BREAKING NEWS; FRANK DOMAYO NAYE AANGUKA MIAKA MIWILI AZAM FC
KIUNGO mkabaji wa Yanga SC, Frank Domayo amesaini Mkataba wa miaka miwili kujiunga na mabingwa wapya wa Tanzania Bara, Azam FC
jioni ya leo mjini Mbeya.
Domayo amesaini Azam FC baada ya kumaliza Mkataba wake wa
miaka miwili na Yanga SC, ambayo alijiunga nayo akitokea JKT Ruvu miaka miwi iliyopita.
Kutoka Jangwani hadi Chamazi; Frank Domayo akisaini
Mkataba wa Azam FC leo
Katibu wa Azam FC, Nassor Idrisa Mohamed ‘Father’ amesema
katika kuendelea kukiimarisha kikosi chao kwa ajili ya msimu
ujao wamepiga hatua nyingine kwa kumsaini Domayo.
Frank Domayo akitia dole gumba, maana yake ni mchezaji
mpya wa Azam FC
“Kama unavyojua, baada ya kumaliza msimu vizuri tukiwa
mabingwa wa Bara, tuligundua mapungufu kwenye kikosi chetu na
kwa ushauri wa mwalimu wetu (Joseph Marius Omog) ndiyo tunayafanyia kazi,”alisema Father.
Domayo anakuwa mchezaji wa wa pili ndani ya siku mbili kusajiliwa na
Azam FC kutoka mabingwa wa zamani na mabingwa wa kihistoria
Tanzania Bara, Yanga SC baada ya jana klabu hiyo kumsaini
mshambuliaji Mrundi Didier Kavumbangu.
CHANZO: BIN ZUBEIRY
jioni ya leo mjini Mbeya.
Domayo amesaini Azam FC baada ya kumaliza Mkataba wake wa
miaka miwili na Yanga SC, ambayo alijiunga nayo akitokea JKT Ruvu miaka miwi iliyopita.
Kutoka Jangwani hadi Chamazi; Frank Domayo akisaini
Mkataba wa Azam FC leo
Katibu wa Azam FC, Nassor Idrisa Mohamed ‘Father’ amesema
katika kuendelea kukiimarisha kikosi chao kwa ajili ya msimu
ujao wamepiga hatua nyingine kwa kumsaini Domayo.
Frank Domayo akitia dole gumba, maana yake ni mchezaji
mpya wa Azam FC
“Kama unavyojua, baada ya kumaliza msimu vizuri tukiwa
mabingwa wa Bara, tuligundua mapungufu kwenye kikosi chetu na
kwa ushauri wa mwalimu wetu (Joseph Marius Omog) ndiyo tunayafanyia kazi,”alisema Father.
Domayo anakuwa mchezaji wa wa pili ndani ya siku mbili kusajiliwa na
Azam FC kutoka mabingwa wa zamani na mabingwa wa kihistoria
Tanzania Bara, Yanga SC baada ya jana klabu hiyo kumsaini
mshambuliaji Mrundi Didier Kavumbangu.
CHANZO: BIN ZUBEIRY

Post a Comment