Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango akichangia hoja bungeni leo
Mtwara,
Kwa ufupi hali ni tete na hakuna amani, mabomu ya machozi ya leo yalitawala
na huduma zote za kijamii zilifufungwa,usafiri, masoko,
maduka na bar zote zimefungwa, daladala, Taxi na Bodaboda hazifanyi
kazi. Kwa ujumla kilichoendelea Mtwara ni mapambano makali kati ya Jeshi la
polisi na wananchi wenye hasira wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato
wa gesi ilihali nchi ikiwa haina sera inayosimamia nishati hiyo.
Kufuatia
Kambi ya Upinzani kuukataa mpango wa serikali wa ujenzi wa bomba la
gesi kutoka Mtwara Mpaka Dar es salaam ilihali Waziri wa Nishati akisoma
hotuba yake.
Jengo la Ofisi ya CCM saba saba limechomwa moto.
Lodge/Hotel
(Shengena) inayoaminika kwamba ndiyo waliyofikia Askari wa Jeshi la
Polisi (FFU) kutoka mikoa ya jirani kwaajili ya operation inayoendelea
imechomwa moto.
Nyumba kadhaa za watumishi wa Serikali zimechomwa maeneo ya Shangani. (habari haijathibitishwa rasmi)
Hili linaendelea wakati bajeti ya nishati na madini ikiendelea kujadiliwa muda huu Bungeni
Post a Comment