SIMBA SC LEO NI KUFA NA KUPONA KWA PRISONS
MABINGWA
watetezi wa soka Tanzania Bara, Simba, Jumatano ya leo wanashuka uwanja
wa Sokoine mjini Mbeya kuvaana na wenyeji Prisons ya Mkoani humo.
Simba
waliyoingia mjini humo juzi, wameweka kambi yao Mbalizi kilomita 20
kutoka Mbeya mjini huku wenyeji wao wakiwa wamejichimbia Tukuyu. Simba
inaingia dimbani ikiwa na kumbukumbu ya kichapo toka kwa Libolo ya
Angola, ikiwa ni pamoja na kugawana pointi na JKT Oljoro katika mchezo
wa ligi kuu.
Kocha
msaidizi wa Simba Jamhuri Kihwelo alisema kuwa timu yao imekuja kucheza
mechi hiyo huku malengo yao yakiwa ni kuchukua pointi zote.
Nae Kocha wa Prisons Jumanne Chale amesema licha ya ukweli kuwa Simba ni timu nzuri lakini anaamini pointi tatu zitabaki Mbeya.
Post a Comment