MASSACRE (MAUAJI YA HALAIKI) SEHEMU 01
Na Nyemo Chilongani
Kila aliyekuwa akizisoma taarifa ambazo zilikuwa zimeandikwa katika magazeti mbalimbali yaliyokuwa yakitoka katika siku hiyo alibaki akishangaa tu. Watu wakashtuka kupita kawaida, habari ile ilionekana kuwasisimua kupita kawaida. Imani juu ya wachungaji ikaanza kuondoka katika mioyo ya watu, hasa waumini wa dini ya Kikristo.
ITAENDELEA KESHO HAPA HAPA
Kila aliyekuwa akizisoma taarifa ambazo zilikuwa zimeandikwa katika magazeti mbalimbali yaliyokuwa yakitoka katika siku hiyo alibaki akishangaa tu. Watu wakashtuka kupita kawaida, habari ile ilionekana kuwasisimua kupita kawaida. Imani juu ya wachungaji ikaanza kuondoka katika mioyo ya watu, hasa waumini wa dini ya Kikristo.
Kanisa
likaonekana kupotea njia, kila kitu
ambacho kilikuwa kinaendelea hasa katika makanisa mbalimbali kilionekana
kuwa kama maigizo juu ya jukwaa au ndani ya luninga. Shetani
akaonekana kuliteka kanisa na kulifanya alivyotaka kulifanya. Dhambi
ambayo
ilionekana kufanyika kwa kiongozi mmoja wa kanisa moja ikaonekana kama
imetokea
katika makanisa yote nchini Tanzania.
Watu wengine wakataka kujitoa kutoka katika imani ya Kikristo kwa kudai
kwamba
shetani alikuwa amemzidi nguvu kila mtu.
Wokovu wote ambao ulikuwa ukiendelea katika
makanisa yote ukaanza kuyumba. Watu wengine wakaahidi kutokuhudhuria tena
makanisani mwao kutokana na imani juu ya viongozi wao kuanza kupotea. Idadi
kubwa ya watu wakaanza kupoteza uaminifu wao juu ya wachungaji wa makanisa yao.
‘MCHUNGAJI
ATAKA KUMBAKA BINTI OFISINI’. Hicho kilikuwa ni kichwa cha habari ambacho
kilikuwa kikisomekana katika magazeti mbalimbali jijini Dar es Salaam. Bado watu walikuwa wakiendelea
kushangaa, hawakuamini kama mchungaji Matimya wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa
Mwenge angeweza kufanya kitu kama kile ambacho
kilikuwa kimeonekana kuandikwa katika magazeti mengi.
Habari ile ilionekana kuwa habari iliyokuwa
na furaha kwa watu wote ambao walikuwa hawawapendi Watumishi wa Mungu. Watu
wakaanza kupeana taarifa majumbani mwao huku kila aliyepewa taarifa ile akaanza
kuelekea barabani kulinunua gazeti moja ambalo lilikuwa na habari ile.
Katika mwaka mzima, habari ile ndio ambayo
ilifanikiwa kuuza nakala nyingi kuliko habari yoyote iliyowahi kuandikwa katika
mwaka huo. Mpaka inafika saa saba mchana, hakukuwa na gazeti lolote lililokuwa
na habari ile ambalo lilikuwa katika meza ya wauza magazeti.
Kila mtu ambaye alikuwa akiyaona magazeti
yale, aliyanunua. Siku ya mwisho ikaonekana kukaribia kutokana na shetani
kuonekana kulivamia kanisa hasa kwa viongozi mbalimbali wa makanisa. Aibu kubwa
ikaanza kulikumba kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge.
“Haiwezekani hata kidogo. Mbona huyu
Mchungaji ni Mtumishi mzuri wa Mungu! Tena kwa sasa anataka kuwa Askofu Mkuu.
Hawezi kufanya hivi” Sauti ya msichana mmoja ilisikika ikiwaambia wenzake huku
mkononi akiwa ameshika Biblia katika kipindi ambacho walikuwa wakitoka kanisani
siku hiyo ya Jumapili.
“Kwa nini isiwezekane kwa mtu kama huyu kufanya hivi? Tumemkaribisha shetani sisi
wenyewe. Acha awatumie watumishi wa Mungu anavyotaka” Mwanamke mmoja alisikika
akisema huku akishika vizuri Biblia yake.
Habari hiyo ndio ambayo ilikuwa imeshika
hatamu katika kipindi hicho. Kila mtu ambaye alikuwa akiiona habari ile na
kuisoma, alishtushwa kupita kiasi. Picha kubwa ya rangi ya mchungaji Matimya
ilikuwa ikionekana vizuri katika kila gazeti ambalo lilikuwa na habari ile.
****
Mchungaji Matimya alikuwa amekaa katika kiti
cha nyuma kabisa ndani ya kanisa lake. Uso wake alikuwa ameuinamisha chini huku
machozi yakimtoka. Mbele yake aliiona aibu kubwa ikiwa imemkuta, hakuelewa ni
kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya ili Watanzania waelewe kwamba hakuwa
amekifanya kile kitu ambacho kilikuwa kikitangazwa sana na vyombo vya habari.
Hakukuwa na mtu ambaye alionekana kumuamini
Mchungaji Matimya, kila mtu kanisani humo alimuona kuwa kama
Mwakilishi wa shetani ambaye aliletwa kanisani humo kwa ajili ya kulitia aibu
kanisa. Ingawa ibada ilikuwa ikiendelea kanisani humo, macho ya washirika wengi
walikuwa yalikuwa yakimwangalia Mchungaji Matimya.
Machozi yale ambayo yalikuwa yakimtoka,
yalionekana kuwa kama ya kinafiki machoni mwa
washirika wa kanisa lile. Mchungaji Matimya hakuwa peke yake, familia yake
ilikuwa pembeni yake. Mkewe, Bi Meriana alikuwa upande wake wa kushoto huku
watoto wake wawili, Benedict na Angelina wakiwa katika upande wa kulia.
Kilio cha chini chini kilikuwa kikisikika
kutoka kwa Bi Meriana. Kila alipokuwa akikumbuka aibu ile ambayo ilikuwa
imemkuta mumewe, alizidi kuumia. Hawakuonekana kufuatilia kitu chochote
kilichokuwa kinaendelea kanisani mule. Vichwa vyao vilikuwa vikifikiria mbali.
Ibada iliendelea kama
kawaida. Mara baada ya muda wa matangazo kuingia, Askofu wa dhehebu hilo la Praise And Worship, Askofu Lugakingira akasimama
na moja kwa moja kuelekea katika madhabau ya kanisa hilo na kuchukua kipaza sauti. Kabla
hajaongea kitu chochote kile, alitulia kwa muda huku akiliangalia kanisa.
Kila mtu alikuwa kimya tayari kwa kusikiliza
kile ambacho Askofu alitaka kukizungumza mahali hapo. Askofu alianzia mbali sana lakini huku lengo lake kubwa
likiwa ni kufika katika kitu ambacho kilimfanya kuja katika kanisa lile katika
siku hiyo ya Jumapili. Mara baada ya kutumia dakika kumi kuongea mambo tofauti
tofauti, hapo hapo akamtaka Mchungaji Matimya kwenda mbele ya kanisa lile.
Huku akionekana kuwa katika lindi la mawazo,
Mchungaji Matimya akainuka kutoka katika kiti alichokuwa amekaa kule nyuma ya
kanisa na moja kwa moja kuanza kuelekea mbele ya kanisa. Minong’ono ikaanza
kusikika kutoka kwa washirika ndani ya kanisa lile, Mchungaji Matimya
hakuonekana kujali, aliendelea kupiga hatua hadi mbele ya kanisa lile.
“Nadhani hakuna mtu asiyejua kitu ambacho
kimenifanya kuja ndani ya kanisa hili kwa siku ya leo. Lilikuwa ni suala ambalo
lilihitaji kumuita Mchungaji Matimya. Niliongea nae kwa kirefu sana na kukiri kila kitu pasipo kuficha kitu
chochote kile” Askofu Lugakingira aliliambia kanisa na kuendelea.
“Ningependa kumpa nafasi ya kulieleza kanisa
kama hiki kitu ambacho kimetawala kila sehemu
ni kweli au kuna uongo wowote” Askofu Lugakingira alisema na kisha kumpa kipaza
sauti mchungaji Matimya.
Mchungaji Matimya hakuongea kitu chochote
kile, alibaki kimya huku macho yake yakiangalia chini. Kila alipotaka kuongea
kitu, aliuona mdomo wake kuwa mzito kufunguka, hakujua aseme kitu gani mbele ya
kanisa na mbele ya familia yake. Kumbukumbu ya maisha yake ya nyuma ikaanza
kujirudia kichwani mwake, katika hatua nyingine, alijuta kwa nini aliitwa kuwa
Mchungaji.
“Nalihitaji kanisa msamaha. Ni kweli nilitaka
kumbaka Judith ndani ya of….” Mchungaji Matimya alisema lakini hata kabla
hajamalizia sentensi yake, akaanza kulia. Sauti ya kilio chake kilisikika
kanisa zima kutokana na kipaza sauti alichokuwa amekishika. Wanawake
wakashindwa kuvumilia, nao wakaanza kulia.
Mtoto wake, Benedict hakuweza kuvumilia
kubaki kanisani hapo akasimama na moja kwa moja kuanza kuelekea nje ya kanisa
lile. Moyo wake uliumia kupita kiasi, maneno ambayo aliongea baba yake mbele ya
kanisa yalionekana kumuumiza kupita kawaida.
Mara baada ya kufika nje ya kanisa, moja kwa
moja akalifuata gari lao na kuingia ndani na kisha kuliwasha. Kila mtu ambaye
alikuwa nje ya kanisa alikuwa akimwangalia Benedict ambaye akaliwasha gari lile
na kuondoka katika eneo lile la kanisa.
Mchungaji Matimya akashindwa kuendelea,
akakikabidhi kipaza sauti kwa Askofu Lugakingira ambaye alikuwa akimbembeleza
kwa kumpiga piga mgongoni. Mchungaji Matimya akazidi kulia zaidi na zaidi,
akapiga magoti chini huku uso wake akiwa ameuinamisha chini kwa aibu huku machozi
yaliyokuwa yakimtoka kuloanisha sakafu ya pale madhabahuni.
“Kila kitu kina sheria zake. Na hili kama
dhehebu la Praise And Worship, mchungaji Matimya hatokuwa mchungaji wa kanisa
hili tena. Tunamfungia kufanya huduma yoyote kwa muda wa mwaka mmoja na nusu”
Askofu Lugakingira aliliambia kanisa.
Idadi kubwa ya washirika ikaonekana
kufurahia. Thamani ya mchungaji Matimya ikaonekana kushuka. Pepo la uzinzi
likaonekana kumvaa mchungaji Matimya ambaye bado alikuwa pale mbele ya kanisa
akiendelea kulia kwa uchungu. Kila kitu ambacho kiliendelea katika maisha yake
kilionekana kuwa kama ndoto ambapo baada ya muda fulani angeamka kutoka katika
usingizi mzito.
****
Uchaguzi wa Askofu mkuu ndio ambao ulikuwa
ukikaribia, siku tano tu ndizo ambazo zilikuwa zimebaki kabla ya uchaguzi huo.
Wachungaji wawili, mchungaji Matimya wa kanisa la Praise And Worship la Mwenge
lililoko jijini Dar es Salaam pamoja na mchungaji Mwakipesile wa kanisa la
Praise And Worship lililokuwa Morogoro ndio ambao walikuwa wakiwania nafasi ya
kuwa Askofu mkuu nchini Tanzania.
Kila mtu alionekana kuwa na nafasi nzuri ya
kuchukua nafasi hiyo lakini mchungaji Matimya ndiye ambaye alionekana kuwa na
nafasi kubwa zaidi. Kila kanisa la dhehebu la Praise And Worship lililokuwa
nchini Tanzania, jina la mchungaji Matimya ndilo ambalo lilikuwa likitajwa mara
kwa mara.
Wachungaji wengi walikuwa wakitamani
Mchungaji Matimya achukue nafasi hiyo kutokana na huduma nzuri ambayo alikuwa
akiitoa katika kanisa lake na makanisa mengine mbalimbali nchini. Hakuwa na
roho ya majivuno kama aliyokuwa nayo mchungaji Mwakipesile.
Kila mtu alivutiwa nae, kila mtu akatamani
mchungaji Matimya achukue nafasi ile na kuwa Askofu mkuu. Asilimia zaidi ya
themanini ya wachungaji wote wa dhehebu hilo walitamani mchungaji Matimya
achukue nafasi hiyo ambayo ilitarajiwa kuachwa na Askofu Lugakingira siku
chache zijazo.
“Ni lazima nifanye kitu” Mchungaji
Mwakipesile alijisemea huku akionekana kukasirika.
Mbele yake hakuona dalili zozote za ushindi
katika nafasi ya Uaskofu. Baadhi ya wachungaji ambao walikuwa katika upande
wake, katika kipindi hicho walikuwa wamemsaliti. Kila kitu katika kipindi hicho
kilionekana kwenda tofauti na matarajio yake ya nyuma.
“Nitamtumia hata mshirika wake mwenyewe”
Mchungaji Mwakipesile aliendelea kujisemea.
Hakutaka kuendelea kubaki Morogoro, kitu
alichokifanya siku iliyofuata ni kuchukua ndege na moja kwa moja kuanza
kuelekea jijini Dar es Salaam. Hakutaka mtu yeyote afahamu juu ya safari yake
hiyo ya ghafla, hakumpa taarifa hizo mtu yeyote zaidi ya msichana mmoja tu,
Judith Simon ambaye alikuwa akiishi ndani ya jiji la Dar es Salaam.
*****
Jina la Judith Simon wala halikuwa geni
masikioni mwa washirika wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge.
Binti huyu alikuwa na sifa zote ambazo msichana wa kisasa na mrembo alitakiwa
kuwa nazo. Alikuwa na wembamba kama waliokuwa nao wasichana ambao walikuwa
wakigombania nafasi ya kuwa mrembo wa Tanzania.
Uso wake ulikuwa mwembamba, alikuwa
akitembea kwa mwendo wa mapozi kana kwamba alikuwa hakanyag ardhi. Kila
aliyekuwa akiuangalia mwendo wa Judith alikiri kwamba binti huyo alikuwa
akitembea mwendo uliokuwa na mvuto kanisani hapo.
Mashavu yake yaipendezeshwa na vishimo
viliwili vilivyokuwa mashavuni mwake ambavyo vilikuwa vikionekana vizuri katika
kila wakati alipokuwa akicheka au kutabasamu. Kila wakati Judith alionekana
kuvutia.
Uzuri wake ulikuwa ukionekana wakati wote.
Haijalishi alikuwa amekarika, amenuna au ametabasamu, muda wote huo uzuri wake
wa asili ndio ulikuwa ukionekana machoni mwa watu wengi.
Judith alionekana kuwa mcha Mungu. Karama ya
Uimbaji ambayo alikuwa nayo ndio ambayo ilimfanya kuzidi kukubalika katika
kanisa hilo
lililokuwa likiongozwa na mchungaji Matimya. Judith akaamua kujiunga na kwaya
mojawapo iliyokuwa kanisani hapo. Kila mtu alionekana kubarikiwa katika vipindi
vyote ambavyo Judith alikuwa akimsifu Mungu. Judith alikubalika na kila mtu
kanisani hapo.
Vijana hawakutaka kubaki nyuma kanisani
hapo, harakati za kumtaka Judith zilikuwa zikiendelea kimya kimya kanisani
hapo. Judith hakutaka kujirahisisha kwa wavulana kitu ambacho kiliwapelekea
vijana wengi kusimamishwa huduma kanisani humo.
“Watu wakijua?” Judith alimuuliza mchungaji
Mwakipesile huku akionekana kuwa na hofu. Mchungaji Mwakipesile hakuongea kitu
chochote, alibaki akimwangalia Judith na kisha kutoa tabasamu.
“Utawaambia au?” Mchungaji Mwakipesile
alimuuliza.
Swali lile likaonekana kuwa gumu kwa Judith,
alibaki kimya huku akimwangalia mchungaji Mwakipesile ambaye alionekana
kumaanisha kile alichokuwa akikiongea kwa wakati huo. Alipoona Judith amekaa
kimya, akachukua glasi iliyokuwa na juisi ya maembe na kisha kupiga fundo moja.
“Kama
hautowaambia nina uhakika hawatojua” Mchungaji Mwakipesile alimwambia Judith
ambaye kwa kiasi fulani woga wake ukaonekana kupungua.
“Na vipi kuhusu malipo?” Judith aliuliza.
“Milioni tano baada ya kukamilisha kazi hii”
Mchungaji Mwakipesile alijibu.
“Sawa” Judith aiitikia na moja kwa moja
kuondoka huku akijiandaa na kazi ambayo alitakiwa kuifanya.
****
Alipomaliza kuongea na viongozi mbalimbali
wa kanisa lake, mchungaji Matimya akaanza kuelekea katika ofisi yake iliyokuwa
pembeni ya kanisa hilo.
Alipoingia ofisini mwake, akaanza kuifuata kiti chake na kukalia, akaichukua
Biblia ambayo ilikuwa mezani na kuanza kusoma baadhi ya maandiko.
Alitulia kimya huku akiendelea kupitia
baadhi ya maandiko. Mara kwa mara uso wake ulikuwa ukionyesha tabasamu kila alipokuwa
akisoma andiko ambalo lilionekana kumvutia. Alitumia muda wa dakika thelathini
kuyasoma baadhi ya maandiko ambayo alikuwa ameyadhamiria kuyasoma katika
kipindi hicho. Alipomaliza kuyasoma maandiko hayo, akaifunika Biblia yake na
kuanza kusali.
Huku akiwa katikati ya sala, mara mlango
ukasikika ukianza kugongwa kitu ambacho kilimpelekea kukatisha sala yake na
kumkaribisha mgongaji. Mlango ukafunguiwa na msichana Judith kuingia. Mchungaji
Matimya akaonekana kushtuka kwani halikuwa jambo la kwaida kwa mgeni kuingia
ndani ya ofisi yake katika kipindi hicho ambacho alijiandaa kufunga ofisi yake.
Judith akaanza kupiga hatua kukifuata kiti
cha wageni na kisha kutulia huku kikiwa mbele ya meza ile pale ofisini. Judith
hakuongea kitu chochote kile, alibaki akimwangalia mchungaji kwa kutumia macho
ambayo yalionyesha mshtuo mkubwa kwa mchungaji Matimya. Mchungaji Matimya
akasimama na kuanza kumsogelea Judith ambaye alibaki kimya akijifikiria namna
ya kufanya kile ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati ule.
“Kuna nini tena judith?” Mchungaji Matimya
alimuuliza Judith.
“Nina kiu mchungaji” Judith alijibu.
“Kiu ya Neno la Mungu au?”
Unataka niwe nakutumia CHOMEZO watu 200 wa
kwanza kulike PAGE YA 2JIACHIE Mtatumiwa imbox chomezo LIKE PAGE YETU
HAPA ==>www.facebook.com/2jiachie
ITAENDELEA KESHO HAPA HAPA
Post a Comment