KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA - 06

“Nilijua utakasirika bosi…”
“Nikasirikie nini?”
“Utajua kumbe naachaga kazi nakwenda kukutana na wanaume nje.”
“Sasa mi nikasirike nini? Wewe si mtu mzima bwana! Lazima utataka kuguswaguswa, kutekenywatekenywa, kushikwashikwa na kupewa jotojoto,” alisema mama Joy huku akionesha kwa viitendo maneno aliyokuwa akiyasema, mfanyakazi huyo akawa anacheka na nguvu ikaanza kumrudia kwa mbali…
“Au siyo, mimi sina wasiwasi hata nikikuona unaingiza mwanaume ndani, ilimradi baba Joy asijue tu, mimi mzungu bwana,” mama Joy alikazia huku akitoka.
Baada tu ya kuondoka, mfanyakazi huyo alifuta ile namba ya baba Joy kisha akaminya namba za shangazi yake kama alitaka kupiga lakini hakupiga.
***
Mzoa taka alikuwa kijiweni na wachafau wenzake. Mazungmzo yao yalitawaliwa na maneno ya kihuni huku wakichimbana mikwara kibao…
“Jamani masela ee…kuna mke wa mnene mmoja ameiva kwangu ileile…kila siku nikienda kuchukua taka ananipa chombo natumia, ameshaniingia hadi room, yaani yuko sawa ile mbaya.”
Wenzake walimkatalia, yeye akawaapia. Alitumbukiza mkono mfukoni na kutoa elfu hamsini…
“Hii amekata leo baada ya kumwendesha kitandani, mwanamke hasikii, sura yangu inamponesha kichefuchefu.”
Masela wenzake walianza kumsakama walitaka aigawe ile elfu hamsini…
“Mwana mzuka basi, ichanechane hiyo fifte, watu tukaning’nie kwenye sembe.”
***
Mama Joy alitembea hadi kwa mlinzi…
“Hebu fungua geti…”
“Unataka kwenda wapi bosi..?”
“Si juu yako kujua..?”
“Mzee anaweza kuniuliza…”
“Kwani hana simu yangu..?”
“Mbona leo alinipigia mimi…”
“Kuhusu nini..?”
“Aliniuliza kama upo.”
Mama Joy alisimama, akageuza…
“Alikuuliza kama mimi nipo? Ukamjibuje..?”
“Nilimwambia upo, akauliza upo na nani..? sikumjibu…”
“Mh!” aliguna mama Joy, akakumbuka muda ule mumewe alipompigia simu wakati yeye anambembeleza mzoa taka na maongezi yao yakawa hivi…
Anamwambia mzoa taka…
“Haa! Mume wangu huyo anapiga…Haloo…”
“Uko wapi wewe..?”
“Nani mimi..?”
“Unaniuliza swali gani hilo..?”
“Niko nyumbani…”
“Na nani..?”
“Nani mimi..?”
“Mama Joy…”
“Abee…”
Baba Joy anakata simu.
Mama Joy alianza kuhisi kuna kitu mumewe amekinasa, akahisi kizunguzungu kichwani…
“Fuko hebu sema ukweli wako, hujamwambia nipo na mtu mwingine ndani..?”
“Sikumwambia mama, labda kama aliongea na Helena.” Helena ni yule msaidizi wa kazi za ndani…
“Mh!” aliguna mama Joy, akakumbuka mambo haya…
“We mbona unaongea kwenye simu kwa kunong’ona sana, unaongea na nani?”
“Shangazi yangu anasema anaumwa sana bosi…”
“Sasa kama shangazi yako anaumwa ndiyo uongee kwa kunong’ona..?”
“Anasema hajisikii vizuri bosi…”
“Khaa! Sasa asipojisikia vizuri yeye ndiyo inakufanya wewe uongee kwa kunong’ona..?”
“Nisamehe mama…”
Mama Joy aligeuza, akarudi ndani. Alipitiliza hadi jikoni…
“We dada…”
“Abee bosi…”
“Baba Joy alikupigia simu leo..?”
Mfanyakazi huyo kwanza alisita kujibu, akili ilijipeleleza ili kutafuta je ajibu ni kweli au akatae?
“Hapana bosi…”
“Hebu lete simu yako.”
Helena aliitoa simu haraka sana huku akionesha unyenyekevu wote. Mama Joy alikwenda kwenye namba zilizopigwa, hakuiona ya mumewe, akaenda zilizopiga pia hakuiona, ila aliikuta ile ya shangazi ikiwa ameseviwa kwa jina la ‘Anti Suzy’…
“Oke, nisamehe sana kwa kukagua simu yako, maana kuna mtu ameniambia baba Joy alikupigia…
“Hapana mama, hajanipigia.”
Mama Joy alirudi sebuleni, akakaa kwenye kochi. Aliwaza kidogo, akampigia simu mumewe.
Sauti ya baba Joy ilikuwa nzito kupindukia…
“Haloo…”
“Halo, baba Joy…”
“Nini?”
“Khaa! Asa mbona unapokea simu unaniuliza nini..?”
“Ulitaka nikuulizeje..?”
“Unajua nataka kukwambia nini..?”
“Wewe mwanamke wewe, usiniletee usanii mimi, we endelea tu,” baba Joy alikata simu.
Mama Joy alibaki ameishika simu yake huku mikono ikitetemeka na wasiwasi juu…
“Helena,” kwa mara ya kwanza alimuita kwa jina mfanyakazi wake huyo…
“Abee bosi…”
“Haraka sana.”
Sekunde kadhaa, Helena akawa amefika…
“Kamuite na Fuko.”
Helena alitoka hadi kwa mlinzi…
“Bosi anatuita, lakini usoni kama hayuko sawasawa…”
“Aah! Kakwambiaje kwani?”
“Kwanza we ndiyo ulimwambia mimi nilipigiwa simu na mumewe..?”
“Sikusema hivyo, nilisema labda alikupigia na wewe, nilitumia neno labda.”
“Nyiye,” mama Joy aliwaita akiwa amesimama nje ya mlango mkubwa.
“Tunakuja mama,” alisema mlinzi huku wakitembea kwa kasi kuelekea alikosimama.
Mama Joy alipowaona wamekaribia, aligeuka kutangulia ndani…
“Tumefika mama…”
Mama Joy aligeuka kuwaangalia kisha akakaa kwenye kochi…
“Nani kati yenu ni mnafiki kwangu..?”
Wote wawili waliangaliana kwa nyuso zenyen wasiwasi…
“Nauliza nani kati yenu ni mnafiki kwangu..?” safari hii mama Joy aliongea huku akipandisha sauti juu…
“Labda mwenzangu bosi, mimi siwezi kuwa mnafiki kwako, hata wewe bosi unajua, ningekuwa mnafiki mzee aliponiuliza uko na nani si ningesema upo na mzoa taka na pia ningesema na mimi niliamkia kwako…”
“Wewe Helena ndiyo mnafiki siyo..?”
Mfanyakazi huyo alitulia kwa muda akimkazia macho bosi wake kisha akasema…
“Mimi si mnafiki kwako bosi, ina labda dhamira inakusumbua…”
“Dhamira inanisumbua..?”
“Ndiyo bosi…”
“Una maana gani..?”
“We bosi unajua mwenyewe, sisi na wewe tuko kwa muda gani, lakini leo hii tuje kuanza unafiki kwako ni kweli..?”
Mama Joy alitulia kwa muda akitafakari, kisha akawaambia…
“Ondokeni zenu.”
***
Siku ya pili, Helena alikuwa akinywa chai jikono wakati simu yake ilipoita. Alikimbilia kuangalia kwenye kioo ni nani aliyepiga…
“Mh!” aliguna kwanza. Alikuwa baba Joy…
“Shikamoo bosi…naomba utume meseji hali mbaya sana wenzio huku nyumbani,” alipomaliza kusema akakata simu.
Baba Joy alihema kwa kasi akijiuliza maswali mengi. Alijikuta akiyarudia yale maneno ya mfanyakazi wake wa ndani…
“Shikamoo bosi…naomba utume meseji hali mbaya sana wenzio huku nyumbani…”
“Kunaweza kuwa kumetokea nini?” alijiuliza. Pia akajiuliza atume meseji au asitume?
Baada ya kuwaza na kuwazua kama dakika tano, aliamua kutuma meseji…
“Kuna nini kwani?” baba Joy aliituma meseji hiyo. Akakaa akisubiri majibu…
“Mkeo kama ameshtuka ulivyonipigia simu, lakini hajaonesha kuamini ila kama anataka kuamini. Tuma meseji tu.”
Baba Joy alikaa kwa muda kisha akamtumia meseji…
“Mimi narudi leo, niko njiani hapa tayari. Nitafikia mahali, mzoa taka akija tu, niambie.”
“Sawa bosi wangu.”
***
Baba Joy aliendesha gari kwa kasi huku kichwa chake kikiwa kimejaa mawazo kibao, hasa ya wivu wa mapenzi. Hapo alikuwa akipita Chalinze…
“Iko siku kila kitu kitakuwa wazi,” alisema moyoni.
Mara simu yake iliita, akaangalia kwenye skrini kisha akasonya. Alikuwa mkewe ndiyo maana alisonya, moyoni alitamani namba aibadilishe, badala ya kuwa My Wife, iwe Malaya wa Mjini…
“Nini?” baba Joy aliuliza kwa sauti iliyojaa machugu…
“Khaa! Yaani unapokea simu yangu na kuniuliza nini…”
“Sema unachotaka kuniambia, kama vipi kata simu…”
“Nakuuliza uko wapi kwani?”
“Arusha Mjini…”
“Ha! Hurudi leo..?”
“Kesho,” baba Joy akakata simu.
Mama Joy alihema kwa kasi. Alijua mambo yameharibika, lakini alijipa moyo kwamba Mungu mkubwa!
Kisa cha mama Joy kuulizia hayo, alijua mzoa taka angefika muda wowote ule kwani jana yake alipoondoka alimwambia asikose kuja kesho.
Alitoka hadi getini…
“Fuko…”
“Ndiyo bosi,” Fuko aliitika kwa heshima zote…
“Hakuna mgeni wangu..?”
“Hakuna bo…”
“Ngo ngo ngooo,” geti kubwa liligongwa…
“Labda huyo…”
“Hebu fungua.”
Fuko alifungua geti, macho ya mama Joy yalikuwa makini kutaka kujua ni nani anaingia maana nyumba yake huingia watu wengi…
“Shikamoo mama,” alikuwa mzoa taka bwana!
ITAENDELEA SIKU YA KESHO
Post a Comment