ad

ad

JUSTIN BIEBER AKERA MASHABIKI WAKE AZOMEWA JUKWAANI

LONDON, ENGLAND
SUPASTAA mtoto wa muziki wa pop, Justin Bieber amezomewa na mashabiki ‘watoto wenzake’ na wazazi wao baada ya kuchelewa kuanza shoo kwa saa mbili ndani ya 02 Arena jijini London, Jumatatu usiku.
Mwimbaji huyo Mcanada aliyesherehekea miaka 19 ya kuzaliwa Ijumaa iliyopita, alitakiwa kuwa kwenye steji saa 2.30 usiku, lakini hakutokea hadi saa 4.20.
Mashabiki wake wengi – ambao walikuwa watoto wa umri mdogo – wakati huo tayari walikuwa wamerudishwa majumbani kwa ajili ya kuwahi kuamka kwenda shule Jumanne asubuhi, huku wengine wakitokwa machozi kwa kutoona shoo yake ambayo walilipa hadi pauni 331 kwa tiketi.
Wafuasi wake kutoka Canada wanaojiita Beliebers ambao wamekuwa wakifuata shoo zake maeneo mbalimbali, pia walikerwa na uchelewaji huo wa kipenzi chao.
Watu 20,000 tayari walijazana uwanjani saa 12.30 jioni — na wazazi wao walirudi kuwachukua saa 4 usiku ambapo shoo hiyo ilipangwa kumalizika, lakini wakati huo Bieber alikuwa bado hajapanda kwenye steji.
Shabiki mmoja, Rikki Townsend, 16, alisema: “Kila mmoja alizomea. Wakati alipofika hakusema hata ‘samahani’ – alianza tu kuimba.”
Baadae Bieber aliomba msamaha mashabiki wake kupitia tweeter, akisema uchelewaji wake ulisababishwa na sababu za kiufundi, na kuahidi kwenda sawa katika shoo nyingine Alhamisi na Ijumaa uwanjani hapo.
Tukio hilo limekuja baada ya staa huyo mtoto pamoja na kampani yake kutimuliwa katika klabu ya Cirque du Soir jijini London Ijumaa iliyopita kwa sababu wote walikuwa wakinuka harufu ya bangi.

Powered by Blogger.