ad

ad

Rais Jakaya Kikwete aifuata Azam Chamazi

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, anatarajiwa kuitembelea Klabu ya Azam, Championi Ijumaa limefahamishwa.
 
Mmoja wa mabosi wa klabu hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema Rais Kikwete anatarajiwa kutua katika Uwanja wa Chamazi uliopo eneo la Mbande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mapema wiki ijayo.
 
Bosi huyo alisema mara baada ya kutua kwa Rais Kikwete katika eneo hilo, atapata nafasi ya kuangalia maendeleo ya klabu pamoja na kufungua uwanja mpya wa klabu hiyo unaojengwa kwa kasi pembeni ya uwanja wa sasa.
 
“Uongozi upo katika maandalizi makubwa katika ugeni huo mzito na kikubwa nadhani rais amevutiwa kirahisi kuja huku kutokana na maendeleo ya haraka ambayo timu yetu imekuwa ikiyapata,” alisema bosi huyo.
Naye Katibu Mkuu wa Azam, Nassoro Idrissa alikiri kuwepo kwa mpango wa ziara hiyo ya rais na kusema kila kitu kitakapokuwa sawa, uongozi wake utatangaza rasmi juu ya jambo hilo.
Powered by Blogger.