ad

ad

SIMBA SC LEO NI KUFA NA KUPONA KWA PRISONS


MABINGWA watetezi wa soka Tanzania Bara, Simba, Jumatano ya leo wanashuka uwanja wa Sokoine mjini Mbeya kuvaana na wenyeji Prisons ya Mkoani humo.
Simba waliyoingia mjini humo juzi, wameweka kambi yao Mbalizi kilomita 20 kutoka Mbeya mjini huku wenyeji wao wakiwa wamejichimbia Tukuyu. Simba inaingia dimbani ikiwa na kumbukumbu ya kichapo toka kwa Libolo ya Angola, ikiwa ni pamoja na kugawana pointi na JKT Oljoro katika mchezo wa ligi kuu.
Kocha msaidizi wa Simba Jamhuri Kihwelo alisema kuwa timu yao imekuja kucheza mechi hiyo huku malengo yao yakiwa ni kuchukua pointi zote.
Nae Kocha wa Prisons Jumanne Chale amesema licha ya ukweli kuwa Simba ni timu nzuri lakini anaamini pointi tatu zitabaki Mbeya.
Powered by Blogger.