ad

ad

USIA WA GURUMO WAGEUZA TAREHE YA MAZISHI, SASA KUZIKWA JUMANNE …alitoa agizo: “Nikifa nisizikwe mapema, mimi ni mtu wa watu”



KIKAO cha familia ya marehemu Muhidin Maalim Gurumo kilichoamua kuwa mazishi ni Jumatatu, kimebadili ratiba ya mazishi na sasa atazikwa Jumane.Mwanzoni kulikuwa na mvutano mkubwa wa siku ya mazishi baadhi wakitaka azikwe Jumatatu na wengine Jumanne.
 Marehemu Muhidin Maalim Gurumo.
Mjomba wa marehemu akasema mbele ya kikao hicho kilichohudhuriwa pia na viongozi wa Msondo Ngoma kuwa Gurumo alitoa agizo asizikwe haraka.
“Gurumo alisema yeye ni mtu wa watu, hivyo akifariki asizikwe haraka ili watu wake wapate taarifa na nafasi ya kumzika,” alisema mjomba huyo wa marehemu.
Hata hivyo mwanzoni taarifa hiyo haikupewa nguvu na badala yake upande wa pili uliokuwa unaongozwa na mtoto wa kwanza wa marehemu ukapitisha kuwa mazishi ni Jumatatu.
Kadri muda ulivyosonga mbele fikra mpya zikaingia na hatimaye usia wa Gurumo ukazingatiwa (licha ya kuwa unakiuka misingi ya kiislam) na sasa ni rasmi kuwa atazikwa Jumanne kijijini kwao Masaki wilayani Kisarawe.
Misingi ya kiislam iko wazi kwamba mtu anapofariki basi azikwe mapema iwezekanavyo.
Mwili wa marehemu Gurumo aliyefariki Jumapili saa 9 alasiri, umehifadhiwa hospitali ya Muhimbili.
Msiba uko nyumbani kwa marehemu  Makuburi jijini Dar es Salaam. ambapo msafara wa kuelekea Masaki utaondoka saa 3 asubuhi siku ya Jumanne.
Pichani juu ni Gurumo (kushoto) enzi za uhai wake akiteta jambo na swahiba wake Hassan Rehani Bicthuka.
Unataka niwe nakutumia stori kama hizi na kila nyingine inayonifikia? jiunge na familia ya 2jiachie.com kwenye  facebook hapa LIKE PAGE YETU HAPA ==> 2JIACHIE

CREDIT: SALUTI5.COM

No comments

Powered by Blogger.