.
Swali aliloulizwa lilikuwa gumu sana, gumu kwa sababu hata mazingira ya swali
lenyewe yalikuwa tata! Kuna wakati alianza kuwaza kwamba, inawezekana Mariam
alikuwa akimtaka ndiyo maana akamwuliza swali lile kama mtego.
Macho ya Ramsey yalibaki
usoni mwa Mariam kwa muda mrefu, akimtizama kwa makini na kumsoma uso wake kama
ulifanana na aliyokuwa anayazungumza. Kwa kiasi kikubwa hakuweza kujua nia hasa
ya Mariam ilikluwa nini kwani katika uso wake hapakuwa na kitu hata kimoja
kilichoonekana kushabihiana na maneno yake.
Hakujua kama alikuwa
anamtania au alikuwa anamwekea mitego! Ramsey akabaki anamwangalia Mariam bila
kufungua kinywa chake kusema neno lolote. Sasa Ramsey akaamua kumwangalia Mariam
kwa umakini zaidi, macho yake yalishuka hadi miguuni mwa Mariam, akaikagua.
Akayapandisha taratibu hadi
kiunoni, hapo akakubali kwamba kweli Mariam alikuwa mwanamke mwenye mvuto wa
kike! Akamwangalia macho yake ya mviringo ambayo yalikuwa pambo tosha katika
chumba kile. Ramsey akahema kwa kasi, kisha akatizama “lips” za Mariam, hakika
zilipendeza sana.
Lakini alikuwa na maswali
yaliyomchanganya kichwani mwake, anaweza kuonekana mwenye tabasamu wakati
alikuwa kwenye kipindi kigumu cha matatizo? Hilo lilizunguka ubongoni mwake
bila kuwa na majibu ya moja kwa moja.
Kila kitu kilikuwa gizani.
Maswali yote hayakuwa na majibu. Mariam ambaye muda wote alionekana kuwa kimya,
sasa alifungua kinywa chake akionekana kuwa na jambo la msingi sana la
kuzungumza naye. Akayatoa macho yake kwa kasi, kama alikuwa haoni vizuri,
akameza fundo moja la mate ambayo bila shaka aliyakusanya kwa muda mrefu sana
mdomoni mwake.
Akawa mtulivu sana, akaanza
kuzungumza: “Nimekuuliza swali Ramsey!”
“Swali?”
“Ndiyo!”
“Mh!”
“Mbona unaguna?”
“Naguna sababu ya maneno yako
Mariam!”
“Yanachekesha au hayana
maana?”
“Siyo kwamba yanachekesha na
wala siyo kwamba hayana maana.”
“Bali?”
“Nina wasiwasi na wewe.”
“Juu ya nini?”
“Ya ulipotoka, sijui kama
umetoka sehemu salama.”
“Nini maana yako?”
“Siyo kawaida yako kuwa hivi
Mariam, nahisi kuna tabia nyingine ambazo unazifanya ambazo mimi nilikuwa
sizijui.”
“Kwanini unasema hivyo
Ramsey?”
“Naweza kukuuliza kitu?”
“Uliza tu!”
“Unakunywa pombe?”
“Hapana.”
“Kweli?”
“Nakuhakikishia, kwani
naonekana nimekunywa?”
“Hapana ila yanayotoka
kinywani mwako ndiyo yanayosababisha nihisi hivyo.”
“Anyway...nisikilize Ramsey,
tufanye hivi, mimi ni mnywaji wa pombe na leo nimekunywa. Halafu baada ya hapo
jibu maswali yangu hata kama ni ya mlevi sawa?”
“Usiseme hivyo...”
“Sasa niseme nini?
Inawezekana umesahau swali, nitakukumbusha...wewe ni kijana mzuri sana, ambaye
roho yako inafanana na tabia yako! Nashukuru kwa hilo, lakini naamini una kazi
nyingi za kufanya umeziacha na kuamua kunisaidia mimi katika kipindi hiki kigumu,
je kwanini umeamua kufanya hivyo?” Mariam aliongea maneno hayo huku machozi
yakimlengalenga machoni mwake.
“Mariam acha kulia, naomba
ufahamu kitu kimoja, nimefanya yote hayo kwa sababu ya mapenzi tu, sina kitu
kingine chochote ambacho kimenifanya nikaamua kukusaidia!”
“Unanipenda?”
“Ndiyo...kama dada yangu,
rafiki yangu wa karibu lakini kubwa zaidi natimiza moja ya amri muhimu
tulizopewa na Mungu, tuliagizwa tupendane Mariam, kwanini nisikusaidie kwa
upendo huo?”
“Kweli?”
“Niamini!”
“Hakuna lingine?”
“Lipi tena?”
“Basi nashukuru sana kama ni
kweli hakuna lingine zaidi ya hilo, umenifurahisha sana Ramsey.”
“Usijali.”
Wakaendelea kuzungumzia mambo
mengine, hadi baadaye Ramsey alipoaga na kurudi chumbani mwake. Hata hivyo
Ramsey aligundua kwamba lazima Mariam alikuwa na kitu kilichomchanganya hasa
kutokana na maswali aliyokuwa akiuliza.
Jioni walikutana kwa ajili ya
chakula cha jioni, baada ya kula Ramsey alishindwa kuvumilia kubaki na maswali
mengi kichwani mwake, akaamua kumuuliza Mariam ili kupata ukweli. Mariam
hakuona sababu ya kuficha jambo, akamweleza ukweli jinsi alivyokwaruzana na
wazazi wake hadi kufikia hatua ya kuondoka wodini bila kuwepo kwa maelewano.
“Lakini wale ni wazazi wako
Mariam, lazima uwasikilize!”
“Hujakosea Ramsey, lakini na
wao hawawezi kunichangulia mtu nitakayeishi naye.”
“Ungewapa nafasi kwanza, hata
kama unampenda huyo Tom kiasi gani lakini waliyokuambia yana maana, unampenda
vipi mtu ambaye alikufukuza na kuwatukana wazazi wako?”
“Najua siyo yeye, ni yule
shetani Mayasa niliyekupa habari zake.”
“Hata kama, lakini wazazi
wako walikuwa na hoja ya msingi.”
“Sasa naona unataka
kuniudhi,” Mariam akasema akionyesha hasira.
“Basi Mariam yaishe,” Ramsey
akaamua kuwa mpole.
*******
Mariam akaendelea kumhudumia
Tom kwa karibu sana, kila siku alikuwa akishinda Muhimbili na kurudi hotelini
usiku. Hakutaka mpenzi wake apate shida, alikiri wazi kwamba hatatokea mwanaume
ambaye atampenda kama alivyompenda Tom.
Tom alikuwa kila kitu kwake,
alimkabidhi maisha yake yote, hakujali mateso na manyanyaso yote aliyompa.
Imani kubwa aliyokuwa nayo moyoni mwake ni siku moja Tom angeamka na kuwa naye
kama mke na mume maana Mayasa ambaye kwake alikuwa ni shetani alikuwa
ameshatoroka.
Hakutaka kusikia kuhusu
wazazi wake, aliamua kuishi maisha yake peke yake, huku mtu muhimu aliyekuwa
mbele yake akiwa ni Tom pekee.
Siku moja Ramsey alimtoa
Mariam na kwenda naye ufukweni, hiyo ni baada ya kumweleza alikuwa na
mazungumzo ya muhimu sana ambayo yalihitaji sehemu iliyotulia ili aweze
kumweleza vizuri jambo ambalo Mariam hakulipinga.
Wakiwa katika hoteli moja,
ufukweni mwa Bahari ya Hindi, Mariam ndiye aliyeanzisha mazungumzo baada ya
kuona Ramsey hazungumzi chochote.
“Enheee Ramsey, ulisema una
mazungumzo muhimu na mimi, muda unazidi kwenda, naona ni bora ukaniambia.”
“Ni kweli, tena ni muhimu
sana.”
“Nakusikiliza, bila shaka huu
ndiyo muda muafaka.”
“Mariam nataka kukuambia
jambo moja muhimu sana, muhimu kwako na kwangu, muhimu kwa maisha yako,” Ramsey
alisema kwa sauti ya utulivu sana.
“Nakusikiliza Ramsey.”
“Nafikiri unakumbuka kuwa
mimi ndiye niliyekuokota Morogoro na kukupeleka hospitalini kwa ajili ya
matibabu!”
“Ndiyo nafahamu.”
“Pia mimi ndiye niliyekuleta
Dar ba kukupeleka hadi hospitalini!”
“Ni kweli.”
“Kwamba mpaka sasa hivi mimi
ndiye ninayegharamia mahitaji yote ya Tom na wewe.”
“Ndiyo!”
“Nimekufanyia mambo mengi
sana ili kukufanya mwenye furaha!”
“Hilo halipingiki.”
“Unajua ni kwanini
nimekufanyia yote haya?”
“Hilo litakuwa moyoni mwako.”
“Kipo kitu kilichonisukuma
mimi kufanya yote hayo Mariam, kipo! Tangu nilipokuona siku ya kwanza, niliona
kitu kwako Mariam, nakumbuka uliwahi kuniuliza sababu ya kukufanyia wema wote
huu lakini nilikujibu jibu la uongo kwa sababu muda wa kukuambia haya
ninayokuambia ulikuwa haujafika.
“Nisikilize kwa makini
Mariam, wewe ni msichana mrembo sana, ambaye unahitaji matunzo, unatakiwa ukae
mahali utulie ukila na kunywa kila unachokitaka. Hupaswi kuwa na huzuni wala
mateso kama uliyonayo hivi sasa, hutakiwi kuwa na msiba mzito moyoni mwako kama
ulionao sasa hivi. Urembo wako haufanani na matatizo uliyonayo. Mariam
unatakiwa kubembelezwa!” Ramsey alipofika hapo alitulia kwa muda kisha
akapeleka glasi yake ya maji ya matunda kinywani kabla ya kuanza tena
kuzungumza.
“Mariam mimi nakupenda, tena
nakupenda kwa mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwangu, nipe nafasi nikuonyeshe
raha za ulimwengu. Achana na yule mlemavu kule Muhimbili, kwanza inawezekana
baada ya kupata fahamu akakufukuza, kwanini uumize moyo wako? Nipe nafasi
nikuonyeshe ninavyokupenda Mariam,” Ramsey alizungumza kwa sauti ya upole sana,
akiamini Mariam angemsikiliza.
“Umemaliza?” Mariam
akamwuliza akivuta midomo.”
“Tayari...”
“Sikiliza....tena sikiliza
kwa makini sana, hivyo vijimsaada vyako visiwe sababu ya kunitongoza. Mwili
wangu una thamani sana, tena ni maalum kwa ajili ya mtu mmoja tu, Tom! Huyo ambaye kwako wewe umeona ni mlemavu
lakini kwangu ni mwanaume, tena mume wa ndoa. Kama umechoka kunisaidia, acha!
Sikulazimishi, lakini mwili wangu, sahau!” Mariam akasema kwa kujiamini sana.
Ramsey akavimba kwa hasira,
hakuzungumza neno lolote zaidi ya kusimama na kuanza kupiga hatua moja baada ya
nyingine akimwacha Mariam mwenyewe ufukweni.
Mariam akafikiria kwa haraka,
akaona giza nene lililokuwa mbele yake, kumuacha Ramsey aondoke kulimaanisha
yeye kutokuwa na mahali pa kulala kuanzia siku hiyo, pia asingeweza kumuhudumia
Tom wake, achilia chakula chake yeye mwenyewe.
Mariam akaanza kulia. Ramsey
aliendelea kutembea bila kugeuka nyuma, akiwa amedhamiria kabisa kuondoka na
kumwacha Mariam pale ufukweni. Mariam akasimama na kuanza kumkimbilia Ramsey
huku akiita jina lake kwa sauti kubwa.
“Ramseeeeeeeyyyy.....” Mariam
aliita kwa sauti kubwa sana.
Ramsey akageuka nyuma,
akasimama akiwa tayari kumsikiliza Mariam, hakuhitaji kitu kingine chochote
zaidi ya penzi lake, vinginevyo aliamua kucha kusaidia tena Mariam.
Beyond Love- 36
Je, anataka kuwambia nini? Atakubali kumsaliti Tom wake?
SONGA NAYO...
Ni kama alikuwa amewahi
kukimbia mbio za marathon, lakini haikuwa hivyo. Mariam hakuwahi kufanya
mazoezi ya riadha hata mara moja, lakini siku hiyo alikimbia kwa mwendo wa
ajabu. Hata yeye alijishangaa.
Alimfikia Ramsey akiwa
anahema kwa kasi ya ajabu, akasimama mbele yake huku akiwa ameyatoa macho yake
kama alikuwa akikimbizwa na mnyama hatari. Ghafla macho yake yakaanza kupatwa
na unyevunyevu, baadaye kidogo machozi yakaanza kumiminika machoni mwake.
“Nyamaza Mariam,
nyamaza...kulia kwako hakutasaidia kitu kama...”
“Kama sitakuambia nakupenda
pia...”
“Ndiyo Mariam, kwanini
unataka kuutesa moyo wangu kiasi hiki? Ni nani ambaye angeweza kufanya yote
haya kwa ajili yako? Ni mimi ninayekupenda pekee ndiye niwezaye kufanya mambo
haya.
“Lakini sasa, unadhani
unafanya vyema kufanyiwa yote haya kwa mapenzi halafu wewe ulipe mabaya?
Angalia mara mbili Mariam,” Ramsey alikuwa akizungumza kwa sauti laini,
taratibu na macho yake yakiwa yameganda usoni mwa Mariam aliyekuwa akilia
wakati wote.
Mariam hakuzungumza kitu,
alitulia kwa muda kabla ya kwenda kujilaza kifuani mwa Ramsey. Ramsey alisikia
raha sana kusikia pumzi za Mariam zikitoka kwa shida akiwa amelala juu ya kifua
chake.
“Najua unanipenda sana
Ramsey, najua...nafahamu kwamba ulifanya yote yale kwa sababu ya mapenzi yako
kwangu...lakini pia unatakiwa kufahamu kwamba sikuwa nafahamu haya mambo mpaka
leo uliponiambia, sikujua kama ulikuwa na jambo hilo moyoni mwako.
“Nashukuru sana kwa kunipenda
na kunipa nafasi ya kwanza moyoni mwako, lakini unatakiwa kufahamu kwamba moyo
wangu una makovu, kama ni sumu nilipewa kali, yenye kuua na kukausha kabisa!
Hali yangu siyo nzuri kihisia....
“Najisikia kumpenda mtu mmoja
tu, Tom! Lakini wema unaonipa nashindwa kujua nitakulipa vipi? Najua ni kiasi
gani unavyoumia juu ya penzi lako kwangu, lakini nitafanyaje?” Mariam aliongea
kwa sauti iliyojaa kwikwi huku machozi yakimiminika mgongoni mwa Ramsey
aliyekuwa kimya akimsikiliza kwa makini sana.
“Kipo kitu cha kufanya
Mariam, kipo...”
“Nini?”
“Kunipenda!”
“Ingeweza kuwa rahisi
kukupenda, lakini siyo kukupenda wewe tu, Ramsey hata mwanaume mwingine yeyote.
Ni kweli wewe ni kijana mzuri sana unayevutia kwa kila kitu, lakini moyo wangu
una sumu, hauwezi tena kumpenda mtu mwingine zaidi ya Tom.
“Tafadhali usiumizwe na kauli
zangu, ni hisia za kweli zinazotoka moyoni mwangu, naomba uzipokee kama
zilivyo, nakupenda kama kaka yangu lakini siyo kimapenzi.”
“Kama hunipendi Mariam?”
“Nakupenda sana, tena sana
lakini siyo kimapenzi, labda kama utanisaidia katika hilo!”
“Kukusaidia nini?”
“Kukupenda!”
“Unamaanisha nini?”
“Nisaidie niweze kupenda
tena, moyo wangu sijui una matatizo gani?”
“Una uhakika na kauli yako?”
“Ndiyo!”
“Kweli?”
“Ndiyo...mbona unaniuliza
mara mbilimbili, kwani huniamini?”
“Nakuamini sana...”
“Sema nakupenda sana Ramsey!”
“Nakupenda sana Ramsey!”
“Hebu niangalie!” Ramsey
akamwambia Mariam ambaye alijitoa kifuani mwake na kusimama mbele yake huku
akiwa ameyatuliza macho yake kwa Ramsey.
Ramsey akatabasamu, Mariam
naye akatabasamu pia.
“Unahisi nini?”
“Kukupenda!”
“Kwahiyo mimi sasa ni mpenzi
wako siyo?”
“Ndiyo, lakini nitaomba
msaada mwingine kutoka kwako!”
“Unahitaji kiasi gani cha
pesa?”
“Siyo pesa Ramsey,
sizungumzii pesa!”
“Bali nini?”
“Tom!”
“Tom? Ameingia vipi tena
kwenye mazungumzo yetu?”
“Naomba uniruhusu niendelee
kumsaidia mpaka atakapopona!”
“Akifa je?”
“Hiyo itakuwa mipango ya
Mungu!”
“Ok, hakuna tatizo katika
hilo.”
Wakasogeleana tena,
wakakumbatiana kwa nguvu, wakaanza kupeana mvua ya mabusu motomoto. Wakafungua
ukurasa wa mapenzi. Hapo sasa wakarudi tena ufukweni ambapo walicheza michezo
ya kimahaba mpaka usiku waliporudi zao hotelini.
*******
Moyo wa Mariam ulikuwa na
maumivu makali sana, alikubali machoni tu kuwa na Ramsey lakini moyoni hakuwa
na hata chembe ya mapenzi kwake. Moyoni mwake kulikuwa na mtu mmoja, Tom.
Hakuwahi na wala hakufikiria kuwa na mtu mwingine zaidi ya Tom.
Alikubali ili aweze kuendelea
kupata misaada yake kwani asingeweza kumhudumia Tom akiwa hana fedha.
Kumkubalia ulikuwa mtihani wa kwanza, lakini mtihani wa pili ambao ungekuwa
mgumu zaidi kwake ni kufanya mapenzi na Ramsey.
Alijiapiza kukabiliana na
hilo mpaka mwisho wa pumzi zake. Ni kweli hakuwa na mapenzi naye, lakini
asingeshindwa kujifanya kuonyesha mapenzi yake kwa kila njia, lakini tatizo
kubwa kwake likawa ni mapenzi, hakutaka kabisa kuruhusu mwili wake uguswe na
mwanaume mwingine zaidi ya Tom wake.
Jioni walikuwa wanakula
pamoja hotelini, Mariam akimlisha na kumbusu kila wakati, alionyesha kila
dalili za wao kuwa wapenzi, ingawa Mariam alikuwa makini sana na kamera za
waandishi wa habari hasa za waandishi wa magazeti ya udaku.
“Angalia bwana, haya maeneo
siyo kabisa. Kuna mwandishi mmoja anaitwa Issa Mnally akituona tu, lazima
atatupiga picha na utashangaa tumetoka kwenye gazeti la Risasi!”
“Issa Mnally?”
“Ndiyo...huyu ni mdaku balaa,
hakuna asiyemjua hapa Bongo. Habari nyingi za Tom amekuwa akiziripoti yeye na
kama siyo yeye basi ni Senchawa, hawa wadaku hawafai kabisa!”
“Usijali mpenzi wangu, tupo
kwenye chimbo hapa hawawezi kutuona.”
“Lakini ni vyema tukichukua
tahadhari.”
“Hakuna shida.”
Wakaendelea kula na kunywa
kwa furaha hadi usiku kabisa, walipoamua kuondoka na kwenda vyumbani mwao
kulala. Mariam aliingia chumbani kwake na Ramsey naye akaenda chumbani mwake.
Muda mfupi baada ya Mariam kuingia chumbani kwake, simu ya mezani ikaita.
Haraka akapokea akijua ni lazima angekuwa ni Ramsey.
“Vipi mpenzi wangu, si
tumeachana muda huu tu,” Mariam alisema maneno hayo mara baada ya kupokea simu.
“Siyo shwari darling!”
“Kwanini?”
“Kuna baridi sana, siwezi
kulala mwenyewe, nahitaji sana joto lako!”
“Lakini mbona bado mapema
sana?”
“Mapema kupata joto lako?
Mbona sikuelewi Mariam, naomba uje chumbani kwangu!”
“Sawa,” Mariam akajibu na
kuamka haraka kisha akavaa na kwenda chumbani kwa Ramsey.
Hakutaka kumuudhi tena, lakini
kikubwa ambacho kilikuwa akilini mwake ni kutomuachia kabisa mwili wake. Hilo
alijihakikishia kabisa kwamba lilikuwa ndani ya uwezo wake. Akatoka nje, kisha
akafunga mlango wake na kwenda chumbani kwa Ramsey.
“Karibu mpenzi wangu!”
“Ahsante sana!” Mariam
akaingia na kwenda moja kwa moja kitandani.
Wakalala wakiwa
wamekumbatiana. Katikati ya usiku, Mariam akiwa amelala fofofo, alisikia mikono
laini ya Ramsey ikipita mwilini mwake. Mwanzoni alihisi alikuwa usingizini,
lakini muda ulivyozidi kwenda ndivyo alivyogundua kwamba kila kilichokuwa
kinatokea kilikuwa yakini!
Akashtuka zaidi alipogundua,
Ramsey alikuwa ameshamvua nguo zake zote na alikuwa mtupu kabisa.
“Ramsey unataka kufanya
nini?” Mariam akasema kwa ukali sana.
“Mbona hivyo mpenzi wangu?
Kwani wewe ni nani wangu enheee? Sisi si ni wapenzi, sasa kuna ubaya gani
kufanya mapenzi?”
“Ubaya upo!”
“Kivipi?”
“Hatujajuana vizuri Ramsey,
lazima tupime kwanza kabla ya kuanza haya mambo!”
“Ninazo kondom!”
“Sipo tayari....kwanza huwa
situmii kondom!”
“Mbona unakuwa hivyo?”
“Nooooo...haiwezekani Ramsey,
naomba uelewe!” Mariam akajitoa kitandani kisha akavaa nguo zake haraka na
kutoka nje, akarudi chumbani mwake.
*******
Hadi inafika saa moja kamili
asubuhi, Mariam alikuwa hajafumba macho yake kulala. Alitumia usiku mzima
kuwaza maisha yake. Hakuwa tayari kumsaliti Tom wake, lakini pia hakuwa tayari
kupoteza misaada ya Ramsey.
“Nitafanya nini mimi jamani?
Mbona dunia inanigeuka kiasi hiki?” Mariam akawaza akilia.
Usiku mzima alikuwa hapokei
simu ya Ramsey, baadaye akaamua kuweka mkonge wa simu pembeni ili kukwepa
usumbufu. Alipoanza kupiga simu yake ya mkononi akaamua kuizima kabisa. Akili
yake ikawa ni juu ya mpenzi wake wa moyo wa Tom.
Akiwa anaendelea kuwaza,
ghafla akasikia mlango ukigongwa, akaenda kufungua. Akakutana na Ramsey akiwa
amebeba begi lake. Akamwangalia Mariam akionekana kuwa na chuki za wazi.
Akaingiza mkono mfukoni kisha akatoa burungutu la pesa na kumrushia kitandani,
baada ya hapo akaingiza tena mkono katika mfuko wa shati kisha akatoa karatasi iliyokuwa
na maandishi na kumpatia.
“Maisha mema!” Ramsey akasema
kisha akafunga mlango kwa nguvu na kuondoka.
Haraka Mariam akafungua lile
karatasi kisha akaanza kusoma kwa makini. Ilikuwa imeandika hivi; Nilikupenda
kwa mapenzi ya dhati, nikakupa kila kitu lakini hukuthamini penzi langu.
Nilikuwa tayari kukupa kila aina ya msaada uliotaka, lakini ukanilipa machungu.
Kuondoka chumbani kwangu
usiku, kumenipa taswira kwamba hunipendi, unanionea kinyaa na ni mwaume ambaye
sina uwezo wa kuwa na wewe. Ahsante sana kwa hilo, naomba na mimi niishie
hapa.
Nimekuachia hizo lakini tano,
nikusaidie katika mwanzo mpya wa maisha yako, maana najua ni kiasi gani utakuwa
katika hali ngumu. Maisha ya hapo hotelini hutayaweza, hivyo nakushauri rudi
nyumbani, ukawaangukie wazazi wako, uwaombe radhi.
Hata hivyo, bado nakupenda,
siku ukiona utaweza kuwa na mimi, basi nipigie simu kwa namba zangu
nilizokuachia. Sina kingine zaidi ya kuendelea kukuambia nakupenda na sitaacha
kukupenda. Huyo Tom ni msumari wako wa milele, lakini mwenye uamuzi wa kuutoa
huo msumari ni wewe mwenyewe.
Akupendaye kwa dhati,
Ramsey.
Mariam alirudia kusoma yale
maneno zaidi ya mara kumi na hakuna sehemu hata moja iliyobadilika! Yalikuwa
maneno makali sana ambayo yaliuchoma moyo wake. Hakuwa na kitu kingine cha
kufanya zaidi ya kulia. Mariam akaanza kulia.
“Lakini nimekumbuka, ipo njia
ya kuepukana na haya matatizo yote, ipo...hapa natakiwa kufa tu, hakuna
kingine. Nife, niende zangu kwa Mungu, yeye mwenyewe anajua kwanini nimeamua
kwenda kwake mapema kabla yeye hajaniita. Nataka kufa, tena leo hii hii!”
Mariam akasema maneno hayo kwa sauti ya chini huku akitokwa na machozi.
Beyond Love- 37
Uamuzi ambao kwa hakika ulikuwa mbaya sana, lakini kwake
ulikuwa uamuzi makini ambao aliamini baada ya hapo angepumzika! Aliamua kufa.
Hilo pekee ndilo lingekuwa pumziko lake la kweli! Machozi yakaanza kutiririka
machoni mwake! Alidhamiria kufa. Je, ni kweli atajiua? Nini kitatokea katika
maisha ya Mariam? SONGA NAYO...
CHUMBA kilikuwa kichungu
kwake, asingeweza kuendelea kuishi pale bila msaada wowote. Bado akilini mwake
hakuweza kujua nini cha kufanya tofauti na uamuzi wa kufa ambao aliuona kuwa ni
bora zaidi.
“Nitakuwa nimepotea kabisa,
sitaonana na mtu yeyote tena, nitakuwa nimepumzika kwa Mungu, mateso na shida
zote yatakuwa yameisha. Kwanini niendelee kuishi kwa shida kiasi hiki? Wazazi
wangu hawanitaki, Ramsey amenikimbia, Tom naye ni mgonjwa, pamoja na kwamba
nampenda lakini bado anaweza akapona na akaendelea kuwa na msimamo wake ule
ule, sasa kwanini nijitese? Kwanini niendelee kuteseka?
“Ni bora kufa, ni bora
niondoke, hiyo ndiyo inaweza kuwa salama yangu, sina kitu kingine cha kufanya
zaidi ya hivyo, acha nikapumzike,” Mariam akawaza akilini mwake huku machozi
mithili ya maji yakimiminika machoni mwake.
Alitulia kwa muda mrefu pale
kitandani, akiendelea kulia, muda ukizidi kwenda. Alitumia muda mwingi akiwaza
maisha yake, hapo ndipo alipokumbuka kwamba hakuwahi kufurahi kabisa katika
maisha yake ya kimapenzi.
Mchana mzima alikuwa akilia,
hakukumbuka kula siku hiyo, usiku akaamua kwenda kununua sumu ya panya ili
ajitoe uhai. Alidhamiria kufa, baada ya kununua sumu yake ya panya, alirudi
hotelini na kutulia kwa muda akijaribu kufikiria maisha yake baada ya kifo
chake.
“Hakuna kitakachoharibika,
sina thamani ya maisha hapa duniani, naamini kwa Mungu kuna afadhali, najua
nitakuwa na dhambi ya kujiua lakini Mungu mwenyewe naamini atanisamehe kutokana
na haya mateso niliyonayo. Sijapenda kufa, ila nalazimika kukimbia matatizo ya
hapa duniani, siwezi kukabiliana nayo, yamenishinda,” Mariam alijisemea moyoni.
Mariam alibadilika sana,
hakuona thamani yake tena duniani, aliamini kwa kufa pekee ndiyo angeweza
kupumzika na kuepukana na matatizo anayoyapata. Alichokifanya ni kuchukua
mkonge wa simu, kisha akabonyeza namba za hotelini.
“Hotelini!”
“Ndiyo habari yako?”
“Salama.”
“Naomba kukusikiliza!”
“Nahitaji soda ya badiri
sana!”
“Soda gani?”
“Yoyote isiyo na gesi sana!”
“Soda gani sasa?”
“Yoyote.”
“Upo chumba namba ngapi?”
“206.”
“Ghorofa ya ngapi?”
“Tatu.”
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
“Ok! Baada ya muda mfupi utaletewa.”
Mariam akachukua kalamu na
karatasi akaanza kuandika ujumbe ambao ungewasaidia wahudumu kufahamu alikuwa
ni nani na ndugu zake ni akina nani. Ulikuwa ujumbe unaosikitisha sana, muda
wote aliokuwa akiandika alikuwa akilia machozi.
Ujumbe huo, ulisomeka hivi;
‘Nimeamua kufa ili kukwepa fedheha ninayoipata hapa duniani, naamini kifo pekee
ndicho kitakachoweza kunitenganisha na kero na matatizo yote ninayoyapata hapa
duniani. Nimeteseka vya kutosha, ninayempenda hanipendi, wazazi wangu
wamenifukuza nyumbani, sina msaada wowote.
Sioni thamani wala faida
yangu duniani, ni heri nife tu, ni wengi wananifahamu, mimi ni mke halali wa
Tom ambaye wengi wamekuwa wakimfahamu kwa jina la Papaa Bill. Naamini kwa
utambulisho huu utawarahisishia kuwapa taarifa wazazi wangu ambao watakuja
kuuchukua mwili wangu na kuuzika.
Naamini kifo ni safari ya
kwenda mbinguni, hivyo basi ni imani yangu kwamba siku moja tutakutana katika
enzi yake Mungu wa mbinguni. Kwaherini ya kuonana.
Mariam.’
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Alipomaliza kuandika ujumbe huo, alirudia kuusoma mara mbili mbili huku akilia. Akiwa anarudia kwa mara ya tatu, mlango wa chumba chake ukagongwa, alijua lazima alikuwa mhudumu. Haraka akafuta machozi yake kisha akaficha karatasi yake, akasogea mlangoni, akafungua mlango.
“Vipi sister?”
“Salama.”
“Mbona kama ulikuwa unalia?
Kuna tatizo?” mhudumu akamwuliza.
“Hapana macho yananisumbua
kaka yangu!” Mariam akadanganya.
“Pole sana!”
“Ahsante!” Wakati Mariam
anajibu hivyo, alijikuta machozi yakimwagika usoni mwake kama maji
yanayotiririka kutoka mferejini.
“Mh! Dada inaonekana una
tatizo, lakini unajaribu kunificha, kwanini usiseme ukweli, naweza kukusaidia
mawazo,” yule mhudumu akamsisitizia.
“Kaka nimeshakuambia macho
yananisumbua lakini kwanini unazidi kuning’ang’aniza niwe na matatizo? Kwanza
siyo kazi yako kujua matatizo yangu, tafadhali fungua soda uondoke!” Mariam
aliongea kwa ukali sana, alionyesha kudhamiria alichokuwa akizungumza.
Yule mhudumu hakuwa na maneno
mengi, akafungua soda kisha akaondoka zake. Mariam akaimimina soda kwenye glasi
kisha akachanganya na ile sumu aliyoinunua, baada ya hapo akaanza kuikoroga kwa
pamoja. Akasimama mwili ukimsisimka, kisha akaiangalia ile glasi, baada ya hapo
akaielekeza mdomoni mwake.
“Eeeh baba naomba upokee roho
yangu,” Mariam akasema maneno hayo glasi ikikaribia kufika kinywani.
Aliamua kufa!
******
Nyumba ilipoteza amani,
furaha yao haikuwepo tena, walishamtafuta Mariam hadi wamechoka na
hawakufanikiwa kumpata. Mama yake Mariam alikuwa akilia muda wote.
Kila walipoenda Muhimbili
kumtafuta Mariam, waliambiwa kuwa huwa anakwenda mara moja moja, jibu ambalo
lilizidi kuwachanganya. Walishaamua kumchukua mtoto wao ili wafanye mazungumzo
na kumuweka sawa, lakini waliumia sana walipomtafuta bila mafanikio.
“Lakini nina wazo mume
wangu,” mama yake Mariam akamwambia mumewe.
“Wazo gani mama Mariam?”
“Tunahangaika na tutahangaika
sana, lakini ipo njia moja tu tunayopaswa kuitumia!”
“Ipi?”
“Tumesahau kumuomba Mungu,
nakuhakikishia kama tukimshirikisha yeye kila kitu kitakuwa sawa, ni lazima
tuwe karibu na Mungu baba Mariam.”
“Ni kweli, tumefanya kosa
kubwa sana mke wangu, hatuna haja ya kupoteza muda, tunatakiwa kuanza kusali
sasa hivi.”
“Haya simama tuombe mume
wangu.” Wote wakasimama, kisha wakashikana mikono, mama Marim akaongoza sala.
Walianza na nyimbo za
kuabudu, ambazo waliimba kwa robo saa kabla ya kuingia kwenye maombi
yaliyowachukua saa nzima! Kila mmoja alikuwa akimuomba Mungu wake, amuepushie
Mariam kwenye mateso na shida zote na hata kama alikuwa na mawazo mabaya ambayo
yalikuwa yanateka akili yake, yashindwe!
“Katika jina la Yesu Kristo
wa Nazareth tumeomba na kushukuru...”
“Aaamen...” baba Mariam
akaitikia.
“Mungu ndiyo kila kitu mume
wangu, nakuhakikishia tutaona majibu yake, Mungu wetu siyo mwongo, maana yeye
mwenyewe tumuombe naye atatujibu, hawezi kutoa ahadi ya uongo, lazima atatujibu
tu, lazima.”
“Ni kweli mke wangu, twende
chumbani tukalale.”
Wakaongozana hadi chumbani
kulala, angalau sasa mioyo yao ilikuwa na amani baada ya kufanya maombi.
*******
“Acha!” Mariam alisikia sauti
hiyo ambayo hakuelewa ilitokea wapi.
Alihisi alikuwa ndotoni,
hivyo akapuuza, akaamua kuipandisha glasi yake hadi kinywani, akiwa anataka
kuanza kunywa, ghafla akahisi mkono wake ukitetemeka kwa kasi, ukazidisha kasi
hadi glasi ikaanguka chini.
Mariam hakuelewa
kilichotokea, chumba kizima kikawa kinanuka harufu ya sumu ya panya. Ilikuwa
harufu mbaya sana, Mariam alichanganyikiwa, hakujua kwanini jambo lile
lilitokea, alichoamua kwa muda huo, ilikuwa ni kurudi tena dukani na kununua
sumu nyingine ili aweze kuendelea na zoezi lake.
Akiwa ndiyo anataka kufungua
mlango ili atoke nje, akashangaa miguu yake inakuwa mizito, sauti nyingine tena
ikasisika, tena kwa sauti ya juu na ya msisitizo zaidi; “Wewe ni msichana mzuri
sana, unayevutia na ambaye una mpenzi mzuri sana, siyo kweli kwamba baada ya
kufa utakuwa umekimbia matatizo, achana na mawazo hayo.
“Unachotakiwa kufanya sasa ni
kwenda kwa wazazi wako, uwaangukie na kuwaomba radhi, bado una nafasi ya kuendelea
kuishi. Mariam badili uamuzi wako...” Mariam alizidi kuchanganyikiwa, hakuweza
kuelewa ilikuwa sauti ya nani na wapi ilipotokea.
Katika hali ambayo hata yeye
mwenyewe hakuitegemea, alijikuta akiahirisha kujiua, moyo wake ukawa
umekunjamana na kuhisi uhitaji wa radhi
za wazazi wake.
“Lazima nirudi nyumbani,
lazima tena usiku huu huu wa leo,” Mariam akawaza na kuchukua begi lake dogo
lililokuwa na nguo zake chache kisha akafunga chumba na kushuka hadi chini
ambapo aliingia kwenye taxi.
“Wapi sister?”
“Jeti, Lumo!”
“Poa.” Dereva akawasha gari
na safari ya kwenda nyumbani kwa wazazi wake ikaanza.
Kwa kuwa hakukuwa na foleni,
dakika ishirini zilitosha kabisa kutoka Magomeni Mapipa katika hoteli aliyokuwa
akiishi hadi Jeti, Lumo. Tayari ilikuwa imeshafika saa saba kasoro za usiku.
Kwa bahati nzuri, nyumba yao ilikuwa barabarani, hivyo alimlipa dereva akashuka
na kuanza kugonga geti.
Muda mfupi baadaye baba yake
akafika getini.
“Nani usiku wote huu?”
“Ni mimi baba!”
“Mariam!”
“Ndiyo!”
“Karibu mwanangu, ngoja
nikufungulie!” Mlango ukafunguliwa na Mariam akaingia.
Mapokezi aliyokutana nayo
hakuyategemea kabisa, baba yake akampokea begi na kuingia naye hadi ndani
ambapo alimwita mama Mariam ambaye hakuamini kilichokuwa mbele yake.
“Mariam ni wewe mwanangu?
Karibu nyumbani mama...” mama yake alisema huku machozi yakianza kumlengalenga.
“Ahsante sana mama,
nawaombeni msamaha wazazi wangu, najua ni kiasi gani nimewavunjia heshima,
nimewakosea adabu na hata kuwadhalilisha mbele ya jamii. Nawaahidi nitakuwa
mtoto mwema kwenu, naachana na mambo yote ya kale na sasa naanza upya maisha
yangu.
“Kama siyo Mungu, kesho
mngepata taarifa za kifo changu, tayari nilikuwa na sumu ambayo niliitayarisha
kwa ajili ya kujiua, nikasikia sauti ya ajabu ikiniambia niache, hapo ndipo nilipoamua
kurudi kwenu wazazi wangu.
“Naamini mkinisamehe na
kunibariki nitaishi maisha mapya,” Mariam alikuwa akisema huku akilia. Mama
yake naye alikuwa akilia sana, maneno ya mwanaye yalikuwa makali sana na
hakuamini kuwa mwanaye alipitia mateso makali kiasi kile.
“Mwanangu, sisi
tumekwishakusamehe siku nyingi sana, huna haja ya kuwa na wasiwasi juu ya
hilo,” baba yake Mariam akasema.
“Nashukuru kusikia hivyo
wazazi wangu, lakini nilikuwa na ombi moja ambalo nawaomba sana mnikubalie!”
“Ombi gani mwanangu, we sema
tu!”
“Naomba mniahidi kwanza kuwa
mtanikubalia!”
“Sema tu!”
“Au basi, tuache tu...”
Mariam akasema akionekana kuwa na wasiwasi sana.
“Akha! Kwanini tena.”
“Basi tu!” Mariam akaanza
kulia, tena kwa sauti ya juu kama ambaye alikuwa amefiwa.
Wazazi wake walishindwa
kuelewa alikuwa na tatizo gani kubwa kiasi cha kushindwa kusema. Vichwa vyao
vikawaka moto, mwenye siri hiyo alikuwa ni Mariam mwenyewe.
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond Love-
38
Mariam akaamua
kujiua, lakini kabla ya hajafanya hivyo anajikuta akijisikia mwenye dhambi sana
kujitoa uhai wake. Akaamua kuahirisha, hapo ndipo alipoona umuhimu wa kwenda
kwa wazazi wake ambao walimpokea kwa mikono miwili.
Mariam
alionekana kuwa na kitu alichotaka kuwaomba wazazi wake, aliporuhusiwa kusema
akasita! Je, ni kitu gani hicho? Atasema? SONGA NAYO...
Furaha waliyokuwa nayo wazazi wa Mariam ilikuwa
haielezeki, lakini sasa ilianza kuyeyuka taratibu. Kutokuwa na mwanao kwa muda
mrefu kiasi kile tena wakiwa hawafahamu mahali alipo lilikuwa pigo kubwa sana
kwao, lakini kilichowachanganya zaidi vichwa vyao ni Mariam kusema ana jambo
alilotaka kuwaomba wazazi wake lakini ghafla anakataa.
Vichwa vyao vikawaza upande wa mabaya zaidi, kwamba
yawezekana alikuwa katika hali ya matatizo makubwa na alikuwa akiogopa
kuwashtua wazazi wake. Mama akaanza kulia kwa uchungu akiamini lazima Mariam
alikuwa na tatizo kubwa lililomkabili.
“Lakini Mariam ni nini? Sema kinachokusumbua basi
mwanangu!” Baba yake akasema kwa uchungu sana akimwangalia Mariam usoni.
“Acha tu baba, naona niachane na hayo mambo!”
“Kwani kuna tatizo?”
“Halijawa tatizo baba!”
“Halijawa tatizo? Unamaanisha nini kusema hivyo?”
“Yaani halijafikia kuwa tatizo na ndiyo nimeona niliache
ili lisiwe tatizo!”
“Hapana, wewe ni mtoto wetu wa pekee, na mimi na mama
yako hatutaki kukuona unasononeka, kama kuna kitu kinakusumbua ni bora ukaeleza
kwa uwazi ili tujue jinsi ya kukusaidia!”
“Baba ni usiku saa hizi, naomba tuzungumze kesho.”
“Lakini ingekuwa ni afadhali tulale tukijua mzigo ulionao
umeshautua!”
“Basi baba, acha niwaambie lakini naomba mniahidi kitu
kimoja kwanza.”
“Nini?”
“Kwamba mtanikubalia.”
“Sema tu mwanangu, kama nilivyokuambia, hatupendi kukuona
ukiwa huna furaha kwa mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu...eleza nini tatizo
mwanangu!”
“Baba ni kweli
niliwakosea kwa mambo mengi, lakini pia napenda kuwaeleza kilichopo moyoni
mwangu!”
“Enheee...”
“Nakubali Tom alinitesa, alininyanyasa na kunifanyia kila
aina ya ubaya lakini mama na baba yangu, bado kuna kitu moyoni mwangu. Bado
nahisi kumpenda sana Tom!” Mariam alizungumza kwa sauti iliyojaa huruma sana.
“Bado unafanya nini? Hivi una akili kweli Mariam? Ni
mangapi amekufanyia yule mpuuzi, una sababu ya kuendelea kuona kwamba eti ana
nafasi kwako, kwanini hutaki kutumia akili yako mwanangu?” Mama yake akamwambia
akiwa ameukunja uso kwa hasira.
“Lakini mama nampenda!”
“Unapenda matatizo? Hivi we’ mtoto una akili gani?”
“Basi mama, tuachane nayo...nimekubali kuachana na Tom,
lakini naomba mniruhusu kufanya jambo moja!”
“Jambo gani?”
“Naombeni mniruhusu nimhudumie mpaka apone, lakini
sitakuwa na uhusiano naye kabisa!”
“Hilo haliwezekani.”
“Sasa nini kinawezekana?”
“Hakuna kinachowezekana.”
Walizozana kwa muda mrefu sana, hadi saa tisa za usiku
walipoingia vyumbani kulala bila kuwepo na maafikiano. Asubuhi hakuna
aliyezungumzia juu ya jambo hilo, lakini akilini Mariam aliamua kukaa
kimya akiwaza jinsi atakavyomhudumia Tom
bila wazazi wake kufahamu.
Tom alikuwa kila kitu katika maisha ya Mariam, alimpenda
kwa mapenzi yake yote na wala hakuweza kujua ni kwanini alijikuta akimpenda Tom
kwa kiasi kile. Hata hivyo hakutaka kujiuliza maswali hayo, alichojua yeye ni
kumpenda Tom tu.
“Nampenda sana Tom wangu, ukweli huu nitausimamia siku
zote na ni lazima nihakikishe naulinda msimamo wangu huu. Najua siku moja Tom
ataujua ukweli kwamba mimi ndiye mwanamke wa maisha yake, mimi pekee ndiye
ninayempenda na wala siyo Mayasa kama anavyofikiria, hili litadhihirika!”
Mayasa akawaza.
Kwa wiki nzima Mariam alikuwa anashinda nyumbani bila
kwenda hospitalini, moyo wake ulimuuma sana lakini aliamua kufanya hivyo ili
kuwapumbaza wazazi wake wasahau kabisa kuhusu Tom. Siku moja asubuhi baada ya
baba yake kwenda kazini, Mariam alimuomba mama yake ruhusa ya kwenda kumuona
rafiki yake.
“Nani?”
“Clara mama!”
“Lakini kwanini yeye asije?”
“Mama yake ni mgonjwa, amenipigia simu jana kunipa
taarifa na kama unavyojua sisi ni marafiki, naona hii ni nafasi yangu ya
kuonyesha ninavyomjali kwa kumfariji mama!” Mariam akadanganya.
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
“Sawa mwanangu, lakini jitahidi basi kuwahi!”
“Usijali mama!”
Mariam akajiandaa kisha akatoka na kwenda zake Muhimbili
tena akitumia gari la mama yake. Aliingia wodini na kumkuta Tom akiwa amelala
kimya kitadani, bado alikuwa akipumulia mashine. Mariam akapiga magoti pembeni
ya kitanda chake, akambusu usoni huku akitamka; “Nakupenda sana Tom wangu,
najua yote uliyonifanyia ni kwa sababu ya shetani tu, wewe na akili yako huwezi
kufanya hayo.
“Namwomba Mungu akujalie, siku moja usimame tena, uone
jinsi ninavyokupenda, naamini siku hiyo itafika na utajua ukweli kwamba mimi
ndiye mwanamke pekee ambaye nakupenda kwa moyo wangu wote.”
Mariam alijikuta akilia akimtizama Tom. Zilikuwa kumbukumbu za kuhuzunisha sana
katika maisha yake, alitamani sana siku moja Tom aamke na warudiane tena kama
mtu na mke wake. Hilo aliamini lazima siku moja litatokea. Baadaye akatoka na
kwenda ofisini kwa daktari wake ili kupata maelezo ya maendeleo ya Tom.
“Ndiyo Dokta anaendeleaje sasa?”
“Matumaini yapo, lakini kama ulivyomuona bado
hajazinduka.”
“Unadhani itamchukua muda gani?”
“Kwa kweli siyo rahisi kukuambia maana bado kuna vipimo
vingine vinaendelea kufanyika, ila tunashukuru kidogo mapigo yake yanaanza
kurudi vizuri, nafikiri baada ya wiki mbili tatu, ataweza kuanza kupumua
mwenyewe.”
“Nitashukuru sana dokta, kwa hiyo atapona?”
“Mategemeo yetu yapo kwa Mungu dada yangu, nafikiri ni
vyema kama tutamwachia yeye!”
“Nashukuru sana dokta!”
“Ok!”
Mariam aliendelea kukaa pale hospitalini hadi usiku
kabisa, baada ya kuhakikisha Tom alikuwa ameshaoga na kula kwa kupitia mpira.
Akarudi nyumbani usiku sana, maelewano na mama yake hayakuwa mazuri lakini
alisingizia kwamba hali ya mama wa rafiki yake haikuwa nzuri, hivyo asingeweza
kumuacha akiwa katika hali mbaya peke yake.
“Lakini kwanini hukutoa taarifa?”
“Nilipitiwa mama!”
“Ndiyo na simu uzime?”
“Iliisha chaji mama!”
“Angalia sana Mariam, sitaki unigombanishe na baba yako!”
“Nisamehe mama.”
Mariam aliendelea kumhudumia Tom kila siku, alifanya
hivyo kwa siri kubwa hadi siku mama yake alipogundua na kumwambia baba yake.
Mariam akatakiwa kuamua jambo moja, kuondoka nyumbani aendelee kumhudumia Tom
au abaki nyumbani lakini aachane na Tom.
“Mama nimechoka na haya masimango yenu, sili chakuka
kikashuka...basi bora niondoke hapa kwenu, nikamsaidie Tom wangu, kwanza
kumbukeni nimefunga naye ndoa. Yule ni mume wangu halali, na nilimuahidi kuwa
nitaishi naye katika shida na raha, sasa kwanini nimtese?”
“Kama unayajua hayo, mbona yeye alikusaliti? Mbona yeye
alikutesa?”
“Umeshasema yeye...kwani huoni kama kuna tofauti kubwa
kati ya yeye na mimi, ninafanya kile nilichoahidi na yeye kwa nafasi yake
anatakiwa kufanya alichoniahidi.”
“Kwahiyo?”
“Narudi Mbezi, nyumbani kwangu, nitaishi maisha yoyote na
nitaendelea kumhudumia mpaka atakapopona, hayo ndiyo maamuzi yangu,” Mariam
alionyesha msimamo wa hali ya juu sana, ilifikia hatua wazazi wake wakashindwa
kumzuia zaidi.
Mariam akaondoka na kwenda zake Mbezi katika nyumba ya
Tom waliyokuwa wakiishi. Nyumba ilikuwa chafu na haikuwa katika mpangilio
mzuri, baadhi ya vitu vilikuwa havipo. Hakusumbua sana kichwa kugundua kwamba
ilikuwa ni kazi ya Mayasa.
Alichokifanya ni kuhakikisha nyumba inakuwa safi, kisha
kazi yake kubwa ikawa ni kumhudumia Tom.
********
MIAKA MINNE BAADAYE
Kama kawaida, asubuhi hiyo Mariam alikwenda Muhimbili,
hiyo ilikuwa ni kama ndiyo kazi yake. Siku hiyo alihisi moyo wake ukienda kasi
sana, alijaribu kujiuliza sababu za hali hiyo kumtokea lakini hakupata majibu.
Akaingia wodini kisha akaketi kitandani akimtizama Tom aliyekuwa akipumua kwa
kutumia mashine.
Kwa miaka minne sasa alilala kitandani bila kujitambua!
Hata hali ya afya yake haikuwa nzuri tena, Tom alitia huruma! Katika hali ya
kushangaza sana, akaona macho ya Tom yanafumbuka taratibu. Tom akatabasamu,
lakini alipogundua kwamba aliyekaa mbele yake alikuwa ni Mariam akakasirika
sana.
“We’ mwanamke umefuata nini hapa? Ondoka utakuja kupigwa
na Mayasa wewe...Mayasa ni mkorofi, kwanini unaendelea kunifuatafuata?
Toka...toka Mariam usije kunisababishia matatizo...” Tom akazungumza kwa sauti
kubwa huku akiyatoa macho.
Hakujua kilichotokea katika maisha yake tena, hakuwa na
habari kwamba alilala kitandania kwa zaidi ya miaka minne. Aliendelea kufoka
huku akimuamrisha Mariam aondoke. Mariam alijikuta akishindwa kuzungumza,
machozi yakaanza kumtoka.
“Tom mume wangu, Mayasa hayupo hapa na wala hawezi
kutokea Tom...mimi ndiye Mariam, mwanamke wa maisha yako, ambaye nakupenda kwa
mapenzi yangu yote. Nakupenda kwa mapenzi ya kweli, sikujali pesa wala utajiri
wako Tom, lakini Mayasa uliyemuona anafaa, leo hayupo unateseka na mimi kwa
miaka yote uliyokuwa umelala.
“Mayasa ameuza kila kitu, amekuachia kibanda cha kulala
tu, hakuna kitu tena mpenzi wangu. Lakini yote hayo najua ni shetani, ndiyo
maana nipo hapa leo kukuonyesha kwamba mimi nina mapenzi ya dhati kwako,”
Mariam aliongea akilia.
Tom alishindwa kuelewa alichokuwa akizungumza Mariam, ni
kama alikuwa akizungumza vitu vigeni. Amelala miaka minne kitandani? Kivipi?
Hilo hakulielewa na wala hakutaka kulipa nafasi kabisa akilini mwake.
“Hivi una kichaa Mariam? Unavyosema Mayasa ameuza vitu
vyangu unamaanisha nini? Nimekuambia toka hapa Mayasa atakukuta na kukufanyia
fujo...ni bora ukaondoka Mariam...” Tom alisema maneno hayo kisha akajitahidi
kuamka, lakini akashindwa!
Hapo akagundua kwamba alikuwa amelazwa hospitalini tena
alikuwa akipumua kwa kutumia mashine! Hakujua kilichotokea, lakini alivyotulia
kwa muda akakumbuka alivyovamiwa na majambazi na kurushiwa risasi akiwa getini
kwake!
Tom akaanza kulia. Mariam naye akaungana naye. Machozi
yakatawala wodini.
“Tom unanipenda?” Mariam akamwuliza Tom, lakini hakujibu
zaidi ya kuendelea kulia.
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond Love- 39
Anaanza kulia, Mariam naye
analia, wote wanaungana kulia kwa furaha. Mariam anamwuliza Tom kama anampenda,
Tom hajibu badala yake anaendelea kulia. Je, nini kitatokea kati ya Tom na
Mariam? SONGA NAYO...
“Tom
niambie basi kama unanipenda?” Mariam anazidi kumkazania Tom swali hilo huku
mvua ya machozi ikiendelea machoni mwake.
Tom
hajibu kitu zaidi ya kuendelea kulia kama mtoto mdogo!
“Tazama
ninavyokupenda Tom, umenisaliti, ukaniletea mwanamke mpaka ndani, ukanifukuza
lakini yote hayo nilishayasahemehe, kilichokuwa ndani ya moyo wangu ni upendo
wa dhati, upendo ambao siku zote umekuwa silaha yangu ya kweli, umeniwezesha
kuwa mvumilivu na mwenye ahadi za kweli, niliuahidi moyo wangu kutokukusaliti
asilani na ndivyo nilivyofanya mpenzi wangu.
“Ni
miaka minne umelala hapa hospitalini, ukiwa huna kumbukumbu ya jambo lolote
lile, nikihangaika na wewe kwa kila hali, nikawa tayari kugombana na wazazi
wangu kwa ajili yako Tom, naomba uamini kwamba nakupenda, upendo wa dhati kutoka
katikati ya moyo wangu...nakupenda sana Tom, naomba uniamini kwa hilo.”
Mariam
alikuwa na uchungu mwingi sana moyoni mwake, pamoja na uchungu aliokuwa nao,
ilikuwa ni siku ya furaha kubwa katika maisha yake, hakutegemea kuisikia tena
sauti ya Tom, kumuona akifumbua macho yake mazuri na kumtizama uso wake.
Alijisikia furaha isiyo na kifani, kwake Tom alikuwa mpenzi mwema, awe mgonjwa
au katika hali yoyote, alichojali ni kumuona Tom wake akiwa mzima!
“Hujanijibu
bado Tom wangu, niambie basi unanipenda?” Mariam akamwuliza tena.
“Nakupenda
Mariam!”
“Nashukuru
kusikia hivyo,” Mariam akasema kisha akambusu katikati ya midomo yake.
“Nakupenda
pia mpenzi wangu, wewe ni wangu wa maisha, nilijua Mayasa alikuwa anakupoteza
na nina imani haikuwa akili yako mume wangu, lazima yule malaya atakuwa
alikuwekea kitu.
“Hata
hao majambazi waliokuvamia, nina wasiwasi nao sana, yawezekana ikawa Mayasa
alitengeneza mchezo!”
“Huna
haja ya kuwaza sana mambo yaliyopita mpenzi, tuyaache kama yalivyo. Enhee
Mayasa yupo wapi?”
“Mayasa?”
“Ndiyo!”
“Ngoja
nikupe stori!” Mariam akaanza kumsimulia Tom kila kitu baada ya yeye kuamua
kwenda kijijini kwao Matombo, Morogoro, akamweka wazi kwamba alisikia Mayasa
alitoroka na aliuza mali zote akiwa mgonjwa.
Hakumficha
kitu chochote, aliweka wazi jinsi alivyoteseka kwa ajili yake. Wote walilia
sana. Tom akaona thamani ya penzi la Mariam kwake, akauahidi moyo wake kuwa
mtulivu na kuendelea kuwa na Mariam pekee, hakutaka kuhaingaika tena.
“Enhee
na mama yuko wapi?”
“Mama?”
“Ndiyo!”
“...Yupo
nyumbani!” Baada ya kufikiria sana, Mariam akaamua kudanganya, hakuona sababu
ya kumweleza ukweli juu ya kifo cha mama yake, kwani alijua wazi ni kiasi gani
angemuumiza.
“Mbona
hukuja naye?”
“Huwa
tunakuja kwa zamu, wiki hii ni yangu, wiki ijayo ni yake, ila akijua kwamba
umeshapata fahamu lazima atakuja!”
“Nitafurahi
sana!”
“Pole
sana mpenzi wangu, najua ni kiasi gani ulivyokuwa katika mateso makali kwa muda
mrefu!”
“Usijali
Mariam wangu, nashukuru pia kwa kuonyesha penzi lako la dhati, hakika haya ni
zaidi ya mapenzi, wewe ni mpenzi wangu wa kweli!” Tom akasema akitoa machozi.
“Nashukuru
kwa kutambua hilo mpenzi, nitakupenda milele!”
“Hata
mimi pia!”
Wakiwa
katikati ya maongezi, Muuguzi alifika na kushangazwa na hali aliyomkuta nayo
Tom, hakutarajia kumuona mgonjwa wake akiwa amerejewa na fahamu baada ya kulala
kitandani kwa siku zote hizo. Akakimbia ofisini kwa daktari haraka kwenda kumpa
taarifa hizo.
“Yule
mgonjwa amezinduka!”
“Yupi?”
“Tom!”
“Kweli?”
“Ndiyo
dokta!”
“Hebu
twende!” Dokta akaongozana na Muuguzi hadi kitandani kwa Tom.
Alipomkuta
akizungumza na Mariam, akamkataza.
“Mariam
mwache kwanza apumzike, bado hajawa na nguvu ya kuzungumza sana kwa wakati huu,
anahitaji muda mwingi wa kupumzika kwanza!”
“Sawa
dokta!”
“Hebu
tupishe kidogo!”
“Sawa!”
“Enhee
Tom, unajisikiaje?”
“Nina
nafuu sasa, Mungu amenipigania!”
“Ni
kweli lazima umshukuru sana Mungu maana yeye ndiye aliyekupa uzima ulionao!”
“Amen!”
“Pole
sana!”
“Nashukuru
sana dokta!”
Baada
ya pale Daktari alimwita Mariam ofisini kwake, kumpa taarifa za maendeleo ya
Tom.
“Mariam
kwanza tunamshukuru sana Mungu kwa kumuwezesha Tom kurejewa na fahamu tena,
lakini kuna jambo moja lazima ulijue, mgonjwa wako amepooza kuanzia shingoni
hadi miguuni, kwasasa kinachofanya kazi ni kichwa tu, lakini napenda kukutoa
wasiwasi kwamba, kama Mungu huyo huyo ndiye aliyemzindua leo baada ya kulala
miaka minne kitandani, basi Mungu huyo huyo ndiye atakayempa nafuu tena. Kifupi
tutegemee muujiza wa Mungu!” Daktari akasema kwa utulivu sana.
Mariam
alikaa kimya kwa muda akifikiria, ni kweli Tom alikuwa na tatizo, lakini kwake
halikuwa tatizo kubwa sana kama angekufa kabisa! Akamshukuru Mungu kwa
kumzindua Tom wake, tegemeo kubwa lilikuwa kwake.
“Hakuna
shida daktari, nimefurahi kumuona akifumbua macho yake tena, mambo mengine
hayo, nayaacha mikononi mwa Mungu mwenyewe!”
“Mungu
atawasaidia!”
“Nashukuru
sana, kazi njema.”
Magazeti
ya mchana ya siku hiyo yalipambwa na habari ya Tom kuzinduka, haikujulikana ni
muda gani waliingia wodini na kuwapiga picha Mariam na Tom, wakati Mariam alipokuwa
akimbusu Tom mashavuni.
Gazeti
la Za Leo ndilo lililokuwa na picha hiyo, pamoja na kichwa kikubwa cha habari
kilichosomeka; HAYA NI ZAIDI YA MAPENZI! Lilikuwa gazeti pekee lililouzika
zaidi kutokana na kuwa na picha ya wapenzi hao wakiwa pamoja hospitalini
asubuhi ya siku hiyo.
*******
Usiku
Mariam alishindwa kulala, alikuwa anawaza ni jinsi gani angeweza kumdanganya
Tom kuhusu mama yake, hakika alikuwa na kazi kubwa sana ya kuzungumza naye na
kumweleza ukweli.
Hata
hivyo, pamoja na kuwaza kwa muda mrefu, baadaye alipitiwa na usingizi mzito.
Asubuhi yake aliamka na kujiandaa kama kawaida kisha akaenda zake hospitalini.
Akamkuta Tom akiwa amelala kitandani macho yake yakiangalia juu.
“Vipi
sweetie?”
“Salama
mama vipi?”
“Shwari
lakini siyo shwari!”
“Kwanini?”
“Sijielewielewi
kabisa, mwili wangu kama umekufa ganzi hivi!”
“Ni
kawaida mpenzi, umelala kitandani kwa muda mrefu sasa, tena nilikuwa nazungumza
na Dokta jana, kasema hali hiyo ni ya kawaida na itapotea polepole ingawa
itachukua muda kidogo!”
“Siamini...”
Tom akasema.
“Naomba
kukuliza Tom, unaamini kama kuna Mungu?”
“Ndiyo!”
“Unaamini
yupo Roho Mtakatifu?”
“Ndiyo!”
“Pia
unaamini kwamba Mungu alimtuma mwanaye mpendwa Yesu Kristo ili afe msalabani
kwa ajili ya dhambi zetu?”
“Ndiyo!”
“Kwahiyo
unaamini juu ya Utatu Mtakatifu?”
“Hakika!”
“Basi
mwachie haya mambo Mungu mwenyewe, naamini utukufu wake utadhihrika!”
“Ni
kweli mpenzi wangu, ahsante sana kwa kunipa moyo, acha Mungu afanye awezavyo,
najua hataniacha nikaabika!”
“Nashukuru
kwa kutambua hilo mpenzi!”
“Enhee
mama yupo wapi?”
“Unasema?”
“Mama
yupo wapi?”
Mariam
hakujibu, alikaa kimya akiwa ameyatuliza macho yake usoni mwa Tom, huku machozi
yakianza kumtiririka machoni mwake. Tom alishindwa kuelewa maana ya machozi ya
Mariam.
“Sasa
unalia nini mpenzi wangu, Mungu atanisaidia, huna sababu ya kulia... kwanini
hujaja na mama? Nina hamu sana na mama yangu!” Maneno ya Tom yalikuwa msumari
wa moto moyoni mwa Mariam, kwani alikuwa na siri nzito sana ambayo kuitoa kwake
lazima awe amejiandaa vya kutosha!
Haikuwa
jambo jepesi kumwambia Tom, moja kwa moja kwamba mama yake alishafariki, tena
alizikwa na Halmashauri ya Jiji. Hilo lilikuwa jambo gumu sana.
Je,
nini kitatokea? Mariam atamweleza ukweli? Nini kitafuata katika maisha yao?
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie

Post a Comment